don-oba
JF-Expert Member
- Dec 8, 2011
- 1,387
- 677
Anawataja km watani wake CCM kusherekea miaka 35 ya kuzaliwa kwake. Anadai kweli wana haki ya kusherehekea kwa kuuza rasilimali za nchi na kuvunja misingi ya azimio la Arusha. Amepekua vitabu 'Hali ya uchumi ya taifa', 'vitabu vya bank kuu', 'kilimo kwanza'. Takwimu zinatofautiana za uchumi hapa nchini. Utapangaje maendeleo pasipokuwa na takwimu?. Wewe hujui familia yako ina watoto wangapi utawezaje kuwanunulia mahitaji?. Anadai taifa limeua base ya uchumi. Anasema kilimo kwanza hakiwezi kuwa na tija kwa kuleta Power Tiller zisizoweza kulima ardhi ya tanzania. Anadai serikali ilikukurupuka bila kufanya utafiti. Anadai Tanzanite inapatikana tanzania peke yake lakini viwanda vya kuikata vipo India...