Katibu Mkuu wa CDM Dr Wilbroad Slaa leo atahitimisha kampeni za udiwani kwa kufanya mikutano mikubwa mitatu katika kata ya Miyenze wilayani Uyui Tabora.
Kuna hamasa kubwa hapa wilayani Uyui na kuna uwezekano mkubwa wa mgombea wa CDM kushinda kwa idadi kubwa ya kura.
Tangu Dr Slaa aje kanda ya ziwa wiki mbili zilizopita amefanya kazi kubwa usiku na mchana kuhakikisga ushindi wa chama chake.Tayari amepiga kampeni kubwa katika kata saba za Lwenzera(Geita),Bugarama(Kahama),Karitu(Nzega),Lubili(Misungwi) na Mwawaza(Shinyanga).
Mbali na Dr Slaa pia viongozi kadhaa wa CDM akiwemo Mwenyekiti Freeman Mbowe watahitimisha kampeni za wagombea wa CDM katika maeneo tofauti nchini.Wakati Mwenyekiti Mbowe atahitimisha huko Kusini Naibu Katibu Mkuu Zitto Kabwe anatarajiwa kuhitimisha huko Rombo katika kanda ya Kaskazini.
Kuna hamasa kubwa hapa wilayani Uyui na kuna uwezekano mkubwa wa mgombea wa CDM kushinda kwa idadi kubwa ya kura.
Tangu Dr Slaa aje kanda ya ziwa wiki mbili zilizopita amefanya kazi kubwa usiku na mchana kuhakikisga ushindi wa chama chake.Tayari amepiga kampeni kubwa katika kata saba za Lwenzera(Geita),Bugarama(Kahama),Karitu(Nzega),Lubili(Misungwi) na Mwawaza(Shinyanga).
Mbali na Dr Slaa pia viongozi kadhaa wa CDM akiwemo Mwenyekiti Freeman Mbowe watahitimisha kampeni za wagombea wa CDM katika maeneo tofauti nchini.Wakati Mwenyekiti Mbowe atahitimisha huko Kusini Naibu Katibu Mkuu Zitto Kabwe anatarajiwa kuhitimisha huko Rombo katika kanda ya Kaskazini.