dos santos
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 256
- 128
Nilikuwa naangalia kipindi maalumu(kimeandaliwa na wizara ya habari) kilichokuwa kinarushwa katika televisheni,kilichokuwa kinaelezea tukio zima la maandamano ya wafauasi wa CHADEMA wakipambana na jeshi la polisi mjini Arusha.Ni picha ambazo sikuwahi kuziona katika chombo chochote cha habari,wakati wanaripoti tukio la ghasia za huko Arusha.
Nilistuka sana kwanini vyombo vyetu vya habari havikuonesha namna viongozi wa CHADEMA walivyokuwa wanawahamasisha wafuasi wao kuvamia kituo cha polisi kuwatoa baadhi ya viongozi waliokuwa wanashikiliwa na polisi.Aidha zilioneshwa picha za mkutanoni viongozi wa chadema walivyokuwa wakiwahamasisha wafuasi wao kufanya fujo eti kwa kuwa baadhi ya viongozi wao walikuwa wamekamatwa.
Alioneshwa Philemon Ndesamburo(mbunge-Moshi Mjini) akizungumza maneno na lugha ambayo haifanani na umri wake.Maneno yake yalijaa uchochezi,yalikosa chembe ya busara ya utu uzima aliokuwa nao.Maneno yake hayakuwa na adabu,hayakutofautiana na mtu aliyekuwa amepata kilevi.Ametia aibu, ametia kinyaa kwa watu wa umri wake na hata kwa familia yake.Ameonesha si mzee wa kupigiwa mfano mzuri katika maamuzi na maneno ya busara.Ni fursa kwa wazee wenzake kumkalisha chini na kumuelekeza namna ya kufikisha ujumbe au kudai haki kwa maneno yasio na matusi.
Pia katika mkutano huo alioneshwa wilbrod Slaa(Katibu Mkuu-CHADEMA).Huyu nae alionesha mfano mbaya wa Kiongozi.Hakuonesha umakini bali umahiri wa kuchochea.Alikuwa na hasira kupita maelezo.Pengine mmoja wa waliokamatwa ni HAWARA yake (first lady wa kuazima).Alionesha kana kwamba amani ya Tanzania ipo mikononi mwake.Ni kiasi cha yeye kuamua iwepo amani ama la.Alionesha ni kiongozi aliyejisahau na anayedanganyika na shangwe za wale wanaomsikiliza anapozungumza.Na hili limewaponza wanasiasa wengi wasio makini Tanzania.
Hakuonesha kama ni kiongozi makini pale linapotokea jambo zito lenye kuhitaji maamuzi ya busara.Hakupima uzito wa kuhamasisha wananchi kwenda kuvamia kituo cha polisi na matokeo yake.Huu ni udhaifu wa viongozi wetu,hutafakari baada ya kutenda.
Viongozi hawa wawili si mfano wa kuigwa hata kidogo,ni wa kulaaniwa na kukemewa na wapenda amani.Ni viongozi wenye kupenda kutimiza kiu na malengo yao hata kwa gharama ya damu za watanzania.Watanzania wenzangu, tuamke wanasiasa wasitumie damu zetu kwa maslahi yao.Mabadiliko yanawezekana si lazima kwa damu zetu.Tutahadhari sana na viongozi ambao hawana njia mbadala ya kufikia malengo yao ya kisiasa isipokuwa kwa kuchochea ghasia na vurugu.
Kiongozi mmoja mashuhuri sana na mwenye akili sana aliwausia watu wake kwamba, "UKITAKA KUFANYA JAMBO KWANZA ANGALIA MWISHO WAKE, LIKIWA LINA HERI BASI LIFANYE NA LIKIWA LINA SHARI BASI LIACHE"
Tuwe mbali na viongozi mahiri wa uchochezi na si makini wa maneno na maamuzi yao.Watanzania wenzangu tutafakari kabla ya kutenda na si kutenda kabla ya kutafakari.Mwenye macho haambiwi tazama.
Nawasilisha
Nilistuka sana kwanini vyombo vyetu vya habari havikuonesha namna viongozi wa CHADEMA walivyokuwa wanawahamasisha wafuasi wao kuvamia kituo cha polisi kuwatoa baadhi ya viongozi waliokuwa wanashikiliwa na polisi.Aidha zilioneshwa picha za mkutanoni viongozi wa chadema walivyokuwa wakiwahamasisha wafuasi wao kufanya fujo eti kwa kuwa baadhi ya viongozi wao walikuwa wamekamatwa.
Alioneshwa Philemon Ndesamburo(mbunge-Moshi Mjini) akizungumza maneno na lugha ambayo haifanani na umri wake.Maneno yake yalijaa uchochezi,yalikosa chembe ya busara ya utu uzima aliokuwa nao.Maneno yake hayakuwa na adabu,hayakutofautiana na mtu aliyekuwa amepata kilevi.Ametia aibu, ametia kinyaa kwa watu wa umri wake na hata kwa familia yake.Ameonesha si mzee wa kupigiwa mfano mzuri katika maamuzi na maneno ya busara.Ni fursa kwa wazee wenzake kumkalisha chini na kumuelekeza namna ya kufikisha ujumbe au kudai haki kwa maneno yasio na matusi.
Pia katika mkutano huo alioneshwa wilbrod Slaa(Katibu Mkuu-CHADEMA).Huyu nae alionesha mfano mbaya wa Kiongozi.Hakuonesha umakini bali umahiri wa kuchochea.Alikuwa na hasira kupita maelezo.Pengine mmoja wa waliokamatwa ni HAWARA yake (first lady wa kuazima).Alionesha kana kwamba amani ya Tanzania ipo mikononi mwake.Ni kiasi cha yeye kuamua iwepo amani ama la.Alionesha ni kiongozi aliyejisahau na anayedanganyika na shangwe za wale wanaomsikiliza anapozungumza.Na hili limewaponza wanasiasa wengi wasio makini Tanzania.
Hakuonesha kama ni kiongozi makini pale linapotokea jambo zito lenye kuhitaji maamuzi ya busara.Hakupima uzito wa kuhamasisha wananchi kwenda kuvamia kituo cha polisi na matokeo yake.Huu ni udhaifu wa viongozi wetu,hutafakari baada ya kutenda.
Viongozi hawa wawili si mfano wa kuigwa hata kidogo,ni wa kulaaniwa na kukemewa na wapenda amani.Ni viongozi wenye kupenda kutimiza kiu na malengo yao hata kwa gharama ya damu za watanzania.Watanzania wenzangu, tuamke wanasiasa wasitumie damu zetu kwa maslahi yao.Mabadiliko yanawezekana si lazima kwa damu zetu.Tutahadhari sana na viongozi ambao hawana njia mbadala ya kufikia malengo yao ya kisiasa isipokuwa kwa kuchochea ghasia na vurugu.
Kiongozi mmoja mashuhuri sana na mwenye akili sana aliwausia watu wake kwamba, "UKITAKA KUFANYA JAMBO KWANZA ANGALIA MWISHO WAKE, LIKIWA LINA HERI BASI LIFANYE NA LIKIWA LINA SHARI BASI LIACHE"
Tuwe mbali na viongozi mahiri wa uchochezi na si makini wa maneno na maamuzi yao.Watanzania wenzangu tutafakari kabla ya kutenda na si kutenda kabla ya kutafakari.Mwenye macho haambiwi tazama.
Nawasilisha