rosemarie
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 6,887
- 3,412
Histori inaonyesha wazi kwamba Viongozi wa Africa wanajaribu kugombea zaidi ya mara moja na wengi wao wanafanikiwa kuingia madarakani kwa sababu waligombea zaidi ya mara moja
mfano mzuri ni John Atta Mills wa Ghana,yeye aligombea mara tatu na akaibuka mshindi mara ya tatu
tunaona kwamba mgombea akigombea mara ya kwanza anakuwa kama anauza zaidi jina lake na uwezo wake kwamba anaweza kuongoza,mara ya pili anakuwa amekubalika kwa watu ambao hawakumkubali mara ya kwanza,
maana yangu ni kwamba Dr Slaa ana uwezo mkubwa wa kushinda kwa kuwa amekubalika zaidi tangu mara baada ya uchaguzi mkuu 2010,Chadema ikifanya makosa na kumsimamisha mtu mwingine itakuwa ni ngumu mno kushinda kwani inakuwa ni mara ya kwanza na historia inaonyesha jinsi ilivyo ngumu mpinzani kushika madaraka kwa mara ya kwanza
Rais Sata alishagombea zaidi ya mara mbili,na Wazambia walipata nafasi ya kumjadili kwa kuwa alithubutu mara ya kwanza na ya pili na kuwaonyesha wapiga kura kwamba ninaweza
alipokuja tena mara ya tatu alisomba kura zote kwani alishajijenga ndani ya mioyo ya wapiga kura kwamba anaweza
Uchaguzi wa madiwani umetufundisha kitu,Chadema mna kazi ya ziada,kukurupuka na kupiga kelele hakusaidii tena,ebu tukae chini tuanze kila kitu upya,fundisho hili ni kubwa mno kwetu wapenda mabadiliko,tulitegemea Chadema kuchukua zaidi ya kata 15,kazi inaendelea
mfano mzuri ni John Atta Mills wa Ghana,yeye aligombea mara tatu na akaibuka mshindi mara ya tatu
tunaona kwamba mgombea akigombea mara ya kwanza anakuwa kama anauza zaidi jina lake na uwezo wake kwamba anaweza kuongoza,mara ya pili anakuwa amekubalika kwa watu ambao hawakumkubali mara ya kwanza,
maana yangu ni kwamba Dr Slaa ana uwezo mkubwa wa kushinda kwa kuwa amekubalika zaidi tangu mara baada ya uchaguzi mkuu 2010,Chadema ikifanya makosa na kumsimamisha mtu mwingine itakuwa ni ngumu mno kushinda kwani inakuwa ni mara ya kwanza na historia inaonyesha jinsi ilivyo ngumu mpinzani kushika madaraka kwa mara ya kwanza
Rais Sata alishagombea zaidi ya mara mbili,na Wazambia walipata nafasi ya kumjadili kwa kuwa alithubutu mara ya kwanza na ya pili na kuwaonyesha wapiga kura kwamba ninaweza
alipokuja tena mara ya tatu alisomba kura zote kwani alishajijenga ndani ya mioyo ya wapiga kura kwamba anaweza
Uchaguzi wa madiwani umetufundisha kitu,Chadema mna kazi ya ziada,kukurupuka na kupiga kelele hakusaidii tena,ebu tukae chini tuanze kila kitu upya,fundisho hili ni kubwa mno kwetu wapenda mabadiliko,tulitegemea Chadema kuchukua zaidi ya kata 15,kazi inaendelea