Elections 2010 Dr slaa usiwaendekeze sana hao wachakachuaji wa kura

shilanona

Member
Oct 31, 2010
55
22
DR SLAA.:A S cry:
Naomba usiwaendekeze sana hao waliotuibia kura zetu halali na kujipachika ushindi kimabavu. Zungumza nao na uwasome machoni kama wana la maana la kukueleza ili kulisaidia taifa letu katika kudumisha demokrasia. Tunachosubiri ni tamko lako ili tuingie mitaani kupambana na serikali hii dhalimu. Kama utawaendekeza sana uchungu wa kuibiwa kura zetu utapoa kama mjane aliyefiwa na mmewe wiki sasa imepita. Kuahirisha mazungumzo na waandishi wa habari hapo kesho kumefanya maandamano yaliyokuwa yamepangwa kufanyika Washington DC leo Jumamosi yasifanyike kwa ufanisi na tumewaomba watanzania wenzetu waliopanga maandamano mjini London, Jumatano wiki ijayo, na kisha Geneva na Ottawa siku ya Alhamisi wasitishe maandamano hayo mpaka utakapotoa TAMKO RASMI:israel:
 
Back
Top Bottom