Dr.Slaa ajibu hoja mbalimbali na kueleza Sera za CHADEMA hapa JF

Nauliza huyu mgombea wa chadema dkt,Slaa kasomea wapi na kasomea nini?

Hii ni muhimu kujua kwani taifa letu kwa sasa linahitaji msomi wa fani kama za kiuchumi kutokana na shida za maisha tulizonazo na kuwa nyuma kimaendeleo.

Nimesikia tetesi eti fani yako ni katika theolojia ya kikatoliki tu.Hivi mkutano mkuu wa chadema waliompitisha walifanya hivyo wakiwa wamelewa au walikusudia nini?

Mimi nilitaka kuchukua fomu lakini nikajuwa katika nchi ambayo elimu kama ya kwangu haithaminiwi na itahojiwa nikaamua kukaa kimya. Au tuseme elimu za dini sasa si tatizo tena?

Hapana hawasomi theology tu; wana elimu kubwa sana kuliko unavyodhani.

Kwanza, elimu ya seminary za kikatoliki ni kama elimu nyingine ila inatolewa kwa ubora wa hali ya juu duniani kote, ndiyo maana miaka yote hapa Tanzania mitihani ya form 4 na form 6 huongozwa na seminari za kikatoliki tu. Hata marekani ambako nimewahi kuishi kwa muda mrefu sana, ninajua kuwa shule za kikatoliki zinaongoza sana.

Baada ya kumaliza form 6 seminari, huwa ama wanaingia chuo kikuu kama wanafunzi wengine wa kitanzania au wanakwenda kusomea filosofi kwa miaka miwili kabla hawajaenda kusoma kule seminari kuu ya Kipalapala Tabora ambapo masomo wanayosoma ni pamoja na Theology, Sociology, Psychology, Islamic Studies, New Testament, Old Testament, Anthropology, Family Law na mengineyo.

At least ungepima pia uwezo wake wa kuchambua mambo ambacho ndicho kipimo kikubwa sana cha elimu kuliko kutilia shaka elimu yake bila msingi wowote wa maana.
 
Ahsante kwa nafasi hii:

1) Chadema, mmejipanga vipi kuhakiksisha tanzania inapiga hatua kiuchumi?

2)Chadema kama mtachaguliwa kuongoza nchi mwaka huu, ni vipi basi mtafanya ili kuhakikisha mnaachana na bajeti tegemezi kutoka nje?

3) Chadema mmejiandaaje kuwafanya watanzania wafanye kazi ambao wengi wao ni wavivu, muda mwingi huutumia vijiweni kupiga soga bila kufanya kazi wakisubiri miujiza itokee?

4) Dar es Salaam ina foleni kubwa ambayo ni kero kubwa, chadema mtawafanyia nini watanzania kuokoa muda unaopotea kila siku bila kujua tunajiibia wenyewe?

5) Kuna watu wengi sana ambao hawafanyi kazi nchini, ikitokea mtu akawashawishi kuunda makambi na kuwapa shule kidogo kuhusu kilimo, vitendea kazi, watajenga nyumba safi, watalima, watacheza mpira safi, na watakuwa na kila sababu ya kukumbuka! je chadema kama chadema mnafikiri nini kuhusu kutumia hii nguvu kazi iliyojaa mijini haina kazi, kutumia majeshi yetu kuwapeleka hawa watu maeneo ambayo yanafaa kwa kilimo na kuwafungulia makambi ya kulima, ili kuondokana na hili balaa la njaa?

6) Tuna watu wengi wasomi waiioko nje nchi, wanaweza kufanya mambo makubwa kwa ajili ya hii nchi yetu, je chadema mnafikiria nini kuhusu hawa watu? Na je kuna mkakati wowote wa kutaka kufanya mageuzi ya mitaala ya elimu ili iendane na hali halisi ya uchumi wetu?
 
Karibu Dr, tuko pamoja nawe,

Swali ukifanikiwa kuwa raisi 2010 october nini vitakuwa vipaumbele vya serikali yako angalau vitatu na nini matarajio yako katika ivyo vipa umbele.

Aksante
 
Chadema ina mikakati gani kuwelimisha wapiga kura kuhusu upigaji kura HAKI NA WAJIBU wao ili CCM iwe 'past tense' madarakani?
 
Dr. Sijapendezwa na uteuzi wa mgombea ubunge jimbo la Karatu kupitia Chadema. Sina hakika atavaa viatu vyako na 'zaidi' kiasi gani? Nahisi kwa elimu na upeo wewe uko mbali sana. Mchango wake kwa wanakaratu hasa utakaomfanya waone anauwezo wa kuvaa viatu vyako ni upi?

Je, kweli jimbo hilo haliangukii mikononi mwa mafisadi tena? Utakuwa msiba tena!!!!!!!!
 
Mheshimiwa Slaaa nimefurahi kama kweli wewe ndio mwenyewe unaejiweka karibu na wananchi kwani kiongozi wa kweli huwa na mda kukutana na wanachi wake, utaratibu huu sio mgeni kwetu ila ulikua bused before kwani uliingiza Rushwa wakati wa Mzee Ruksa ile style ya kukutana na wanachi kila mwezi baadae haikuwa tena wananchi ikawa ni kina Dewji.

suali langu kuu tokea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi kulianzishwa mfumo wa Mgombea Mwenza amabe hana kazi inayoonekana ina wabenefit Watanzania , Je Chadema ikishinda Urais itaendelea na mfumo huu wa Rais na Makamo wa Rais na Waziri Mkuu kwenye mfumo wa Serikali Tatu? Unaonaje ukatufafanulia huu mfumo wa serikali tatu utakuaje?

Kuhusu Muungano mimi sio mwanachama wa Chama chochote kwa mda huu ila ningetaka kufahamu sera ya Chadema kuhusu mgawanyo wa mapato na madaraka baina ya Zanzibar na Tanganyika?

Tatu Kila siku tunasikia kunaKamati za Matatizo ya Muungano yanatatuliwa na Viongozi walio chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi bila ya kuwashirikisha wadau wengine jee Chadema ina muelekeo gani wa kuimarisha Muungano , mfano hivi karibuni tumesikia Wazanzibari wansema Nishati hawataki iwe sehemu ya Muungano jee matatizo haya yatatatuliwa kwa kura ya maoni au kwa njia gani?

Nne,Tunsikia majority ya Wazanzibari wanataka kuona Zanzibar inapewa uanachama kwenye East African community na FIFA kama vile Rwanda na Burundi jee msiamamo wa Chadema ni upi kuhusu haya kwani hivi karibuni utakumbuka msuguano wa Mizengo Pinda Kusema Zanzibar siio Nchi na matokeo yake Wabunge wa Zanzibar wkabadilisha Katiba yao na kuweka kifungu kinachosema Zanzibar ni nchi?

Jee Chadema inaitambua Zanzibar kama ni nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano au ni sehemu ya Jamahuri ya Muungano wa Tanzania.

Ntanguliza Shukran Zangu.
 
Back
Top Bottom