Elections 2010 Dr Slaa ni Kiboko; Serikali yaamuru Bei za saruji, nondo zishushwe, sera za Chadema!

Not_Yet_Uhuru

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
1,304
431
SERIKALI YATEKELEZA KAULI ZA DR SLAA NA SERA ZA CHADEMA TAYARI!!

Serikali ya CCM wanakimbiana kutokana na Nguvu na ukweli wa Uwezo wa Dr Slaa, yaogopa kila kitu kinachosemwa katika Sera za CHADEMA. Sasa imefikia kujikanyaga hadi kuamuru waziri wake afanye jinsi ashushe bei za Saruji, nondo na bidhaa nyingine...Aibuu!



WanaJF, taarifa ya nipashe ipo chini hapa....

----------------------------------
NA GAZETI LA NIPASHE
20th October 10

Serikali: Bei za saruji, nondo zishushwe

Richard Makore


Serikali imeviagiza viwanda vya saruji na nondo nchini kuhakikisha vinapunguza bei ya bidhaa hizo kwa kuwa hakuna sababu yoyote ya msingi inayochangia zipande mara kwa mara.
Agizo hilo lilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara Viwanda, Biashara na Masoko, Joyce Mapunjo, alipozungumza na NIPASHE kuhusu upandaji holela wa bidhaa hizo.
Alisema uzalishaji wa saruji na nondo ni mkubwa lakini hajui kwanini wazalishaji hao wanazipandisha na kuwafanya wananchi wa kawaida kushindwa kuzinunua.
Aliahidi kufuatilia kwenye viwanda hivyo ili aelezwe sababu zinazowafanya wazidi kupandisha bidhaa zao kwa mauzo ya jumla na hivyo kuwafanya wauzaji wa rejareja nao kupandisha bei.
Bei ya nondo yenye milimita 10 yenye urefu wa futi 40 kwa sasa ni Sh.10,000 kutoka Sh. 8,000 milimita 12 Sh. 13,000 badala ya Sh. 12,000 na bei ya mfuko mmoja wa saruji hivi sasa ni Sh. 13,000 badala ya Sh. 12,000.
Na katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa Wakala wa Serikali Biashara na Leseni nchini (Brela), Esteriamo Mahingila, aliwataka wazalishaji na wakulma kujiwekea malengo ili kuhakikisha wanaziwekea nembo bidhaa zao zote wanazozalisha.
Mahingila alikuwa akizungumza na wadau mbalimbali wakiwemo wataalamu wa masuala ya hakimiliki duniani ambao wanahakikisha bidhaa zinakuwa na nembo na alama kabla ya kuuzwa.

------------------------------------
CCM TUNAWAARIFU UKWELI HUU! Subirini KIDOGO muone nchi inavyoongozwa kuanzia hapo baada ya kura hapo 31 Oct. Wananchi watafumbuka macho na gharama zitakuwa chini wafurahie maziwa na asali katika nchi yao. Mtasahaulika mara moja katika historia!!
 
Hata wakishusha cement hadi 8000/= hawachaguliwi na mtu!
Wakubali tu kuwa wanatoa harufu ya muozo, hatuwataki!
 
Mh! hili sijui,
Lakini si ajabu mbona mambo mengi tu ya Dr. Slaa huwa wanasema hivyo hivyo kuwa mwongo hayatekelezeki halafu wanafanya.
huko ni kutapatapa ili kuwahadaa wananchi, maana watapandisha kesho tu, na hao wapiga kura wake walie
 
Walisema watapeleka umeme Busanda waliposhinda hawakupeleka hatuwapi ushindi tutampa slaa kumbe inawezekana kumbe hata elimu bure tutaweza tunaomba wagombea wote wa Upinzani wawaeleze wananchi kwamba hiyo ni rushwa kutoka serikali kwenda kwa wanachi baada ya uchaguzi hakuna kitu kitattekelezwa
 
CCM kwa rushwa mbona kawaida yao, Lkini mwaka huu ushenzi wao imekula kwao,
Wamelikoroga, lazima walinywe
 
Serikali haitakiwi iagize viwanda inatakiwa utoe kodi kwenye hizo bidhaa automaticaly bei zitapunguza bila ya kutoa ushuru haiwezekani................
 
CCM kimebaki chama cha COPY and PASTE!! - Chadema ndiyo wanaongoza nchi hii - kila DR Slaa anachosema wanatekeleza na bado utasikia wanafuta ada zote za shule.

Wanakumbuka shuka kumeshakucha.
 
CCM kimebaki chama cha COPY and PASTE!! - Chadema ndiyo wanaongoza nchi hii - kila DR Slaa anachosema wanatekeleza na bado utasikia wanafuta ada zote za shule.

Wanakumbuka shuka kumeshakucha.

Mbona nimesikia nadhani leo asubuhi kwenye mapition ya magazeti kuwa CCM inatoa elimu bure tayari......Sikumbuki ni gazeti gani ila anayekumbuka anaweza kunisaidia.
 
Wanampigia Dr. Slaa kampeni hivyo. Watanzania watajua kumbe ilikwa inawezekana, lakini haikuwa hivyo mpaka Dr. Slaa alipotamka. Watanzania watajua kuwa mtetezi wao ni nani hasa!
 
hata wafanye vp haja sijisaidii n'go, ccm wakujisitiriiii kwa fweza za walipa kodi mmetuletea ukatiliii..
 
hata washushe mfuko wa cement ufike buku shi tano na bati mia 2 hawapati kura
 
Hivi vitu vinawezekana ni basi tu hawataki kukubali!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1
 
Mh! hili sijui,
Lakini si ajabu mbona mambo mengi tu ya Dr. Slaa huwa wanasema hivyo hivyo kuwa mwongo hayatekelezeki halafu wanafanya.
huko ni kutapatapa ili kuwahadaa wananchi, maana watapandisha kesho tu, na hao wapiga kura wake walie

Nakumbuka pia kwamba sisiemu waliiba sera ya CUF ya kufuta kodi ya maendeleo iliyokuwa ni mzigo kwa wananchi. Ilikuwa ni enzi zile Mramba akiwa waziri wa fedha. Sisiemu kwa copy and paste hawajambo!
 
Yuko wapi yule Kilaza Kamalaaaaa, nchi hii bwna bila mtulinga haiendi.
 
Back
Top Bottom