Dr Willibrod Slaa
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 675
- 1,523
Recta,Dr Slaa je unakubaliana na mimi kuwa huenda tukahitaji sheria ya kudhibiti idadi ya vyama vya siasa, labda vibaki viwili tu ili kweli kuleta maana na tija, hasa kwa wananchi?
Na ningetaka kujua, kwa kutizama namna ambavyo mfumo wa siasa ulivyobadilika hapa nchini toka chama kimoja na sasa vyama vingi, ikiwa siasa inachukua sehemu kubwa sana katika kuelezea maendeleo ya nchi na wananchi, je nipe mtizamo wako, are we better off now au before tulipokuwa na chama kimoja?
Does this so called multiparty democracy deliver what it was meant to deliver
Asante kwa kusisitiza maswali yako yote yajibiwa.
i) Sikutaka kujibu swali kuhusu malumbano ya CCM kwa kumsingi inawahusu wao. Kwa sasa kuna vikao vinaendelea ikiwa ni vikao vya kupokea Taarifa ya Mwinyi. Nisingependa kutolea kauli jambo ambalo silifahamu, sina information inayonifanya niwe na informed opinion. Vinginevyo, nitakuwa ninatoa hisia tu, ninaona hatari sana kujenga Taifa linalojijenga kwenye misingi ya Hisia. Sitaki "indovination" pia kwa kuwa inatuingiza katika ulimwengu wa "Political Utopia" ambao hauna manufaa kwa Taifa wala kwa mchakato wa siasa. Subira yavuta heri, na punde mambo yatakuwa hadharani, wakati huo tutayatolea opinion. Kwa wote pia iwe indicator ninapoacha kujibu hoja ni kwa sababu I may not have the inclination at the material time for lack of adequate information.
ii) Swala la kuweka Wagombea kwa kuachiana niliisha kulijibu awali. Msimamo wangu bado ni huo huo.
iii) Swala la Katiba, nimeisha kulijibu. Mabadiliko ya Katiba yatawezekana tu tukiwa na uwiano mzuri wa Wabunge wa Upinzani na wa Chama Tawala ndani ya Bunge. Mabadiliko ya Katiba yanatawailiwa na Katiba yenyewe, na unahitaji theluthini mbili siyo ya Wabunge wote, bali ya kila Upande wa Mwungano separately. Huu ni mchakato ambao kwa mazingira ya sasa haiwezekana, na ndani ya Bunge Serikali imeisha kusema Katiba "haitaandikwa upya". Lakini nikasema tusilie lie wala kuomboleza. Let us be proactive. Tunaweza kushinda na Katiba hiyo hiyo mbovu. Ushahidi ni maeneo tuliyoshinda sasa, hatukuwa na Katiba nyingine bali hii hii mbovu. Tunachohitaji ni "determination", kujipanga vizuri na kuwa na mikakati thabiti. Full stop. Tutaishinda ccm tukiamua na Watanzania wakituelewa vizuri wakatuunga mkono.