Dr. Slaa: Mchakato wa katiba mpya kuanza ndani ya miezi minne nikipewa madaraka

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Maelfu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam jana walijitokeza kumlaki mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilibroad Slaa, ambaye wakati akihutubia wananchi pamoja na mambo mengine, ameahidi kuanza mchakato wa utengenezaji wa katiba mpya ndani ya miezi minne kama atapewa dhamana ya kuongoza nchi.

Dk. Slaa ambaye hadi jana asubuhi alikuwa ameshadhaminiwa na Watanzania 1,397,757 kutoka mikoa 20 Tanzania Bara na Visiwani, alikuwa akitokea Zanzibar alikokwenda kutafuta wadhamini, akiwa ameambatana na viongozi wakuu wa chama hicho akiwemo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, ambapo aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere majira ya saa 6:50 mchana na baadaye kuhutubia umati mkubwa wa wananchi waliojitokeza kumsikiliza katika viwanja vya Jangwani.

Wakati akitoa hutuba, Dk. Slaa alisema kero nyingi zinazoikabili nchi kwa sasa zinatokana na Katiba ya nchi kuwa na kasoro nyingi na kwamba iwapo itaandikwa upya kwa kuzingatia matakwa ya wananchi wengi, itasaidia kutatua kero hizo.

"Siku hizi kila mahali ni foleni, ukienda polisi ni foleni, mahakamani, benki, barabarani kote ni foleni huku chai ya 'wakubwa' kwa mwaka inagharimu zaidi ya bilioni 30, wabunge wanapandishiwa mishahara kila siku na kulipwa posho kubwa wakati mwananchi wa kawaida akiteseka kwenye lindi la umaskini, hizi ni kero zinazohitaji ufumbuzi wa haraka," alisema Dk. Slaa na kushangiliwa.

Dk. Salaa, ambaye alihutubia kwa takribani dakika 40 kuanzia saa 12:03 jioni, alisema Tanzania inahitaji viongozi watakaoweza kupanga matumizi sahihi ya rasilimali zilizopo ili zinufaishe umma badala ya kuwanufaisha wachache huku wengi wakiumia.

Kwa wakati wote ambao Dk. Slaa alikuwa akihutubia wananchi walikuwa wakimshangilia kwa kumwita 'Rais, Rais' jambo lililokuwa likimlazimu kukatisha hotuba yake kila mara.

Awali, Mbowe alisema Chadema kinamuunga mkono Maalim Seif Hamad Sharif ambaye anawania Urais kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi (CUF) visiwani Zanzibar.

Alisema kuwa chama hicho hakitasimamisha mgombea urais kwa upande wa Zanzibar na kwamba wafuasi wake watampa kura za urais Maalim Seif. Hata hivyo, alisema Chadema kitasimamisha wagombea wa ubunge na uwakilishi visiwani humo ili kuweka nguvu ya upinzani ndani ya Baraza la Wawakilishi.

Hata hivyo, alisema Chadema haiungi mkono uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa visiwani Zanzibar kwa maelezo kwamba uundwaji wake hautamaliza siasa za chuki visiwani humo.

Kwa upande wa Bara, alisema chama hicho kimeshindwa kuungana na vyama vingine kwa kuwa baadhi ya vyama vya siasa vimekuwa vikifanya mzaha kwa kushabikia CCM.
Alisema katika uchaguzi wa mwaka huu, Chadema kitapambana ipasavyo ili kuhakikisha kinapata ushindi na kueleza kwamba wamechoshwa na wizi wa kura aliosema umekuwa ukifanywa na Chama Cha Mapinduzi.

"Chadema tumeamua kumuunga mkono Maalim Seif kule Zanzibar lakini tutasimamisha wagombea ubunge na uwakilishi wa Baraza. Kwa upande wa Bara, nadhani wote mnafahamu kwamba tunavyama 17 vya siasa, vya kweli na vya mzaha. Hatuwezi kuungana na vyama vinavyocheza ngoma ya CCM," alisema na kuongeza "Haki ya Mungu, ama zao ama zetu...lugha ya kusema tumeibiwa kura mwaka huu tutaiacha. Chadema tunapenda amani lakini mwaka huu ikibidi na sisi tutaiba kura, tumechoka."

Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Said Arf, alisema afya ya Dk. Slaa ni imara na kwamba anaweza kufanyakazi bila tatizo lolote hivyo kuwaomba wananchi wamchague kuwa rais wakati wa uchaguzi. Alionya kwamba chama hicho hakiwezi kugawanywa na propaganda ya udini ambayo imeanza kunadiwa na wapinzani wao wa kisiasa wanaodai kwamba Dk. Slaa ni chaguo la Kanisa Katoliki.

Wakili wa maarufu nchini, Mabere Marando, ambaye ni miongoni mwa mawakili wanaowatetea watuhumiwa wa wizi wa EPA, alisema washtakiwa waliofikishwa mahakamani ni matawi na kwamba CCM haitaweza kuwakamata watuhumiwa wakubwa.

Alisema kuwa watuhumiwa waliofikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa EPA ni watu wadogo, lakini vigogo waliohusika hawajachukuliwa hatua yoyote na kwamba ushahidi anao.

Hata hivyo, akisoma dua ya kufungua mkutano huo, Sheikh Said Mwaipopo, alisababisha wananchi kushangilia katikati ya swala alipomwomba Mungu awadhalilishe wezi wote wa rasilimali za nchi.

Aidha, msafara wa Dk. Slaa ambao uliwasili uwanja wa ndege wa zamani majira ya saa 6:50 mchana, ulikuwa ukisimama kila wakati njiani wakati ukielekea Jangwani, kutokana na magari ya wananchi kuingilia jambo lililoibua mgogoro baina ya vijana wa usalama wa Chadema na askari wa usalama barabarani, katika mataa ya Tazara.
 
Tumeshuhudia kwamba mtu anapopata umaarufu fulani huwa akiingia madarakani anachomekea vitu ambavyo ni vigumu watu wakivishtukia mapema!

1. Rais Mwinyi alikuwa chaguo la Nyerere na kwa wakati huo alionekana ni "kijana," kwa hiyo ali-take advantage ya kuchomekea masuala ya OIC ambayo yalikuja kushtukiwa baadaye hata hivyo.

2. Kikwete alipata umaarufu mkubwa sana, hata baadhi ya viongozi wa dini wakawita kuwa ni "chaguo la Mungu," aka-take advantage hiyo kuchomekea mambo ya Mahakama ya Kadhi kwenye Ilani ya Uchaguzi, 2005. Baada ya kushtukiwa akadai eti sio yeye aliyeitunga Ilani hiyo na hatimaye kuwaruhusu Waislamu waunde Mahakama za Kadhi wenyewe badala ya kuingiliwa na Serikali!

3. Maalim Seif alipozungumza na Rais Karume na kuleta matumaini mapya ya kuwaunganisha Wazanzibari, watu wa mataifa mbalimbali pamoja na wa hapa nchini waliwasifu sana. Hao wazee bila kujali kwamba kuna kitu kinaitwa "Muungano" wakachomekea suala la "Zanzibar ni miongoni jwa nchi mbili" huku wakijua kwamba kufanya hivyo ni kuvunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 ambayo Karume mwenyewe aliapa kuilinda! Mpaka sasa "kuchomekea huko" hatujaelewa kunaashiria nini? Labda ndio mwisho wa Muungano wetu kama baadhi ya watu walivyodai! Au kwa maneno mengine, JK ameachiwa nchi ambayo haipo kisheria!

4. Kwa mantiki hiyo ni vema kujua ni mambo gani ambayo Dkt Slaa kama taingia Ikulu atayafanya ili ajifunge kwa maneno yake! Asidai kwa ujumla wake tu kwamba "Nitabadili Katiba ndani ya siku 100!" That is not enough!

5. Dkt Slaa atupatie rasimu ya Katiba atakayoitunga ili tujue mapema! Tutakuja kuwekewa mambo ya akina Kadhi ndani ya Katiba yetu kwa shinikizo la baadhi ya watu!

6. It is the time now! Show us the draft, Dkt Slaa!
 
Buchannan, Katiba hatungwi na rais! Hayo yote uliyoyaorodhesha si mambo yaliyoletwa na marais uliowataja bali ni matukio yaliyotokea katika urais wao. Hivi ni vitu viwili tofauti. Dr. Slaa hawezi kukupa rasmu ya Katiba yake kwa kuwa haipo. Ana mapendendekezo yake ambayo amekwisha kuyaweka wazi. (Soma Gazeti la Raia Mwema la wiki hii). Hayo pamoja na ya wadau wengine ndiyo yataingizwa katika Rasmu ya Katiba (kama CCM itakuwa imeondoka) na kupitishwa na wananchi kupitia Bunge au Baraza la Katiba (Consituent Assembly). Ikibidi kabla ya hapo inaweza kuitishwa kura ya maoni (referendum) kuhusu haja ya kuwa na Katiba mpya au la. Kama una maswali kwa Dr. Slaa basi yawe kuhusu sera zake binafsi au za CHADEMA.
 
naamini dr.slaa angekuwa mtunga katiba lazima kitu cha kwanza angeshauri mahakama ya kadhi na oic
 
Buchannan, Katiba hatungwi na rais! Hayo yote uliyoyaorodhesha si mambo yaliyoletwa na marais uliowataja bali ni matukio yaliyotokea katika urais wao. Hivi ni vitu viwili tofauti. Dr. Slaa hawezi kukupa rasmu ya Katiba yake kwa kuwa haipo. Ana mapendendekezo yake ambayo amekwisha kuyaweka wazi. (Soma Gazeti la Raia Mwema la wiki hii). Hayo pamoja na ya wadau wengine ndiyo yataingizwa katika Rasmu ya Katiba (kama CCM itakuwa imeondoka) na kupitishwa na wananchi kupitia Bunge au Baraza la Katiba (Consituent Assembly). Ikibidi kabla ya hapo inaweza kuitishwa kura ya maoni (referendum) kuhusu haja ya kuwa na Katiba mpya au la. Kama una maswali kwa Dr. Slaa basi yawe kuhusu sera zake binafsi au za CHADEMA.

Ok, nashukuru nitapitia gazeti hilo!
 
naamini dr.slaa angekuwa mtunga katiba lazima kitu cha kwanza angeshauri mahakama ya kadhi na oic

Kwani bila OIC na Mahakama za Kadhi binadamu hawezi kuishi mpaka unadai kwamba eti KITU CHA KWANZA?
 
Hebu wana J.F tuijadili kauli ya Dr Slaa kuwa angechaguliwa kuwa Rais wa TZ angetupatia katiba mpya ndani ya siku 100 za kuwepo kwake Ikulu. Je, kauli hii ina ukweli wowote kwa kuzingatia mchakato mzima wa upatikanaji wa katiba mpya.
 
Ndio inaukweli! hii ya sasa watu wanatajirikia hapo na miela ya hiyo tume ya katiba.... ulaji ndio maana wanajikokota kumaliza mapema.
 
hv ulikuwepo kipindi cha uchaguzi na ukasikia alicho kuwa anakizungumza dk slaa? Au unakurupuka tu na aujui unacho andika hapa jf na ukizingatia hili jukwaa linatembelewa na watu makini, kajipange upya alafu ulete topic yako hapa kwenye jukwaa
 
Alisema mchakato ungeanza ndani ya siku 100, sio katiba ndani ya siku 100, badilisha huo upotoshaji ndio tuchangie.
 
Jifunze kusikiliza vizuri kabla ya kusema chochote, acha kuishi kwa kuamini propaganda.

Dr. Slaa alisema
''ATAHAKIKISHA MCHAKATO WA KUANDIKWA KATIBA UNAANZA NDANI YA SIKU 100 TOKA AMEINGIA IKULU''
Na wala hakusema katiba mpya itapatikana ndani ya siku 100
 
Hakusema hivyo...ndugu Majanikv umesema vizuri, alisema ataanza mchakato wa kuandika katiba mpya ndani ya siku 100 kama unahitaji nikutumie maelezo mengine( full nondo ) niambie maana kila kitu alichokuwa anakisema wakati wa kampeni nimekihifadhi kwa komputa yangu
 
Jamani wana Great Thinkers tumevamiwa na virus dhidi ya viongozi wetu na chama chetu kwa ujumla,hivi wewe habibi mchange nyakarungu mmetumwa na nani kwa unafiki huu??Ni lini dokta alisema atawapa katiba mpya ndani ya siku 100??Kama wewe sio kipofu kuanzia machoni mpaka masaburini mwako basi wewe ni shetani wa mguu mmoja!!!!UKWELI NDIO HUU!!!TUTAANZISHA MCHAKATO WA KATIBA MPYA NDANI YA SIKU 100 TUTAKAPOINGIA MADARAKANI!!!-acha unafiki wako utavalishwa shanga humu ndani...
 
Alisema mchakato ungeanza ndani ya siku 100, sio katiba ndani ya siku 100, badilisha huo upotoshaji ndio tuchangie.

Yale yale ya "Tuko kwenye mchakato". Nadhani angekuwa firm kwa kusema angetupatia Katiba Mpya ndani ya kipindi fulani; uwe mwaka ama miaka miwili lakini eti Mchakato ungeanza baada ya siku 100 bila kutaja ungeisha lini ilikuwa kama danganya toto vile.
 
Povu la nini. Weka ushahidi kutetea hoja yako ikwezekana video siyo pooooovu hadi kwenye masaburi.
 
*Unajua matatizo yakuchukua maneno unayo yataka wewe?

*Unajua matatizo ya kusikiliza unapo pataka wewe?

Hebu wana J.F tuijadili kauli ya Dr Slaa kuwa angechaguliwa kuwa Rais wa TZ angetupatia katiba mpya ndani ya siku 100 za kuwepo kwake Ikulu. Je, kauli hii ina ukweli wowote kwa kuzingatia mchakato mzima wa upatikanaji wa katiba mpya.
 
..too much money and time is wasted ktk mchakato.

..Issa Shivji na Mark Bomani wangeweza kuandika katiba mpya in 100 days.

..sasa hivi wanakwenda kuongea na wananchi ambao hawana uelewa wowote ule na masuala ya katiba.

..mapesa wanayofuja yangeweza kujenga vyuo kadhaa vya VETA wenetu wakasoma humo.
 
Back
Top Bottom