Dr. Slaa anasa nyaraka za siri za CCM za kuingiza silaha nchini

Mikael Aweda

JF-Expert Member
Dec 17, 2010
2,973
3,901
Wakuu,
Gazeti la Tz daima leo limeibuka na taarifa ya Dr Slaa kudai kuwa anazo nyaraka za siri za ccm kuagiza na kuingiza silaha kwa ajili ya vijana wa ccm waliowekwa ktk makambi mbali mbali hapa nchini. Lengo la vijana hao ni kudhibiti Chadema. Dr Slaa anasema tunaposema kuwa ccm imedhamiria kufanya vurugu hatutanii, tuko serious.
wakati huo huo,
Gazeti limeelezea pia kwa urefu maelezo ya Dr Slaa na msafara wake kufuatiliwa ktk operesheni yake ya M4C na gari lisiloeleweka. Kufuatilia hali hiyo Dr Slaa aliwaagiza idara ya ulinzi kutoa taarifa polisi ktk wilaya husika lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyiwa kazi.
Gazeti pia lilimpigia simu Nape Nnauye kuhusu madai hayo naye akakana. Akifafanua Nape alisema, Dr Slaa mwongo mbona makontena ya kura za wizi alizosema zimeingizwa nchini hazijaonekana?

My take.
Nape, absence of evidence is not evidence for absence of evidence. Kutokuonekana kwa ushahidi si ushahidi wa kubatilisha mashitaka. Je, kama makontena hayo yamefichwa baada ya siri kuvuja ni nani ajuaye? Ukizingitia kuwa polisi wetu wameshakuwa policcm.

UPDATE,
HABARI KAMILI HII HAPA KWA UREFU

Aituhumu kuingiza nchini silaha kimyakimya
*Asema lengo lake ni kutaka kuihujumu Chadema
KATIBU Mkuu wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, kwa mara nyingine tena ameibua tuhuma nzito dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Dk. Slaa amedai kuwa, anazonyaraka zinazoonyesha namna chama hicho tawala kinavyoingiza silaha nchini zikiwamo bunduki bila vibali wala kuzikatia leseni.

Dk. Slaa alisema, CCM inaingiza silaha hizo na kuwapatia vijana wake waliowekwa katika kambi maalumu, kwa ajili ya kufundishwa mbinu za kuwashughulikia wapinzani wao kisiasa hususan
Chadema.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Morogoro wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea tathmini ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), pamoja na Operesheni Sangara iliyoanza mkoani hapa Agosti 8 mwaka huu.

"Kwa hapa Morogoro mjini tunazo taarifa, tumeshaambiwa kuna vijana kama 10-20 wa CCM wanaandaliwa kufanya njama za kuhujumu CHADEMA.

"Watavalishwa kombati kama hizi za kwetu, watafanya fujo ili ionekane ni sisi, wamepewa sumu, tindikali na sindano kwa ajili ya kukamilisha hizo hujuma wanazopanga dhidi yetu.

"Kwa baadhi yetu tunaowafahamu CCM, hili si suala jipya, walifanya hivyo hivyo wakati wa uchaguzi mdogo Igunga, moja ya kambi yao ilikuwa Ilemo na Iramba.

"Huu ndio mtindo wao, wana tabia ya kuingiza hata bunduki nchini bila kibali wala leseni wanapatia vijana, kisha wakishafanya hivyo wanajiandaa kuhamishia tuhuma
CHADEMA.

"Mtakumbuka Wilson Mukama (katibu mkuu CCM) aliwahi kutamka wakati ule tukiwa Igunga kuwa, tumeingiza makomandoo nchini, alisema hadharani.

"Kumbe wao tayari wameshaweka vijana kambini na wanafundisha, tena waliohusika kufundisha ni polisi na usalama wa taifa. Tulitoa taarifa polisi juu ya masuala yote na ushahidi tukawapatia wafuatilie, lakini mpaka leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa," alisema Dk. Slaa.

Dk. Slaa alisema kuwa, chama chake hakitatoa taarifa polisi juu ya njama hizo za vijana kuandaliwa na wala hakina mpango wowote wa kuishitaki CCM kwa njama za kukihujumu.

Dk. Slaa alisema, kufanya hivyo ni sawa na kupeleka kesi ya nyani kwa ngedere, ingawa alisisitiza kuwa wakati utakapofika wataweka hadharani nyaraka hizo.

Aliongeza kuwa, kudhihirisha CCM hawatanii katika kutaka kufanya vurugu, hivi karibuni kumekuwa na matukio ya msafara wao kuandamwa na watu wasiojulikana.

Dk. Slaa alisema, watu hao wamekuwa wakitumia magari tofauti na kueleza kuwa, juzi wakiwa wanatoka Gairo, Gari lenye namba T886 AVS aina ya Prado lilikuwa likiwafuatilia.

"Juzi walifanya hivyo tukiwa Mvomero tukatoa taarifa Polisi jana na leo asubuhi tumepata taarifa ambazo hatuwezi kuzipuuza kuwa, kuna vijana kuanzia 10-20 wakiwa na Sumu Sindano pamoja na visu, wanawawinda watu walio katika operesheni kwa ajili ya kuwadhuru, "alisema Dk Slaa.
 
Slaa achana na kuitegemea Polisi wala usalama wa Taifa kwa usalama wako na familia yako mimi ni mmoja wa watu ambao siwategemei tena Polisi na usalama wa Taifa kwa usalama wangu na Familia yangu, nimeamua kuwategemea na kuwekeza zaidi katika ulinzi binafsi, wee unategemea mtu kama Dr Ulimboka asingebweteka kuwategemea Polisi kwa ulinzi wake yangemkuta yaliyomkuta? Au nchi ingekuwa kweli ina watu wa usalama leo hii ingeshindwa kuyakamata mabilioni yaliyowekwa na mafisadi Uswisi?
 
Naona machine ya Lister Peter (Tanzania daima) inaendelea kumwaga pumba, hivi ni kweli Dr Slaa anaweza kutamka uupzi wa aina hii au wakati anazungumza sukari ilikuwa imepanda?
 
Magazeti ifikie hatua muwe mnaelewa aina ya majibu mtakayopata wakati wa kuthibitisha habari kabla hata ya kuuliza. Ukimuuliza Nape issue yoyote ya Dr Slaa lazima ataweweseka na kutoa majibu ya ku-panic, heri wangeruka kwa mwenye mbwa Mukama mwenyewe aliyewahi kutuletea ushahidi wa maghaidi toka Libya na Pakistani walioingia Igunga.
 
Sipati picha Chama cha Mabwepande wakiwa wapinzani,sasa unapita pale mnazi mmoja unakuta wale waganga njaa wamekaa wanasubiri amri waende kupiga domo mitaani na kuzua mikutano kwa kuwabeba wananchi na pesa ndogo ndogo(kama wataweza tena)....watakimbiana hawa wanafiki wote tutawaona live maana sasa wanajificha kwenye kutoa povu
 
Wakuu,
Gazeti la Tz daima leo limeibuka na taarifa ya Dr Slaa kudai kuwa anazo nyaraka za siri za ccm kuagiza na kuingiza silaha kwa ajili ya vijana wa ccm waliowekwa ktk makambi mbali mbali hapa nchini. Lengo la vijana hao ni kudhibiti Chadema. Dr Slaa anasema tunaposema kuwa ccm imedhamiria kufanya vurugu hatutanii, tuko serious.
wakati huo huo,
Gazeti limeelezea pia kwa urefu maelezo ya Dr Slaa na msafara wake kufuatiliwa ktk operesheni yake ya M4C na gari lisiloeleweka. Kufuatilia hali hiyo Dr Slaa aliwaagiza idara ya ulinzi kutoa taarifa polisi ktk wilaya husika lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyiwa kazi.
Gazeti pia lilimpigia simu Nape Nnauye kuhusu madai hayo naye akakana. Akifafanua Nape alisema, Dr Slaa mwongo mbona makontena ya kura za wizi alizosema zimeingizwa nchini hazijaonekana?

My take.
Nape, absence of evidence is not evidence for absence of evidence. Kutokuonekana kwa ushahidi si ushahidi wa kubatilisha mashitaka. Je, kama makontena hayo yamefichwa baada ya siri kuvuja ni nani ajuaye? Ukizingitia kuwa polisi wetu wameshakuwa policcm.

MAWEEEEEEEEEE!!!! Jamani haya sio yale Mambo ya Mstaafu NGUNGURI Kua chama cha kina YAKHEEE KIMEINGIZA MAKONTENA YA MAJAMBIA KUVURUGA AMANI. NA SAMPLE TUKA ONYWESHWA. YAANI WAO MAJAMBIA POLISI BUNDUKI. JAMANI?
LEO TENA CHICHIEM WANAANDAA VIJANA WOA. YAANI WAPAMBANE NA JW AU POLISI? MMMMHHHH! AMAKWELI SISI WADANGANYIKA.
 
Kuna mtu jana aliibuka na thread humu kwamba kuna silaha zimeletwa kwa ajili ya kuwabambikia CDM. Naona Mods waliifuta. Haya mambo ya kutishana na silaha si mazuri. Dr. weka mambo hadharani isije ikawa ni kama ile signature ya Ritz hapa JF
 
Last edited by a moderator:
yule mzee wa vimwana ana uchu sana na urais,yaani hadi leo haamini kuwa alishindwa kwenye uchaguzi mkuu uliopita kwa hiyo kila siku anaibuka na uzushi mpya.wajinga ndio wadanganyikao
 
Kurasa 1 kati ya 3
wilbrod%20slaa.jpg
Dk. Wilbrod Slaa

*Aituhumu kuingiza nchini silaha kimyakimya
*Asema lengo lake ni kutaka kuihujumu Chadema
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, kwa mara nyingine tena ameibua tuhuma nzito dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Dk. Slaa amedai kuwa, anazonyaraka zinazoonyesha namna chama hicho tawala kinavyoingiza silaha nchini zikiwamo bunduki bila vibali wala kuzikatia leseni.

Dk. Slaa alisema, CCM inaingiza silaha hizo na kuwapatia vijana wake waliowekwa katika kambi maalumu, kwa ajili ya kufundishwa mbinu za kuwashughulikia wapinzani wao kisiasa hususan Chadema.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Morogoro wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea tathmini ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), pamoja na Operesheni Sangara iliyoanza mkoani hapa Agosti 8 mwaka huu.

“Kwa hapa Morogoro mjini tunazo taarifa, tumeshaambiwa kuna vijana kama 10-20 wa CCM wanaandaliwa kufanya njama za kuhujumu CHADEMA.

“Watavalishwa kombati kama hizi za kwetu, watafanya fujo ili ionekane ni sisi, wamepewa sumu, tindikali na sindano kwa ajili ya kukamilisha hizo hujuma wanazopanga dhidi yetu.

“Kwa baadhi yetu tunaowafahamu CCM, hili si suala jipya, walifanya hivyo hivyo wakati wa uchaguzi mdogo Igunga, moja ya kambi yao ilikuwa Ilemo na Iramba.

“Huu ndio mtindo wao, wana tabia ya kuingiza hata bunduki nchini bila kibali wala leseni wanapatia vijana, kisha wakishafanya hivyo wanajiandaa kuhamishia tuhuma CHADEMA.

“Mtakumbuka Wilson Mukama (katibu mkuu CCM) aliwahi kutamka wakati ule tukiwa Igunga kuwa, tumeingiza makomandoo nchini, alisema hadharani.

“Kumbe wao tayari wameshaweka vijana kambini na wanafundisha, tena waliohusika kufundisha ni polisi na usalama wa taifa. Tulitoa taarifa polisi juu ya masuala yote na ushahidi tukawapatia wafuatilie, lakini mpaka leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa,” alisema Dk. Slaa.

Dk. Slaa alisema kuwa, chama chake hakitatoa taarifa polisi juu ya njama hizo za vijana kuandaliwa na wala hakina mpango wowote wa kuishitaki CCM kwa njama za kukihujumu.

Dk. Slaa alisema, kufanya hivyo ni sawa na kupeleka kesi ya nyani kwa ngedere, ingawa alisisitiza kuwa wakati utakapofika wataweka hadharani nyaraka hizo.

Aliongeza kuwa, kudhihirisha CCM hawatanii katika kutaka kufanya vurugu, hivi karibuni kumekuwa na matukio ya msafara wao kuandamwa na watu wasiojulikana.

Dk. Slaa alisema, watu hao wamekuwa wakitumia magari tofauti na kueleza kuwa, juzi wakiwa wanatoka Gairo, Gari lenye namba T886 AVS aina ya Prado lilikuwa likiwafuatilia.

“Juzi walifanya hivyo tukiwa Mvomero tukatoa taarifa Polisi jana na leo asubuhi tumepata taarifa ambazo hatuwezi kuzipuuza kuwa, kuna vijana kuanzia 10-20 wakiwa na Sumu Sindano pamoja na visu, wanawawinda watu walio katika operesheni kwa ajili ya kuwadhuru, ”alisema Dk Slaa.
 
Kama tunakaribisha siasa chafu, basi tutegemee vita mbaya ya wenyewe kwa wenyewe.
 
yule mzee wa vimwana ana uchu sana na urais,yaani hadi leo haamini kuwa alishindwa kwenye uchaguzi mkuu uliopita kwa hiyo kila siku anaibuka na uzushi mpya.wajinga ndio wadanganyikao

Mkuu,
Umeenda vituo vya polisi ktk wilaya husika ili kujua kama ni kweli taarifa hizo zimepelekwa au la!
Je, una uhakika kiasi gani kwamba hizo nyaraka hana! Nyaraka za EPA mlisema hivyo, hivyo, mkaumbuka baadaye.
Hebu tupe, ameshasema kweli mara ngapi na uwongo mara ngapi ili ushawishi jukwaa hili likuamini wewe.
Unadhani kwanini watz wanamwanini sana mpaka akachakachuliwa kura? je, kwa kuwa ni mkweli au ni mzushi?
 
Wakuu,
Gazeti la Tz daima leo limeibuka na taarifa ya Dr Slaa kudai kuwa anazo nyaraka za siri za ccm kuagiza na kuingiza silaha kwa ajili ya vijana wa ccm waliowekwa ktk makambi mbali mbali hapa nchini. Lengo la vijana hao ni kudhibiti Chadema. Dr Slaa anasema tunaposema kuwa ccm imedhamiria kufanya vurugu hatutanii, tuko serious.
wakati huo huo,
Gazeti limeelezea pia kwa urefu maelezo ya Dr Slaa na msafara wake kufuatiliwa ktk operesheni yake ya M4C na gari lisiloeleweka. Kufuatilia hali hiyo Dr Slaa aliwaagiza idara ya ulinzi kutoa taarifa polisi ktk wilaya husika lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyiwa kazi.
Gazeti pia lilimpigia simu Nape Nnauye kuhusu madai hayo naye akakana. Akifafanua Nape alisema, Dr Slaa mwongo mbona makontena ya kura za wizi alizosema zimeingizwa nchini hazijaonekana?

My take.
Nape, absence of evidence is not evidence for absence of evidence. Kutokuonekana kwa ushahidi si ushahidi wa kubatilisha mashitaka. Je, kama makontena hayo yamefichwa baada ya siri kuvuja ni nani ajuaye? Ukizingitia kuwa polisi wetu wameshakuwa policcm.

ZZK kweli ni jembe aliwahu kuwaambia viongozi wenzake wa CHADEMA wabakize akiba ya maneno sasa leo inaonekana KIBABU KIBACHELA kimeishiwa hakina jipya hii single ya leo inabidi akaifanyie remix
 
Wakuu,
Gazeti la Tz daima leo limeibuka na taarifa ya Dr Slaa kudai kuwa anazo nyaraka za siri za ccm kuagiza na kuingiza silaha kwa ajili ya vijana wa ccm waliowekwa ktk makambi mbali mbali hapa nchini. Lengo la vijana hao ni kudhibiti Chadema. Dr Slaa anasema tunaposema kuwa ccm imedhamiria kufanya vurugu hatutanii, tuko serious.
wakati huo huo,
Gazeti limeelezea pia kwa urefu maelezo ya Dr Slaa na msafara wake kufuatiliwa ktk operesheni yake ya M4C na gari lisiloeleweka. Kufuatilia hali hiyo Dr Slaa aliwaagiza idara ya ulinzi kutoa taarifa polisi ktk wilaya husika lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyiwa kazi.
Gazeti pia lilimpigia simu Nape Nnauye kuhusu madai hayo naye akakana. Akifafanua Nape alisema, Dr Slaa mwongo mbona makontena ya kura za wizi alizosema zimeingizwa nchini hazijaonekana?

My take.
Nape, absence of evidence is not evidence for absence of evidence. Kutokuonekana kwa ushahidi si ushahidi wa kubatilisha mashitaka. Je, kama makontena hayo yamefichwa baada ya siri kuvuja ni nani ajuaye? Ukizingitia kuwa polisi wetu wameshakuwa policcm.

huu ni ujinga,uongo na uzushi mtakatifu.mwenye uwezo wa kuagiza silaha hapa nchini ni jeshi na polisi tu.yale makontena ya CUF yaliyokuwa na VISU yako wapi??yale makontena yalikuwa na kura kutokea msumbiji uako wapi???slaa acha cheap popularity,umechuja wewe.
 
Mkuu,
Umeenda vituo vya polisi ktk wilaya husika ili kujua kama ni kweli taarifa hizo zimepelekwa au la!
Je, una uhakika kiasi gani kwamba hizo nyaraka hana! Nyaraka za EPA mlisema hivyo, hivyo, mkaumbuka baadaye.
Hebu tupe, ameshasema kweli mara ngapi na uwongo mara ngapi ili ushawishi jukwaa hili likuamini wewe.
Unadhani kwanini watz wanamwanini sana mpaka akachakachuliwa kura? je, kwa kuwa ni mkweli au ni mzushi?

uongo wa kwanza ni pale alipodanganya kanisa kuwa atatii sheria za mungu matokeo yake akaasi.
pili alipoaminiwa na ROSE kamili matokeo yake akamtelekeza yeye pamoja na watoto akaanza uzinifu na Josephine

uongo mwingine ni huu kwamba CUF wameingiza kontena la visu na lile la kura kule mpakani na msumbiji
 
Majibu ya Nape ni swadakta Dr Slaa ni muongo mkubwa, mwizi, mnafiki, msaliti, na ugonjwa wa kisukari umeathiri ubongo wake kwa sehemu kubwa.
 
Back
Top Bottom