Dr Slaa atoa Onyo kali kwa wabunge wa CCM

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amesema ameshangazwa na taarifa za tishio la wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) za kutaka kugomea kujadili muswada huo. Amesema endapo watayagomea marekebisho hayo na kuyarudisha kwa Rais Kikwete anaweza kuamua kuvunja Bunge kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, juu ya taarifa za wabunge wa CCM kutishia kugomea mjadala wa marekebisho hayo. Alisema wabunge wa CCM wanapaswa kuzingatia utaratibu uliotumika kupata maoni mbalimbali yakiwamo ya vyama vya upinzani, taasisi zisizo za kiserikali ambazo zilitoa maoni yake.

Alibainisha kuwa wabunge wa CCM wasiozidi 300 hawawezi kuzuia maoni ya Watanzania wasiopungua milioni 40 na endapo watafanya hivyo watakuwa wanamwelekeza rais kuvunja Bunge. "Wabunge wa CCM wakumbuke kwamba serikali imepeleka muswada huo kwao si kwa sababu yametolewa mapendekezo na CHADEMA au chama cha siasa tu, umejadiliwa na Watanzania wengi. "Kama kweli wataugomea na kuurudisha kwa rais tena, rais anaweza kuamua kuvunja Bunge kwa mujibu wa Katiba," alisema.

Dk. Slaa alisema anashangazwa sana na wabunge wa CCM ambao wamekuwa wakijigamba kwamba serikali inayoongozwa na chama chao ni sikivu halafu hao hao tena washindwe kutekeleza yaliyofikiwa na serikali hiyo hiyo. Alisema wabunge ni lazima waonyeshe uzalendo wao kwa Watanzania kwa kujadili muswada wa mabadiliko ya sheria badala ya kushindana na mamlaka ya rais


SOURCE:TANZANIA DAIMA
 
Ningefurahi kama JF tungepata copy ya mswaada huo in Swahili.
Nina uhakika hakuna mabadiliko ya maana yaliyofanywa... but I stand to be corrected.
 
inasemekana wabunge wa CCM hawana shida na huo muswada,ila wanachotaka JK aridhie posho zao ndo kila kitu kitaenda sawa.Mkono mtupu haulambwi ati!

hahaa haaaa wana hali ngumu ile mbaya hao wabunge wa CCM, ndio maana wanalilia nyongeza ya posho, walichukua mikopo wakati wa kampeni, unakuta sasa hivi wakati wa kuirejesha wanakatwa mpaka wengine wanabaki na laki 2... Hahaa haaa kwanini wasikomalie nyongeza ya Posho?
 
Hivi wabunge wa chadema waliposusia bunge walikosa uzalendo? Na kama ndivyo dr Slaa alichukua hatua gani?
 
slaa nae kichwa chake kama katuni . Eti wabunge wasiozidi mia tatu watakuwa wamekataa maoni ya watanzania milion arobain, hivi hao watanzania wako mfukon mwake,au mdomoni mwake yeye ameonana lini na watanzania wengi kuliko walionana na wawakilishi milion arobain. Wabunge ni wawakilishi wa kikatiba wa wananchi je slaa anqmwakilisha nani. Masaburi makubwa kichwani
 
Hivi wabunge wa chadema waliposusia bunge walikosa uzalendo? Na kama ndivyo dr Slaa alichukua hatua gani?

Fuatilia tena walichosusia halafu linganisha na wa CCM wanachotaka kususia kisha utapata jibu kwa urahisi kuliko unavyoelewa sasa.
 
slaa nae kichwa chake kama katuni . Eti wabunge wasiozidi mia tatu watakuwa wamekataa maoni ya watanzania milion arobain, hivi hao watanzania wako mfukon mwake,au mdomoni mwake yeye ameonana lini na watanzania wengi kuliko walionana na wawakilishi milion arobain. Wabunge ni wawakilishi wa kikatiba wa wananchi je slaa anqmwakilisha nani. Masaburi makubwa kichwani

kapige mswaki kwanza...asubuhi asubuhi unakurupuka na kuanza kuongea..kwa mujibu wa katiba mswada ukirudishwa kwa rais kwa mara ya pili,ndani ya siku 21 anatakiwa kuvunja bunge...chadema walipoenda kumuona rais,hao hao wabunge wa ccm wakamshauri akutane na vyama vyote,vyama vyote vilitoa maoni ikulu(at least vilivyotaka kutoa maoni)wakiwemo wao ccm,sasa inakuwaje watake kugomea mswada...naamini tatizo sio mswada,tatizo ni posho..
 
slaa nae kichwa chake kama katuni . Eti wabunge wasiozidi mia tatu watakuwa wamekataa maoni ya watanzania milion arobain, hivi hao watanzania wako mfukon mwake,au mdomoni mwake yeye ameonana lini na watanzania wengi kuliko walionana na wawakilishi milion arobain. Wabunge ni wawakilishi wa kikatiba wa wananchi je slaa anqmwakilisha nani. Masaburi makubwa kichwani

Sio lazima kumuonyesha kila mtu kuwa wewe ni zezeta! Usingeleta upupu wako huu usingejulikana kuwa wewe ni zezeta.
 
slaa nae kichwa chake kama katuni . Eti wabunge wasiozidi mia tatu watakuwa wamekataa maoni ya watanzania milion arobain, hivi hao watanzania wako mfukon mwake,au mdomoni mwake yeye ameonana lini na watanzania wengi kuliko walionana na wawakilishi milion arobain. Wabunge ni wawakilishi wa kikatiba wa wananchi je slaa anqmwakilisha nani. Masaburi makubwa kichwani

Mods-Ilishakubalika hapa Masaburi ni matusi tunaomba haki itendeke kwa wote
 
kapige mswaki kwanza...asubuhi asubuhi unakurupuka na kuanza kuongea..kwa mujibu wa katiba mswada ukirudishwa kwa rais kwa mara ya pili,ndani ya siku 21 anatakiwa kuvunja bunge...chadema walipoenda kumuona rais,hao hao wabunge wa ccm wakamshauri akutane na vyama vyote,vyama vyote vilitoa maoni ikulu(at least vilivyotaka kutoa maoni)wakiwemo wao ccm,sasa inakuwaje watake kugomea mswada...naamini tatizo sio mswada,tatizo ni posho..

Hawa wabunge wa ccm walitaka kumblackmail mwenyekiti /Rais kuwa ule muswada utakwama kama asingeridhia matakwa yao ya posho; sasa mwenzao kawastukia na kuwaelimisha kuwa hicho kitendo chao kinaweza kumfanya avunje bunge!! Ikabidi wanywee kwani bunge likivunjwa na wao wanamadeni lukuki,pia hawana uhakika wa kurudi mjengoni ingekuwa imekula kwao!! Hawa vilaza hawaoni mbali zaidi ya pua zao.
 
Nikwamba Magamba kwaö wanaona aibu tupu. Wakigomea muswada aibu na pia wakiujadili na wakaupitisha ni aibu kwa vile wanadai ni mapendekezo ya cdm. Wapo njiapanda.
 
Mnawakumbuka Wanaharakati? Tulisema mswaada wa Katiba usisomwe kwa mara ya pili. Sasa leo mbona kila mtu anaweweseka? Bado shughuli ndio kwanza inaanza,lazima tutoane ngeu kwanza
 
slaa nae kichwa chake kama katuni . Eti wabunge wasiozidi mia tatu watakuwa wamekataa maoni ya watanzania milion arobain, hivi hao watanzania wako mfukon mwake,au mdomoni mwake yeye ameonana lini na watanzania wengi kuliko walionana na wawakilishi milion arobain. Wabunge ni wawakilishi wa kikatiba wa wananchi je slaa anqmwakilisha nani. Masaburi makubwa kichwani
we
ni mtoto mdogo sana ndo maana mawazo yako ni ya kitoto...ndo shida ya intgernet za bure dada akirudi kazini basi kuchezea laptop yake mpaka mnapost mautumbo haya...hebu tupishe hapa
 
mmmh! Pengine ni namna yangu ya kufikiri! Mi nahisi kama Slaa sasa unanichanganya! Kwani wao wakigoma si nao pia wanatumia haki yao ya kutoa maoni kama Ndugu zetu wanapotoka bungeni wasipokubaliana na jambo? Au unataka kusema wapinzani wakitoka bungeni huwa ni tisha toto maana mnajua hakuna lolote litabadilika kutokana na namba? Au huwa ni kiini macho tu? Watanzania tufikiri kweli ni watetezi? Kauli yako imekaa kichama tawala kuliko upande wa pili...au? Kama wanagoma si wagome tu! Si ndio itaonyesha mmewatingisha?
 
slaa nae kichwa chake kama katuni . Eti wabunge wasiozidi mia tatu watakuwa wamekataa maoni ya watanzania milion arobain, hivi hao watanzania wako mfukon mwake,au mdomoni mwake yeye ameonana lini na watanzania wengi kuliko walionana na wawakilishi milion arobain. Wabunge ni wawakilishi wa kikatiba wa wananchi je slaa anqmwakilisha nani. Masaburi makubwa kichwani

A.S.S Crap
 
hahaa haaaa wana hali ngumu ile mbaya hao wabunge wa CCM, ndio maana wanalilia nyongeza ya posho, walichukua mikopo wakati wa kampeni, unakuta sasa hivi wakati wa kuirejesha wanakatwa mpaka wengine wanabaki na laki 2... Hahaa haaa kwanini wasikomalie nyongeza ya Posho?

Sio wa CCM tu kwa taarifa yako hata CDM wabunge wao wako hoi , wamekopa kwenye mabenki. Mfano, Mnyika Tshs 200m (CRDB), Selasini Tshs 210m (CRDB)

 
Back
Top Bottom