kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,732
Leo Kumefanyika mkutano wa hadhara ambao umekwisha muda mfupi uliohutubiwa na viongozi mbali mbali wa CDM, lengo la mkutano lilikuwa ni kupongezana wana CDM kwa ushindi wa kesi, katika mkutano huu Dr. slaa amewapongeza wananchi wa Igunga katika kufanikisha ushindi wa kesi hii kwani walijitolea kwa hali na mali, pia amewaambia Polisi waepuke kutumika kisiasa kwani mwisho wa siku uhaibika kwa kukamata wananchi wasio na hatia na kuwaachia huru kama wakiona hawawezi kuacha basi wavue uniform na waingie kwenye ulingo wa siasa. Pia amegusia tamko la CCM kutaka kukata rufaa juu ya hukumu iliyotolewa na amesema kila kipengele kilichotolewa hukumu kina ushahidi madhubuti hivyo CCM watajisumbua bure kukata rufaa. pia amezungumzia suala la Magufuli kuuganganya umma wakati wa kesi kuwa ni mgonjwa mahututi na kushindwa kuja kutoa ushahidi wakati huohuo adubuhi akionekana kujibu maswali bungeni na hii Dr. Slaa amesema kama serikali inakuwa na waziri anayedanganya adharani na makusudi basi hapo hakuna serikali kwa hiyo kama Kikwete angekuwa kiongozi madhubuti angekuwa amekwisha mfukuza kazi magufuli kwa uongo ulioidhalilisha serikali yake. mwisho amewataka wanachi wa Igunga kushiriki Sensa kikamilifu kwani ni muhimu kwa maendeleo ya Taifa letu.