knownless
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 172
- 46
Kiongozi mkuu wa upinzani na mwanasiasa machachari nchini Dr Wilbrod Slaa anaanza ziara ya siku kumi katika mikoa ya Tabora,Shinyanga na Mwanza.
Dr Slaa ambaye pia ni katibu mkuu wa CDM anaanza ziara hiyo leo na atafuatana na watendaji na maafisa mbalimbali kutoka makao makuu ya CDM.
Ziara hiyo ya Dr Slaa itachukua siku kumi na pamoja na mambo mengine atakagua miradi ya maendeleo inayosimamiwa na chama chake,kufanya mikutano ya ndani na wanachama pamoja na viongozi katika kila eneo na pia kuhutubia mikutano ya hadhara kutangaza sera na kuingiza wanachama wapya.
Source:Nipashe.
atakuja lini unyamwezini?