Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Wakuu,
Gazeti la Tz daima leo limeibuka na taarifa ya Dr Slaa kudai kuwa anazo nyaraka za siri za ccm kuagiza na kuingiza silaha kwa ajili ya vijana wa ccm waliowekwa ktk makambi mbali mbali hapa nchini. Lengo la vijana hao ni kudhibiti Chadema. Dr Slaa anasema tunaposema kuwa ccm imedhamiria kufanya vurugu hatutanii, tuko serious.
wakati huo huo,
Gazeti limeelezea pia kwa urefu maelezo ya Dr Slaa na msafara wake kufuatiliwa ktk operesheni yake ya M4C na gari lisiloeleweka. Kufuatilia hali hiyo Dr Slaa aliwaagiza idara ya ulinzi kutoa taarifa polisi ktk wilaya husika lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyiwa kazi.
Gazeti pia lilimpigia simu Nape Nnauye kuhusu madai hayo naye akakana. Akifafanua Nape alisema, Dr Slaa mwongo mbona makontena ya kura za wizi alizosema zimeingizwa nchini hazijaonekana?
My take.
Nape, absence of evidence is not evidence for absence of evidence. Kutokuonekana kwa ushahidi si ushahidi wa kubatilisha mashitaka. Je, kama makontena hayo yamefichwa baada ya siri kuvuja ni nani ajuaye? Ukizingitia kuwa polisi wetu wameshakuwa policcm.
UPDATE,
HABARI KAMILI HII HAPA KWA UREFU
Aituhumu kuingiza nchini silaha kimyakimya
*Asema lengo lake ni kutaka kuihujumu Chadema
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, kwa mara nyingine tena ameibua tuhuma nzito dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Dk. Slaa amedai kuwa, anazonyaraka zinazoonyesha namna chama hicho tawala kinavyoingiza silaha nchini zikiwamo bunduki bila vibali wala kuzikatia leseni.
Dk. Slaa alisema, CCM inaingiza silaha hizo na kuwapatia vijana wake waliowekwa katika kambi maalumu, kwa ajili ya kufundishwa mbinu za kuwashughulikia wapinzani wao kisiasa hususan Chadema.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Morogoro wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea tathmini ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), pamoja na Operesheni Sangara iliyoanza mkoani hapa Agosti 8 mwaka huu.
"Kwa hapa Morogoro mjini tunazo taarifa, tumeshaambiwa kuna vijana kama 10-20 wa CCM wanaandaliwa kufanya njama za kuhujumu CHADEMA.
"Watavalishwa kombati kama hizi za kwetu, watafanya fujo ili ionekane ni sisi, wamepewa sumu, tindikali na sindano kwa ajili ya kukamilisha hizo hujuma wanazopanga dhidi yetu.
"Kwa baadhi yetu tunaowafahamu CCM, hili si suala jipya, walifanya hivyo hivyo wakati wa uchaguzi mdogo Igunga, moja ya kambi yao ilikuwa Ilemo na Iramba.
"Huu ndio mtindo wao, wana tabia ya kuingiza hata bunduki nchini bila kibali wala leseni wanapatia vijana, kisha wakishafanya hivyo wanajiandaa kuhamishia tuhuma CHADEMA.
"Mtakumbuka Wilson Mukama (katibu mkuu CCM) aliwahi kutamka wakati ule tukiwa Igunga kuwa, tumeingiza makomandoo nchini, alisema hadharani.
"Kumbe wao tayari wameshaweka vijana kambini na wanafundisha, tena waliohusika kufundisha ni polisi na usalama wa taifa. Tulitoa taarifa polisi juu ya masuala yote na ushahidi tukawapatia wafuatilie, lakini mpaka leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa," alisema Dk. Slaa.
Dk. Slaa alisema kuwa, chama chake hakitatoa taarifa polisi juu ya njama hizo za vijana kuandaliwa na wala hakina mpango wowote wa kuishitaki CCM kwa njama za kukihujumu.
Dk. Slaa alisema, kufanya hivyo ni sawa na kupeleka kesi ya nyani kwa ngedere, ingawa alisisitiza kuwa wakati utakapofika wataweka hadharani nyaraka hizo.
Aliongeza kuwa, kudhihirisha CCM hawatanii katika kutaka kufanya vurugu, hivi karibuni kumekuwa na matukio ya msafara wao kuandamwa na watu wasiojulikana.
Dk. Slaa alisema, watu hao wamekuwa wakitumia magari tofauti na kueleza kuwa, juzi wakiwa wanatoka Gairo, Gari lenye namba T886 AVS aina ya Prado lilikuwa likiwafuatilia.
"Juzi walifanya hivyo tukiwa Mvomero tukatoa taarifa Polisi jana na leo asubuhi tumepata taarifa ambazo hatuwezi kuzipuuza kuwa, kuna vijana kuanzia 10-20 wakiwa na Sumu Sindano pamoja na visu, wanawawinda watu walio katika operesheni kwa ajili ya kuwadhuru, "alisema Dk Slaa.
Gazeti la Tz daima leo limeibuka na taarifa ya Dr Slaa kudai kuwa anazo nyaraka za siri za ccm kuagiza na kuingiza silaha kwa ajili ya vijana wa ccm waliowekwa ktk makambi mbali mbali hapa nchini. Lengo la vijana hao ni kudhibiti Chadema. Dr Slaa anasema tunaposema kuwa ccm imedhamiria kufanya vurugu hatutanii, tuko serious.
wakati huo huo,
Gazeti limeelezea pia kwa urefu maelezo ya Dr Slaa na msafara wake kufuatiliwa ktk operesheni yake ya M4C na gari lisiloeleweka. Kufuatilia hali hiyo Dr Slaa aliwaagiza idara ya ulinzi kutoa taarifa polisi ktk wilaya husika lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyiwa kazi.
Gazeti pia lilimpigia simu Nape Nnauye kuhusu madai hayo naye akakana. Akifafanua Nape alisema, Dr Slaa mwongo mbona makontena ya kura za wizi alizosema zimeingizwa nchini hazijaonekana?
My take.
Nape, absence of evidence is not evidence for absence of evidence. Kutokuonekana kwa ushahidi si ushahidi wa kubatilisha mashitaka. Je, kama makontena hayo yamefichwa baada ya siri kuvuja ni nani ajuaye? Ukizingitia kuwa polisi wetu wameshakuwa policcm.
UPDATE,
HABARI KAMILI HII HAPA KWA UREFU
Aituhumu kuingiza nchini silaha kimyakimya
*Asema lengo lake ni kutaka kuihujumu Chadema
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbrod Slaa, kwa mara nyingine tena ameibua tuhuma nzito dhidi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Dk. Slaa amedai kuwa, anazonyaraka zinazoonyesha namna chama hicho tawala kinavyoingiza silaha nchini zikiwamo bunduki bila vibali wala kuzikatia leseni.
Dk. Slaa alisema, CCM inaingiza silaha hizo na kuwapatia vijana wake waliowekwa katika kambi maalumu, kwa ajili ya kufundishwa mbinu za kuwashughulikia wapinzani wao kisiasa hususan Chadema.
Dk. Slaa alitoa kauli hiyo jana mjini Morogoro wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea tathmini ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C), pamoja na Operesheni Sangara iliyoanza mkoani hapa Agosti 8 mwaka huu.
"Kwa hapa Morogoro mjini tunazo taarifa, tumeshaambiwa kuna vijana kama 10-20 wa CCM wanaandaliwa kufanya njama za kuhujumu CHADEMA.
"Watavalishwa kombati kama hizi za kwetu, watafanya fujo ili ionekane ni sisi, wamepewa sumu, tindikali na sindano kwa ajili ya kukamilisha hizo hujuma wanazopanga dhidi yetu.
"Kwa baadhi yetu tunaowafahamu CCM, hili si suala jipya, walifanya hivyo hivyo wakati wa uchaguzi mdogo Igunga, moja ya kambi yao ilikuwa Ilemo na Iramba.
"Huu ndio mtindo wao, wana tabia ya kuingiza hata bunduki nchini bila kibali wala leseni wanapatia vijana, kisha wakishafanya hivyo wanajiandaa kuhamishia tuhuma CHADEMA.
"Mtakumbuka Wilson Mukama (katibu mkuu CCM) aliwahi kutamka wakati ule tukiwa Igunga kuwa, tumeingiza makomandoo nchini, alisema hadharani.
"Kumbe wao tayari wameshaweka vijana kambini na wanafundisha, tena waliohusika kufundisha ni polisi na usalama wa taifa. Tulitoa taarifa polisi juu ya masuala yote na ushahidi tukawapatia wafuatilie, lakini mpaka leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa," alisema Dk. Slaa.
Dk. Slaa alisema kuwa, chama chake hakitatoa taarifa polisi juu ya njama hizo za vijana kuandaliwa na wala hakina mpango wowote wa kuishitaki CCM kwa njama za kukihujumu.
Dk. Slaa alisema, kufanya hivyo ni sawa na kupeleka kesi ya nyani kwa ngedere, ingawa alisisitiza kuwa wakati utakapofika wataweka hadharani nyaraka hizo.
Aliongeza kuwa, kudhihirisha CCM hawatanii katika kutaka kufanya vurugu, hivi karibuni kumekuwa na matukio ya msafara wao kuandamwa na watu wasiojulikana.
Dk. Slaa alisema, watu hao wamekuwa wakitumia magari tofauti na kueleza kuwa, juzi wakiwa wanatoka Gairo, Gari lenye namba T886 AVS aina ya Prado lilikuwa likiwafuatilia.
"Juzi walifanya hivyo tukiwa Mvomero tukatoa taarifa Polisi jana na leo asubuhi tumepata taarifa ambazo hatuwezi kuzipuuza kuwa, kuna vijana kuanzia 10-20 wakiwa na Sumu Sindano pamoja na visu, wanawawinda watu walio katika operesheni kwa ajili ya kuwadhuru, "alisema Dk Slaa.