Elections 2010 Dr slaa atachaguliwa lakini hatashinda

Gurudumu

JF-Expert Member
Feb 5, 2008
2,349
261
Nimetoka mazoezini sasa hivi. Nilipitia kibanda cha magazeti kununua machache. Kulikuwa na watu 8 niliokadiria umri wao kuwa Kati ya miaka 25 hadi 40. Mjadala ulikuwepo wenye hisia mchanganyiko kati ya furaha, hasira, matumaini, na kukata tamaa. Ilikuwa hivi;

mtu1. Yaani leo sijalala, hakiamungu. Furaha, mimi nilikuwa namsoma slaa kwenye magazeti tu na kwenye tv wanamtoa sentensi moja au mbili. Jana anaulizwa maswali live yani anajibu chap chap na majibu yake yameenda shule na yanaingia akilini. Yaani siamini, si mchezo mwanagu. Ulimwona?

Mtu 2: Mimi husikiliza zile hotuba za kikwete za kwenye tv za kila siku, sijui huwa ccm wanazilipia? Yaani Kama ulimsikiliza Slaa unagungua kikwete ni mzitooo! Anaongea Kama babu aliyeshiba mnazi anasimulia wajukuu hadithi jikoni usiku, na wajukuu wenyewe wanasinzia.

Mtu 1: nakuambia tusubiri hiyo tarehe 31, mimi nikitoka kupiga kura nakaa na radio yangu na kalamu na daftari, kuandika matokeo nchi nzima.

Mtu 3: shida ya ccm wapiga kura ni wengi mwaka huu kuliko wanachama wa ccm. Wengi vijana ambao hawajawahi kuhudhuria semina za ccm na kulipwa posho. Wanataka mustakabali wa maisha yao, wanahangaika maisha magumu, ccm haina majibu yenye akili.

Mtu 4: tumia dayansi bwana, sisi wazoefu. Vijana hawawezi kushinda kwenye foleni jua kali ili wapige kura. Hawatulii, wana mambo mengi biashara nini starehe, siyo rahisi. Lakini wazee, wamama? Yuko radhi kukaa tangu asubuhi hadi usiku hata bila kula.

(kunakuwepo ukimya fulani baadhi wakitikisa vichwa kuafiki)

mtu 5: lakini mnawajua ccm katika kuiba kura?

Mtu 1: Slaa kasema kila mtu alinde kura, Tena anasema mbona karatu, musoma, kigoma, na moshi wameweza kulinda kura?

Mtu 6: mnajidanganya, taratibu zimeshabadilika. Utalindaje kura wakati umeambiwa ukishapiga kura nenda nyumbani. Hakuna tena mambo ya kukaa mita 100. Unafikiri wao wajinga. Hao mawakala wenu watawekwa sawa, na nyie mtabaki kulalamika tu.

(kunatokea mjadala wa hasira kali wengine wakionesha kukata tamaa)

Kwa hiyo, iko wazi kwamba dr slaa atachaguliwa. Je, atashinda?
 
Mtu 6: mnajidanganya, taratibu zimeshabadilika. Utalindaje kura wakati umeambiwa ukishapiga kura nenda nyumbani. Hakuna tena mambo ya kukaa mita 100. Unafikiri wao wajinga. Hao mawakala wenu watawekwa sawa, na nyie mtabaki kulalamika tu.

Ulipaswa uwaelimishe ya kuwa NEC imesema ni rukhsa kwa wapigakura kuwa mita 100 kutoka katika vituo vya kupigia kura kujihakikishia haki ikitendeka....Ulitakiwa uwaelimishe hilo ili huo mkanganyiko usingelitokea...
 
haya ndiyo niliyokuwa nayo ugomvu wiki iliyopoita.. kuimba sana CCM wataiba kura watakatisha watu tamaa..
 
Uchaguzi wa mwaka huu ni so interesting:-

Ni

strong candidate of a rather not strong party against Strong party but Candidate not the Best!

Ni mgumu kwa kuwa hauwezi kulinganisha apple to apple....
 
Nakubali sikuwaelimisha, lakini hata Mimi sikujua kwamba tume ilirudisha msimamo huu, Asante kuniarifu

Mkuu MM, nakubaliana na mantiki yako, only if vote rigging was not yet widely believed. Kwa kuwa kwa sasa ndiyo hofu ya wapiga kura wengi, kunahitajika constant authoritative mass clarification kuanzia sasa had siku ya kupiga kura. Short of this, all hopes and desire for change will only be just that.
 
yani mimi kuna mzee mmoja wa ccm nimegombana nae kuhusu hayo maswala hadi mwisho wa siku akaniambia kuwa wasomi wa chuo kikuu tutaishi kwa tabu iwapo serikali ya ccm itaingia madarakani maana tunawasumbua sana tunajifanya tunaijua nchi nami nikamjibu iwapo ccm itaingia madarakani itaujutia uongozi wake milele maana watanzania wamechoshwa na uonevu wao
 
Uchaguzi wa mwaka huu ni so interesting:-

Ni

strong candidate of a rather not strong party against Strong party but Candidate not the Best!

Ni mgumu kwa kuwa hauwezi kulinganisha apple to apple....

Safi sana Kasheshe inaonekana mdahalo wa jana umekufanya umkubali Slaa. Maana kukiri hadharani kwamba Slaa ni strong candidata in a weak party inatosha kusema kwamba upo tayari kumpa kura yako. Party siyo shida kwa kuwa Tanzania na watanzania siyo mali ya chama. Utekelezaji wa majukumu ya serikali utafanywa na watanzania na si CHADEMA. Mchague Slaa na karibu nyumbani Kasheshe.
 
Uko sawa Dr slaa atapigiwa kura lakini hata shinda kuwa Rais na hata yeye anaonesha kukata tamaaa.
 
HAMNA MTU ALIYEKATA TAMAA, ushindi chadema itashinda kutoka mwaka huu watu wamejiandaa tofauti na 1995, huu ni mwaka wa mabadiliko vijana wengi wamajiandikisha tofauti na miaka mingine
 
Kura hazitaibiwa kama sisi tutasimama imara kulinda tukishapiga kura tukae 100 mitres hadi matokeo yabandikwe nje ya kituo hili litazuia mtu mwenye nia ya kuiba/ kurubuni wasimamizi/mawakala hadi matokeo yatoke. kuwana mawazo negative ni kweli tutawakatyisha tamaa wapigakura.
 
Sasa kuna huo mkanganyiko kuhusu kukaa mita 100 na kupiga kura na kwenda nyumbani. Je, uongozi wa chadema utatoa kauli kuweka sawa Hilo?
 
Mabadiliko ambayo watanzania wanayaona yanakuja ni sauti ya Mungu, na hakuna mtu wa kuyazuia, ccm wakijaribu kuyazuia wanaiingiza nchi katika maangamizi makubwa. Tunawaomba wasitupeleke huko kwa manufaa ya nchi yetu, tusikilize sauti ya Mungu, na tayari ameshatupatia viashiria.
 
Kama atachaguliwa maana yake si atashinda?
Hakuna wasiwasi ni kusubiri tu kumwapisha,maana kila mtanzania sasa ameshachoka na ccm
hat hao wanaohudhuria mikutano ya kikwete ni kupata tu burudani za bure lakini hawamchaguo ng'o
nimetoka mazoezini sasa hivi. Nilipitia kibanda cha magazeti kununua machache. Kulikuwa na watu 8 niliokadiria umri wao kuwa kati ya miaka 25 hadi 40. Mjadala ulikuwepo wenye hisia mchanganyiko kati ya furaha, hasira, matumaini, na kukata tamaa. Ilikuwa hivi;

mtu1. Yaani leo sijalala, hakiamungu. Furaha, mimi nilikuwa namsoma slaa kwenye magazeti tu na kwenye tv wanamtoa sentensi moja au mbili. Jana anaulizwa maswali live yani anajibu chap chap na majibu yake yameenda shule na yanaingia akilini. Yaani siamini, si mchezo mwanagu. Ulimwona?

Mtu 2: Mimi husikiliza zile hotuba za kikwete za kwenye tv za kila siku, sijui huwa ccm wanazilipia? Yaani kama ulimsikiliza slaa unagungua kikwete ni mzitooo! Anaongea kama babu aliyeshiba mnazi anasimulia wajukuu hadithi jikoni usiku, na wajukuu wenyewe wanasinzia.

Mtu 1: Nakuambia tusubiri hiyo tarehe 31, mimi nikitoka kupiga kura nakaa na radio yangu na kalamu na daftari, kuandika matokeo nchi nzima.

Mtu 3: Shida ya ccm wapiga kura ni wengi mwaka huu kuliko wanachama wa ccm. Wengi vijana ambao hawajawahi kuhudhuria semina za ccm na kulipwa posho. Wanataka mustakabali wa maisha yao, wanahangaika maisha magumu, ccm haina majibu yenye akili.

Mtu 4: Tumia dayansi bwana, sisi wazoefu. Vijana hawawezi kushinda kwenye foleni jua kali ili wapige kura. Hawatulii, wana mambo mengi biashara nini starehe, siyo rahisi. Lakini wazee, wamama? Yuko radhi kukaa tangu asubuhi hadi usiku hata bila kula.

(kunakuwepo ukimya fulani baadhi wakitikisa vichwa kuafiki)

mtu 5: Lakini mnawajua ccm katika kuiba kura?

Mtu 1: Slaa kasema kila mtu alinde kura, tena anasema mbona karatu, musoma, kigoma, na moshi wameweza kulinda kura?

Mtu 6: Mnajidanganya, taratibu zimeshabadilika. Utalindaje kura wakati umeambiwa ukishapiga kura nenda nyumbani. Hakuna tena mambo ya kukaa mita 100. Unafikiri wao wajinga. Hao mawakala wenu watawekwa sawa, na nyie mtabaki kulalamika tu.

(kunatokea mjadala wa hasira kali wengine wakionesha kukata tamaa)

kwa hiyo, iko wazi kwamba dr slaa atachaguliwa. Je, atashinda?
 
Back
Top Bottom