Dr. Slaa, wewe unanisaidiaje ktk matatizo haya yanayonipata mwanachama wako?

Mikael Aweda

JF-Expert Member
Dec 17, 2010
2,973
3,901
Nimeanza kazi ya kuajiriwa miaka 7 iliyopita. Jana jioni nikakwama kwenye foleni masaa mengi sana nikafika nyumbani saa 3 usiku. nikaanza kuwaza mgawanyo wa masaa yangu baada ya kukaa kwenye foleni. Nikaanza kutafakari kama ifuatavyo:

MUDA NILIOKA NJIANI.
Kwa siku napoteza masaa 4; Asubuhi 2 na jioni 2. Hii inatokana na foleni. Kama siyo foleni nisingetumia muda huo. Siku 6 za wiki natumia masaa hayo kwenda kazin na kurudi, kwa kuwa nafanya hadi jumamosi. Ni jumapili tu ndo siendi kazini.

Kwa hiyo, Ktk siku 30 nafanya kazi siku 26 za mwezi ( toa jumapili tu). Hivyo, masaa 4 kwa siku * 26 siku za mwezi ni sawa masaa 104 kwa mwezi zinapotea njiani.

Kwa mtazamo huo huo, Masaa 104 kwa mwezi ni sawa na masaa 1248 kwa mwaka.

Kwa mantiki hiyo, kwa miaka 7 niliyoajiriwa,muda niliokaa kwenye foleni ni swa na masaa 1248 (ya mwaka * miaka 7 = masaa 8736 kwa miaka 7.

Baada ya hapo nikataka kujua masaa haya 8736 ni miaka mingapi. Nikagundua kuwa masaa 8736 nikagawa kwa 24 (masaa kwa siku) ninapata siku 364. Mwaka una siku 365/366.

Hiyo ni kusema Dr Slaa nimekaa njiani (ndani ya daladala + gari binafsi) kwenda kazini au kurudi nyumbani muda wa mwaka moja kasoro siku moja ( 364). Je, una mawazo mapya ya kunisaidia?

MUDA NILITUMIA OFISI
Kwa siku nafanya kazi masaa 8 (Mara mbili ya muda niliokaa njiani) Kwa hiyo kwa mwezi natumia masaa 208 Ofisini (8 ya siku * siku 26 za mwezi toa jumapili). Kwa mwaka natumia masaa 2496 ofisini. Kwa miaka 7 nimetumia masaa 17,472 ofisini. Nikigawa kwa saa 24 ( idadi ya maasa kwa siku) ninapata siku 728 ambazo ni wastani wa miaka 2.

Kwa hiyo ndani miaka 7. Nimefanya kazi miaka 2 nimekaa njiani (dala dala au gari binafsi) mwaka 1 . Masaa yaliyobaki ni ya kulala, kupumpizika kazi nyinginezo ikiwepo kujenga Chadema nk.

Je, mgawanyo huu unaweza kunitoa ktk umaskini na kuniletea Maendeleo nikawa na malori na vituo vya mafuta Rizi1?. Mimi naona hapana ndio maana nihitaji ushauri wako.

Hoja yangu ni kuwa siwezi kukaa barabarani masaa manne (Mwaka1 ktk miaka 7) kila siku halafu nikategemea maendelea. Ninahitaji mawazo mapya ya kunitoa hapa. Dr Slaa unanishaurije?

Gharama.
Rafiki yangu anakaa Kibamba na anafanya kazi mjini. Anatumia Tsh 7,000 Kila siku kama gharama ya ziada ya foleni. Bila foleni angetumia 10,000 kwa gari yake ndogo. Lakini kutokana na foleni kwa siku anatumia 17,000/=

Ziada ya 7,000/= anayoingia rafiki yangu ni hasara ya Tsh ngapi ktk miaka 11 aliyofanya kazi? Je, WanaDar es Salaam wote wanapata hasara ya muda + pesa ya kiasi gani kwa siku, mwezi na mwaka?

Je,Dr Slaa ungenisaidiaje kama ungekuwa umeingia ikulu 2010? Na kama umechakachuliwa kura unanipa ushauri gani? Maana hata muda wa Kufanya kazi za Chadema niko bara barani.

Mawazo yangu tu yaliyonikuta kwenye foleni ya Jana.
 
Mikael, sijaelewa kwanini umeelekeza hili swali kwa Dr Slaa?
 
FJM,
Kwa sababu sina matumaini yo yote kwa jk na serikali yake. Sasa hata kama Dr hayupo ikulu nataka kujua mawazo yake. Na kama inawezekana tufanyie kazi hata kwa njia ya mikutano ya hadhara na hoja za wabunge wetu. Kama haiwezekani basi tuombe Mungu mpaka 2015 tutakapopata serikali mpya ambayo itaniondolea matatizo yangu. Nimechoka na foleni.
 
Swali zuri sana. Dr Slaa kama kiongozi wangu wa moyoni ningependa kuona ni kwa jinsi gani unaweza kuitoa nchi hii katika taabu hii.
 
hawa watu wa Daresalamu wanaosota kwenye foleni ndio hao kila siku wanaikumbatia ccm iweje leo dr Slaa akujibie? yeye alichosema ni kuwamkimchagua kikwete ni janga na mtajuta sasa hivi mnaanza kujuta munamuuliza uliza nini tena . mmelikoroga linyweni wenyewe , na wewe AWEDA
 
Na ifahamike kuwa nikikokotoa hasara inayotokana na muda tunaopoteza njiani sote tuanaofanya kazi ktk jiji la Dsm, Ni sawa na kujiingiza ktk umasikini usio na sababu kwa makusudi. Huku tunasherehekea miaka 50 ya uhuru kwa kutumia BIL karibu 70. Tafakari.
 
kwa hiyo kama wengine tuna majibu tubaki nayo kwa kua swali ni kwa Dokta Slaa? haya mkuu ngoja tumsubiri dokta
 
Hizo hesabu zako zimenichanganya sana, nimeingiza facts zangu kwenye hiyo equation yako nakugundua kwamba, mimi katika hiyo miaka saba nimefanya kazi miaka miwili na nusu, na nimepoteza barabarani mwaka mmoja na miezi tisa. Naendelea kufanya analysis kuona kama mimi ndio chanzo cha tatizo au La. I am real very shocked.
 
hawa watu wa Daresalamu wanaosota kwenye foleni ndio hao kila siku wanaikumbatia ccm iweje leo dr Slaa akujibie? yeye alichosema ni kuwamkimchagua kikwete ni janga na mtajuta sasa hivi mnaanza kujuta munamuuliza uliza nini tena . mmelikoroga linyweni wenyewe , na wewe AWEDA

Black Bat,
sijilaumu kwa sababu sijapigia kuraccm hata jimbo nililokuwa naliogoza kama mkiti wa Jimbo oct 2010 tuliiondoa ccm. Hata hivyo, nalinywa kwa sababu wanadsm wenzangu wameichagua ccm.
 
Black Bat,
sijilaumu kwa sababu sijapigia kuraccm hata jimbo nililokuwa naliogoza kama mkiti wa Jimbo oct 2010 tuliiondoa ccm. Hata hivyo, nalinywa kwa sababu wanadsm wenzangu wameichagua ccm.

natambaua sana mchango wako ..wengi wape walichokitaka wanakipata sasa hivi:glasses-nerdy:
 
Aweda, Dr na CDM hawakusanyi Kodi, elekeza swali hili kwa JJK na Magufuli, unless otherwise liwe swali la Jamvin, Dr, na tem mzima iko kwenye mazishi ya kamanda wetu BOB. so siyo issue kuelekeza kwa Dr.
 
Mkuu Michael,
Katika ukokotoaji wako umesahau kupigia hasara unayopata kwa kutumia gari katika barabara mbovu na zenye mashimo.
Ukipiga gharama ya spea na matengenezo unapata kwa mwaka unafanyia kazi gari yako badala ya maendeleo yako na familia yako.
 
Kwa nini suala lako usilielekeze kwa Waziri kivuli wa uchukuzi kutoka kambi rasmi ya upinzani Bungeni? Rais Dr Slaa ni mtu mkubwa sana.
 
Ideal nzuri ila hata dr akijibu hilo swali la kufirika majibu yake nayo yatakuwa ya kufikirika mi naona asijibu tuu!
 
Hawezi kukusaidia kwasababu akiingia ikulu hapo itabidi uongeze saa lingine la kusubiri msafara wake upite.

Mambo yatakuwa ni yale yale.
 
Kwanza wewe unahitajika kumsaidia Dr. Slaa kutoa elimu ya uraia kwa wananchi na kufungua matawi ya CHADEMA po pote ulipo.
 
Jibu ni rahisi mno,

Ondoa mabingwa wa statistics na analysis, all 50 years leading imitatively. Yametufanya watanzania tuonekane imbecile mbele ya mataifa mengine kwa ajili ya kuombaomba kila kukicha. Yanajisifia kujenga km 11,000 za barabara, ati ndio achievement ya kujisifia, 90% ya ujenzi huo ni mikopo na misaada watakayoilipa watoto zetu.

Miaka sita ya JK deni la taifa trilioni 13, akimaliza kipindi chake itakuwa balaa. Ondoa magamba nchi isonge mbele.
 
Aweda, Dr na CDM hawakusanyi Kodi, elekeza swali hili kwa JJK na Magufuli, unless otherwise liwe swali la Jamvin, Dr, na tem mzima iko kwenye mazishi ya kamanda wetu BOB. so siyo issue kuelekeza kwa Dr.

Dr Slaa anaweza kujibu au asijibu. Majibu yako na wengine ndo lengo la makala yangu. Ingewa personal kwa Dr Slaa ningempigia simu au kumtumia yeye binafsi. Mjadala unaendelea kwenye uzi huu ndio lengo lenyewe. Kufikirisha watu na kuwaamsha ili wajue kwa undani hasara ya foleni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom