Tumaini Makene
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 2,642
- 6,070
Wakuu
Jana Jumanne, timu kadhaa zinazounda timu moja ya Operesheni Sangara-M4C ilikuwa inamalizia kiporo cha Mvomero, ambako kabla ya mapumziko ya siku mbili kwa ajili ya Siku Kuu ya Eid-El-Fitr, kata kadhaa zilibaki katika mashambulizi makali ya Jumamosi. Mashambuzi hayo yamemng'oa Amos Makalla kutoka huko Dar es Salaam kuja jimboni kusalimia wananchi! Anakumbuka shuka kumekucha...
Katika mikutano aliyofanya jana na timu yake, Dkt. Slaa alitoa more facts juu ya zile tuhuma nzito alizotoa juzi kwenye press conference kuwa CCM wamekuwa wakiingiza nchini silaha bila vibali wala kulipia leseni, kisha wanawapatia vijana wao wanaowekwa kwenye makambi mbalimbali (kama ile ya Ulemo, Iramba, Singida, wakati wa uchaguzi mdogo Igunga) ambayo hutumika kuandaa na kufundisha vijana kwa ajili ya kufanya utekaji, utesaji na hata kuua...
Katika hatua ya mbele zaidi, amesisitiza kuwa kama ambavyo hawajawahi kuchomoka katika mtego mwingine wowote ule hasa katika masuala ya ufisadi na kuhujumu maendeleo ya watu wa nchi hii, katika hili la kuingiza silaha nchini kwa nia ya kudhibiti CHADEMA na kudhuru viongozi wake (wapinzani wao wa kisiasa) "CCM hawatachomoka pia".
"Kwa hili pia CCM hawachomoki, wamo kwenye mtego wetu tena kwa mara nyingine, leo naanza kwa kutoa kidogo tu, wakiendelea kuja na maneno matupu nitatoa facts na nyaraka zingine zaidi, na sasa katika hatua hii suala hili linamhusu Kikwete akiwa kama Mwenyekiti wa CCM na Amiri Jeshi Mkuu, ndiye anayehusika na masuala haya, afanyie kazi suala hili ili Watanzania wapate majibu ya kina na ukweli.
"Wakati wa uchaguzi mdogo Igunga waliweka vijana kwenye makambi kama pale Ulemo, Iramba mkoani Singida, wakifundishwa mbinu za kuteka, kutesa na kuua, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya CCM kudhibiti wapinzani wao kisiasa, wakilenga CHADEMA na hasa kudhuru viongozi wake. Waliwapatia bunduki, mojawapo ni silaha iliyotengenezwa China, yenye uwezo wa kubeba risasi 8 kwenye magazine yenye namba J137, walikuwa nayo vijana hao kambini.
"Tunamtaka Kikwete, kama Amiri Jeshi Mkuu na pia akiwa Mwenyekiti wa CCM atuambie, silaha hii iliingiaje nchini na kwa nini ilikuwa mikononi mwa CCM, tutashusha nondo zaidi, kuendelea kuivua nguo CCM na mikakati ya kumaliza wananchi wa nchi hii wasiokuwa na hatia," alisema Dkt. Slaa katika vijiji mbalimbali vya Kata za Langali na Mlali, Mvomero, Morogoro.
Jana Jumanne, timu kadhaa zinazounda timu moja ya Operesheni Sangara-M4C ilikuwa inamalizia kiporo cha Mvomero, ambako kabla ya mapumziko ya siku mbili kwa ajili ya Siku Kuu ya Eid-El-Fitr, kata kadhaa zilibaki katika mashambulizi makali ya Jumamosi. Mashambuzi hayo yamemng'oa Amos Makalla kutoka huko Dar es Salaam kuja jimboni kusalimia wananchi! Anakumbuka shuka kumekucha...
Katika mikutano aliyofanya jana na timu yake, Dkt. Slaa alitoa more facts juu ya zile tuhuma nzito alizotoa juzi kwenye press conference kuwa CCM wamekuwa wakiingiza nchini silaha bila vibali wala kulipia leseni, kisha wanawapatia vijana wao wanaowekwa kwenye makambi mbalimbali (kama ile ya Ulemo, Iramba, Singida, wakati wa uchaguzi mdogo Igunga) ambayo hutumika kuandaa na kufundisha vijana kwa ajili ya kufanya utekaji, utesaji na hata kuua...
Katika hatua ya mbele zaidi, amesisitiza kuwa kama ambavyo hawajawahi kuchomoka katika mtego mwingine wowote ule hasa katika masuala ya ufisadi na kuhujumu maendeleo ya watu wa nchi hii, katika hili la kuingiza silaha nchini kwa nia ya kudhibiti CHADEMA na kudhuru viongozi wake (wapinzani wao wa kisiasa) "CCM hawatachomoka pia".
"Kwa hili pia CCM hawachomoki, wamo kwenye mtego wetu tena kwa mara nyingine, leo naanza kwa kutoa kidogo tu, wakiendelea kuja na maneno matupu nitatoa facts na nyaraka zingine zaidi, na sasa katika hatua hii suala hili linamhusu Kikwete akiwa kama Mwenyekiti wa CCM na Amiri Jeshi Mkuu, ndiye anayehusika na masuala haya, afanyie kazi suala hili ili Watanzania wapate majibu ya kina na ukweli.
"Wakati wa uchaguzi mdogo Igunga waliweka vijana kwenye makambi kama pale Ulemo, Iramba mkoani Singida, wakifundishwa mbinu za kuteka, kutesa na kuua, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya CCM kudhibiti wapinzani wao kisiasa, wakilenga CHADEMA na hasa kudhuru viongozi wake. Waliwapatia bunduki, mojawapo ni silaha iliyotengenezwa China, yenye uwezo wa kubeba risasi 8 kwenye magazine yenye namba J137, walikuwa nayo vijana hao kambini.
"Tunamtaka Kikwete, kama Amiri Jeshi Mkuu na pia akiwa Mwenyekiti wa CCM atuambie, silaha hii iliingiaje nchini na kwa nini ilikuwa mikononi mwa CCM, tutashusha nondo zaidi, kuendelea kuivua nguo CCM na mikakati ya kumaliza wananchi wa nchi hii wasiokuwa na hatia," alisema Dkt. Slaa katika vijiji mbalimbali vya Kata za Langali na Mlali, Mvomero, Morogoro.