Gwalihenzi
JF-Expert Member
- Oct 21, 2011
- 5,125
- 1,300
Busara zaidi kama ukimshauri kipenzi chako Philipo Mulugo afute kabisa masomo ya uraia, Civics na General Studies kwenye hizi shule kwani yana wapatia uwanja walimu kumwaga sera za vyama vya siasa wanavyoviunga mkono bila kudhibitiwa! na mwaka 2015 hauko mbali !Nitamshauri msajili wa vyama vya siasa, apige marufuku kwa viongozi wa vyama vya siasa wasio na wadhifa wowote rasmi wa umma, kualikwa kuwa wageni rasmi wa mahafali ya shule za chekechea, msingi na sekondari ili kuwakinga watoto wetu na political indoctrination kwenye siasa. Tena kanuni itasisitiza hata hao viongozi wa siasa wenye utumishi rasmi wa umma, ni marufuku kuhutubia siasa kwenye mahafali zozote za shule ili kuepuka kuzigeuza shule kuwa ulingo wa siasa!.
Katazo hili, sio mahsusi kwa Dr. Slaa bali kwa wanasiasa wote!. Shule zihesabiwe kama nyumba za ibada, iwe ni marufuku kabisa kupiga siasa shule za chekechea, msingi na sekondari, siasa zianzie vyuoni ambako wanafunzi wanaingia wakiwa wameshatimiza majority age of 18!.