Dkt. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

Sam GM

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
535
28
JF imekuwa ni mahali pa kupashana habari na kuweza pia kuzungumzia mambo ya historia yetu na mwelekeo wa nchi.

Kuna Huyu bwana anajulikana kama marehemu Dr Kleruu, mie nimekuwa nikimsikia katika wimbo wa Mbaraka Mwinshehe kuwa alikuwa mwanamapinduzi.

Je, kuna yeyote anaweza kutupatia taarifa kumhususu huyu Dr Kleruu alikuwa nani hasa na uana mapainduzi wake ulikuwa vipi katika historia na siasa za Tanzania?




Mnara wa kumbukumbu kifo cha Dr. Kleruu kijijini Isimani



Mtoto wa Said Mwamwindi



=== Historia ya Dr. Kleruu kwa ufupi ===

HISTORIA: MKULIMA ALIYEMUUA MKUU WA MKOA SIKU YA KRISMASI-

ILIKUWA siku ya Sikuku ya Noeli almaarufu Christmas mnamo mwaka 1971. Mkuu mpya wa Mkoa wa Iringa aliyehamishiwa hapo akitokea Mtwara, Dkt. Wilbert Kleruu, msomi wa Shahada ya Uzamivu (PhD) wa Uchumi wa kijamaa katika Kilimo aliuawa na Mkulima aitwaye Said Mwamwindi.

Kipindi hicho kulikuwa na kampeni ya kutaifisha mashamba ya wakulima wakubwa na kuyafanya mashamba ya kijiji. Na Dkt. Kleruu alipelekwa Iringa ili akatekeleze kazi hiyo kwani kipindi hicho Iringa ilikuwa na wafanyabiashara wakubwa waliomiliki mashamba makubwa ya Kilimo hasa maeneo ya Isimani.

Katika eneo hilo la Isimani kulikuwa na mkulima mmoja aliyekuwa anamiliki takribani hekari 400 za mashamba na mfanyabiashara aliyekuwa anamiliki majumba Iringa mjini - Said Mwamwindi-
Kwa wakati ule ilishauriwa angalau kila mtu awe na shamba lisilo zidi hekari 4. Jambo ambalo lilileta mvutano mkubwa kati ya wakulima wakubwa na Serikali.

Sasa siku hiyo ya Christmas, Dkt. Kleruu alikwenda Isimani akiwa katika utekelezaji wa sera ya kutaifisha mashamba. Moja kwa moja alikwenda hadi shambani kwa Mwamwindi, na kumkuta analima.

Mkuu huyo wa Mkoa akamuuliza mbona unalima shamba lako mwenyewe na si la kijiji? Mwamwindi akajibu, sioni tatizo hakuna mtu shambani, leo ni Jumapli tena ni sikukuu.

Maneno yale yalimuudhi Dkt. Kleruu, ambaye alikuwa akisifika kwa ukali, kutekeleza sera za serikali na maneno makali au kutukana watu hadharani pale wanapo fanya makosa.

Dkt. Kleruu baada ya kuudhika alimtukana Mwamwindi tusi lililomlenga mama yake ambaye tayari alikuwa marehemu. Mwamwindi alihoji inakuwaje anamtukania mama yake, huku akimuonyesha kaburi alimozikwa?

Mkuu wa Mkoa, aliendelea kuja juu, huku akisema kaburi ndio nini? Huku akilipiga mateke kaburi la Mama yake Mwamwindi. Kwa kabila la wahehe makaburi yana heshima yake, kwani ndipo nyakati nyingine hutumika katika sala, matambiko na mila kadha.

Kitendo kile kilimghadhabisha Mwamwind, na kuanza kukimbia kuelekea nyumbani. Mkuu wa Mkoa akadhani Mwamwindi anamkimbia, akaamua kumfuata.

Alipofika nyumbani, tayari Mwamwindi alisha ingia ndani na kuchukua bunduki yake, Dkt. Kleruu baada ya kuona hali ile mara moja alianza kumuomba msamaha, lakini hasira zilimuwaka Mwamwindi kama moto wa nyika; hakuwa na msamaha, alimfyetulia risasi kichwani Dkt. Kleruu na kumuua.

Baada ya kumuua, Mwamwindi aliuchukua mwili ya Mkuu wa Mkoa na kuuweka ndani ya gari (inadaiwa kwenye boneti) alilokuja nalo Mkuu huyo wa Mkoa.

Kisha alichukua kofia ya Dkt. Kleruu na kuivaa, akaingia ndani ya gari na kuanza safari ya kuelekea Iringa mjini tena akipita njia isiyo ruhusiwa kwani barabara ilikuwa 'one way'.

Alipo karibia mjini, askari walishangaa ni nani anaye pita njia isiyo ruhusiwa, ila mara waligundua ilikuwa gari ya RC wa Iringa, hivyo walidhani amepata dharura.

Gari lilipowasili kituoni, Polisi walijiandaa kupiga salute, mara alishuka Mwamwindi akiwa na bunduki yake na kuelekea ndani (counter). Askari walipigwa na butwaa.

Alipofika aliwaambia "Nendeni mkachukue Nguruwe wenu ndani ya gari," na Kisha akakabidhi bunduki yake.

Lilikuwa tukio la kustaajabisha, na kushangaza na lililofanyika kwa haraka sana.

Baada ya taarifa kuenea, msako wa polisi ulianza mara moja. Ila katika msako huo, Polisi waliwakamata baadhi ya watu walio kuwa wakinywa bia kwa furaha, shangwe na nderemo baada ya kusikia Dkt. Kleruu ameuawa. Kwani wanadai alikuwa na dharau.

Kesi ya Mwamwindi alipelekwa haraka sana na ndani ya miezi kadhaa, Juni 1972, Mwamwindi alihukumiwa kunyongwa hadi kufa, ikiwa ni moja ya hukumu chache za kunyongwa zilizo wahi kuidhinishwa.

Inadaiwa Mwalimu. Nyerere alihuzunishwa sana na kifo hicho, na hata kesi ya Said Mwamwindi ilipoisha na kupewa hukumu ya kifo, Inasemekana Nyerere hakusita kusaini, na ni mojawapo ya hukumu tatu tu za kifo zilizotekelezwa wakati wa utawala wa Nyerere

MICHANGO YA WADAU:

Dr Wilbert Kleruu alikuwa mzaliwa wa mkoa wa Kilimanjaro sehemu iitwayo Mamba (au Mwika), Moshi vijijini ambako siku hizi kunaitwa Vunjo. Alisomea uchumi wa kijamaa hadi ngazi ya PhD, na hasa alikuwa agricultural economist.

Alifanya kazi kwa karibu sana na Mwl Nyerere ambaye alimpenda sana, maana alimwona ni muumini wa siasa yake ya ujamaa na kujitegemea. Alijituma na kuiamini kwa moyo wake itikadi hiyo, kwamba ukombozi wa nchi utapatikana kwa mapinduzi ya kilimo cha kijamaa (ndio uanamapinduzi anaozungumziwa).

Alijitahidi pia kutekeleza itikadi hiyo kwa vitendo, na ndiyo iliyomgharimu maisha yake mwaka 1971 alipokuwa mkuu wa mkoa wa Iringa. Siku moja ya jumapili (hakuwa na jumapili huyu mjamaa) alikwenda kwenye shamba la mkulima mmoja aliyeitwa Saidi Mwamwindi, ambaye alikuwa na shamba kubwa sana, kwa lengo la kufuatilia maagizo yake aliyokuwa ametoa kuhusu shamba hilo, ndipo alipokorofishana na mkulima huyo maana yeye hakuzikubali hata kidogo hizo sera za kijamaa. Mwamwindi alikwenda nyumbani kwake akachukua gobore lake, akamfuata Dr Kleruu alipokuwa akampiga risasi na kumwua, kisha akapakia mwili wake kwenye Land Rover yake (pick up short chassis) na kupeleka kwenye kituo cha polisi ambako pia alijisalimisha.

Nyerere alihuzunishwa sana na kifo hicho, na hata kesi ya Saidi Mwamwindi ilipoisha na kupewa hukumu ya kifo, Nyerere hakusita kusaini, na ni mojawapo ya hukumu tatu tu za kifo zilizotekelezwa wakati wa utawala wa Mwl Nyerere.

Wengine wataongezea, lakini kama hapo ulipo unaweza kupata vitabu, tafuta kitabu kiitwacho "The Egalitarian Moment: Asia and Africa 1950-1980" kilichoandikwa na Donald Anthony Low (1995), habari hii ya Dr Kleruu iko kwenye ukurasa wa 52-53, kwenye chapter yenye heading "Richer Peasants and the State".

Unaweza pia kusoma journal article iliyoandikwa na Phillip Raikes mwaka 1979: Agrarian Crisis and Economical Liberalisation in Tanzania kwenye jarida la Journal of Modern African Studies Vol 17(no.2) pg 309-316, ambayo nimejaribu kukuwekea link yake hapa chini. Kifo cha Dr Kleruu kiliwahuzunisha watu wengi hasa wakulima wadogowadogo wa huko Iringa ambao walikuwa wakifurahia alivyokuwa ananyang'anya mashamba kwa wakulima wakubwa ili yalimwe kijamaa. Pia alikuwa ana tabia ya kuwafokea watumishi wa serikali hata wakurugenzi kwenye mikutano ya hadhara, pale alipoona sera zake za kijamaa hazijafuatwa kama alivyotaka, yaani alikuwa na ule ujamaa wa kibabe hasa uliokuwa Urusi (ajabu ni kwamba huyu alisomea Marekani!). Kwa namna fulani (ama kiasi kikubwa) alikuwa na 'ukali' kama ule wa Marehemu Sokoine. Raikes (1979) anaandika hivi kuhusu kifo cha Dr Kleruu kwenye rejea niliyotaja:

"...the emergence of the assassin of the Regional Commissioner as a 'folk hero', seems to me a misreading. Dr Wilbert Kleruu had achieved a certain local popularity largely because of his habit of abusing civil servants in public. His expro- priation of the 'rich' peasants also seems to have been quite popular, especially of course with those who received the land. As for the various stories which went the rounds in the aftermath of the murder, I can only go by second hand gossip...." (uk 315).
Anaendelea:

"The point stressed was that Mwinyi killed Kleruu for calling him a dog (said to be an unallowable insult among the Hehe) in front of his wife (which made it the more unforgivable). In short, it was seen by Mwinyi as a means to preserve his honour, and this would help to explain why he gave himself up immediately" (uk 316). Mwamwindi alijulikana pia kama "Mwinyi" kwa maana ya "Lord"

Historia ya Isimani imejaa a lot of hardship. Wakulima waliohamia huko walikuta ni pori tuu na wakaclear mashamba na kuanza kulima kwa tabu sana, maji yanachotwa mbali, chakula shida, wanyama pori nao tele, etc.

Babu yangu alikuwa mmojawapo wa wakulima wa mwanzo huko Isimani; mama yangu anasimulia walivyokuwa wanaenda mbali sana kufuata maji ya kunywa na kupikia. Maisha yalikuwa duni na magumu sana. Ikumbukwe hii ni kabla ya sera ya vijiji vya ujamaa, azimio la Arusha nk. Sera hizi zilivyoingia mkoani Iringa, serikali iliwataka watu wote wahamie katika vijiji vya ujamaa na kuwe na communal farming. Hii iliwakuta wakulima wengi mahala pabaya sana manake mashamba waliotoil kuyalima yangechukuliwa kuwa ya vijiji vya ujamaa. Hatimaye walikubali ila ikaonekana kwamba kijiji cha ujamaa Isimani kina mashamba mengi tayari, na wakulima wengine wakakubaliwa waendelee kuyashughulikia mashamba yao zile siku ambazo sio za kijiji, na jumapili ndio siku isiyo ya kijiji na Mwamindi na wakulima wale wa mwanzo kule Isimani wakawa wanatend mashamba yao siku za jumapili.

Kutoka Iringa mjini Kleruu ameamua kwenda Isimani bila ya mlinzi/dereva. Ikumbukwe pia ameshakuwa very unpopular na wanyalukolo na word was out kuwa yeyote atakayempata kwanza ammalize (haya ni maneno ya wanyalukolo wa enzi hizo) Alipopita kwa Mwamindi na akamuona Mwamindi yupo shambani kwake ndipo akamfuata huko huko na kuanza kumkejeli. Inasemekana Kleruu alikuwa ana kifimbo kama kile cha Mwalimu na akaanza kumchomachoma kifuani Mwamindi huku akimwambia"wewe nani kakupa ruhusa kulima jumapili? Si ulitakiwa kulima kwenye shamba la kijiji cha ujamaa tuu?" etc etc.

Mwamindi akaingia ndani akachukua shot gun yake(nadhani ilikuwa zile wanaziita two-two rifle, popular sana enzi hizo) na akatokea kwa nyuma (nyumba za waHehe zina mlango/dirisha mdogo kwa nyuma) na akamtwanga risasi na kikafuata kilichoelezwa hapo juu. Ila alipofika Iringa alikwenda kwanza kwa wake zake na kuwaambia alichofanya ndipo akaenda police station. Kuna mzee mmoja alipishana na Land Rover ya Kleruu na akashangaa kumuona Mwamindi anaendesha, na hapo hapo akajua soo limetokea, akapita shambani kwa Mwamindi na akaelezwa kilichotokea. Vilevile, kule mtaani watu walishangaa Mwamindi anaendesha kari la mkuu wa mkoana limepaki kwake! Waliokuwa wanajua walielewa mara moja nini kimetokea!

Siku ile pale Isimani, the current popular mayor of Iringa was present as a very young boy. Maggid muulize atakupa story yote ya the first political assassination in Tanzania. Ya Karume ilikuwa next the following year, I think.

-----------------------------

Jana Jumamosi jioni nilikuwa na mazungumzo marefu na Bw. Amani Mwamwindi. Mstahiki Meya wa Iringa aliyemaliza muda wake. Huyu ni mwana wa marehemu Saidi Mwamwindi ambaye simulizi juu ya kilichotokea kule Isimani mwaka 1971 tumeifuatilia.

Bw. Amani Mwamwindi alikubali kufanya mazungumzo nami hiyo jana nyumbani kwake Mlandege hapa Iringa. Ni simulizi ya kusikitisha, kusisimua na yenye kutoa mafunzo. Inahusu pia maarifa ya uongozi na dhana nzima ya utawala bora. Naandika haya saa saba za usiku Jumapili. Ngoje nikapumzike. Baadae Jumapili ya leo nitaanza kuwasilimua niliyosimuliwa.

Kumekucha. Jumapili saa kumi na mbili asubuhi. Naanza kusimulia nilichosimuliwa;

Nimefika Nyumbani kwa Amani Mwamwindi. Ni majira ya saa kumi na nusu jioni. Ni nyumba ya kawaida sana katikati ya eneo wanaloishi watu wengi, karibu kabisa na soko. Ni kata ya Mlandege.

Nagonga mlango mkuu. Anayenifungulia ni Amani Mwamwindi.
" Karibu Bwana Mjengwa". Tunafahamiana, tumewahi kukutana kabla. Miguuni hana viatu, amevaa soksi nyeusi.


Ananikaribisha kiti sebuleni. Anaagiza nilitewe kinywani. Naye anakaa kitini. Mazungumzo ya ana kwa ana. Kichwani najiuliza; unaanzaje mahojiano na mtu aliyefiwa baba yake kwa kunyongwa miaka arobaini iliyopita?

"Bw. Mwamwindi, pole sana kwa tukio lile la mwaka 1971. Mimi nimelifuatilia kiasi. Kuna simulizi nyingi mitaani. Nimeanzisha mjadala bloguni. Vijana wengi wanaonyesha kuwa na kiu ya kutaka kujua ukweli hasa wa tukio lile. Kwa vile uko hai, nikaona nikutafute tusikie kutoka kwako."

Mwamwindi ananiangalia usoni.
" Alaa!" Anatamka. Kisha kinafuata kimya.

Nakumbuka, kuwa nimetoa maelezo ya utangulizi, sijauliza swali.
" Je, ni kweli kuwa Dr Kleruu alikwenda Isimani kwa marehemu mzee Mwamwindi kuhimiza suala la kilimo ndipo akakutana na kifo chake? " Namwuliza kwa staili ya kurusha mshale bila kulenga hasa ninachotaka kupiga. Namjengea mazingira ya kuogelea katika kile anachokijiua. Na swali hili kwake analiona zuri sana.

" Swali zuri, umeuliza kama Kleruu alikwenda kuhimiza kilimo. Hapo ndipo lilipoanzia tatizo."

Nakumbuka swali muhimu kabla hajaendelea.

" Mzee Mwamwindi, hivi ulikuwa na umri gani siku hiyo ya tukio?"
" Nilikuwa na miaka 21, na marehemu mzee alikuwa na miaka 42."

Nauliza tena.
" Tunasoma kuwa ilikuwa siku ya Krismasi. Je, ilikuwa ni Jumapili au siku gani? Na wewe ulikuwapo nyumbani kwa mzee?"
" Ni kweli ilikuwa siku ya Krismasi, Desemba 25, 1971. Ni siku ya Jumamosi" Anajibu Mwamwindi.

" Turudi kwenye tatizo lilipoanzia" Namwomba Mzee Amani Mwamwindi.

" Kulikuwa na tofauti ya kimtazamo. Na ugomvi ulianzia siku ya Alhamisi, Desemba 23 kwenye ukumbi wa welfare pale Mshindo. Kleruu aliwakusasanya wakulima wakubwa wa Isimani. Nataka ujue kuwa Isimani ilikuwa na wakulima wakubwa sana na mmoja wao ni marehemu baba yangu. Mle ukumbini kulitokea malumbano makali sana baina ya wazee wale na mkuu wa mkoa Kleruu.

Wazee hakukubaliana na Kleruu kuwaita pale kuzungumzia kilimo cha eka mbili au tatu wakati wao kila mmoja ukubwa wa shamba ulianzia eka mia mbili. Na tayari walikuwa na ushirika wao. Mimi nikiwa na miaka 21 nilikuwa karani wa chama cha ushirika.

Siku ile Mzee alitoka kwenye mkutano ule na kuja nyumbani kwangu hapa tulipo, Mlandege. Akanieleza juu ya mkutano ule na jinsi walivyokosana kimazungumzo na Kleruu. Akaniambia, kuwa mle mkutanoni alimwambia Kleruu ni vema akawasaidia wale ambao hawajaanza hata kutembea kuliko kuhangaika na watu wenye uwezo wa kutembea na kukimbia. Na baba yangu hakwenda shule.


Kwenye Umoja wao wa wakulima wa Isimani, baba na wenzake walijipanga vema. Walishaanza kuzungumzia haa uwezekano wa kumlipa mwanasheria, hata kama ni wa kutoka Uingereza, aje kuwatetea katika uovu ule wanaotaka kufanyiwa. Hawakukubaliana na utekelezaji wa sera za Ujamaa kwa staili ile aliyotaka Kleruu. Kuingia kwenye ushirika na wengine wakati wao walishaanza zamani. Fikiri, wao walifyeka mashamba yao tangu miaka ya hamsini. Hoja yao ni kuwa mapori yalikuwa hayajaisha kwa wengine kwenda kufyeka na kulima. " Anazungumza Mzee Mwamwindi. Anaonekana kuwa na mengi sana, na hamu ya kusimulia zaidi. Nabaini pia, kuwa kwake yeye mkuu yule wa mkoa ni Kleruu na hamtaji kama ' Dr Kleruu'. Namwacha aendelee.

" Sasa baada ya ile alhamisi, mzee akashinda Ijumaa. Jumamosi ikawa siku ya Krismasi. Kwa vile wafanyakazi wake wa shambani walikuwa mapumziko ya krismasi. Na yeye ni mwislamu, na alikuwa mchapa kazi kweli, basi, alikwenda shamba lake la jirani akiwa na mdogo wangu, sasa ni marehemu, anaitwa Mohamed. Wakawa wanalima kwa trekta.

Siku hiyo Kleruu, pamoja na kuwa ni Mkristo, aliamua kutokula Krismasi. Alivaa kofia yake ya pama. Inaaminika alibeba pistol yake pia. Kleruu akaendesha mwenyewe gari lake la mkuu wa mkoa aina ya Peugeot Injection, rangi ya bluu. Katika orodha yake, Kleruu alikuwa na watu watatu wa kuwashughulikia miongoni mwa wakulima wale wakubwa wa Isimani. Target nambari moja alikuwa Bw. Rashid Juma wa Nyangólo. Nambari mbili ni marehemu baba. Namba tatu simjui.

Kleruu alipofika Nyang'olo hakumkuta mkulima Rashid Juma. Siku hiyo ya Krismasi Rashidi Juma alipata habari, kuwa kuna ng'ombe wake walipotelea milimani. Alikwenda huko milimani kusaka ng'ombe wake. Hivyo, Kleruu akafunga safari kurudi kwa target namba mbili, baba yangu Mzee Mwamwindi. Ni njia hiyo hiyo, Nyang´'olo iko mbele ya ilipokuwa ngome ya mzee." Anasema Mwamwindi akionekana kuzama katika simulizi inayomgusa. Nami namsikiliza kwa makini.

"Basi, Kleruu akafika kwa Mzee. Baba akiwa shambani akaliona gari la Kleruu limesimama nje ya mji wake. Kisha akamwona Kleruu akitembea kumfuata shambani. Baba alihisi tu, kuwa Kleruu amekuja na shari.

Kleruu akamwuliza Mzee kwa ukali, " Mbona mnafanya kazi leo siku ya Krismasi?". Baba akamwomba Kleruu waende wakuzungumze nyumbani. Akamwambia mdogo wangu Mohammed aendelee kulima. Mzee akatangulia mbele, nyuma anamfuatia Kleruu. Kabla ya kufika kwenye nyumba yake wakayapita makaburi. Kleruu akamtamkia baba mzee Mwamwindi; " Hapa ndipo unapozika mirija yako?" Alitamka hivyo huku akimtomasa tomasa mzee na kifimbo alichoshika mkononi.

Jambo hilo lilizidi kumkasirisha marehemu mzee. Akafika nyumbani kwake. Mlangoni alisimama mke wake mdogo. Inaonekana mzee alishafanya uamuzi. Jana yake alikwenda kuwinda. Hakupata mnyama. Bunduki yake moja aia ya riffle kati ya bunduki zake mbili ilikuwa bado ina risasi. Akamwambia mke wake mdogo huku Kleruu akiwa anasikia;
" Kanichulie bunduki yangu"

" Je, aliposikia hayo Dr Kleruu alifanyaje?"

" Nadhani alipigwa na butwaa. Hakuamini kama baba angefikia hatua hiyo"

"Na ilikuwaje basi Mwamwindi alipoletewa bunduki?"

" Ilienda haraka, Mzee Mwamwindi akainua bunduki yake. Tayari ilikuwa loaded na risasa tangu jana yake alipotoka kuwinda. Kleruu aliinua mikono yote miwili kama mtu anayesalimu amri. Mwamwindi akampiga risasi ya kwapani. Kleruu akabaki hai. Akapiga risasi nyingine. Ikamwua pale pale." Anasimulia Mzee Amani Mwamwindi.

Kinafuatia kimya. Anainama, namwona usoni, kuwa huzuni imemjia. Bila shaka, ni kitendo kile cha baba yake kumpiga risasi na kumwua Dr Kleruu ndicho kilichoashiria mwanzo wa ukurasa mgumu katika familia ya Mwamwindi , Isimani na pengine Iringa kwa ujumla.

Nafikiria kumwuliza swali lifuatalo; Risasi ya pili ya Mzee Mwamwindi ilimpiga Dr Kleruu katika sehemu gani ya mwili? Nasitisha swali hilo. Litasubiri mara nyingine. Mzee Amani Mwamwindi anaendelea kunisimulia;

" Mdogo wangu Mohammed akiwa shambani alisikia mlio wa bunduki. Alidhani kuwa baba amepigwa risasi. Alikimbia kurudi nyumbani. Na pale ilipowekwa kumbukumbu ya Kleruu nyuma yake ndio ilipokuwa nyumba ya mzee. Hivyo, pale ulipowekwa mnara ni mbele ya nyumba. Kwa sasa nyumba hiyo haipo.

Alipofika nyumbani, Mohammed akamkuta baba amesimama, na Kleruu amelala chini, amekufa. Mzee alichukua kofia ya pama ya Kleruu, akaivaa. Akaingiza mkono mifukoni mwa Kleruu, akachukua funguo za gari la Kleruu. Mzee alimwambia mdogo wangu amsaidie kumwinua Dr Kleruu. Mzee alimshika miguuni na mdogo wangu Mohammed alimshika kwenye mikono. Wakamwingiza kwenye buti la gari.

Baba akaendesha mwenyewe gari lile la Mkuu wa Mkoa Kleruu, Peogeot Injection, rangi ya bluu likiwa linapepea bendera ya taifa. Aliendesha kuelekea mjini Iringa. Njiani kuna walioshangaa kumwona Mwamwindi akiendesha gari la Mkuu wa Mkoa huku akiwa kichwani amevalia pama la Kleruu.

Mzee alipoingia mjini Iringa breki ya kwanza ilikuwa hapa tulipo, nyumbani kwangu Mlandege. Kama nilivyosema, wakati huo nilikuwa kijana wa miaka 21. Nilishakuwa na mji wangu, nilijenga kibanda changu hapa tulipo. Nilifanya kazi kama karani wa Ushirika. Siku ile ya tukio nami nilikwenda kwenye shamba langu Ifunda.
Basi, Mzee alipofika hapa nyumbani akaambiwa kuwa nimekwenda shamba Ifunda. Alisikitika sana." Anasema Mzee Mwamwindi huku naye bado akionyesha huzuni machoni. Miaka 40 baada ya tukio.


Alipotoka hapa alipita nyumbani kwake pale Mshindo, na baadae akasimama kwa binamu yake. Ile nyumba ya njano nyuma ya benki ya CRDB, si unaijua?" Ananiuliza.

" Ndiyo" Namjibu.
" Pale alikuwa anakaa binamu yake na baba. Basi, alipofika pale akakutana n abinamu yake. Binamu yake yule alishangaa kumwona mzee akiwa na damu kwenye nguo zake. Akashangaa pia kumwona akiwa na gari la Kleruu lenye bendera ya taifa ikipepea. Akamwuliza nini kimetokea? Mzee hakuweza kuongea akaeleweka. Alitamka; " Nimeenda kwa Amani ( Mimi) nimeambiwa kaenda shambani kwake Ifunda". Alionekana kuchanganyikiwa.

Akaingia kwenye gari. Akaendesha moja kwa moja hadi Kituo cha polisi. Akamkuta polisi kijana. Akashuka, akamwambia; " Njoo chukua mzigo wako". Akaweka chini pia kofia ya pama ya Kleruu.

Polisi alipofungua buti ya gari akashangaa kuona mzigo wenyewe ni mwili wa Mkuu wa Mkoa, Dr Kleruu. Mzee akawa amejisalimisha.

Niliporudi nyumbani kutoka Ifunda nikazikuta habari hizo mbaya. Nikaenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa Mzee pale Mshindo. Nikawakuta akina mama wanalia. Ilikuwa ni kilio. Hiyo bado ilikuwa ni Jumamosi, siku ya Krismasi. Nikauliza; kuna aliyekwenda kumwona baba pale polisi? Jibu likawa hapana. Nikaenda moja kwa moja polisi ili nikamwone baba na nimsikie kauli yake.

Nilipofika polisi nikaanza kujieleza kwa askari polisi kuomba ruhusa ya kuongea na Mzee. Wakati nikifanya hivyo mzee nae alisikia sauti yangu. Akatamka; " Mwanangu huyo, mruhusu niongee nae". Nikaongea na Mzee.

Chanzo: Majid Mjengwa

Mwanzoni mwa miaka ya 1970 Mkulima said Mwamwindi alikabiliwa na shitaka la kumwua Dr Wilbert Kleruu, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa wakati huo.

Mshitakiwa Mwamwindi alijitetea kuwa alipokuwa anamwua marehemu Kleruu alirukwa na akili . Hivyo, akapotewa na fahamu ya kuweza kuelewa kile alichokuwa anakitenda. Jaji Onyiuke kutoka Nigeria aliukataa utetezi wa Mwamwindi kwa kutilia maanani kwamba baada ya mshitakiwa kughadhibishwa ndipo alipokwenda ndani kuchukua bunduki ambayo aliitumia kumwua marehemu.

Mwezi Oktoba mwaka 2010, nikiwa njiani kwenda Dodoma na Arusha, nilipita kijijini Isimani. Hapo ndipo yalipokuwa makazi ya Mwamwindi. Ni umbali wa kilomita zipatazo 40 kutoka Iringa Mjini. Kijijini Isimani Saidi Mwamwindi bado anaonekana ni shujaa kwa kukataa kunyanyaswa na Mkuu wa Mkoa. Inasimuliwa, kuwa ilikuwa siku ya Jumapili , tena siku ya Krismasi, pale Mkuu wa Mkoa, Dr Kleruu, alipofika Isimani na kumkemea Mwamwindi mbele ya wake zake kwa vile alifanya kazi za shamba siku ya Sikukuu.

Inasimuliwa, kuwa Dr. Wilbert Kleruu alifikia hata hatua ya kuanza kudhihaki makaburi ya mababu zake Mwamwindi akimwambia Mwamwindi: "Humu ndimo mlimozika mirija yenu". Alifanya hivyo huku akionyesha makaburi yake kwa kutumia fimbo aliyoshika mkononi. Mwamwindi alikasirika sana. Akaficha hasira yake. Kutoka makaburini, Mwamwindi aliongozana na Kleruu hadi nje ya nyumba yake. Akamwomba Mkuu huyo wa Mkoa abaki nje. Mwamwindi akaingia ndani chumbani.

Mke wake Mwamwindi alimwona mume wake akichukua bunduki na kusimama dirishani. Mama huyo alidhani mumewe amepanga kwenda kuwinda. Kumbe, Mwamwindi alitokea dirishani na kumwelekea Kleruu aliyedhani Mwamwindi angetoka nje kwa kupitia mlangoni.
Basi, Mwamwindi akamlenga Mkuu wa Mkoa sawa kichwani. Dr kleruu alinyosha mikono juu na kuomba asemehewe. Mwamwindi alikaa kimya. Kisha akafyatua risasi. Kishindo kilisikika kijijini. Baada ya hapo, kwa mikono yake, Mwamwindi akaubeba mwili wa Mkuu wa Mkoa na kuuweka nyuma ya boneti ya gari alilojia mkuu huyo wa mkoa.

Mwamwindi alichukua kofia ya pama aliyovaa Kleruu. Akaivaa kichwani na kuanza kuendesha gari hilo hadi kituo cha polisi Iringa. Waliokutana na Mwamwindi njiani walimshangaa akiendesha gari hilo la Mkuu wa Mkoa akiwa amevalia kofia ya mkuu huyo. Hatimaye Mwamwindi akafika kituo cha Polisi.

Akatoka na kwenda mapokezi. Hapo akaripoti tukio kwa kutamka; " Nendeni mkamchukue mbwa wenu nyuma ya gari!".

Tukio lile bado linatuachia maswali? Je, ni kwanini Dr Kleruu alikwenda nyumbani kwa Mwamwindi siku ya Jumapili na hususan siku ya Krismasi?

Je, yawezekana Mwamwindi na Dr Kleruu walikuwa na ugomvi mwingine kabla ya tukio?

Kuna waliokuwepo na wanasimulia kana kwamba ilikuwa ni jana tu. Mmoja wa watu hao ni mwana wa Mkulima Said Mwamwindi aitwaye Amani Mwamwindi ambaye ndiye Meya wa Manispaa ya Iringa kwa sasa. Amani Mwamwindi anakumbuka nini juu ya siku hiyo?

hi wana JF,
Nimewasili jana jioni toka shamba kwenye shughuri zangu za kujitafutia Riziki, njiani nilinunua Gazeti la Mwananchi. Duh, lina bonge la Makala isomekayo MKULIMA ALIYEMPIGA RISASI,KUMUUA RC KLERUU. Kwa wale wanaopenda kufahamu Histori ya Nchi hii, nawashauri Mtafute gazeti la Mwananchi la tangu Juzi (tar. 20 June, 2016) ili muweze kufahamu ujasiri wa Mzee Mamwindi.

Nawatakia usomaji mwema.

View attachment 358893View attachment 358894


Habari nyingine inayohusiana na habari hii fuatilia
- Binti wa Dkt. Wilbert Kleruu atoa ya moyoni

Viongozi na Wanasiasa wengine waliowahi kukumbana na matukio ya kupigwa riasasi
- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

- Simulizi: Kisa na Mkasa wa Mauaji ya Jenerali Imran Kombe (Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa-TISS)

- Kifo chenye utata cha Waziri Nicas Mahinda

- John Mwankenja auawa kwa risasi

- Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania

- TANZIA - Waziri Salome Mbatia afariki dunia, maswali yaibuka!

- Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA

- Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ashambuliwa kwa risasi na Watu wasiojulikana

- Askari polisi aliyepigwa risasi na majambazi Tanga afariki
 
Kaka gm,Naona ingekuwa busara kama post hii ungeulizia kule kwenye Thread ya Field Marshall ES inayohusu Historia,kuna Waheshimiwa kule wana kumbukumbu nzuri wangekupa mengi kuhusu huyu Mzee Kreluu.Lakini kwa kifupi tu,na kwa ufahamu wangu,nitakupa maelezo yafuatayo kuhusu Mzee Kreluu.

Dr Kleruu alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa,Aliuawa siku ya Krismas mwaka 1971.Kifo chake kilizungukwa na utata mkubwa,na kilimtia simanzi nyingi Marehemu Julius Kambarage Nyerere ( Rais wa Jamhuri) ambaye pamoja na Mzee Kawawa (Waziri Mkuu),Dr Kleruu alikuwa rafiki yao mkubwa. Msiba wa Dr Kleruu uliisikitisha Nchi nzima...kwa sababu alikufa kwa kupigwa risasi na mtu maarufu huko Iringa aliyejulikana kwa jina la Alhaj Abdallah Mwamwindi.

Kisa cha mauaji ya Dr Kleruu hakipo wazi;Serikali ilitoa tamko kuwa Alhaji Mwamwindi alikataa Amri ya serikali ya kuhamia kwenye vijiji vya Ujamaa kwa madai kuwa eneo alilokuwa anaishi lina makaburi na shamba alilorithi,na kwa mila ya huko (Iringa) huwezi kuishi mbali na makaburi ya ndugu zako.Serikali kwa kutumia vyombo vya dola (Polisi) wakatumia nguvu kumuhamisha Alhaji Mwamwindi,hiyo ilimchukiza Mwamwindi na kuishia kumpiga risasi Mkuu wa Mkoa......maelezo hayako wazi kama Dr Kleruu alikuwepo kwenye tukio siku ya Kumuhamisha Mwamwindi na ukizingatia kuwa mauaji yalitokea siku ya Krismas (siku ya mapumziko).

Kuna Taarifa nyingine ambayo ilikuwa inasema kuwa,kulikuwa kuna chuki,kati ya Mfanyabiashara Mwamwindi na Mkuu wa Mkoa Dr Kleruu,na Mkuu wa Mkoa akaichukulia Amri ya serikali ili kumkomoa Mwamwindi. Mfanyabiashara huyo akamvizia Mkuu wa Mkoa ambaye alikuwa anatoka na mkewe mdogo...alimpiga risasi na kuipeleka maiti ya Mkuu wa Mkoa kituo cha Polisi Iringa mjini.....na kwa dharau akawaambia Polisi "kamchukueni mbwa wenu kwenye buti la gari yangu"......baada ya kuichukua hiyo maiti ya Mkuu wao wa kazi Polisi walimtia kizuizini Alhaj Mwamwindi,alihukumiwa kifo na alinyongwa.

Kwa mtazamo wangu sikuuona uwanamapinduzi wa Dr Kleruu,labda ni usimamizi imara wa Azimio la Vijiji vya ujamaa.Mkuu gm hiyo ndio historia fupi ya Marehemu Dr Kleruu....ni wazi utapata maelezo zaidi kwa wanaolifahamu hilo.
 
Jf imekuwa ni mahali pa kupashana habari na kuweza pia kuzungumzia mambo ya historia yetu na mwelekeo wa nchi. Kuna Huyu bwana anajulikana kama marehemu Dr Kleruu, mie nimekuwa nikimsikia katika wimbo wa Mbaraka Mwinshehe kuwa alikuwa mwanamapinduzi, Je kuna yeyote anaweza kutupatia taarifa kumhususu huyu Dr Kleruu alikuwa nani hasa na uana mapainduzi wake ulikuwa vipi katika historia na siasa za Tanzania?
Dr Wilbert Kleruu alikuwa mzaliwa wa mkoa wa Kilimanjaro sehemu iitwayo Mamba (au Mwika), Moshi vijijini ambako siku hizi kunaitwa Vunjo. Alisomea uchumi wa kijamaa hadi ngazi ya PhD, na hasa alikuwa agricultural economist.

Alifanya kazi kwa karibu sana na Mwl Nyerere ambaye alimpenda sana, maana alimwona ni muumini wa siasa yake ya ujamaa na kujitegemea. Alijituma na kuiamini kwa moyo wake itikadi hiyo, kwamba ukombozi wa nchi utapatikana kwa mapinduzi ya kilimo cha kijamaa (ndio uanamapinduzi anaozungumziwa).

Alijitahidi pia kutekeleza itikadi hiyo kwa vitendo, na ndiyo iliyomgharimu maisha yake mwaka 1971 alipokuwa mkuu wa mkoa wa Iringa. Siku moja ya jumapili (hakuwa na jumapili huyu mjamaa) alikwenda kwenye shamba la mkulima mmoja aliyeitwa Saidi Mwamwindi, ambaye alikuwa na shamba kubwa sana, kwa lengo la kufuatilia maagizo yake aliyokuwa ametoa kuhusu shamba hilo, ndipo alipokorofishana na mkulima huyo maana yeye hakuzikubali hata kidogo hizo sera za kijamaa. Mwamwindi alikwenda nyumbani kwake akachukua gobore lake, akamfuata Dr Kleruu alipokuwa akampiga risasi na kumwua, kisha akapakia mwili wake kwenye Land Rover yake (pick up short chassis) na kupeleka kwenye kituo cha polisi ambako pia alijisalimisha.

Nyerere alihuzunishwa sana na kifo hicho, na hata kesi ya Saidi Mwamwindi ilipoisha na kupewa hukumu ya kifo, Nyerere hakusita kusaini, na ni mojawapo ya hukumu tatu tu za kifo zilizotekelezwa wakati wa utawala wa Mwl Nyerere.

Wengine wataongezea, lakini kama hapo ulipo unaweza kupata vitabu, tafuta kitabu kiitwacho "The Egalitarian Moment: Asia and Africa 1950-1980" kilichoandikwa na Donald Anthony Low (1995), habari hii ya Dr Kleruu iko kwenye ukurasa wa 52-53, kwenye chapter yenye heading "Richer Peasants and the State".

Unaweza pia kusoma journal article iliyoandikwa na Phillip Raikes mwaka 1979: Agrarian Crisis and Economical Liberalisation in Tanzania kwenye jarida la Journal of Modern African Studies Vol 17(no.2) pg 309-316, ambayo nimejaribu kukuwekea link yake hapa chini. Kifo cha Dr Kleruu kiliwahuzunisha watu wengi hasa wakulima wadogowadogo wa huko Iringa ambao walikuwa wakifurahia alivyokuwa ananyang'anya mashamba kwa wakulima wakubwa ili yalimwe kijamaa. Pia alikuwa ana tabia ya kuwafokea watumishi wa serikali hata wakurugenzi kwenye mikutano ya hadhara, pale alipoona sera zake za kijamaa hazijafuatwa kama alivyotaka, yaani alikuwa na ule ujamaa wa kibabe hasa uliokuwa Urusi (ajabu ni kwamba huyu alisomea Marekani!). Kwa namna fulani (ama kiasi kikubwa) alikuwa na 'ukali' kama ule wa Marehemu Sokoine. Raikes (1979) anaandika hivi kuhusu kifo cha Dr Kleruu kwenye rejea niliyotaja:

"...the emergence of the assassin of the Regional Commissioner as a 'folk hero', seems to me a misreading. Dr Wilbert Kleruu had achieved a certain local popularity largely because of his habit of abusing civil servants in public. His expro- priation of the 'rich' peasants also seems to have been quite popular, especially of course with those who received the land. As for the various stories which went the rounds in the aftermath of the murder, I can only go by second hand gossip...." (uk 315).
Anaendelea:

"The point stressed was that Mwinyi killed Kleruu for calling him a dog (said to be an unallowable insult among the Hehe) in front of his wife (which made it the more unforgivable). In short, it was seen by Mwinyi as a means to preserve his honour, and this would help to explain why he gave himself up immediately" (uk 316). Mwamwindi alijulikana pia kama "Mwinyi" kwa maana ya "Lord"
 
Kuna siku nilisafiri na mmoja wa wakwe wa huyu Alhaj Abdallah Mwamwindi, hadithi aliyonipa ni kwamba Dr Kleruu siku hiyo ya Christmas alienda shambani kwa Mwamwindi na siku hiyo Mwamwindi alikuwa akilima. Alifika akapaki gari lake uwanjani katika nyumba ya Mwamwindi akamuita Mwamwindi ambaye alikuwa shambani mbali kidogo na pale alipopaki gari.

Mwamwindi alipofika mkuu wa mkoa akamuuliza kwanini hataki kuahama na kwanini alikuwa analima siku kuu. Mkuu wa Mkoa alipiga kofi Mwamwindi mbele ya wake zake. Mwamwindi akasema unanipiga kofi mbele ya wake zangu. Akaingia ndani akachukua shortgun na kumpiga mkono wa kulia. Mkuu wa Mkoa akasema nimalize kwa sababu umenikata mkono sina sababu ya kuishi.

Ndipo Mwamwindia akammalizia akapakia kwenye buti ya gari na kupeleka polisi. Alipofika pale Polisi walijua ni Mkuu wa Mkoa wakajipanga na kupiga salute kisha Mwamwindi akateremka katika gari ile na kuwaendea pilosi akawaambia kachukueni nguruwe wenu kwenye gari.
 
Bubu Msemaovyo,

Jina lake sio Abdallah, ni Saidi. Mwaka 2004 nilikwenda Iringa kwa shughuli zangu na nilibahatika kukutana na meya wa manispaa wakati ule, Amani Saidi Mwamwindi ambaye ni mtoto wa huyo mzee. Sijawahi kumhoji huyo mstahiki meya kuhusu baba yake, lakini kama ulivyoona kwenye article niliyotoa kwenye post yangu hapo juu, yalisemwa mengi sana kuhusu mazingira ya kifo cha Dr Kleruu.

Hata hivyo Mwamwindi alijisalimisha polisi na alimwaga ukweli wote mahakamani wakati wa kesi yake, na utetezi wake mkubwa ulikuwa kwamba alipatwa na hasira kali akashindwa kujizuia. Lakini ukisoma kesi yake kama ilivyoripotiwa kwenye Law Reports, Jaji alikataa kigezo cha hasira kwa maelezo kuwa mshitakiwa alipata nafasi ya kwenda nyumbani kuchukua gobole, na kurudi kumuua marehemu, kwa hiyo malicious intent ilikuwako na si hasira peke yake (najua kuna wanasheria humu wanaweza kutuongezea).
 
Kuhani,

Unajua si wakati wote ushahidi wa daktari unachukuliwa uzito, inategemea anavyoutetea mahakamani. Katika ile kesi maarufu ya fundi cherehani Ali Maumba aliyelawiti watoto wengi Dar miaka ya 1986-7(nadhani, sikumbuki mwaka kwa usahihi), watoto wale waliolawitiwa walipelekwa hospitali ya Muhimbili kupimwa, na daktari alithibitisha kuwa walilawitiwa, lakini ushahidi wake mahakamani ulitupiliwa mbali wakati wa rufaa, alishindwa kuutetea ule ushahidi ukaonekana hauna uzito. Ninavyofahamu ushahidi wa kutokuwa na akili timamu unaweza kumfaa mtu iwapo itathibitishwa kuwa wakati wa tendo husika hakuwa na akili timamu. Hilo sidhani kama Dr Pendaeli aliweza kulithibitisha na kulitetea mahakamani, pengine mawakili wa Jamhuri walimshinda kwa hoja.

BTW wakati baba yangu akifanya kazi Mamlaka ya Kahawa kule Moshi mid 70's to mid 80's (sisi pia tuliishi Moshi wakati huo), huyu Dr W.S. Pendaeli alikuwa na kliniki yake kwenye ground floor ya jengo la KNCU (ile yenye KNCU hotel), ilikuwa ya private na general (sio psychiatry), ingawa mwenyewe alikuwa psychiatrist. Ndipo tulipokuwa tunaenda kutibiwa (kukwepa foleni Mawenzi maana kule dawa zilikuwa za bure, lakini foleni yake ndio ilikuwa balaa!).

Basi ilikuwa babu ukimkuta na akijua unasoma sekondari basi anakusemesha kiingereza. Natamani kujua aliko huyu mzee, alini-influence sana na kile kiingereza chake miaka ile.
 
Mwawado,

Mwawando,

Shukrani sana kwa maelezo na historia ya Dr Kleruu, at least umetoa mwanga hasa wa huyu Dr. kwa watu ambao hatukuwa tunamfahamu kabisa.

Thanks
 
Nakupa kidogo na wengine watachangia. Dr Wilbert Kleruu alikuwa mzaliwa wa mkoa wa Kilimanjaro sehemu iitwayo Mamba (au Mwika), Moshi vijijini ambako siku hizi kunaitwa Vunjo. Alisomea uchumi wa kijamaa hadi ngazi ya PhD, na hasa alikuwa agricultural economist.

Kithuku,

Maelezo mazuri sana na nashukuru pia kwa PDF na maelezo mengine ambayo yanatoka katika journal. Thanks
 
Alikuwa daktari wa nini huyu Kleruu? Alikuwa kabila gani?

Nyani McCain,

Sina uhakika alikuwa kabila gani lakini kwa maelezo ya Kithuku ni kuwa alikuwa mzaliwa wa Kilimanjaro na alikuwa daktari wa uchumi.

Originally Posted by Kithuku
Nakupa kidogo na wengine watachangia. Dr Wilbert Kleruu alikuwa mzaliwa wa mkoa wa Kilimanjaro sehemu iitwayo Mamba (au Mwika), Moshi vijijini ambako siku hizi kunaitwa Vunjo. Alisomea uchumi wa kijamaa hadi ngazi ya PhD, na hasa alikuwa agricultural economist. Alifanya kazi kwa karibu sana na Mwl Nyerere ambaye alimpenda sana, maana alimwona ni muumini wa siasa yake ya ujamaa na kujitegemea.
 
kleruu alikuwa pia na binti tulikaa naye mitaa ya daimond jubilee,upanga nakumbuka tulikuwa tunamwita mama twambi,unfortunately binti wa huyu mama,TWAMBI,perished in the fire iliyotokea katika boarding school kilimanjaro some years ago
 
Taarifa zingine zinasema kuwa Kleruu alimkuta Mwamwindi akilima shamba lake na Trekta lake Isimani siku ya 25/12/1971.Alipomkuta akamuuliza kwa nini analima kwenye shamba lake na siyo kwenye shamba la kijiji cha ujamaa?

Mwamwindi akajibu kuwa kuna tatizo gani kwani siku hiyo ilikuwa ni sikukuu hivyo hakuwa na sababu ya kuwa kwenye shamba la kijiji cha ujamaa kulima kwani watu walikuwa nyumbani wakisherehekea sikukuu.

Taarifa zinasema kuwa Mkuu wa mkoa akakasirika akamtukana Mwamwindi akamwambia “KUMAMAYO”.Alipotukanwa tusi hilo Mwamwindi akaja juu akamwambia utanitukanaje KUMAMAYO wakati mama yangu alishakufa siku nyingi na kaburi lake lile pale ? Akalionyesha kwa Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa mkoa Kleruu akazidi kukasirika akasema kaburi ndio nini? akaenda juu ya kaburi na kuanza kupiga mateke lile kaburi.(Hakujua kuwa wahehe kimila huwezi kumtukania mzazi aliyekufa na huwezi chezea kaburi la marehemu sababu makaburi kwa wahehe ni maeneo matakatifu na huyajengea na kuyaenzi na kuyatumia kwa ibada za matambiko.)

Baada ya Kleruu kupiga mateke kaburi alimwona Mwamwindi anakimbia mbio kwenda nyumbani kwake.Kleruu alipoona anakimbia akaanza kumfukuza nyuma akijua anamkimbia. Hakujua mila za wahehe wenye hasira kuwa ukigombana naye hutakiwi umfukuze ila ukimbie haraka sababu huko aendako anaenda kuita watu wakutandike au anaenda kufuata silaha au anaenda kujinyonga kwa hasira.

Kleruu akawa anamfukuza kuelekea nyumbani kwa Mwamwindi .Mheshimiwa Kleruu hakujua mila ingine ya wahehe isemayo kuwa mhehe huwa “hapigwi nyumbani kwake na yuko tayari kujiua au kuua mtu kuliko kupigwa nyumbani mbele ya mke,watoto au dada zake”.Kitendo cha Kleruu kumfuata mhehe yule akampige nyumbani kilikuwa hatarishi kwa Kleruu.

Basi alipofika nyumbani Mwamwindi akaingia ndani akachukua bunduki akawa anatoka nayo mbio akamtandika Risasi Kleruu aliyekuwa anakuja nyumbani kwa Mwamwindi kisha akapakia maiti kwenye gari ya mkuu wa mkoa na kuipeleka Iringa mjini kituo cha polisi ambako hata polisi walishikwa butwaa maana hawakujua ilikuwaje mkuu wa mkoa atoke peke yake kiziara ya kikazi bila wao kutaarifiwa hadi auawe huko.Ilikuwa kizaazaa.Hawakujua maskini polisi,usalama wa taifa n.k watajieleza nini kwa Raisi Julius Nyerere.

Kwa wahehe Mwamwindi anaheshimika kama shujaa na mtetezi wa makaburi na marehemu wa wahehe ndiyo maana alikuwa na ujasiri wa ajabu hata kujipeleka mwenyewe polisi akijua kuwa kitendo chake kimila kilikuwa sahihi kabisa.Pia ukichukulia kuwa siku hiyo ilikuwa sikukuu ambayo Kleruu kama mchaga alitakiwa awe Moshi akila Krismasi na wachaga wenzie badala ya kwenda kuchokoza wahehe vijijini ambao hawana cha kula Krismasi.

Wahehe hawana kinyongo na familia yake ndiyo maana waliweza kumchagua hata mwanae kuwa meya wa manispaa ya Iringa na wanaona fahari kuwa na meya mtoto wa mwamwindi.

Kleruu kama Mkuu wa Mkoa alienda na gari ya serikali akijiendesha mwenyewe na hakuwa na mlinzi kitu ambacho pia hakikuwa sahihi katika matumizi ya mali za umma.Na ki-protokali ziara za mkuu wa mkoa ilibidi serikali ya tarafa,kata na kijiji wataarifiwe ujio wake lakini hawakutaarifiwa.Aliingia tu yeye kama yeye! Ndio maana hata Mwamwindi alimwona kama mhuni aliyekuja kumfuata kwa visa vyake anavyojua yeye.

Pia ingalikuwa ni ziara ya kiserikali huko kijijini angeambatana na viongozi wa wilaya polisi,n.k Hakufanya hivyo. Ningekuwa jaji nadhani nisingemnyonga Mwamwindi hadi nipate majibu ya kueleweka.

Kesi ya Mwamwindi ni moja ya kesi ambazo wanasheria wanapaswa kuzipitia upya hukumu zake kuona kama alitendewa haki kunyongwa na pia ni fundisho kwa wataalamu wa saikolojia za kisheria na kivita na uendeshaji wa utawala bora.
 
Du inaonekana hii issue inachanganya kidogo, kwa mtizamo wa haraka haraka unaweza kusema kuwa Mwamwindi ndiye alikuwa mwana mapinduzi hapa lakini ukiangalia pia issue ya mada sina uhakika wana sheria watasemaje, ni dhahiri kuwa hata kama angekuwa ameuwa kwa kutokukusudia mwelekeo wa siasa wa kipindi hicho kwa vyevyote ungemhukumu tu kwa kumuondoa mkuu wa Mkoa ( I am only speculating though).

Pia ukifuatilia hizi post za wana JF waliochangia na kutoa maelezo ya huyu Dr Kleruu, kwa upande mwingine inaonekana kama hasa alikuwa mkereketwa wa ujamaa au alikuwa anatumia madaraka yake vibaya. Nafikiri angeweza kuwa na compromising solution ya kudeal na watu ambao walikuwa na mashamba makubwa zaidi ya hivo alivofanya kama maelezo ya Kithuku yanavyosema hapa:

Kifo cha Dr Kleruu kiliwahuzunisha watu wengi hasa wakulima wadogowadogo wa huko Iringa ambao walikuwa wakifurahia alivyokuwa ananyang'anya mashamba kwa wakulima wakubwa ili yalimwe kijamaa. Pia alikuwa ana tabia ya kuwafokea watumishi wa serikali hata wakurugenzi kwenye mikutano ya hadhara, pale alipoona sera zake za kijamaa hazijafuatwa kama alivyotaka, yaani alikuwa na ule ujamaa wa kibabe hasa uliokuwa Urusi (ajabu ni kwamba huyu alisomea Marekani!). Kwa namna fulani (ama kiasi kikubwa) alikuwa na 'ukali' kama ule wa Marehemu Sokoine.
 
Dr kleruu alikuwa mzaliwa wa mamba, na kaburi lake liko kando ya barabara inayoanzia himo-kilacha hadi mwika, niliona valuation report kwa ajili ya compensation ya watu wanaoathiriwa na ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami,kwenye jalada kabisa wameweka kaburi lake, kwani nalo linapaswa kuhamishwa, hivyo ni mchaga wa marangu
 
Kwa wahehe Mwamwindi anaheshimika kama shujaa na mtetezi wa makaburi na marehemu wa wahehe ndiyo maana alikuwa na ujasiri wa ajabu hata kujipeleka mwenyewe polisi akijua kuwa kitendo chake kimila kilikuwa sahihi kabisa.Pia ukichukulia kuwa siku hiyo ilikuwa sikukuu ambayo Kleruu kama mchaga alitakiwa awe Moshi akila Krismasi na wachaga wenzie badala ya kwenda kuchokoza wahehe vijijini ambao hawana cha kula Krismasi.

Netanyahu,

Shukrani kwa maelezo yako!

Je waweza fafanua kidogo unamaana gani unaposema "Mwamwindi anaheshimika kama shujaa na mtetezi wa makaburi na marehemu wa wahehe" Natanguliza shukrani.
 
..silaha inabidi zitumike kwa ajili ya kujihami tu.

..naamini siyo watoto wa Dr.Kleruu peke yao walioathirika[kisaikolojia,kiuchumi,..] kutokana na kifo cha mzee wao.

..watoto wa Alhaji Mwawindi nao lazima waliishi kwa taabu kutokana na matendo ya mzee wao.

..kwa wale ambao tuna familia, kabla ya kuchukua uamuzi wowote mkubwa, hujiuliza uamuzi huo utakuwa na athari gani kwa wanetu.
 
Hivi nani anaweza kutoa maelezo sahihi "Ni kwa nini Mwalimu alitia saini kifo cha Mwamwindi, wakati ripoti ya Madaktari wakiongozwa na Dr.Pendaeli waliithibitishia Mahakama kwamba Mtuhumiwa alikuwa na Ugonjwa wa Akili?".

Alhaj Mwamwindi aliua Desemba/1971 na mapema June/1972 kesi ilikuwa imekwishamalizika...Ni vipi kesi hii ya mauaji iliyohitaji uchunguzi wa muda mrefu iliendeshwa kihara haraka namna hiyo?Ni kweli kwamba Mwalimu alitia saini adhabu ya kifo kwa sababu tu kifo kilimuhusu rafiki yake?Mbona alikawia na hatimaye kumuacha huru Mama Liundi ambaye aliuawa watoto wake wawili kwa kuwatilia sumu kwenye chakula?(wakati hukumu ya mahakama ilikuwa ni adhabu ya kifo?)..

Kama mtakumbuka Mwalimu alikataa kuonana na watu kutoka England ambao walifuatilia kesi ya Mwamwindi....Mwl aliwaambia anafikiri waondoke tu...kwa sababu walikuja mwezi April/1972 siku ambayo karume nae alipigwa risasi Zanzibar....mara baada ya mazishi ya Karume Mwalimu alirudi Butiama kwa siku 7 na kusema wazi kwa kiingereza kwamba inabidi afanye "re-evaluation ya behaviour yake".Ni kwa nini alisema maneno hayo? unafikiri hiyo iliharakisha kusaini kifo cha Mwamwindi? au aliona yaliyomtokea Karume yanaweza kutokea kwake pia?Wakulu mnaolifahamu hili tunaliombea maelezo...
 
Nadhani katika kusaini hukumu ile Mwl Nyerere alikuwa katika capacities mbili: Ya kwanza kama Rais wa nchi ambaye sheria inasema ndiye atakayeridhia utekelezwaji wa hukumu ya kifo inapotamkwa na mahakama, lakini ya pili ni capacity ya kibinadamu ya kutaka kumlipia rafikiye kisasi, ambayo hii inaelekea ilimzidi. Imagine katika miaka 23 ya uongozi wake, ni watu wengi sana walihukumiwa adhabu za kifo, lakini aliridhia 3 tu, mojawapo ikiwa hii ya Mwamwindi.

Labda zingeletwa na hizo hukumu nyingine alizosamehe tukaona hazikumgusa binafsi naweza kufuta maneno yangu, lakini nahisi kutekelezwa kwa hukumu hii haraka haraka kulichangiwa pia na ukweli kwamba kosa lililotendwa lilimuumiza Nyerere binafsi. Hivi kwa mfano ukipigana na mtu mtaani ukamuumiza halafu ukakamatwa ukashitakiwa mahakamani, na huko ukakuta hakimu ni baba mzazi wa mlalamikaji, unatarajia nini? Sisemi ilikuwa sawa Nyerere kuendeshwa na hisia binafsi, lakini tunapaswa kuangalia pia namna ya kudhibiti hali kama hii.

Katika mahakama zetu kuna utaratibu (sijui kama umeandikwa au la) kuwa hakimu akiona kesi husika ana maslahi nayo, huwa anajitoa na kuomba ipangiwe hakimu mwingine. Kwa rais wa nchi hali ikoje? Hivi mtu akihukumiwa kunyongwa kutokana na kutenda jambo ambalo liligusa maslahi binafsi ya rais (rafiki yake, familia yake nk), rais anaweza kusema kuwa 'anajitoa' katika suala la kuridhia utekelezwaji wa hukumu hiyo?
 
Back
Top Bottom