Ninamheshimu sana Dr.W.Slaa kwa utendaji uliotukuka na moyo alioonesha wa uzalendo. Ndiyo maana kila wakati napenda kutoa angalizo kwake kuhusu uhakiki wa habari kabla hajazitolea tamko. Nasema hivi kwa sababu pindi atakapokuwa Rais, itakuwa aibu kubwa kwa Taifa Tanzania kuwa na kiongozi anayekurupuka katika kauli zake. Ni aibu sana.
Pata picha Dr.Slaa anahutubia UN pale New York halafu anatoa statements ambazo ni za kubahatisha, dunia itatuangalia kwa jicho gani? Au utakuwa ndiyo wakati sasa Tanzania ikiwa ni zamu yake kuhutubia,wajumbe wanaona ndiyo muda muafaka wa kuvuta sigara nje? Ndiyo!! wenzetu wanathamini sana taarifa zilizo sahihi na kuhakikiwa.
W.Slaa bado anayo nafasi nzuri ya kujirekebisha katika kutoa kauli ambazo zinaleta upotoshaji. Huhitaji kutoa kauli za kubahatisha ili hadhira ikukubali,, toa tu taarifa sahihi watu watakupenda bado. Akiweza hilo, sifa zingine tayari anazo.
Huwa nashangaa pindi tunapoandika posts za kumkosoa Dr.SLAA zinafutwa au kutishiwa kufungiwa, na kumwagiwa matusi kedekede. Kumkosoa Slaa ni kumjenga na kumsaidia. Sasa ikiwa tutamsifia tu, si yatakuwa yaleyale, mgema akisifiwa tembo hulitia maji? Sasa kama unaogopa kumkosoa au kumpa ushauri leo,, akiwa Rais utaweza?
Tujenge utamaduni wa kukosoa viongozi pasina woga wala uadui.
Pata picha Dr.Slaa anahutubia UN pale New York halafu anatoa statements ambazo ni za kubahatisha, dunia itatuangalia kwa jicho gani? Au utakuwa ndiyo wakati sasa Tanzania ikiwa ni zamu yake kuhutubia,wajumbe wanaona ndiyo muda muafaka wa kuvuta sigara nje? Ndiyo!! wenzetu wanathamini sana taarifa zilizo sahihi na kuhakikiwa.
W.Slaa bado anayo nafasi nzuri ya kujirekebisha katika kutoa kauli ambazo zinaleta upotoshaji. Huhitaji kutoa kauli za kubahatisha ili hadhira ikukubali,, toa tu taarifa sahihi watu watakupenda bado. Akiweza hilo, sifa zingine tayari anazo.
Huwa nashangaa pindi tunapoandika posts za kumkosoa Dr.SLAA zinafutwa au kutishiwa kufungiwa, na kumwagiwa matusi kedekede. Kumkosoa Slaa ni kumjenga na kumsaidia. Sasa ikiwa tutamsifia tu, si yatakuwa yaleyale, mgema akisifiwa tembo hulitia maji? Sasa kama unaogopa kumkosoa au kumpa ushauri leo,, akiwa Rais utaweza?
Tujenge utamaduni wa kukosoa viongozi pasina woga wala uadui.