Elections 2010 Dr Slaa Moshi

Kule rumande hata mahabusi wanaingizwaga watu wa usalama kwa kazi maalumu, nadhani sasa CCM wana kila sababu ya kutumia mbinu za akiba kuwapoteza baadhi ya watu. Msihofu watanzania.

atakayenyoosha mkono na kukudhuru ni mtanzania mwenzako ambaye anaimba ana mapenzi mema na nchi yake ilhali ni mapenzi mema kwa genge lake.

Asante kwa kujibu kero iliyokuwa inanisumbua! Maana sikuweza kuona ni kwa nini mahabusu wafanye walichokifanya. Mahabusu sio watu wa kukata tamaa, maana wanatuhumiwa tu, na kila siku inayokuja wana matumaini ya kutoka. Hizo chuki gani walikuwa nazo na huyu baba wampige walivyofanya! Hili la kwanza.

Pili nilikuwa nawaza pengine alipelekwa mahabusu ya watuhumiwa wale waliokwishakata tamaa. Mahabusu ya watu sugu waliokwisha ua au kufanya maasi kiasi wao ni raha kumwongezea mwenzao mateso. Lakini nalo hili halikukaa sawasawa. Kwa nini mtu huyu awekwe na hao. Au polisi wetu wanawachanganya mahabusu bila kujali asilia za makosa yao. Hili sikuliweza kabisa, nilipata na msongo wa mawazo.

Baada ya kukusoma sasa napata afueni. Walifanya janja apigwe na watu wa usalama...Lakini UWT ni watu wabaya kiasi hicho..hmmmm naweza nikaamini, niliwahi kuwasikia jinsi walivyokuwa wanatesa watu wakati ule wa Presidential Dentation, enzi zile,,,,,inawezekana! Kumbe BADO SSSEMU wanaendeleza kale ka mchezo. Jamani wagombea kuweni makini. Simu zenu zina sehemu ya kubonyeza kuashiria hatari moja kwa moja kwa watu wa karibu nanyi (hasa kama una Samsun, unabonyeza kwa pembeni mara 4 na watu uliowaorodhesha wanapata onyo kwamba uko na shida, watakufuatilia watafanya wanachoweza usiwahishwe mahabusu, watatumaliza hao!)
 
Hii makala imekaa kishabiki mno. Kwa vile imetolewa na Gazeti linalomolikiwa na CHADEMA basi hii story ni mbinu za kisiasa. Yale yale ya Lamwai na Mrema !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Tuzungumze hoja na siyo majingu.

Kama ni ya kishabiki kamwuulize RPC wa Kilimanjaro kuhusu gari la Chadema na mambo ya GPS!
 
Ndugu wanamapinduzi kwa mara ya kwanza kwa miaka mingi nilijiunga na wananchi wa Moshi kumpokea Dr Slaa na kuandamana mitaani Moshi kupitia Double Street, Soko la Kati, Arusha Road hadi Uwanja wa Mashujaa. Sijawahi kuona maandamano makubwa kama haya hapa Moshi.

Maandamano yalipopita mbele ya Ofisi za CCM Arusha Road, viongozi wa CCM waandamizi na wafuasi waliotoka kuangalia umati wa wananchi ukienda Mashujaa walijawa na hofu machoni. Viongozi wa maandamano na Mkuu wa Polisi walihimiza kuelekea uwanjani na kusihi wasiwabeze wana CCM kwa kurindima ofisini kwao, kwa hivyo amani ikatunzwa.

Mkutano ulikuwa na amani na hotuba za sera na kujinadi hakuna ngoma, hakuna Ze Comedy, hakuna taarabu hakuna lolote. Sera, Mikakati na Wagombea. Hakuna watu walioletwa kwa FUSO, au Mabasi au Hiace, watu wote walikuja wenyewe kwa lengo la kumpokea na
kumsikiza mwanabidii mwenzetu wanayemwita Rais Mtarajiwa - Dr Slaa. Tens upon tens of thosands of Moshi residents.

Wananchi wachache niliozungumza nao kila mmoja anasema - TUMECHOKA TUNATAKA TURUDISHIWE NCHI YETU. I can not prove this but I am sure even CCM knows that there is something happening under this sacred soil. There seems to be a thirst for honest leadership that
characterized our land in the days of Mwalimu.

Mwisho, mzee mmoja aliniambia maneno yafuatayo, "Mangi Meli wa Moshi alinyongwa hapa na Wajerumani kwa kukataa kuishi amepiga magoti na kusimamia uhamishaji wa mali zetu kwenda kwa Kaisari. Sisi tunasimamia hilo hilo ila wakati huu hatutanyongwa na tutawatimua
hawa mafisadi na kuirudisha nchi yetu mikononi mwetu" . Words to this effect. As this 60-70 year old man spoke, he was shaking
and I could see his eyes well-up with tears. I was moved by the depth of emotion and his belief of having being deeply wronged.

wanamapinduzi wenzangu, the best we can do is to peacefully shaperon this electoral process and let the people's will be freely expressed and respected by us all. Anything else does not bode well for the future our country.

Join the movement and be a part of something bigger than yourself.
 
Yaani CCM wameshanza Plan B yao mapema hivi? Maana Plan B yao ni ya kuleta vurugu kama wakiona wanashindwa. Walishatangaza hakuna mtu anayeweza kuwafanya lolote. Na nadhani maoni ya ya ajabu ya Mhariri wa Daily News ni sehemu ya uzinduzi wa hii Plan B ya CCM.

Itabidi wananchi wajilinde dhidi ya CCM. Wakati wa kupigania UHURU, hatukumwaga damu. Kuingoa CCM ni vigumu kuliko kumng'oa mkoloni wa Kiingereza. Mwingereza alikuwa na uungwana kiasi. Hawa mafisadi wa CCM ni kizazi cha nyoka. Hawana uungwana. Tutakubali kweli kikundi kidogo cha majangili wenye uchu wa kuendelea kuhodhi madaraka watunyime haki ya kuchagua viongozi tunaowataka?

CCM hawataacha kuhujumu mikutano ya CHADEMA na kupiga watendaji wake kwa kubadilika na kuwa waungwana. Njia pekee ni kwa CHADEMA, na lukuki ya wananchi wanaowaunga mkono, kuihakikishia CCM kwamba they will fight back when provoked.

Tuweke vile vile orodha ya makamanda wa Polisi watakaoshiriki kwenye kuleta hizi vurugu za CCM. Tukishwang'oa CCM, kwa kura au kwa peoples power (maana lazima wakati huu wangoke), tutawashughulikia wakandamizaji wote kwa kutumia vyombo vya sheria. Kamanda yoyote atakayeamuru mwananchi apigwe ataajibishwa baadaye.
 
Mungu uwe nao watu hawa! Tazama jana nilikuwa pale royal palm nikajiuliza wale watu waliovaa nguo za kijani wenye sura za kihindi walivyokuwa wanajichana na bufee, nikajiuliza tena kuhusu wale akina mama niliokutana nao wakiwa wamembeba mwenzao mja mzito kule makongori kwenda lupa, h ata nilipowapa lifti nikidhani wananenda karibu bado niliendesha gari kwa saa zima kufika lupa tinga tinga kwenye zahanati, kelele za mja mzito yule kwa maumivu makali, yakanikumbusha tena jinsi kikwete anavyouza sura kwa mabango ya tshs 2,000,000,000 wakati kile kijiji kabla ya lupa walihitaji zahanati ya shsilingi milioni tisa tu! Umelaaniwa wewe kikwete, salma (imelda marcos), ridhiwan(chemical ali), rostam(mobuto), lowasa(bokasa), nk kamwe hamtaitawala tena nchi hii ya mungu, mtaendelea kumtumainia shetani wenu kupitia sheik yahye
 
Slaa1%286%29.jpg

Mgombea urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa.



Mgombea urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa, amedai serikali imewaagiza wakuu wa mikoa, wilaya na wakurugenzi wa halmashauri nchini, kuisaidia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ishinde mwaka huu.
Dk Slaa alitoa madai hayo wakati akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni za urais zilizofanyika mjini Moshi jana.
Alisema Chadema ina mtandao ndani ya serikali na katika usalama wa taifa, uliosababisha kupata taarifa na mikakati inayopangwa kwa lengo la kuibeba CCM.
“Hapa nina barua ya serikali ya Septemba 19, mwaka huu iliyotumwa kwa ma-DC, RC na wakurugenzi wa halmashauri ambao pia ni wasimamizi wa uchaguzi, zikiwaelekeza kutumia gharama yoyote ili CCM ishinde,” alisema.
Aliongeza: “mimi ninamwambia Kikwete (Rais Jakaya Kikwete) kuwa asicheze na amani ya Watanzania, aheshimu utawala wa sheria na demokrasia,” alisema.
Alisema Chadema haitakuwa tayari kuona wananchi wakinyang’anywa haki yao ya demokrasia, iwapo serikali itatumia nguvu kuwabeba wagomnbea wa CCM. Pia, Dk Slaa alisema haoni sababu ya kupewa ulinzi na askari polisi kwa vile jeshi hilo linachangia kuhujumu kampeni zake.
Alisema polisi wameonekana kuibeba CCM na kutolea mfano tukio la juzi usiku, ambapo askari waliwakimbiza vijana waliokuwa wakipima maeneo ya kutua helikopta, maarufu kama GPS huko Moshi Vijijini.
Alisema helikopta anayoitumia kwa kampeni za urais ilishindwa kufika kwenye maeneo mengi kama ilivyokusudiwa, baada ya polisi kushikilia gari lililokuwa likimpeleka mtaalam wa kupima GPS juzi usiku.
“Kamanda wa polisi mkoani hapa, naapa nitakufa na wewe kama kazi zangu zitakwama…nasikia mnamshikilia dereva pamoja na gari kwa shinikizo la Dk. Cyrill Chami,” alisema. Dk Chami ni mgombea ubunge wa Moshi Vijijini kupitia CCM ambaye hata hivyo Dk Slaa hakufafanua zaidi kuhusu ushiriki wake (Chami) katika sakata hilo.
Dk Slaa alihoji, “umeleta ulinzi wa polisi hapa kufanya nini.” alihoji Dk. Slaa.
Alilitaka jeshi la polisi kuliachia gari hilo na dereva wake ili kazi ya kupima GPS ifanyike kwa ufanisi.
Akisimulia mkasa wa kukimbizwa na polisi, mpimaji wa GPS, Gwakisa Gwakisa, alisema Dk. Chami akiwa na polisi kwenye gari yake binafsi, alianza kuwafuata kuanzia eneo la Uru na kwamba walipomaliza kupima GPS eneo hilo, walielekea Mkoringa lakini Dk Chami aliendelea kuwafuata.
“Tukiwa Mkoringa baada ya kumaliza kupima GPS gari ya Chami lilikuja likiwa imewasha taa full, tulivyoona vile na sisi tuliwasha full halafu tukazima,” alisema.
“Wao wakazidi kuja, tukahisi si watu wazuri tukakimbia,walitufukuza kuanzia Mkoringa hadi Keys hoteli,” alisema.
“Tukiwa getini tukaona mlinzi anachelewa kufungua ikabidi mimi niruke geti na dereva akaondoa gari, nadhani walikimbizana naye hadi walipomkamata,” alisema.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'hoboko alisema gari la Chadema lililokamatwa limetokana na tuhuma ambazo zimewafikia kituoni hapo.
Ng'hoboko alisema kuwa gari hiyo ilipita katika eneo la Kibosho majira ya saa 8:00 lakini liliposimamishwa, dereva hakusimama. Alisema gari hilo iliyokuwa likiendeshwa na dereva ambaye hakuweza kufahamika, lilifichwa mafichoni na dereva wake kukimbia.
Alisema kuwa walipofika eneo hilo waliikuta gari hiyo likiwa peke yake na ndipo walipoamua kuichukua na kuiweka kituoni hapo.
Kamanda huyo alisema kuwa tuhuma ambazo wamefikishiwa ni kwamba zinadaiwa kuwa usiku huo, yalitolewa mabango ya Rais Jakaya Kikwete pamoja na mgombea ubunge wa eneo hilo
Alisema kuwa hawajafanya njama zozote za kutaka kukwamisha kampeni za Dk. Slaa kwani mpaka sasa dereva wa gari hilo hajajitokeza.
"Unajua kuna tuhuma ambazo zimetufikia hivyo kuhusiana na suala hilo nitalitolea ufafanuzi kwa waandishi kesho (leo) ila mpaka sasa dereva bado hajajitokeza," alisema.
Habari hii imeandikwa na Restuta James Moshi na Beatrice Shayo, Dar es Salaam.




CHANZO: NIPASHE
 
Hiyo ndo " amani na utulivu' jana niliandika kwamba badala ya vyombo kusistizia amani visistizie haki kwanza, hakuna amani bila haki tusipobadilisha wimbo we are doomed to failure
 
Hiyo ndo " amani na utulivu' jana niliandika kwamba badala ya vyombo kusistizia amani visistizie haki kwanza, hakuna amani bila haki tusipobadilisha wimbo we are doomed to failure

Usemalo ni kweli kabisa. Hakuna amani bila haki. Makaburu walitaka South Africa yenye amani bila haki, lakini Mandela akakataa, akasema "Freedom is worth fighting for, and if necessary, dying for". Tunataka uchaguzi wa amani, lakini wenye haki vile vile. Amani bila haki hapana!
 
kugombea urais!!, kunasa nyaraka!!, macho yangu mwaka huu. Nilidhani siasa ni kunadi sera !!

Ni kweli siasa ni kunadi sera; lakini sera si AHADI za kujenga barabara, kununua meli, kutoa fedha za kununua mazao, kupandisha hadhi hospitali, n.k. sera ni hatua za kimfumo zinazochukuliwa kuhamasisha matokeo maalum kiuchumi na kijamii.

Kwa mfano, tunatarajia mgombea azungumzie mtazamo wake (na wa chama chake) kuhusu masuala kama viwango vya umiliki wa shughuli za uwekezaji katika maeneo mbalimbali kati ya serikali na watu binafsi na kati ya wananchi na wageni; mfumo na uwiano wa viwango vya kodi; jinsi ya kuimarishaji ukusanyaji wa mapato ya serikali; ugharamiaji wa elimu na huduma za afya kati ya serikali na wananchi; uhuru wa masoko kwa wakulima; kuboresha mfumo wa serikali ikiwa ni pamoja na uajiri, uteuzi na uwajibishaji wa watendaji; uboreshaji wa sheria mbalimbali zinazoathiri haki za wananchi na usimamizi wake; n.k. Sio mtu anatuahidi ujenzi wa miundombinu, hospitali, vyombo vya usafiri; n.k. halafu anadai hizo ndio sera ilhali vigezo vya kuimarisha uchumi na ufanisi serikalini ili kuongeza uwezo havigusii kabisa. Hizo zinabakia kuwa porojo kuwazuga wasio na uwezo wa kuchambua. I really hate it when "crooks" try to pass "illusions" for policy.
 
kugombea urais!!, kunasa nyaraka!!, macho yangu mwaka huu. Nilidhani siasa ni kunadi sera !!

Mwaka huu macho ni yetu,Nasubiri kuona CCM wanadawana mpaka mbao zilizojengea maghorofa yao.Kwani CCM nimegundua bila Dola Na fedha za wizi haina kitu.Sasa Tusubiri Mungu nipe uzima nifikie na nishuhudie kwa macho yangu mwenyewe.
 
kugombea urais!!, kunasa nyaraka!!, macho yangu mwaka huu. Nilidhani siasa ni kunadi sera !!

Whistle blower atabaki kuwa whistle blower tu. Bora hata afanye hivyo kwani akianza sera anaishi kutoa ahadi ya kujenga treni ya umeme ya Mwanza Dar.
 
Chadema uwekeni huo waraka kweye Front page ya magazeti ya kesho, ili kila Mtanzania na jamii yote ya Kimataifa iuone.

watauwekaje hadharani na kwenye magazeti wakati waraka wenyewe haupo?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom