Kama nimekusoma vizuri una maana madiwani wawili wa Sengerema na mmoja wa Arusha Sombetini. Baada ya kikao cha bunge turudishiwe ile operation Twanga Kotekote tuwaraaaaammbeeeee hawa magamba.
Asante sana kwa taarifa, hii inatia hamasa magamba wengine kujiunga na CHADEMA tayari kwa harakati za ukombozi wa kweli wa Tanzania ya watu wapole, wastaarabu, wanyenyekevu, wakarimu, lakini siyo wanyonge!
Serikali na CCM kama walifikiria kutokuwepo Dr. Slaa kwenye bunge na hatimaye mizengwe ya kumtoa ubunge Godbless Lema ni mafanikio sasa hali imegeuka kilio na kusaga meno kwa Serikali na Chama chake CCM. Uhuru na nafasi waliyo nayo pamoja na ushawishi mkubwa, hali kadhalika mizengwe iliyotumika kumvua ubunge ndiyo chachu ya wananchi wengi kuwaona watu hawa ni wapigania uhuru wa kweli kama Madiba wa bondeni.
Shibodo alisema Makapa kusema maneno ya ovyo yasiyostahili kwa mtu mkubwa kama yeye ikiwemo matusi, dharau na dhihaka dhidi ya wananchi wa tanzania kupitia vyama vya upinzani yamewakasirisha sana Watanzania, leo yametimia, moto huu kuuzima ipo kazi, na hadi kufikia 2015 CCM yatabaki mabua tu.
Dr Slaa na Lema wanazidi kuchanja mbuga kuimarisha uhai wa Chadema
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.