Dr Shein Huyooo!

makamu rais hana uwezo wa kuwaondoa mafisadi tz. wameshaota mizizi mikubwa mno.
 
Du ina maana Pinda sasa yeye ndiye?aminiaa jamaa anatisha sana kwa sasa......balaa sana ...sasa hao kina Chenge watadhibitiwa kwa tamko la Pinda?

Pinda alisema kosa si kosa kosa nipale unaporudia, nadhani Pinda awadhibiti iwapo Chenge atarudia tena....hahahahahaha Tanzania bwana aibu tupu!!
 
Kwa kweli Shein ni mtu mstaarabu sana. Mungu amemjalia nguvu ya ajabu ya kuweza kujizuia kujihusisha na ufisadi. Je wangapi wanaweza?
 
Kuna huyu bwana Mwiba anasema kuwa eti Shein hafai na kwa nini aliukataa uprezidaa na kuukubali kuwa VP wakati kikatiba anaweza kuwa prezidaa ianpoteka prezidaa aliyepo akatoka.Mi nadhani Shein alikuwa honest kusema ukweli wake kabisa,maana alijua ni kwa kiasi gani ufisadi umezama ndani ya system nzima.Hivyo akakiri kuwa ni bora asibebe lawama ya kuwadanganya watz wakati asingeweza kufanya hayo,huu ni uwazi na ukweli in real sense.At least in all his years in office Shein has come out clean.
 
Baadhi ya sponsors wa Diaspora forum wamejitoa baada ya kusikia JK haji. Walikuwa wanategemea publicity na kupiga picha na JK.

Inasemekana pia kuna Wahindi wengi waliomba ubalozi ili wakutane na JK, baada ya kuona ni Shein, wakaomba majina yao yaondolewe.
Nnanukuu:"Je kuna Biashara gani Pale Ikulu???" mwisho wa Kunukuu.
 
Hivyo akakiri kuwa ni bora asibebe lawama ya kuwadanganya watz wakati asingeweza kufanya hayo,huu ni uwazi na ukweli in real sense.At least in all his years in office Shein has come out clean.

Mkuu Ibambasi,

Heshima mbele, yaaani ni exactly alivyosema katika moja ya sentesi zake wakati akikataa kugombea urais, kwenye kikkao cha siri alisema kwamba "....siwezi kwenda kuwadanganya wananchi, wakati ninajua nafsini mwangu kuwa ninasema uongo...".
 
Mkuu Ibambasi,

Heshima mbele, yaaani ni exactly alivyosema katika moja ya sentesi zake wakati akikataa kugombea urais, kwamba "....siwezi kwenda kuwadanganya wananchi, wakati ninajua nafsini mwangu kuwa ninasema uongo...".

Huyu mzee msitaarabu sana, haiwezi CCM, CCM inataka watu wa kusema uongo kama bwana makamba, hata kitu ambacho kiko wazi unakanusha, huyu mzee aliona hilo ataliweza, mfano mzuri ni muhafaka wa zanzibar CCM wameshindwa kusema ukweli wakatafuta sababu ya kuwanya CUF wajitoe.
CCM yote inuka ufisadi na ukitaka kuuondoa nafikiri lazima watakuua au watakutafutia kaufisadi kako kadogo uangaike nako, IGP hakuwa mwendawazima aliposema nchi imeshatekwa na magaidi tusipokuwa makini watailipua. magaidi wenyewe ni mafisadi hakina Chenge na mkapa wameshilia mikononi mwao ndo maana JK ansema waachwe wapumzike wakati ni wezi wakubwa.
 
Back
Top Bottom