Dr. Shayo wa UK si bingwa wa uchumi

Umejadili halafu umesema hutajadili,nimekupa mfano wa NOTTINGHAM,LEICESTER NA WARWICK kama mfano najua vizuri sana kwani siwezi kuifananisha OXFORD au Cambridge huko sio kwetu mimi na wewe ndio nikakupa Nottingham wajipime na chuo chako-Southbank.

kukusaidia kama najua nikupe ranking za mwaka huu 2009.

1.Oxford 2.Cambridge 3.Imperial College.4.London school of Economics-LSE. 5.ST.Andrews. 6.Warwick 7.University College London-UCL.

8.Durham University. 9.York 10.Bristol 11-King's College London. 12-loughborough 13-Exeter University. 14-Leicester University.
15-Bath University 16-Nottingham.

ninajua chuo kama OXford wazuri zaidi kwenye utawala,siasa etc wakati Cambridge kwenye sayansi.

Kings college London kwenye sheria na medicine, LSE ni wakali kwenye uchumi na siasa. Warwick wazuri sana kwenye sheria,UCL kwenye sheria n.k
Naomba usiwadanganywe watanzania Southbank sio chuo bomba au unapata kamisheni kwa kuwapeleka hapo chuoni?

kukusaidia University ranking league table 2009 timesonline.co.uk wameonesha kuwa chuo cha London Southbank ndio cha mwisho kwa kushika nafasi ya mwisho ya 113.

watanzania vyema tuwe tunafanya tafiti kwenye kuchagua vyuo wenzetu wazungu wana guide maalum kwenye chaguzi za vyuo-THE ESSENTIAL GUIDE TO PICKING THE RIGHT PLACE kwenye vyuo vikuu.timesonline wana huduma hiyo.jaribuni kupitia website ya chuo kimoja hadi kingine hata kama gazeti lingine litakuwa na mtazamo tofauti hauwi mbali wanaweza kusema LSE ni ya nne na Imperial ni ya tano. lakini hawawezi kuweka Southbank nafasi hata ya 90 lazima kiwe mkiani kabisa.

ukitizama michuzi blog kuna chuo anakitangaza London school of Commerce kuwa wanatoa digri kwa miaka miwili au MBA kwa pound elfu 3900 na wana intake sita kwa mwaka kitu kama hicho waTanzania inabidi tufanyie utafiti wa kutosha kabla ya kujisajili, kwangu mimi hakijanikalia vizuri chuo cha intake sita kwa mwaka na digri kwa miaka miwili.kama MBA ni £3900 bora mtu usome IFM wana masters kozi zina link na chuo cha UK kwa fikra zangu.
hahaha dah umeua
 
inawezekana Dr.Shayo si BINGWA WA UCHUMI lakini shahada yake ya kwanza ni ya UCHUMI. Alimaliza mwaka kati ya mwaka 93 au 94 kama sikosei, pale MLIMANI. Baada ya hapo alifanya Masters ya development studies. Namfahamu
 
inawezekana Dr.Shayo si BINGWA WA UCHUMI lakini shahada yake ya kwanza ni ya UCHUMI. Alimaliza mwaka kati ya mwaka 93 au 94 kama sikosei, pale MLIMANI. Baada ya hapo alifanya Masters ya development studies. Namfahamu

Kumfahamu sio hoja,mie simfahamu zaidi ya kumuona kwenye blogs ila details zake nimezipata.hakusoma Uchumi alisomea Hesabati.amekuwa akimpinga hadi gavana Ndullu kuwa yeye ni mchumi kuliko professor Ndullu sijui anapata nini kujiita mtalaam wa uchumi badala ya fani yake ya mazingira ambayo hivi sasa inalipa sana,tunapenda kupewa elimu ya CLIMATE CHANGE n.k lakini mtalaam wetu anatuangusha kukimbia fani nyingine.

Ushauri kwa DR.Shayo bado hujachelewa kama imetokea umependa kuwa mchumi hivi sasa basi jiunge na chuo chochote kwa part time usome kozi za uchumi, hapo chuoni kwako hakuna kozi ya uchumi basi nenda Westminster university kwa part time course ila kwa sasa usitumie business card kama alizosema YEBO YEBO unazigawa zenye maelezo kuwa ni professor wa uchumi na usijitangaze kama ufanyavyo kuwa ni mtalaam wa uchumi. usije kutufikisha kwa kina Warioba,Kamala,Mary Nagu,mahanga na Mathayo David.
 
hao jamaa ni wakali wakuchambua mada(mashaka na shayo) ukisoma makala zao utawaaminia sana. Hata kama wamesomea uvuvi wa samaki lakini kitaaluma wamekubuhu.
 
hao jamaa ni wakali wakuchambua mada(mashaka na shayo) ukisoma makala zao utawaaminia sana. Hata kama wamesomea uvuvi wa samaki lakini kitaaluma wamekubuhu.

huwezi kukubuhu bila kuingia darasani kama wamesomea samaki watakuwa wazuri kwenye samaki tu.kama wakali waingie darasani shayo achukue uchumi na mashaka sheria.wataonesha ukali wao darasani lakini sio kutengeneza cards kuonesha kuwa ni professor na kuwapa kina yebo yebo wasiojua kitu.sema wamekubuhu kwenye kukopi na ku paste.
 
hao jamaa ni wakali wakuchambua mada(mashaka na shayo) ukisoma makala zao utawaaminia sana. Hata kama wamesomea uvuvi wa samaki lakini kitaaluma wamekubuhu.

KIVIPI UNASEMA WAMEKUBUHU KIUCHUMI???????KIUBABAISHAJI AU???Wabongo tatizo letu hatuna uchambuzi wa kina, jamaa akitoa maelezo kidogo na vijidefinition kiduuuuchu without "critical thinking" basi wanamwona amebobea kumbe hana kitu.Endeleeni kuwaita hivyo hivyo kuwa ni wachumi sijui kutoka wall street au London.Lakini RA nae si kasoma Oxford tehe tehe tehe ....kwikwikwikwi....wajinga ndo waliwao.:rolleyes::rolleyes:
 
ukitizama michuzi blog kuna chuo anakitangaza London school of Commerce kuwa wanatoa digri kwa miaka miwili au MBA kwa pound elfu 3900 na wana intake sita kwa mwaka kitu kama hicho waTanzania inabidi tufanyie utafiti wa kutosha kabla ya kujisajili, kwangu mimi hakijanikalia vizuri chuo cha intake sita kwa mwaka na digri kwa miaka miwili.kama MBA ni £3900 bora mtu usome IFM wana masters kozi zina link na chuo cha UK kwa fikra zangu.

London School of Commerce iko affiliated with University of Wales, Institute Cardiff na ndiyo awarding board na London School of Technology iko affiliated na East London University.

GBP 3950 ni discount kwa Watanzania tu, Vyuo vya UK vina ada tofauti tofauti, wenzetu wanajitahidi sana kuwa market strategies makini. Hapo hapo kuna wanaolipa GBP 6900. Kimetumia low price strategy kukamata masoko. Ni miongoni mwa vyuo vyenye wanafunzi wengi kwa sasa kina takribani ya wanafunzi 4000 kutoka nchi mbalimbali, ukiondoa Universities, Pia wako very strictly na mahudhurio hivi sasa wanatumia biometric kumoniter mahudhurio. Ukikosa kipindi kimoja PIA HOME OFFICE WANAFAHAMU. Mimi sisomi hapo ila nakifahamu na nina jamaa zangu wako hapo na marketing officer wa hapo ni rafiki yangu.

Kuhusu suala la intake siyo hoja, inafuatana na miundo mbinu mlizonazo na mipangilio yenu. Vyuo vingi sana vya UK vina intake 3 kwa mwaka.

Haitakuwa sahihi kulinganisha intake za TZ na UK, Kumbuka vyuo vyetu bado vina kasumba ya ukiritimba, kwao mwanafunzi si valuable customer ndiyo maana ni jambo la kawaida ukaaply usijibiwe sababu zinazokufanya ukataliwe. Vyuo vyetu vinahitaji ubunifu zaidi. Mfano tuangalia University of London utapata picha.

Juzi rafiki yangu mmoja kapokea barua kutoka Bradford University aliomba awali akakubaliwa ila aka opt chuo kingine, wanamuuliza kama kuna tatizo lolote ameliona awaeleze ili warekebishe. Sasa vyuo vyetu jamani tuwe wakweli toka lini wakataka feedback kutoka kwa customers wao?

Hitimisho kigezo cha ukubwa na udogo wa ada si hoja, vipo vyuo ada ni GBP45,000 (TZS 94, 500,000) kwa MBA na vingine ni 75,000 (Hapo zaidi ni kwa Universities). Pia kumbuka UK ni mabepari walio kubuhu hivyo usikimbilie kuangalia uwingi wa ada angalia ubora, contents na facilities.
 
Wakuu samahanini nimekosea kuchapa naomba nilipo sema GBP 75,000 ISOMEKE GBP 7,500. SAMAHANINI KWA USUMBUFU UTAKAO NA ULIOJITOKEZA
 
london school of commerce iko affiliated with university of wales, institute cardiff na ndiyo awarding board na london school of technology iko affiliated na east london university.

Gbp 3950 ni discount kwa watanzania tu, vyuo vya uk vina ada tofauti tofauti, wenzetu wanajitahidi sana kuwa market strategies makini. Hapo hapo kuna wanaolipa gbp 6900. Kimetumia low price strategy kukamata masoko. Ni miongoni mwa vyuo vyenye wanafunzi wengi kwa sasa kina takribani ya wanafunzi 4000 kutoka nchi mbalimbali, ukiondoa universities, pia wako very strictly na mahudhurio hivi sasa wanatumia biometric kumoniter mahudhurio. Ukikosa kipindi kimoja pia home office wanafahamu. Mimi sisomi hapo ila nakifahamu na nina jamaa zangu wako hapo na marketing officer wa hapo ni rafiki yangu.

Kuhusu suala la intake siyo hoja, inafuatana na miundo mbinu mlizonazo na mipangilio yenu. Vyuo vingi sana vya uk vina intake 3 kwa mwaka.

Haitakuwa sahihi kulinganisha intake za tz na uk, kumbuka vyuo vyetu bado vina kasumba ya ukiritimba, kwao mwanafunzi si valuable customer ndiyo maana ni jambo la kawaida ukaaply usijibiwe sababu zinazokufanya ukataliwe. Vyuo vyetu vinahitaji ubunifu zaidi. Mfano tuangalia university of london utapata picha.

juzi rafiki yangu mmoja kapokea barua kutoka bradford university aliomba awali akakubaliwa ila aka opt chuo kingine, wanamuuliza kama kuna tatizo lolote ameliona awaeleze ili warekebishe. Sasa vyuo vyetu jamani tuwe wakweli toka lini wakataka feedback kutoka kwa customers wao?

hitimisho kigezo cha ukubwa na udogo wa ada si hoja, vipo vyuo ada ni gbp45,000 (tzs 94, 500,000) kwa mba na vingine ni 75,000 (hapo zaidi ni kwa universities). Pia kumbuka uk ni mabepari walio kubuhu hivyo usikimbilie kuangalia uwingi wa ada angalia ubora, contents na facilities.
katika vyuo nilivyoweka hapo juu kama bristol.lse kipi kina intake tatu?vina intake ya sept tu. Acha kudanganya.jamani ingieni kwenye vyuo vilivyowatajia hakuna intake tatu ,kama uko uk kwanini usiende cardiff kwenyewe? Kama ni affiliated baki nyumbani usome ifm nao affiliated.
 
katika vyuo nilivyoweka hapo juu kama bristol.lse kipi kina intake tatu?vina intake ya sept tu. Acha kudanganya.jamani ingieni kwenye vyuo vilivyowatajia hakuna intake tatu ,kama uko uk kwanini usiende cardiff kwenyewe? Kama ni affiliated baki nyumbani usome ifm nao affiliated.


Kanda2 NATHANI UNAONGEA USICHOKIJUA AU UNASIMULIWA. HAPA CHINI NAKUPA IN TAKE ZA UNIVERSITY OF OXFORD NA UNIVERSITY OF CAMBRIDGE KWA PROGRAM ZA UZAMILI NA UZAMIVU TU. Undergraduate sijaziweka.


University of Oxford ni 21/11/2008, 9/01/2009 au 23/01/2009 na 13/03/2009 hiyo ni kwa 2009/2010

University of Cambridge kama nilivyopest hapa chini

When to apply
It is in your interest to apply as soon as possible. Please check the ‘Courses and subjects’ section for information on course closing dates. If no closing date is shown, the deadline for applications is two months before the start of the first term of the course (31 July, 31 October and 31 January for starts in October, January and April respectively). We will not process late applications.

If you are applying for funding in parallel with your academic application, see 'Costs and funding'. Please note that funding deadlines may be significantly earlier than course closing dates.


Nina mifano ya vyuo vingi. SASA VIBISHIE NA HIVYO VYUO au Vilinganishe na hiyo sample ya tuvyuo twako.

Kama nilivyosema intake si kielelezo cha ubora ila inafuatana na initiative za vyuo pamoja na demand ya soko.

Kwa pointi zako basi tuvyuo twako ni bora kuliko Oxford na Cambridge.

Mahali ambapo unadhani nadanganya/au sijaelewa please USISITE KUNISAHIHISHA ILA USIPOTOSHE UMMA.

Pia fahamu kuwa mifumo ya vyuo inafuatana pia na advancement ya miundo mbinu ikiwamo na IT
 
inawezekana Dr.Shayo si BINGWA WA UCHUMI lakini shahada yake ya kwanza ni ya UCHUMI. Alimaliza mwaka kati ya mwaka 93 au 94 kama sikosei, pale MLIMANI. Baada ya hapo alifanya Masters ya development studies. Namfahamu


Asanet sana Mwanamalundi kwa taarifa hii. Nami namfahamu Dr. Shayo kama Mchumi kwa B.A (Economics) then akachuka Masters ya Development Studies (sijui areas of specialization) vyote ni pale UDSM na akabakishwa kuwa Assistant Lecturer pale IDS na ndipo alipoenda kwa PhD yake Uingereza na akafanikiwa kuimaliza PhD yake tena kwa muda mfupi na mwishowe aliajiriwa huko Uingereza.

Jamani nataka kusema hivi, acheni hatred posts!!! Kama mtu mmegombana a kukosana jambo fulani msifanye JF mahali pakuja kudhalilisha watu. Tuheshimu jukwaa letu. Mleta mada ameiweka kana vile kuna kaugomvi maana anadiriki hata kusema eti kuwa Shayo hajawahi kusoma Economics. Je waongo hapa ambao kweli wamegundulika kuwa ni waongo kama mleta thread anaweza kupewa adhabu gani hapa?? Mods inabidi mpeni warning, hata kama ni verbal (in writing) itasaidia kwani hatuwezi kwa na members ambao wanaleta thread za kupotosha!!!

Ila tu ninahisi wameingiliana anga hawa watu!!! At least I know comrade Dr. Hilderbrand Shayo, he is handsome I can say.........Sisemi mengi!!!
 
Kanda2 NATHANI UNAONGEA USICHOKIJUA AU UNASIMULIWA. HAPA CHINI NAKUPA IN TAKE ZA UNIVERSITY OF OXFORD NA UNIVERSITY OF CAMBRIDGE KWA PROGRAM ZA UZAMILI NA UZAMIVU TU. Undergraduate sijaziweka.


University of Oxford ni 21/11/2008, 9/01/2009 au 23/01/2009 na 13/03/2009 hiyo ni kwa 2009/2010

University of Cambridge kama nilivyopest hapa chini

When to apply
It is in your interest to apply as soon as possible. Please check the ‘Courses and subjects’ section for information on course closing dates. If no closing date is shown, the deadline for applications is two months before the start of the first term of the course (31 July, 31 October and 31 January for starts in October, January and April respectively). We will not process late applications.

If you are applying for funding in parallel with your academic application, see 'Costs and funding'. Please note that funding deadlines may be significantly earlier than course closing dates.


Nina mifano ya vyuo vingi. SASA VIBISHIE NA HIVYO VYUO au Vilinganishe na hiyo sample ya tuvyuo twako.

Kama nilivyosema intake si kielelezo cha ubora ila inafuatana na initiative za vyuo pamoja na demand ya soko.

Kwa pointi zako basi tuvyuo twako ni bora kuliko Oxford na Cambridge.

Mahali ambapo unadhani nadanganya/au sijaelewa please USISITE KUNISAHIHISHA ILA USIPOTOSHE UMMA.

Pia fahamu kuwa mifumo ya vyuo inafuatana pia na advancement ya miundo mbinu ikiwamo na IT

Ndugu yangu nashukuru lakini mimi similiki chuo chochote.London school of Commerce chuo chako unachokipigia debe kina intake sita kwa mwaka za undergraduate ya miaka miwili. kwanza sijawahi kuona undergraduate ya miaka miwili.pili kwa majengo au facility zipi walizonazo hao LSC kuwa na intake sita?. unasema inategemeana na miundo mbinu hao wanaweza kuwa na miundo mbinu kuwashinda Durham au London school of Economics?

Oxford,Cambridge na orodha ya vyuo vyote nilivyoweka hapo juu hakuna chenye intake mbili za undergraduate kwa mwaka.mbona umeweka program za masters ambayo sio mjadala wetu,kwani kama masters ndio mjadala basi London Southbank university hatuwezi kuwajadili kama university kwani wana kozi mbili au tatu tu za masters ambazo ni full time.tunapozungumzia Udsm au Udom tunasema mwaka wa masomo huanza september tukizungumzia undergraduate ambao ndio msingi wa hoja, masters ni ziada.

Uzuri wa mambo kila kitu kiko kwenye mtandao tizameni andikeni email kwenye vyuo hivyo havina intake tatu kwa mwaka. pia chuo kama London School of Commerce anachokipigia debe ndugu yangu hakina uwezo wa kuwa na walimu bora, wengi wao ni wahindi au wanigeria.dasarani huwezi kukutana na mzungu,mmarekani au taifa lolote lililoendelea zaidi ya wa sri-lanka,wabangaladeshi,wa ivory coast na watanzania.utajifunza nini katika mazingira hayo? ni bora uwe IFM au Udsm.

msidanganyike na ada kuwa rahisi siku zote bure ghali ni msemo wa kiswahili.

intake sita kwa mwaka jengo la vyumba sita.CBE iko mbali sana kwa London school of Commerce.jaribuni kupitia website.le.ac.uk tizameni kozi ngapi wanato na cv za walimu halafu tizameni London School of commerce kina kozi gani na walimu wa aina gani? ufisadi uko wa aina nyingi kuwa na elimu ya mazingira na kujifanya kuwa ni mchumi au kuwalaghai watu wasome chuo chenye Intake sita kwa mwaka kikiwa hakina facilities, huo ni wizi MTUPU kwa watanzania wenzetu.
 
Asanet sana Mwanamalundi kwa taarifa hii. Nami namfahamu Dr. Shayo kama Mchumi kwa B.A (Economics) then akachuka Masters ya Development Studies (sijui areas of specialization) vyote ni pale UDSM na akabakishwa kuwa Assistant Lecturer pale IDS na ndipo alipoenda kwa PhD yake Uingereza na akafanikiwa kuimaliza PhD yake tena kwa muda mfupi na mwishowe aliajiriwa huko Uingereza.

Jamani nataka kusema hivi, acheni hatred posts!!! Kama mtu mmegombana a kukosana jambo fulani msifanye JF mahali pakuja kudhalilisha watu. Tuheshimu jukwaa letu. Mleta mada ameiweka kana vile kuna kaugomvi maana anadiriki hata kusema eti kuwa Shayo hajawahi kusoma Economics. Je waongo hapa ambao kweli wamegundulika kuwa ni waongo kama mleta thread anaweza kupewa adhabu gani hapa?? Mods inabidi mpeni warning, hata kama ni verbal (in writing) itasaidia kwani hatuwezi kwa na members ambao wanaleta thread za kupotosha!!!

Ila tu ninahisi wameingiliana anga hawa watu!!! At least I know comrade Dr. Hilderbrand Shayo, he is handsome I can say.........Sisemi mengi!!!

Maandishi yako tutayaamini vipi wewe mwenyewe ukisema sijui alichukua eneo gani?Mie sijagombana na DR.Shayo na siwezi kumvunjia heshima kwani natambua kama mtalaam wa mazingira.

Aliyeleta uongo ni Yebo yebo kuwa DR.Shayo ni associate professor wa uchumi wakati muajiri wake kasema ni mtalaam wa mazingira yuko kitengo cha Construction, jee Yebo yebo apewe adhabu gani kwa kupotosha watu? na kusema uongo wa dhahiri? sina shuki na DR.Shayo always nimekuwa nikisema kuwa jamaa ni msomi na ninamwita DR. post zote. tittle ya thread ni ushuhuda wa haya. nimesema DR.SHAYO WA UK SI BINGWA WA UCHUMI. maana nakubali kuwa ni dr. na bingwa ila si bingwa wa uchumi ni bingwa wa mazingira,hapo hakuna tusi wala kupotosha.

JF sio kama michuzi blog ukimpa zawadi ya fulana na ukimwambia mimi ni jack Pemba ndio agent wa wachezaji UK bila kuliiza anakupaisha.
hapo tunahoji ndio maana EPA ETC vita vyake vilianzia hapa kwa nguvu za kina FIELD MARSHAL ES na wenzake.
 
London School of Commerce iko affiliated with University of Wales, Institute Cardiff na ndiyo awarding board na London School of Technology iko affiliated na East London University.

GBP 3950 ni discount kwa Watanzania tu, Vyuo vya UK vina ada tofauti tofauti, wenzetu wanajitahidi sana kuwa market strategies makini. Hapo hapo kuna wanaolipa GBP 6900. Kimetumia low price strategy kukamata masoko. Ni miongoni mwa vyuo vyenye wanafunzi wengi kwa sasa kina takribani ya wanafunzi 4000 kutoka nchi mbalimbali, ukiondoa Universities, Pia wako very strictly na mahudhurio hivi sasa wanatumia biometric kumoniter mahudhurio. Ukikosa kipindi kimoja PIA HOME OFFICE WANAFAHAMU. Mimi sisomi hapo ila nakifahamu na nina jamaa zangu wako hapo na marketing officer wa hapo ni rafiki yangu.

Kuhusu suala la intake siyo hoja, inafuatana na miundo mbinu mlizonazo na mipangilio yenu. Vyuo vingi sana vya UK vina intake 3 kwa mwaka.

Haitakuwa sahihi kulinganisha intake za TZ na UK, Kumbuka vyuo vyetu bado vina kasumba ya ukiritimba, kwao mwanafunzi si valuable customer ndiyo maana ni jambo la kawaida ukaaply usijibiwe sababu zinazokufanya ukataliwe. Vyuo vyetu vinahitaji ubunifu zaidi. Mfano tuangalia University of London utapata picha.

Juzi rafiki yangu mmoja kapokea barua kutoka Bradford University aliomba awali akakubaliwa ila aka opt chuo kingine, wanamuuliza kama kuna tatizo lolote ameliona awaeleze ili warekebishe. Sasa vyuo vyetu jamani tuwe wakweli toka lini wakataka feedback kutoka kwa customers wao?

Hitimisho kigezo cha ukubwa na udogo wa ada si hoja, vipo vyuo ada ni GBP45,000 (TZS 94, 500,000) kwa MBA na vingine ni 75,000 (Hapo zaidi ni kwa Universities). Pia kumbuka UK ni mabepari walio kubuhu hivyo usikimbilie kuangalia uwingi wa ada angalia ubora, contents na facilities.

Hakuna chuo chenye intake tatu UK nikiwa na maana ya universities jamaa anataka kudanganya .vyuo kama London school of Commerce sidhani TCU wanakitambua.

muwe makini isije kuwa mambo ya kina Kamala,Nagu,warioba,nchimbi,mathayo David wamekuja na vyeti kutoka vyuo visivyojulikana.kwanini wengine walipe elfu sita na mia tisa na watanzania walipe elfu tatu,jee wenye chuo wanatupenda sana watanzania? huko East London ada elfu saba nani ataacha kwenda kwenye chuo chenyewe na kwenda affiliated kwa tofauti ya pounds mia moja.University za chini ada yake huanzia pounds elfu sita hadi saba, chuo kama Bangor ni kizuri na ada ni ya chini unapata L.L.M kwa elfu sita.www,bangor.ac.uk

utaambiwa kuwa chuo kiko affiliated na University of wales-Cardiff jee walimu na library utatumia ya Cardiff au utafundishwa na wahindi na WANIGERIA?

Elimu sio cheti ubora wa chuo,walimu na vifaaa kama library. chuo kama hicho hakina vitabu japo elfu moja kwenye library yake.wakati university of wales wana library yenye vitabu hadi laki saba.

Ushauri kwa watanzania waende kwenye vyuo vya maana kuliko hivi zicollege kwenye hivi vi college kuna mapungufu mengi mfano hakuna uongozi wa wanafunzi kama rais wa chuo,mawaziri etc kitu muhimu kwa mwanafunzi.jamaa anasema kina wanafunzi elfu nne,wakati London Metropolitan University wana wanafunzi elfu 40.www,londonmet.ac.uk

Vyuo kama hivi labda unasoma professional courses kama ACCA,CIMA,CFA N.K ndio unaweza kwenda lakini baada ya kufanya utafiti wa kutosha.
 
Ndugu yangu nashukuru lakini mimi similiki chuo chochote.London school of Commerce chuo chako unachokipigia debe kina intake sita kwa mwaka za undergraduate ya miaka miwili. kwanza sijawahi kuona undergraduate ya miaka miwili.pili kwa majengo au facility zipi walizonazo hao LSC kuwa na intake sita?. unasema inategemeana na miundo mbinu hao wanaweza kuwa na miundo mbinu kuwashinda Durham au London school of Economics?

Oxford,Cambridge na orodha ya vyuo vyote nilivyoweka hapo juu hakuna chenye intake mbili za undergraduate kwa mwaka.mbona umeweka program za masters ambayo sio mjadala wetu,kwani kama masters ndio mjadala basi London Southbank university hatuwezi kuwajadili kama university kwani wana kozi mbili au tatu tu za masters ambazo ni full time.tunapozungumzia Udsm au Udom tunasema mwaka wa masomo huanza september tukizungumzia undergraduate ambao ndio msingi wa hoja, masters ni ziada.

Uzuri wa mambo kila kitu kiko kwenye mtandao tizameni andikeni email kwenye vyuo hivyo havina intake tatu kwa mwaka. pia chuo kama London School of Commerce anachokipigia debe ndugu yangu hakina uwezo wa kuwa na walimu bora, wengi wao ni wahindi au wanigeria.dasarani huwezi kukutana na mzungu,mmarekani au taifa lolote lililoendelea zaidi ya wa sri-lanka,wabangaladeshi,wa ivory coast na watanzania.utajifunza nini katika mazingira hayo? ni bora uwe IFM au Udsm.

msidanganyike na ada kuwa rahisi siku zote bure ghali ni msemo wa kiswahili.

intake sita kwa mwaka jengo la vyumba sita.CBE iko mbali sana kwa London school of Commerce.jaribuni kupitia website.le.ac.uk tizameni kozi ngapi wanato na cv za walimu halafu tizameni London School of commerce kina kozi gani na walimu wa aina gani? ufisadi uko wa aina nyingi kuwa na elimu ya mazingira na kujifanya kuwa ni mchumi au kuwalaghai watu wasome chuo chenye Intake sita kwa mwaka kikiwa hakina facilities, huo ni wizi MTUPU kwa watanzania wenzetu.

Rafiki yangu Kanda2 unanifurahisha, nakuja June kama upo TZ natamani nikuone MAANA wewe unasifa zote za kuwa mpiganaji wa kweli.

Ila sikuweka undergraduate kwa sababu za msingi maana ulizungumzia MBA. Lakini pitia vizuri website utaona.

Pia nadhani hauifahamu vizuri system ya higher learning ya UK, kwa hiyo hata nikieleza hutanielewa KIMSINGI iko tofauti na TZ. Kuna level zipo (Ukiwaona NACTE watakufafanulia) Kimsingi pale first year wanakuwa awarded Diploma na Advanced Diploma ambayo ni level 3, then mwaka wa pili ni wanatop up digrii, ila nilazima uwe na UK Qualifications.

Miaka miwili digrii ni normal sana, ILA LAZIMA UWE NA UK Qualifications. Kawaone NACTE watakufafanulia vema hizo level maana wao wanazo.

Halafu vyeti vyao vinatoka University of Wales, Institute Cardif na University of East London as awarding Board.

Pale ni kweli panawanafunzi wengi mpaka huwa wanakataa kurecruit, ila wana Compus tatu kwa hapo London.

Ni miongoni mwa vyuo vinavyokubalika hata home office (Walishapongezwa kwa umakini)

Wahadhiri wanao ambao ni very respected kama umesoma Marketing nadhani umekutana na Profesa Geoff Lancaster huyo ni baadhi tu ya walimu.

Pia fahamu waingereza ni wavivu na hawapendi kusoma hilo hata Brown aliwaeleza walipokuwa wanaandamana wakipinga nafasi nyingi kushikwa na wageni.

Kama hauko UK, ni vema ukafanya utafiti kwa kuwasiliana na BAC (British Accreditation Council for Independent Further and Higher Education).
 
Hakuna chuo chenye intake tatu UK nikiwa na maana ya universities jamaa anataka kudanganya .vyuo kama London school of Commerce sidhani TCU wanakitambua.

muwe makini isije kuwa mambo ya kina Kamala,Nagu,warioba,nchimbi,mathayo David wamekuja na vyeti kutoka vyuo visivyojulikana.kwanini wengine walipe elfu sita na mia tisa na watanzania walipe elfu tatu,jee wenye chuo wanatupenda sana watanzania? huko East London ada elfu saba nani ataacha kwenda kwenye chuo chenyewe na kwenda affiliated kwa tofauti ya pounds mia moja.University za chini ada yake huanzia pounds elfu sita hadi saba, chuo kama Bangor ni kizuri na ada ni ya chini unapata L.L.M kwa elfu sita.www,bangor.ac.uk

utaambiwa kuwa chuo kiko affiliated na University of wales-Cardiff jee walimu na library utatumia ya Cardiff au utafundishwa na wahindi na WANIGERIA?

Elimu sio cheti ubora wa chuo,walimu na vifaaa kama library. chuo kama hicho hakina vitabu japo elfu moja kwenye library yake.wakati university of wales wana library yenye vitabu hadi laki saba.

Ushauri kwa watanzania waende kwenye vyuo vya maana kuliko hivi zicollege kwenye hivi vi college kuna mapungufu mengi mfano hakuna uongozi wa wanafunzi kama rais wa chuo,mawaziri etc kitu muhimu kwa mwanafunzi.jamaa anasema kina wanafunzi elfu nne,wakati London Metropolitan University wana wanafunzi elfu 40.www,londonmet.ac.uk

Vyuo kama hivi labda unasoma professional courses kama ACCA,CIMA,CFA N.K ndio unaweza kwenda lakini baada ya kufanya utafiti wa kutosha.

Kanda2 usiwavunje moyo wapiganaji, Pale alikuwepo mtanzania mmoja sasa hivi karudi TZ ambaye alikuwa kaajiriwa ndiye aliyejenga HOJA KUHUSIANA NA KIPATO CHA MTANZANIA. ilipita kwa shida na ikakubalika iwepo scholarship MASHARTI ni kwamba lazima atakayekubaliwa alipe deposit ya GBP 2950.

MIMI SISOMI HAPO ILA NAKIFAHAMU NA HAWANA MCHEZO NA MAHUDHURIO YA DARASANI. Pia hata admission zao hawana mchezo maana ukiwa na Advanced Diploma au Postgraduate Diploma lazime usome foundation 4 months ndiyo uendelee na MBA yao.

NAOMBA NISIJE NIKAWA AFISA UHUSIANO WAO, wasiliana nao. Nadhani hapa lengo ni kupanuana MAWAZO na si kubishana.

VINGINEVYO MIMI NA OPT KWENYE WIN -LOSE, hivyo kama ni kubishana basi umeshinda.
 
Rafiki yangu Kanda2 unanifurahisha, nakuja June kama upo TZ natamani nikuone MAANA wewe unasifa zote za kuwa mpiganaji wa kweli.

Ila sikuweka undergraduate kwa sababu za msingi maana ulizungumzia MBA. Lakini pitia vizuri website utaona.

Pia nadhani hauifahamu vizuri system ya higher learning ya UK, kwa hiyo hata nikieleza hutanielewa KIMSINGI iko tofauti na TZ. Kuna level zipo (Ukiwaona NACTE watakufafanulia) Kimsingi pale first year wanakuwa awarded Diploma na Advanced Diploma ambayo ni level 3, then mwaka wa pili ni wanatop up digrii, ila nilazima uwe na UK Qualifications.

Miaka miwili digrii ni normal sana, ILA LAZIMA UWE NA UK Qualifications. Kawaone NACTE watakufafanulia vema hizo level maana wao wanazo.

Halafu vyeti vyao vinatoka University of Wales, Institute Cardif na University of East London as awarding Board.

Pale ni kweli panawanafunzi wengi mpaka huwa wanakataa kurecruit, ila wana Compus tatu kwa hapo London.

Ni miongoni mwa vyuo vinavyokubalika hata home office (Walishapongezwa kwa umakini)

Wahadhiri wanao ambao ni very respected kama umesoma Marketing nadhani umekutana na Profesa Geoff Lancaster huyo ni baadhi tu ya walimu.

Pia fahamu waingereza ni wavivu na hawapendi kusoma hilo hata Brown aliwaeleza walipokuwa wanaandamana wakipinga nafasi nyingi kushikwa na wageni.

Kama hauko UK, ni vema ukafanya utafiti kwa kuwasiliana na BAC (British Accreditation Council for Independent Further and Higher Education).

Hatushindani tunaelimishana.hakuna traditional university yeyote kati ya zile nilizotaja including Oxford na Cambridge zinazotoa kozi au zenye intake kwa undergraduate zaidi ya moja kwa mwaka ukinithibitishia hilo nitakubali kuwa DR.Shayo ni bingwa wa uchumi na si mazingira.

unasema system ya Tanzania na UK ni tofauti sio kweli.elimu yetu ni ya UK,bunge letu,sheria zetu wao ni jumuiya ya madola na sisi ni wanachama wao.labda uwambie watu wanaotoka china,japan au Iran kwao ndio system tofauti.

mimi napenda kuwaambia watanzania tuwe wadadisi na wenye kutafiti kwenye kwenda kwenye vyuo hasa kama hiki.

Mzovya mimi najitahidi kufuatilia mambo haya ya elimu ingawa elimu yangu ni darasa la saba lakini duniani ya sasa ni kijiji mitandao inatupa uhalisia hata kama hatuko ulaya.

ukisoma gazeti la The Guardian la UK la tarehe 11,may 2009 wameorodhesha vyuo vikuu vya UK na chuo cha DR.Shayo kimeshika nafasi ya pili kwa umwisho.
wakati Times walikiweka cha mwisho kuonesha kuwa magazeti haya hayajiandikii tu ila yana wataalaam wanaofanya tafiti hizi.

Watanzania jaribuni kupitia website ya chuo cha LONDON SCHOOL OF COMMERCE www,lsclondon.co.uk kwenye website tu utajua kuwa chuo hiki kina mushkeli.wana kozi tatu za masters MCS TOURISM AND MANAGEMENT,MSC MANAGEMENT AND HOSPITALITY NA MBA GENERAL.na tunaambiwa kuna wanafunzi elfu nne.kozi hizo zinamfaa mtanzania gani? labda watu wa Tanapa na bodi ya utalii Tanzania,

rafiki yangu kasema chuo hiki kina wanafunzi hadi kinawakataa, kama ndivyo kwanini wamepunguza Ada? kwani price strategy ya marketing unapunguza ada ili upate wanafunzi wengi au mauzo makubwa au wateja wengi,hawa wamepunguza kutoka elfu sita na mia tisa hadi £3950. watu hawa wanaokataa wanafunzi wameweka Tangazo lao michuzi blog na wanalipia, wakisisitiza kuwahi kujisali kabla ya mwisho wa offer-(sale).hili linathibitisha kuwa chuo hiki hakina soko na watanzania ndio eneo lao pekee la kuwachukulia pesa zao kwani tumekuwa wazito kwenye kufanya utafiti au tunaingia mambo kichwa kichwa.

tujihadhari inawezekana kabisa hii ni sampuli nyingine ya DECI unajua unapata kumbe unapatikana.

kama Ada pounds elfu tatu bora mtu uende India au Malaysia au Uganda ukasome kwenye chuo chenye hadhi ya chuo sio usome NEW DELHI lakini cheti na chuo chenyewe kiko Bombay.

kwanini umefunga safari hadi huko na usifike kwenye chuo chenyewe? kwani ukienda London school of commerce hutakutana na wenye nchi au walimu bora na facility hakuna, kama ni cheti cha bei ndogo soma DISTANCE LEARNING ukijua mateals na cheti kinatoka kwenyewe kuliko kwa third party.
hivi umesoma London school of Commerce umeenda kuomba kazi na anatakiwa referee ambaye ni mwalimu wako utatoa reffence Cardiff au hapo London school of commerce?

kwani lecturer wa Cardiff hafundishi LSC huko yuko Mhindi Mr.Patel.mfano timu yangu ya Yanga imekusajili lakini hujacheza mazoezi na Yanga hapa kaunda hata siku moja na wala kocha KOndic hajawahi kukuona jee wewe unafaidika na unatumia facility za Yanga?

Umesema niwaone NACTE unakusudia NECTA ambao wanahusika na elimu ya O level na A level sio elimu ya juu kama hizo Diploma unazosema. au unakusudia Acrrediation council ya Tanzania? nayo sio kazi yake kuhakiki vyeti kazi zao kutizama ubora wa vyuo na elimu wanayotoa kwa vyuo vya ndani ya nchi na usajili wa vyuo.

umesema niwasiliane na British ACCREDIATION COUNCIL hawa si goverment body ni charity organisation na vyuo vikuu kama Leeds university huwezi kuona BAC wanajihususha nao. hawa wana deal na vi college vya mtaaani.

Umesema kuna professor wa Marketing hapo chuoni kwako lakini website ya chuo haisemi kuwa kuna huyo professor hivyo ni ngumu kwangu kuamini maneno hayo ni sawa na Yebo yebo aliyeandika kuwa dr.shayo ni associate professor bila ushahidi na nimembana hajarudi tena hadi leo kabaki kutoa Thanks tu alifikiri ataniburuza ameshindwa TA itaweza JF?

umesema kuwa Waingereza wavivu TUNAKUPA MFANO mikoa ambayo imeshikiliwa na wageni mfano wahindi kama BRADFORD,Birmingham,Leicester ambako umesema kuna rafiki yako aliomba ukitizama website za vyuo vyao wanaoshika na kufundisha ni wazungu www,bradford,ac.uk,University of Leicester au www.barmingham.ac.uk anachokisema Gordown Brown hata Majjid Mjengwa aliwahi kuandika hapa kwenye Rai ni kuwa namba ya waingereza ni ndogo wanaohitimu kuliko wachina na wahindi wanaomaliza kwa mwaka milioni 4 na 2 respectively.

kuna jamaa yangu alikuja huko huko kusoma chuo cha mtaani kozi ya Acca chuo cha London school of Accounting and Management-LONDONSAM ukitizama website ya chuo hiki hata kama cha mtaani lakini kina watalaam kwa kiasi fulani ingawa naamini watakuwa on part time basis cheki website yao..

wengine ni London school of Accountancy,Kaplan zamani Emil wolf au BPP ni vyuo vyenye hadhi kuliko LSC kwani college hizi kama tuition providers kwa professional courses kama ACCA,CIMA,CFA n.k lakini school of commerce hata professional courses hawana kama hizo.

umegusia sana AWARDING BODIES najua wazi kozi kama ya diploma na Advance diploma ya business inatoka IAM au institute of Administrative management halafu ndio mnampeleka mtu Cardiff au kwa kugha yako Top up.

Rafiki umesema kuwa kuna mtanzania ndio alileta hiyo discount sawa ni jambo zuri lakini ujuwe kuwa hapa tunazungumzia maisha ya watu.wazungu walipokuwa wanatawala makoloni au kutafuta watumwa walikuwa na watu wanawatumia kutoka same backgruond. tusipumbazwe na vidiscount vya wahindi na tukawaingiza mkenge ndugu zetu kwa kuwapeleka LSC KWENYE BURE GHALI AU DECI.

lengo la mjadala huu kuwafungua watanzania tuwe tunaumiza kidogo vichwa haswa kwenye maamuzi yanayogusa future zetu.

ndugu yangu amekuwa akikazia kila dakika na kukoza maneno KUWA HOME OFFICE wanakitambua chuo. HOME OFFICE hao hao mara ngapi wanatoa visa kwa wana bongo fleva jee wao ni watalaam wa bongo fleva?au wanawapa visa watu wakiamini ni genuine kumbe ni wauza madawa ya kulevya.HOME OFFICe hao hao wanadanganywa na wapemba ambao ni watanzania wanawambia ni wasomali hatimaye wana wapa pasipoti za Uingereza,nilisoma gazeti moja kuwa kuna wahamiaji haramu laki tano kama ni taasisi makini yasingekuwa hayo.

hujawahi kusikia wakuu wa Home office wamejiuzulu kwa maskendo? taasisi inayodanganywa na wapemba iko makini na kuipa mfano?wahindi waliotufundisha EPA watashindwa kuwazuga HOME OFFICE na college kama LSC?
The bottom line home office sio academicians wala hawajui taaluma ni nini?hivi mtu akisema Mzumbe kuna walimu feki jibu kuwa nenda mambo ya ndani kwani kuna wazungu walipewa visa kuja kutembelea chuo kikuu cha Mzumbe,Mambo ya ndani inahusika nini na taaluma?

NIMELAZIKA KUANDIKA sana ili watu wapate ujumbe naamini kuna ya msingi out of my pumba.niliowaboa mtanisamehe natanguliza uzalendo itakuwa aibu na ajabu mtu afunge safari kwenye kusoma kwa mzungu anakutana na MR.PATEL darasani.
 
NIMELAZIKA KUANDIKA sana ili watu wapate ujumbe naamini kuna ya msingi out of my pumba.niliowaboa mtanisamehe natanguliza uzalendo itakuwa aibu na ajabu mtu afunge safari kwenye kusoma kwa mzungu anakutana na MR.PATEL darasani.

Cha ajabu hapo ni kipi? Usinichekeshe kanda2, kwani mtu anaenda kusoma ulaya ili akafundishwa na mzungu?
 
Maandishi yako tutayaamini vipi wewe mwenyewe ukisema sijui alichukua eneo gani?Mie sijagombana na DR.Shayo na siwezi kumvunjia heshima kwani natambua kama mtalaam wa mazingira.

Aliyeleta uongo ni Yebo yebo kuwa DR.Shayo ni associate professor wa uchumi wakati muajiri wake kasema ni mtalaam wa mazingira yuko kitengo cha Construction, jee Yebo yebo apewe adhabu gani kwa kupotosha watu? na kusema uongo wa dhahiri? sina shuki na DR.Shayo always nimekuwa nikisema kuwa jamaa ni msomi na ninamwita DR. post zote. tittle ya thread ni ushuhuda wa haya. nimesema DR.SHAYO WA UK SI BINGWA WA UCHUMI. maana nakubali kuwa ni dr. na bingwa ila si bingwa wa uchumi ni bingwa wa mazingira,hapo hakuna tusi wala kupotosha.

JF sio kama michuzi blog ukimpa zawadi ya fulana na ukimwambia mimi ni jack Pemba ndio agent wa wachezaji UK bila kuliiza anakupaisha.
hapo tunahoji ndio maana EPA ETC vita vyake vilianzia hapa kwa nguvu za kina FIELD MARSHAL ES na wenzake.

Mzee ninadhani wewe Binafsi hujawahi kusoma Uchumi na mtu akikuambia ni Economist sijui unaelewaje? Dr shayo ni Economist , kwenye Economics unaweza ukatumia anlytical tools unazozi acquire na ukaamua ku specialize in any Field. Na kazi ya Mchumi ni kushauri methods ambazo zitaboresha uses of scarce resources Efficiently na kupunguza costs , ndio maana kuna wachumi wa waliobobea katika mambo ya kilimo, wachumi wa fedha, wachumi wa ,ma,mbo ya sheria na hata siasa, so whe n you speaking about ecomics is a very big field. Kuhusu swala la Dr shayo kufanya kazi kwenye kitengo cha construction ni sawa, it means he understand the Material economics, always katika ujenzi we want to reduce cost, kama utafiti wake unahusu kupunguza galama za ujenzi bila kuadhiri mazingira yes it make sense, he is still an economist, Kampuni kama IKEA inatumia wachumi ku fanya utafiki wa miti itayokuwa haraka na inayopatikana kwa bei nafuu, so si shangai kwa mchumi kufanya kazi za mazingira because mazingira is still a component of means of production. Wachumi wote waliowengi they use econometrics , statistics and some computational models kufanya research in any field. Labd kwa nyongeza tu, watu wengi wenye PHD za Uchumi unakuta hata fani zao za kwanza sio uchumi, wengine huwa ma engieer, wanasiasa, uwezo wake wakufanya Research using Econometrics models , make him mchumi than a title on his PHD

Pili kuhusu hiyo shule ya london hiyo shule ni longolongo na itakuwa hairuhusiwi kisheria kutoa Degree labda inatoa degree kupitia vyuo vingine, university zote zenye charter ya Universiity in UK website zao zinaishia na ac.uk mfano kama jamiiforum ingekuwa university website yake ingekuwa www.jamii.ac.uk because u have to reach certain starnadrd ya kutambulika na charter ya university ya UK ili uweze kutumia hiyo ac.uk ukiona chuo chochote kinatumia ..com ujue ni longolongo
 
Bonyezeni hapo;

Higher education funding council for England: Summary of 2009-10 grants

Column ya 5, bonyeza in order of grant reduction.

Kanda2, achana na huyo anayeng'ang'ania LSC ni college za maana. Mimi ningependa kujua kama kuna wazungu wazawa wanasoma hivyo vi-college uchochoro. msidanganye watu, kama wewe unapenda kisomo na una hiyo £3000, please please go to India, SA au Malaysia, au baki tu Tanzania, utapata kisomo cha maana zaidi. Kama unataka kujilipua au ili mradi umekuja ulaya, basi dandia boti ya LSC. If you go to these colleges, chances of being employed in your field is close to zero.

Halafu sijawahi kuona ''Associate Prof.'' hana hata article kwenye Journal ya maana. Nina access na Journal karibu zote, naomba article ya Economy yoyote aliyoandika, hata journal ya development studies. Kama anatafuta njia ya kuingia siasa ya bongo 2010, awadanganye huko, ila sisi tutachambua utumbo.
 
Back
Top Bottom