Dr. Shein kuelekea 2015...

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
834
Inaelekea Shein ni mkimya sana. Makamo wetu wa raisi huyu kwangu mimi ndiye ninayeona anayefaa kuongoza nchi 2015. Hayupo kwenye spotlight sana kama viongozi wengine wakuu. Katika viongozi tulionao mimi naona huyu mzee ni moja kati ya waliyo bora maana haendekezi siasa za jukwaani. Sijui kwa nini yeye hatajwi kati ya moja ya watu wanaoweza kumrithi JK, labda mwenyewe hautaki uraisi. Ukilinganisha na viongozi wengine wanao tajwa tajwa sasa mimi naona so far namsupport Shein for 2015.

Sababu zangu ni zifuatazo.
1.Hajaonyesha tamaa wala uchu wa madaraka.

2.Hana skendo yoyote kubwa anayo tajwa kuhusika.

3.Haelekei kuwa na makundi

4.Ni mpole na hapendi spotlight kitu ambacho kinaweza kuashiria he is all action and no talk.

5.Tetesi niliyo sikiaga ni kwamba 2005 Kikwete alikua na mgombea mwenza wake mwenyewe lakini baada ya majadiliano wakaona kwamba Shein ndiyo anafaa kuwa kwenye tiketi ya chama.

Sijui kama mwenyewe ana ndoto za 2015 lakini kwenye kundi la sasa yeye anaonekana kufaa kuliko wenzie. Wanaweza kutokea wengine wanaofaa kabla ya 2015 ila kwa sasa nimemuona huyu. Haya ni maoni yangu tu wakuu sijui nyie mna semaje.
 
..hata ziara zake za mikoani viongozi wa huko wanamuogopa yeye kuliko wengine wote, heshima yake iko juu.
 
Yes mzee yuko vizuri sasa sijui kama yeye mwenyewe anataka kuwa au ana nia...si lazima uwe na nia kwanza..harafu ukiwa raisi inabidi kwenye kampeni uanze kuongea sana....na yeye ni mzee wa mkasi wake pale anafanya mambo.
 
Hivi kuna jambo gani ambaye amelifanya huyu mzee mpaka mkadhani anafaa kuchukua uongozi wa nchi? binafsi naona kama ni mtu ambaye ana kosa ushupavu wa kubeba mzigo mzito huu wa nchi masikini na iliyojaa ufisadi. Samahani lakini...mimi naona kama yupo yupo tu.....nielimisheni
 
Inaelekea Shein ni mkimya sana. Makamo wetu wa raisi huyu kwangu mimi ndiye ninayeona anayefaa kuongoza nchi 2015. Hayupo kwenye spotlight sana kama viongozi wengine wakuu. Katika viongozi tulionao mimi naona huyu mzee ni moja kati ya waliyo bora maana haendekezi siasa za jukwaani. Sijui kwa nini yeye hatajwi kati ya moja ya watu wanaoweza kumrithi JK, labda mwenyewe hautaki uraisi. Ukilinganisha na viongozi wengine wanao tajwa tajwa sasa mimi naona so far namsupport Shein for 2015.

Sababu zangu ni zifuatazo.
1.Hajaonyesha tamaa wala uchu wa madaraka.

2.Hana skendo yoyote kubwa anayo tajwa kuhusika.

3.Haelekei kuwa na makundi

4.Ni mpole na hapendi spotlight kitu ambacho kinaweza kuashiria he is all action and no talk.

5.Tetesi niliyo sikiaga ni kwamba 2005 Kikwete alikua na mgombea mwenza wake mwenyewe lakini baada ya majadiliano wakaona kwamba Shein ndiyo anafaa kuwa kwenye tiketi ya chama.

Sijui kama mwenyewe ana ndoto za 2015 lakini kwenye kundi la sasa yeye anaonekana kufaa kuliko wenzie. Wanaweza kutokea wengine wanaofaa kabla ya 2015 ila kwa sasa nimemuona huyu. Haya ni maoni yangu tu wakuu sijui nyie mna semaje.

nakupendekeza wewe naona unafaa zaidi
 
Hivi kuna jambo gani ambaye amelifanya huyu mzee mpaka mkadhani anafaa kuchukua uongozi wa nchi? binafsi naona kama ni mtu ambaye ana kosa ushupavu wa kubeba mzigo mzito huu wa nchi masikini na iliyojaa ufisadi. Samahani lakini...mimi naona kama yupo yupo tu.....nielimisheni

Heshima mbele mkuu. Makamu wa raisi kazi yake ni kumsaidia raisi. Kuna kazi ambazo raisi hawezi kuzifanya zote yeye atapewa na makamu wa raisi. Pia kuna wizara ambazo zipo chini yake. Wewe kwa nini unadhani anakosa ushupavu? Kwa sababu siyo muongeaji au haongei sana kwenye vyombo vya habari? Kumbuka ni makamo wa raisi na kuna mambo ambayo yana takiwa yashikiwe kidete na raisi mwenyewe kama hilo swala la ufisadi. Mimi jamaa naona ni all action and no talk siyo kama hawa wanasiasa wetu wengine ambao huongea sana lakini hauoni chochote.
 
Heshima mbele mkuu. Makamu wa raisi kazi yake ni kumsaidia raisi. Kuna kazi ambazo raisi hawezi kuzifanya zote yeye atapewa na makamu wa raisi. Pia kuna wizara ambazo zipo chini yake. Wewe kwa nini unadhani anakosa ushupavu? Kwa sababu siyo muongeaji au haongei sana kwenye vyombo vya habari? Kumbuka ni makamo wa raisi na kuna mambo ambayo yana takiwa yashikiwe kidete na raisi mwenyewe kama hilo swala la ufisadi. Mimi jamaa naona ni all action and no talk siyo kama hawa wanasiasa wetu wengine ambao huongea sana lakini hauoni chochote.

Asante mkuu. Lakini bado sijapata kitu cha kushika hapo. Kama yeye ndiye anayemsaidia rais, anatakiwa anakolegea rais yeye apakazie. Sawa jamaa sio muongeaje, hiyo siyo sifa ya kuwa rais. Ni kipi hasa ambacho mtu anaweza akasema Shein alikisimamia kikaa vizuri? Huyu mzee ni kama Sumaye, japo yy anaweza akawa sio fisadi lakini hana ile drive na determination ya ku-dare mambo kwa maslahi ya taifa. Huyu alikuwa picked na Mzee Mkapa kwa maslahi binafsi kama alivyofanya kwa Sumaye.
Tatizo anaweza akawa kondoo kabisa mafisadi wakatamalaki...bado nahitaji kuelimishwa tafadhali.
 
Inaonekana wengi mnaona anafaa! jamani toeni elimu kwa wengine kama kweli ana mshiko....maana wengine tunamuona yupo yupo tu.

Mkuu heshima mbele tena. Mimi naona kikubwa ni kwamba as far as we no huyu mzee ni msafi. hajawahi kutajwa kuwa na mambo yoyote ya kifisadi kwa hiyo hamna hata circumstantial proof kuhusu hilo. Katika wakati ambao karibia serikali nzima kila mtu ana skendo inafaa nchi iongozwe na mtu safi.

Pili hana makundi na haelekei kuwa katika moja ya makundi yanayo gombana ndani ya CCM. Nadhani hili lita saidia kama akipata uraisi haitakuwa rahisi kwake kupachika tu watu kujaza marafiki na kwa ajili haelekei kuwa na mkono au ushirikiano na mafisadi siyo rahisi kutuingizia mafisadi baraza la mawaziri.

Najua upole si sifa ya uraisi lakini hata uongeaji nao si sifa ya kuwa raisi mzuri na mfano tunao hapo ni JK.

Lakini again haya ni maoni yangu tu labda wadau watani sahihisha.
 
;;;;;;;;;;;;;;;.
Sababu zangu ni zifuatazo.
1.Hajaonyesha tamaa ;;;;;;;;;;;;;;;;;;;.

2.Hana skendo.......

3.Haelekei kuwa na makundi

4.Ni mpole .

5.Tetesi niliyo sikiaga ni kwamba 2005 Kikwete alikua na mgombea mwenza wake mwenyewe lakini baada ya majadiliano wakaona kwamba Shein ndiyo anafaa kuwa kwenye tiketi ya chama.

Haya ni maoni yangu tu wakuu sijui nyie mna semaje.

MWANAFALSAFA,
Mkuu, Hizo ndo sifa za Rais anaye faa Tanzania?

Mbona umerahisisha sana wadhifa huu?

Rais tunaye anayeifaa Tanzania ni yule mwenye mawazo ya kuibadilisha Tanzania kutoka katika uozo uliopo kuilekea katika maendeleo, na ambaye amejitokeza kuisemea Tanzania na serikali iliyoko madarakani.

Shein yuko katika serikali iliyoko madarakani, na anakubaliana nayo ndo maana bado yuko madarakani.
 
MWANAFALSAFA,
Mkuu, Hizo ndo sifa za Rais anaye faa Tanzania?

Mbona umerahisisha sana wadhifa huu?

Rais tunaye anayeifaa Tanzania ni yule mwenye mawazo ya kuibadilisha Tanzania kutoka katika uozo uliopo kuilekea katika maendeleo, na ambaye amejitokeza kuisemea Tanzania na serikali iliyoko madarakani.

Shein yuko katika serikali iliyoko madarakani, na anakubaliana nayo ndo maana bado yuko madarakani.

Ok mkuu kwa hiyo unaona anayefaa yuko nje ya serikali mkuu? Na kama siyo Shein kwa sasa unaona nani mwenye muelekeo wa kufaa kumpokea JK? Kwa sasa mimi naona upinzani kuchukua ni ndoto labda yatokee mabadiliko ya ghafla na ya uhakika otherwise yoyote tutake ishia kumchagua atakuwa ndani ya serikali au CCM. Hapa tuna badilishana mawazo tu ndiyo niya ya thread.
 
Shein is a good guy.
Anafaa kuongoza Tanzania......

Mkuu, sijui una maana gani haswa kusema Shein is a good guy...so, anafaa kuongoza Tanzania.

Nadhani Tanzania inahitaji Rais shupavu, mwenye vision, anayejua tatizo letu hasa ni nini, mwenye ushujaa wa kuchagua watu makini wa kumsaidia katika vita ya kuondoa umaskini na ufisadi na mwenye nguvu na uwezo wa kufanya maamuzi mazito wakati wowote bila kumuogopa mtu yeyote.

Shein, kwa mtazamo wangu, hana sifa hizo.

Hana mvuto na kama vile yupo yupo tu. Kwa uelewa wangu mdogo, naona tungekuwa fine tu hata kama cheo cha makamu wa rais kingefutwa. Sasa sijui ni kutokana na udhaifu wa mzee huyu au system iliyopo imemfanya mzee kufichwa
 
Hivi kuna jambo gani ambaye amelifanya huyu mzee mpaka mkadhani anafaa kuchukua uongozi wa nchi? binafsi naona kama ni mtu ambaye ana kosa ushupavu wa kubeba mzigo mzito huu wa nchi masikini na iliyojaa ufisadi. Samahani lakini...mimi naona kama yupo yupo tu.....nielimisheni
PUMBA!!!!Mwinyi,Kikwete na Mkapa walifanya nini mpaka wakaweza kuchukua uongozi wa nchi.Fikiria kwanza kabla ya kuteremsha pumba zako hapa.
 
Mkuu, sijui una maana gani haswa kusema Shein is a good guy...so, anafaa kuongoza Tanzania.

Nadhani Tanzania inahitaji Rais shupavu, mwenye vision, anayejua tatizo letu hasa ni nini, mwenye ushujaa wa kuchagua watu makini wa kumsaidia katika vita ya kuondoa umaskini na ufisadi na mwenye nguvu na uwezo wa kufanya maamuzi mazito wakati wowote bila kumuogopa mtu yeyote.

Shein, kwa mtazamo wangu, hana sifa hizo.

Hana mvuto na kama vile yupo yupo tu. Kwa uelewa wangu mdogo, naona tungekuwa fine tu hata kama cheo cha makamu wa rais kingefutwa. Sasa sijui ni kutokana na udhaifu wa mzee huyu au system iliyopo imemfanya mzee kufichwa

Kiongozi Sinyolita,

Matatizo ya utawala, sio kwa Tanzania tu bali kwa dunia nzima, hayasababishwi na kukosa viongozi wenye vision au lack of good ideas. Matatizo ya uongozi ni kukosekana kwa maadili. Rais hafanyi kazi peke yake, yuko kwenye timu inayounda taasisi ya urais ambayo ndio inayomuwezesha Rais kufanya maamuzi. Mara nyingi (au mara zote) Rais hupata ushauri mzuri wa kitaalam wa jinsi ya kushughulikia mambo, na huwa juu ya Rais na wanasiasa wenzake kama wafuate ushauri huo au lah. Kumbuka mfano wa white paper na mchakato wa serikali tatu.
Iwapo tutapata kiongozi mwenye maadili yanayomuwezesha kuwa muaminifu kwa kiasi kikubwa kwa wananchi kuliko kwa ''comrades'' then tutataua sehemu kubwa ya umasikini unaotusumbua.
Shein mpaka sasa ameonekana kuwa na maadili na uaminifu. Ndio maana naunga mkono wazo la kumpendekeza kuwa kiongozi wa Tanzania.
Swala kutokuwa na mvuto ni mapema mno kulitolea uamuzi, nafasi aliyo nayo haimuhitaji kujiweka mbelembele, ila kitu ambacho ninaweza kusema ni kwamba watu wanaomfahamu wanajua kuwa ana mvuto ndio maana amefika pale alipo hivi sasa.
 
Watu wanaomfahamu wanajua kuwa ana mvuto ndio maana amefika pale alipo hivi sasa.

Kamanda ZeM, nina imani watu wengi tunahisi amefika hapo alipo kwa sababu waheshimiwa walitaka mtu asiye na uwezo wa kuwa-challenge, mtu wa 'yes' 'yes' na mtu wasiyemuhofia kwa lolote....

Frankly, sioni huyu Dr. Chein akipewa nafasi ya kugombea urais whether 2010, 2015 au muda wowote ule!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom