Elections 2010 Dr.Slaa kutoongea na waandishi wa habari kesho jumapili

dr wakati ukiendelea kuungana na watanzania kuugulia kuibiwa kwa kura zetu wabunge wako wa viti maalum wanaugua ugonjwa wa sintofahamu kwani hawajui wanaenda mjengoni au la pls watangazie wajue namba zao

Mawazo na matazamo wa kihabithi.
CHADEMA wanafuata taratibu walizojiwekea chini ya sheria.
Huko CCM hata zoezi dogo la kutoa maoni yako binafsi nilazima usubiri BOSI wako akuruhusu.
Uhuru ulipatikana Miaka50 ilopita mmeuuza kwa bei ya Shanga sasa mnataka na wengine wafuate nyayo zenu.

Nyie Nambari ONE,Hapa mnachezewa Delay tactics kiduuuuchu tu, mnahaha kwa kukosa shibe ya Umbeya Hiii Hii Hii!:first:
Nyayo wenzenu watafuata Makinda wenu sisi tunatengeneza Trail Mpya.
KEEP UP Dr Slaa.
 
Kweli inabidi jamaa ajilinde sana maana mafisadi hawaaminiki! Dr. usikaribishwe drinks au chakula, hatuwaamini hao! take care of yourself man!
 
ukweli unaumaa............kikwete kachaguliwa na watu mil.5 kati ya mil.43......shame on him na hapo ni baada ya kuchakachua
 
Hii itawasumbua sana sana kwa akili zenu za ubishoo.
Ukinunua gari mpya mpaka umpe mwanao akalingishie wazee wenzio woote.
Kila jambo likitokea kwenu kipimo cha ufanisi ni kiasi gani mtaliza makalio yenu mbwaaataaa! yakusikika nchi nzima
Wake zenu wakinunua gagulo mpya ni lazima wazivae mlegezeo ili kila njemba ione ikiwa ni pamoja na vijust.Aibu yetu wote
Mnaleta Ubishoo na UHillsider mambo 2nd year enzi zileee Mlimani Univ. Masikini hamkui akili mnakua mafuvu ya vichwa Mashavu Midomo na makalio.

Umeacha main Topic kwa vile ni Fupa alolishindwa Fisi, unalenga personal issue zenye kujaa chumvi ambazo tusema tuwaweke Viongozi wa CCM hapa tuwajadili katika dulu hizo watakaa uchhi wa mnyama mbele za wakwe zao. Mlete Kikwete hapa Mlete Makamba Mlete January hapa. Leta Baraza lote la mawaziri wake kwa waume hakuna hata mmoja atabaki kavaa nguo.
Una nyumba ya Vioo usianze kurusha mawe.

Salute!:smile-big::smile-big::smile-big:
 
katika facebook yake,Dr Salaa ameandika hivi:
Tunaulizwa kwaninii hatukushiriki kutangazwa au kuapishwa kwa JK

Tungeweza vipi kuhudhuria kutangazwa kwa mshindi au kuapishwa kwa Rais ambaye ametangazwa katika mazingira ya wasiwasi na mchakato mzima? Hatuna tatizo binafsi na Kikwete au hata yeye kuwa Rais, tatizo letu la msingi kabisa ni kuwa mchakato wa utangazaji matokeo ulikuwa mbovu sana kutishia kuaminika kwa matokeo hayo. Kama Kikwete angeshinda kwa asilimia 99 au asilimia 50.01 kwenye mchakato ulio huru, wazi na wa haki tusingelalamika kabisa.

Hivyo, kama tungeshiriki kama watu wanavyopendekeza na kukumbatiana kama walivyofanya wengine tungekuwa tumetuma ujumbe kuwa hatuna matatizo na mchakato mzima wa matokeo. Tungehalalisha vitendo vya tume na watumishi wake kuvuruga uchaguzi.

Tulipanga kuzungumza na waandishi kesho, lakini imeahirishwa kwani kuna mchakato unaoendelea na ambao tunataka kuona utafikia wapi. Tunawasihi wanachama, mashabiki na wapenzi wetu waendelee kutulia wakati huu ili kutupa nafasi ya kuandaa mpango mzuri wa mwitikio wetu.

asanteni.

Dr Slaa ungeshiriki kwenye utangazwaji matokeo na hatimaye pia kwenye kuapishwa kwa Mchakachuaji Mkuu ningekuona wewe famfa tu..nashukuru uliliona hilo mapema!
 
Dr wa ukweli tuna shauku ya kusikia chochote kutoka kwako. Moyo wangu umeumizwa na tume ya uchaguzi, na sijui utaona vipi! Watanzania kupania kuweka kiongozi wao lakini mamruki wakatangaza matokeo tofauti na yale yaliyo ripotiwa kwenye nakara za wakala wa vyama na wamesigh hizo doc.

Binafsi sikutaka kujua aliyeshinda isipokuwa nilitaka kuona matokeo yanatoka kama yalivyo kwenye vituo. lakini kutoa matokeo tofauti na hali halisi yaliyoonesha kwenye vituo, ni jambo ambalo limeendelea kuuma roho yangu. 2+2=4, huwezi kusema 2+2=3 hapa ukiona kila aliyefanya hesabu hii anapewa tick, ujue mwalimu husika hana lolote.

MUNGU ALIYE WAOKOA WANA WA ISRALE MIKONONO MWA FARAO BILA PANGA WALA JESHI, BASI TUNAZIDI KUOMBA NASI MUNGU ATATUONDOA KWENYE MAKUCHA YA HUU UDHARIM.
 
katika facebook yake,Dr Salaa ameandika hivi:
Tunaulizwa kwaninii hatukushiriki kutangazwa au kuapishwa kwa JK

Tungeweza vipi kuhudhuria kutangazwa kwa mshindi au kuapishwa kwa Rais ambaye ametangazwa katika mazingira ya wasiwasi na mchakato mzima? Hatuna tatizo binafsi na Kikwete au hata yeye kuwa Rais, tatizo letu la msingi kabisa ni kuwa mchakato wa utangazaji matokeo ulikuwa mbovu sana kutishia kuaminika kwa matokeo hayo. Kama Kikwete angeshinda kwa asilimia 99 au asilimia 50.01 kwenye mchakato ulio huru, wazi na wa haki tusingelalamika kabisa.

Hivyo, kama tungeshiriki kama watu wanavyopendekeza na kukumbatiana kama walivyofanya wengine tungekuwa tumetuma ujumbe kuwa hatuna matatizo na mchakato mzima wa matokeo. Tungehalalisha vitendo vya tume na watumishi wake kuvuruga uchaguzi.

Tulipanga kuzungumza na waandishi kesho, lakini imeahirishwa kwani kuna mchakato unaoendelea na ambao tunataka kuona utafikia wapi. Tunawasihi wanachama, mashabiki na wapenzi wetu waendelee kutulia wakati huu ili kutupa nafasi ya kuandaa mpango mzuri wa mwitikio wetu.

asanteni.
With this brief, laden with mature and wise sentiments, Dr Slaa continues to prove those doubters out there wrong (again.....and again).
He's a really a prez material (not like those Bongowood impostors currently occupying our good statehouse).
 
Dr slaa anafahamu kuwa kwenye wakati kuna majira na tena kuna wakati wa kusema na wakati wa kukaa kimya.vyovyote hekima inakuongoza.wengine wanaongozwa na tiss,wengine wanalindwa na mapepo/majini wabaya lakini wewe unalindwa na logos!wakati ukifika utaongea na wajeuri ukiwaambia wawahi kortini huwa wanakimbilia kwenye bia wanakaa kimya!
Tupo bega kwa bega na wewe na tena tunasubiria mkakati wa kumfuata adui hadi nyumba kumi kuanzia january 2011 hadi october 2015 tuone kama daudi hatamshinda goliathi!
 
Dr W P Slaa, is the president for all us who are the followers of CHADEMA!
wewe u rais wetu, na ni rais wetu sisi walalahoi na waamka taabani.
Tunakupenda na tunakujali ndiyo maana hata tulikuchangia Tsh. 350/- zetu kwa sms kupitia simu zetu ili uweze kupata mafuta ya Chopper yako.Huo ndio uliokuwa uwezo wetu sisi wana wa wakulima wa jambe la mkono.
Tunazidi kufunga na kusali na kuomba ili yeye aliye Mkuu kuliko mkuu wa ulimwengu huu wa giza. ufisadi, wizi, na udanganyifu, akuwezeshe na akupe busara na hekima ya kufanya maamuzi yenye mkono wake wa kutuongoza na kutuonyesha njia iliyo sahihi.

Amen..........
 
katika facebook yake,Dr Salaa ameandika hivi:
Tunaulizwa kwaninii hatukushiriki kutangazwa au kuapishwa kwa JK

Tungeweza vipi kuhudhuria kutangazwa kwa mshindi au kuapishwa kwa Rais ambaye ametangazwa katika mazingira ya wasiwasi na mchakato mzima? Hatuna tatizo binafsi na Kikwete au hata yeye kuwa Rais, tatizo letu la msingi kabisa ni kuwa mchakato wa utangazaji matokeo ulikuwa mbovu sana kutishia kuaminika kwa matokeo hayo. Kama Kikwete angeshinda kwa asilimia 99 au asilimia 50.01 kwenye mchakato ulio huru, wazi na wa haki tusingelalamika kabisa.

Hivyo, kama tungeshiriki kama watu wanavyopendekeza na kukumbatiana kama walivyofanya wengine tungekuwa tumetuma ujumbe kuwa hatuna matatizo na mchakato mzima wa matokeo. Tungehalalisha vitendo vya tume na watumishi wake kuvuruga uchaguzi.

Tulipanga kuzungumza na waandishi kesho, lakini imeahirishwa kwani kuna mchakato unaoendelea na ambao tunataka kuona utafikia wapi. Tunawasihi wanachama, mashabiki na wapenzi wetu waendelee kutulia wakati huu ili kutupa nafasi ya kuandaa mpango mzuri wa mwitikio wetu.

asanteni.
Jumapii saa 2 usiku niliwasha jenereta yangu nikajiunga na ITV nikitaka kujua Dr. Slaa kasema nini - lakini wapi.
Nadhani siku nyingine mtumie vyombo mbalimbali vya habari kutupa taarifa. Hii facebook ni wangapi wanaijua huko vijijini?. Nakuhakikishia mpaka sasa kuna watu wengi hawajui kwa nini Dr. Slaa hakuongea na waandishi wa habari. Nimepigiwa simu na rafiki toka mwanza anasema 'mbona vyombo vya habari haviongelei alichowaeleza DR. Slaa'!
 
Back
Top Bottom