Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Imeandikwa na Fidelis Butahe na Salim Said
SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kuagiza mitambo ya kuzalisha umeme ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), iwashwe wadau mbalimbali wamepokea kwa hisia tofauti uamuzi huo huku, Dk Willibrod Slaa, akisema uamuzi huo hautasaidia kuondoa kero za umeme nchini.
Mitambo ya IPTL, ilisimama kuzalisha umeme baada ya kubainika kuwa ilikuwa ikiuza umeme wake kwa bei ya juu.
Wiki iliyopita Dk Slaa, alielezea kushangazwa kwake na hatua ya Rais Kikwete kuzungumza lolote kuhusu tatizo la umeme ambao makali yake yanazidi kuongezeka.
Lakini jana akizungumza na gazeti hili, Slaa alisema hatua hiyo ya rais haitasaidia na kusisitiza kuwa upungufu wa maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme unajulikana tangu mwaka 2005.
"Kipindi hiki chote alikuwa wapi, hebu tujiulize ni kiasi gani cha fedha ambacho Watanzania wamekikosa kutokana na kukosekana kwa umeme, Bunge liliiagiza serikali inunue mitambo ya IPTL lakini ilikataa hivi sasa ndio inaona umuhimu wake," alisema Dk Slaa.
Dk Slaa mbaye ni Katibu Mkuu wa Chadema, hatua kamwe hatua hiyo haitasaidia kutatua tatizo la muda mrefu la umeme hapa nchini na kwamba serikali inapaswa kutafuta suluhisho la kudumu badala ya utaratibu wa zima moto.
Katika agizo lake kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Rais Kikwete alitaka kuhakikisha kuwa umeme unapatikana haraka iwezekanavyo na kuitaka Wizara ya Nishati na Umeme, kwa kushirikiana na Tanesco, kusimamia masuala yote ya kiufundi.
Masuala hayo ni pamoja na upatikanaji haraka wa mafuta, ili umeme wa IPTL uanze kuzalishwa mara moja.
Hali kadhalika aliitaka Wizara ya Fedha na Uchumi, kuhakikisha kuwa inatafuta fedha za kuwezesha ununuzi wa mafuta na mahitaji mengine muhimu, ili umeme uweze kuzalishwa.
Rais pia aliiagiza Wizara ya Katiba na Sheria, kusimamia masuala ya kisheria kuhusu suala hilo.
Agizo hilo la Rais Kikwete limekuja siku kadhaa baada Dk Slaa, Zitto Kabwe na wafanyabiashara mbalimbali, kumuomba aingilie kati ili kulinusuru taifa katika maafa makubwa ya kiuchumi yanayosababishwa na tatizo la umeme.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Juma Duni Haji, alisema uamuzi huo ni ishara ya kwamba Rais Kikwete ameanza kutapatapa.
"Huu ni mwaka wa nne tunaimbiwa nyimbo za matatizo ya umeme lakini serikali ya Rais Kikwete imeshindwa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili" alisema Duni.
Alisema kitendo hichno ni cha aibu kubwa kwa serikali ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Kikwete.
"Miaka mitano inakaribia kumalizika sasa lakini serikali imeshindwa kutatua kero moja tu kwa wananchi ambayo ni umeme, tunapoteza mabilioni ya fedha kutokana na kukosekana kwa nishati ya umeme," alisema.
Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Samwel Ruhuza alisema kinachoiponza serikali ya awamu ya nne ni kutosikiliza ushauri wa wapinzani na wataalamu mbalimbali.
"Serikali imekuwa na tabia ya kupenda kutibu ugonjwa kuliko kutafuta kinga kwanza," alisema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Fordia, Bubelwa Kaiza, alisema hatua ya rais kuagiza mitambo ya IPTL kuwashwa ni jambo zuri kwa kuwa serikali ina mamlaka kisheria kufanya hivyo.
Kaiza ambaye ni mwanasheria alisema jambo hilo ni la dharura na kusisitiza kuwa rais lazima atakuwa ameshauriana na wanasheria wake.
"Rais kipindi chote alikuwa kimya ni wazi kuwa alikuwa akijadiliana na wasaidizi wake ili kuona jinsi ya kutatua tatizo hili, ni uamuzi mzuri kwa maslahi ya taifa, binafsi ninampongeza," alisema Kaiza.
Mitambo ya IPTL ina uwezo wa kuzalisha megawati 90 hadi 100 za umeme ambazo zinatosha kuziba pengo la megawati 80 katika Gridi ya Taifa na kumaliza mgawo unaolikabili taifa.
Mgawo wa umeme ulioanza wiki mbili zilizopita, umetokana na kuharibika kwa mtambo wa Songas UGT1 wenye uwezo wa kuzalisha megawati 20, mtambo mmoja wa Kihansi unaotoa megawati 60 na Hale uliokuwa unazalisha megawati nane.
SOURCE: MWANANCHI
SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kuagiza mitambo ya kuzalisha umeme ya Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), iwashwe wadau mbalimbali wamepokea kwa hisia tofauti uamuzi huo huku, Dk Willibrod Slaa, akisema uamuzi huo hautasaidia kuondoa kero za umeme nchini.
Mitambo ya IPTL, ilisimama kuzalisha umeme baada ya kubainika kuwa ilikuwa ikiuza umeme wake kwa bei ya juu.
Wiki iliyopita Dk Slaa, alielezea kushangazwa kwake na hatua ya Rais Kikwete kuzungumza lolote kuhusu tatizo la umeme ambao makali yake yanazidi kuongezeka.
Lakini jana akizungumza na gazeti hili, Slaa alisema hatua hiyo ya rais haitasaidia na kusisitiza kuwa upungufu wa maji katika mabwawa ya kuzalishia umeme unajulikana tangu mwaka 2005.
"Kipindi hiki chote alikuwa wapi, hebu tujiulize ni kiasi gani cha fedha ambacho Watanzania wamekikosa kutokana na kukosekana kwa umeme, Bunge liliiagiza serikali inunue mitambo ya IPTL lakini ilikataa hivi sasa ndio inaona umuhimu wake," alisema Dk Slaa.
Dk Slaa mbaye ni Katibu Mkuu wa Chadema, hatua kamwe hatua hiyo haitasaidia kutatua tatizo la muda mrefu la umeme hapa nchini na kwamba serikali inapaswa kutafuta suluhisho la kudumu badala ya utaratibu wa zima moto.
Katika agizo lake kupitia Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Rais Kikwete alitaka kuhakikisha kuwa umeme unapatikana haraka iwezekanavyo na kuitaka Wizara ya Nishati na Umeme, kwa kushirikiana na Tanesco, kusimamia masuala yote ya kiufundi.
Masuala hayo ni pamoja na upatikanaji haraka wa mafuta, ili umeme wa IPTL uanze kuzalishwa mara moja.
Hali kadhalika aliitaka Wizara ya Fedha na Uchumi, kuhakikisha kuwa inatafuta fedha za kuwezesha ununuzi wa mafuta na mahitaji mengine muhimu, ili umeme uweze kuzalishwa.
Rais pia aliiagiza Wizara ya Katiba na Sheria, kusimamia masuala ya kisheria kuhusu suala hilo.
Agizo hilo la Rais Kikwete limekuja siku kadhaa baada Dk Slaa, Zitto Kabwe na wafanyabiashara mbalimbali, kumuomba aingilie kati ili kulinusuru taifa katika maafa makubwa ya kiuchumi yanayosababishwa na tatizo la umeme.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Juma Duni Haji, alisema uamuzi huo ni ishara ya kwamba Rais Kikwete ameanza kutapatapa.
"Huu ni mwaka wa nne tunaimbiwa nyimbo za matatizo ya umeme lakini serikali ya Rais Kikwete imeshindwa kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili" alisema Duni.
Alisema kitendo hichno ni cha aibu kubwa kwa serikali ya awamu ya nne inayoongozwa na Rais Kikwete.
"Miaka mitano inakaribia kumalizika sasa lakini serikali imeshindwa kutatua kero moja tu kwa wananchi ambayo ni umeme, tunapoteza mabilioni ya fedha kutokana na kukosekana kwa nishati ya umeme," alisema.
Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Samwel Ruhuza alisema kinachoiponza serikali ya awamu ya nne ni kutosikiliza ushauri wa wapinzani na wataalamu mbalimbali.
"Serikali imekuwa na tabia ya kupenda kutibu ugonjwa kuliko kutafuta kinga kwanza," alisema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Fordia, Bubelwa Kaiza, alisema hatua ya rais kuagiza mitambo ya IPTL kuwashwa ni jambo zuri kwa kuwa serikali ina mamlaka kisheria kufanya hivyo.
Kaiza ambaye ni mwanasheria alisema jambo hilo ni la dharura na kusisitiza kuwa rais lazima atakuwa ameshauriana na wanasheria wake.
"Rais kipindi chote alikuwa kimya ni wazi kuwa alikuwa akijadiliana na wasaidizi wake ili kuona jinsi ya kutatua tatizo hili, ni uamuzi mzuri kwa maslahi ya taifa, binafsi ninampongeza," alisema Kaiza.
Mitambo ya IPTL ina uwezo wa kuzalisha megawati 90 hadi 100 za umeme ambazo zinatosha kuziba pengo la megawati 80 katika Gridi ya Taifa na kumaliza mgawo unaolikabili taifa.
Mgawo wa umeme ulioanza wiki mbili zilizopita, umetokana na kuharibika kwa mtambo wa Songas UGT1 wenye uwezo wa kuzalisha megawati 20, mtambo mmoja wa Kihansi unaotoa megawati 60 na Hale uliokuwa unazalisha megawati nane.
SOURCE: MWANANCHI