Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Madactari, Dr. Ulimboka anaendelea vizuri. Inasemekana Madactari wameendelea kupokea vitisho kwa njia ya sms. Mgaya (Katibu TUCTA) amesema wapo kwenye mchakato wa kuliwasilisha jambo hilo kwenye shirika la kazi Duniani (ILO)
Mungu amsaidie apone haraka. Mengineyo haki itatendeka hata ikiwa miaka mbele watajulikana, kina Kombe walifanyiwa mchezo kama huu..tumwombee Mungu apone.
Asante kamanda Isack kwa kutuhabarisha kupitia picha safi sana na asante mungu, majaribu ya mungu ni mengi hata yesu aliuawa wakati alikuja kuwakomboa wanadamu
Nimesikia kuwa kesho itabidi afanyiwe operation ya taya, ambalo limeharibiwa vibaya ! Nilichopenda ni kuwa ma Dr. wamechachamaa na wanafanya ulinzi wao wenyewe, na hata askari waliotaka kuingia ndani ya chumba leo wakati Dhaifu anakaribia kwenda wametolewa benzi, huyu wamesema watamlinda wenyewe na hawataki hawa "wajambazi" walete sumu zao wala kumkaribia !
Safi sana hii na kaza buti wasomi nyie mpaka kieleweke !! Vasko Da Gama safari hii lazima atolewe nishai na wajaza mabakuli !
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.