Mh Mbowe ni kiongozi mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.
Vyovyote vile itavyoelezwa waliomakini twaelewa alichoimanisha. mambo madogo kama hayo hayatutoi roho, sisi sio nynyiem bana, hakuna kulala.
Mh Mbowe ni kiongozi mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.
oi! tu update kaka!!!!!!!!!!
oi! tu update kaka!!!!!!!!!!
mods naomba ubadilishe heading isomeke Live updates: Dr Slaa kuunguruma Ziba Igunga leo.
majira ya saa saba mchana kiongozi mkuu wa upinzani nchini na katibu
mkuu wa Chadema Dr Slaa atahutubia mkutano wa hadhara ktk kijiji cha
Ziba wilaya ya Igunga.Dr Slaa atafika Ziba akitokea Kayenze uyui Tabora
alikokuwa akihitimisha kumnadi mgombea wa udiwani wa CDM.
Nitakuwa live kuwaletea habari.
Source; Katibu mwenezi CDM Igunga.Diwani Vicent.
Tena wakati Huu Ni msimu wa ngoma maeneo hayo nani aache kuangalia Utamaduni wake akamsikilize Mchungaji aliyeshindwa kuchunga Kondoo wa Bwana na kukimbilia kuchunga mbwa mwitu, atawaweza kweli. Halafu hajaoa.
Hana jipya na nadhani hata mwenyewe atabaini kuwa mwitikio wa Wananchi kuhudhuria mikutano Yake umepungua. Wananchi wa Ziba na Vijiji Jirani vya Ulaya, Iborogero, Burangamirwa, Uchenjegele, Chomachankola, Miguwa, Mbogwe, Nkinga, Mwisi, n.k. Chapeni Kazi zenu za kujiletea Maendeleo badala ya Kwenda kusikiliza hotuba za silaa zisizokuwa na tija
Kama maneno haya ni yako
sawa ,kama umetumwa wote na alyekutuma hamna***** mimi nakukaribisha au
subiri picha uome sio hao tu uliowataja hadi Nata Mwangoye ,Itobe
,Samuye watatia timu kumuona kamanda wa ukweli.Acha wale kwa sasa wana
kazi ya kusuluhisha migogoro iliyotokana na mipasuka ya rushwa za
uchaguzi.
Mh Kasulumbayi
anawashukuru wana Igunga kwa kuchagua mabadiliko,maana ccm walikuwa
wanaita mkoa wa Tabora ni ghala lao la kura (stock).Uchaguzi wa Igunga
umeamusha wana tabora.
Kama hujui
kuongea uongo huwezi kuchaguliwa kuwa kiongozi ccm.hicho ndicho kigezo
cha kupata uongozi amesema Kasulumbayi.
Uongo wa ccm
umeambukizwa mpaka kwa polisi.kama serikali inaongozwa na waongo wote
waliochini ya serikali wanalazimishwa kusema uongo.Kamanda Kova
akadanganya aliyemteka ulimboka ameungama kanisani ni mkenya.Waziri
Nchimbi amemdanganya mpaka jaji mstaafu Ihema akasema uongo tume ya
Mwangosi.
Picha zaidi
wewe acha kumtukana baba wa taifa bana. JKN ameishi maisha ya kuigwa ndugu yangu,Slaa anaishi maisha ya kuogopwa, JKN hakutupa mke na watoto na kukimbilia kimada.Dr Slaa ni mkombozi wa kweli. In short ndiye Nyerere wa sasa.
Dr Slaa
amewashukuru wanaigunga kwa kuichagua Chadema,pamoja na ccm kuchakachua
matokeo. mahakama imetengua ushindi wa Kafumu.Wamesema eti jaji ni
rafiki yake na Mbowe.
wameweka
kusudio la kukata rufaa lakini hawajakata rufaa.hii ni kuwafanya
wanaigunga wakose mwakilishi maana wanajua uchaguzi ukirudiwa
watashindwa.Tumegundua njama zao tutaipindua hii mara moja,usalama wa
taifa mliopo hapa pelekeni taarifa.
Dr slaa:
Mapolisi mnatuaibisha jana kule Rwenzera kijana wetu amepigwa na watu wa
ccm tukampigia simu ocd hakwenda kwa wakati muafaka.Baadaye gari la
polisi linakwenda wanamchukua kijana wakamtupia kwenye gari.na ndani ya
gari alikuwepo m/kiti wa ccm na kreti la bia na viroba vya konyagi
askari wamelewa.nawaagiza mapolisi kama mmeshindwa kazi vueni magwanda
yetu mturudishie.