Kwa wafuatliaji wa siasa za hapa kwetu Tanzania, mtakumbuka ya kwamba Dr. Slaa alikuwa mwanachama mtiifu wa CCM kabla ya kuasi chama na kukimbilia CHADEMA.
Hata hivyo, mpaka leo hii Dr. Slaa hajawahi kukabidhi kadi ya CCM.
kama aliilipia mara kadhaa anayo haki ya kuiweka kama souvenir.pengine kesho vichaa fulani kam hawa walioanzisha thread watataka aje thibisha kuwa aliwahi kuwa mwanachama na card yake aonyeshe.
kweli shule na vyuo vyetu vina kazi sana kama ndio watu wanafikiri hivi. Kama hajarudisha manake kuwa anayo? Yaani hakuna uwezekano mwingine wowote ule? Mimi pia niliwahi kuwa na kadi ya CCM na hadi leo sijairudisha na sina mpango wa kuirudisha....
kadi si lazima urudishe kuthibitisha kuwa si mwanachama,, KUTOILIPIA ada tu kwa muda uliowekwa inakuwa umejitoa uanachama. kama hailipii ada wewe unawashwa nini?
Jana nilikuwa kijiweni na vijana tunakunywa kahawa nikasikia wanasema Dr. Slaa alitumwa na Nyerere kuingia upadri ili ajue huko mapadri wanafanya nini na hakuwa na utashi wa kweli.
Kwa kifupi wanasema alitumwa na serikali na ni mtu wao hadi leo. Vijana wakawa wanaonyesha wasiwasi juu ya Dr. Slaa na wakasema afadhali Mbowe. Leo naona hii post nimeshangaa. Naona mitandao ya Urais ndani ya CDM inafanya kazi kwa umakini mkuu.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.