Dr. Shayo wa UK si bingwa wa uchumi

wewe babu katafute kazi nyingine ya kufanya hacha umbea na wivu. Tupo hapa tunachungulia. Hapa siyo ze-utamu ambako wadau wanamwaga datazzzzz za kipuuzi

shayo ni msomi , kwa hiyo kama unapingamizi na elimu yake, mwandikie barua au mpigie simu. Hacha kujadili watu kama una kitu cha kuchangia katika mada zake, basi ilete badala ya kumjadili mtu binafsi

Mdau anatumia haki yake ya kikatiba kutoa maoni yake. Wewe kama unaona umbea nenda kwenye thread ambazio unaona sio umbea..ebo!
 
Vichwa vyenye ubongo timilifu hujadili masuala,vichwa vyenye ubongo wenye uwezo mwepesi hujadili watu...need I say more?

wewe hujawahi kuwajadili watu humu? VC wa mzumbe hajajadiliwa humu kwenye jf?
 
wewe hujawahi kuwajadili watu humu? VC wa mzumbe hajajadiliwa humu kwenye jf?

Kwa theory hiyo,why ROSTAM and not BAKHRESA?au MOHAMMED DEWJI?au hata MENGI?(Mind you I'm not referring to Kanda ya Ziwa bali why ROSTAM became to pick katika hiyo ishu ya EPA na sio hao wengine -ambao wana-fit in your hypothesis)
Quod erat demonstrandum !
 
1. South Bank University ni miongoni mwa vyuo hapa London vinavyoheshimika. Mimi nakijua na nipo hapa London.

2. Naomba ufahamu kuwa rank zinazotolewa na mitandao za vyuo hazina ukweli hata wa 80% mfano hapa UK kuna university nyingi sana na ipo mitandao mingi inayojaribu kuvirank mfano unaweza ukakuta mtandao A umeirank metropolitan University ya 60 mtandao B unaweza irank ya 20 na mtandao C ukairank ya 113 hapo utaona uwiano haupo.

3. Kingine kila mtandao unacriteria zake.

4. Pia mtu kuitwa bingwa kwa kiingereza ni expert AU Specialist ni kwamba anatakiwa awe na Masters digree. Sasa ni vema ukaweka hapa CV ya Dr Shayo kabla hujaanza kumponda.

Kukaa London sio sababu ya wewe kujua kila kitu nina mashaka na ukaaji wako London na ukashindwa kujua kuwa London South bank sio chuo cha maana.
hebu jaribu kupita kwenye Academic Departments za chuo cha LEICESTER University of Leicester au Warwick Welcome to the University of Warwick linganisha na chuo chako cha Southbank London South Bank University - become what you want to be halafu uje kutuambia kuwa walio rank ni wajinga.
pia pitia CV za staff wa vyuo hivi mfano kitengo cha sheria Leicester malecturer wao walivyokwenda shule.

kingine maeneo ya South Bank yanathibitisha sio chuo bora kwani kipo eneo la wajamaica ambao si wasomaji na hao ndio wanafunzi wa south bank.

yaani sawa na chuo kipo mtaa wa congo wakati Mzumbe au Udom au Udsm mandhari yake tu yanathibitisha kuwa wako kwenye eneo la kusoma.
watanzania muwe wenye kufanya utafiti hata kama hatujafika ulaya lakini information zote ziko kwenye mitandao.

hata kozi za south Bank nyingi ni part time kwa masters hilo linathibitisha hawana namba ya kutosha ya wanafunzi. mfano wa kozi ya MBA iko very shallow na haiko recognised na Association of MBA au kwa kifupi AMBA.
Tizameni MBA program ya Nottingham university na South bank halafu mjue kuwa pumba ni zipi na mchele ni upi?

kaka Yebo yebo naona hujanijibu tena, hoja sio kama DR.Shayo hajasoma ila amesoma kozi nyingine na kujifanya mtalaam wa uchumi.

Udsm kuna watu walikuwa wanasoma sociology lakini wanajifanya wako Law ni hulka ya watu.
 
Huyu jamaa ni mjanja mjinga mmoja hivi. Hivi anadhani kujiita mchumi ndio ujiko? Kwa kusoma utumbo wake kwenye mitandao ni ushahidi tosha kuwa jamaa ni mweupe.

No wonder yupo busy na ku advertise his ignorance kule michuzi
 
Last edited:
Yebo yebo.
Umeona vitu alivyoweka Yoyo hapo juu? DR.shayo yuko kitengo cha Environment hakuna uchumi hapo source ni chuo chenyewe sio Yebo yebo.

mnaosema tusijadili watu jee tunajadili nini kila siku humu?mara Rostam, mara Mengi kwani mtu kujipa sifa ambayo sio yako sio ufisadi?

Kamala,Nagu,Nchimbi wamejadiliwa sana humu kwanini tuwajadili wakati elimu yao haihusiani na siasa zao? acheni double standard zenu.

mnaweza kupitia universities league table kujua kuwa London southbank University si chuo cha maana.hili litawasaidia wanaotaka kwenda kusoma UK wawe waangalifu kwenye kuchagua vyuo.

DR.Shayo ni bingwa wa mazingira amsaidie waziri DR.batilda Burian kwenye uchumi awaache kina Professor Ndullu na Lipumba.

Nawe weka vielelezo vyako kutetea hoja yako la sivyo inabakia kuwa ni habari ya udaku na chuki binafsi. stupid minds discuss people!
 
Kwa muda mrefu mdau wa UK Dr.Shayo amekuwa akiitumia blog ya Issa Michuzi na kujifanya kama ni mtaalam wa uchumi toka London Southbank university wakati ukweli ni kuwa Dr.Shayo ni bingwa wa mazingira na hana hata certificate ya uchumi.

nia yangu ni kuwaweka wazi wenzangu,kwani tumewahi kumpata bwana Jack Pemba akisema yeye ni ajenti wa mpira toka UK wakati website ya Fifa haisemi hivyo.

ukipitia website ya London SouthBank University www.lsbu.ac.uk chuo hicho hakina kozi hata ya diploma ya uchumi na pia si katika vyuo bora UK.
Naomba wanaomjua DR.Shayo au DR.Shayo mwenyewe atupe ukweli wa habari labda nilivyofahamu mimi ni tofauti.

Hivi karibuni alifanya Interview kama mtalaam wa uchumi toka UK mimi niliamini hivyo hadi nilipoelezwa tofauti. hili linatusaidia huko mbele ya safari kwani kuna watu wamewahi kuja hapa nchini wakisema wamehitimu utawala marekani wakapewa UVC wa Mzumbe wakati ukweli sio ulivyo.
kinga ni bora kuliko tiba.
Duh basi sio momi na wewe je kaka usomi wako ni kiwango gani?
 
Nawe weka vielelezo vyako kutetea hoja yako la sivyo inabakia kuwa ni habari ya udaku na chuki binafsi. stupid minds discuss people!

Kwa hiyo DR.shayo ni mchumi? niweke nini wakati Southbank wenyewe wamesema kuwa ni mtu wa mazingira yuko kitengo cha construction.kwa habari zaidi chuo hiki hakina HATA kitengo cha uchumi wachilia mbali kuwa na kozi ya certificate ya uchumi. shayo kasomea mazingira ..PERIOD.
jaribu kuona hawa wenzenu walivyo University of Leicester au Welcome to the University of Warwick
kwanini ujipe sifa si zako kama sio ulaghai?
ndugu yangu prevention is bette than cure.
 
Nawe weka vielelezo vyako kutetea hoja yako la sivyo inabakia kuwa ni habari ya udaku na chuki binafsi. stupid minds discuss people!

Vielelezo gani unataka zaidi ya maelezo ya chuo chenyewe. kwanini wewe usije na hivyo vielelezo kukanusha kauli yangu.kina professor Lipumba wanajulikana wamesoma STANFORD UNIVERSITY lakini Shayo kasoma wapi uchumi?

angekuwa anatupatia habari kwenye michuzi blog siku ya mazingira duniani au kuchangia pale tunapomuona dada yetu DR.Burian anaposafisha stendi ya Ubungo siku ya mazingira duniani amekuwa mchoyo wa kutupa elimu aliyo nayo au alisoma kozi hiyo kwa kulazimishwa? ndio maana kwenye michuzi blog utamsikia akisema maneno machache akiyarudiarudia nayo ni demand and supply.
 
"kuja hapa nchini wakisema wamehitimu utawala marekani wakapewa UVC wa Mzumbe wakati ukweli sio ulivyo.
kinga ni bora kuliko tiba"


Isuue ya Mzumbe si hivyo, jamaa alisoma ila chuo hakitambuliki yaani hakikuwa registered, na hili ni tatizo la kawaida kwani hata bongo zipo secondari kibao zisizokuwa na usajili.
 
hapana mkuu hukunisoma vema.....nilisema watu watamuambia ana hate....lakini ukweli ni kuwa jamaa sio bingwa wa uchuni ndio wale wale wakina mashaka wa wall street ya North carolina.....
-
labda sijajua tafsiri vizuri

https://phonebook.lsbu.ac.uk/php4/person.php?name=shayo.h
yani hapo imekuchukua dakika moja tu ukaja na link
the beauty of the internet

unajua marekani kama mtu unafanya kwenye financial instutition hata kama aiko nyc wanakuita unafanya wall street...

wenyewe wapo humu ndani watakutoa roho..
 
Kwa muda mrefu mdau wa UK Dr.Shayo amekuwa akiitumia blog ya Issa Michuzi na kujifanya kama ni mtaalam wa uchumi toka London Southbank university wakati ukweli ni kuwa Dr.Shayo ni bingwa wa mazingira na hana hata certificate ya uchumi.

nia yangu ni kuwaweka wazi wenzangu,kwani tumewahi kumpata bwana Jack Pemba akisema yeye ni ajenti wa mpira toka UK wakati website ya Fifa haisemi hivyo.

ukipitia website ya London SouthBank University www.lsbu.ac.uk chuo hicho hakina kozi hata ya diploma ya uchumi na pia si katika vyuo bora UK.
Naomba wanaomjua DR.Shayo au DR.Shayo mwenyewe atupe ukweli wa habari labda nilivyofahamu mimi ni tofauti.

Hivi karibuni alifanya Interview kama mtalaam wa uchumi toka UK mimi niliamini hivyo hadi nilipoelezwa tofauti. hili linatusaidia huko mbele ya safari kwani kuna watu wamewahi kuja hapa nchini wakisema wamehitimu utawala marekani wakapewa UVC wa Mzumbe wakati ukweli sio ulivyo.
kinga ni bora kuliko tiba.

Jamani, mimi kwanza naanza kwa kumpongeza huyu mtu, kama anaweza kuongelea fani ambayo hana 'formal qualifications' nadhani anastahili pongezi, inawezekana akaweza kufafanua maswala (hoja ) ya uchumi kuliko hata wale wenye PhD za uchumi.
Pili, siku hizi kuna degree za online, inawezekana amefanya(au bado ni candidate wa) online degree ya mambo hayo ya uchumu, mfano MBA zipo za aina nyingi na zinapatikana kiurahisi duniani kote, hivyo nadhani anaweza akawa na sifa ya kuongea na kuchangia mada mbalimbali za uchumi.
Tatu, inawezekana huyu bwana ni 'SELF READER' wa maswala ya uchumi, yaani inawezekana kutokana na interest aliyonayo kwenye uchumi, akawa anasoma vitabu mbali mbali, journals, magazines nk za uchumi, mtu kama huyu anaweza akawa 'uptodate' kuliko hata mtu mwenye masters au PhD aliyopata, mathalani 1998, na akawa mzembe wa kujisomea(self continue proffesional education) naakaendekeza pombe tu .. ukiwapambanisha watu hawa wawili, nadhani huyu wa kwanza atamwaga cheche(points) kuliko mwenye PhD lakini cha pombe.
Nimalizie kwa kuwaomba watanzania wenzangu tu pende kujisomea mambo malimbali tofauti na fani yako, usikomae tu na Labda IT au Engeneering, soma basic madicine, uchumi,arts, genetics nakadha wa kadha.
Mwisho kabisa, sijafurahishwa na huyo Dr Shayo alivyo jitambululisha kuwa yeye anafundisha huko London, nadhani atakuwa anafanya Post-doctoral au kitu kingine, angejitambulisha kwa uhalisia wake, nadhani angepata sifa zaidi kuliko sasa hivi ambapo watu wanamnyooshea vidole.
 
kwa mujibu wa london south bank wameandika kuwa dr.shayo position yake ni senior research fellow.

Department ya engineering,science and the built environment.
Yuko section ya property,surveying and construction.

Huo u associate professor wa economics umempa wewe.
Kwanza chuo chenyewe hakina kozi hata moja ya uchumi tizama website yao.
Wangesema kama yuko kitengo cha uchumi acha kuwafagilia watu kibubusa.

mimi nashangaa, kwa nini tunakuwa tunajenga hoja kama watoto wachekechejea? Hivi unataka iandikwe bachelor of economics au? Hujui karibia kila kozi japo si zote wanafundishwa uchumi?, wanafundishwa project planning and management as a module? Hivi unadhani hata maainjinia hawali dozi za uchumi? Unafahamu source ya planners, hujui planning field imekuwa developed from engeneering?. Sometimes hoja nyingine zina bore sana samahanini kama nimekosea kukomenti hivyo but sina neno mbadala.
 
Kukaa London sio sababu ya wewe kujua kila kitu nina mashaka na ukaaji wako London na ukashindwa kujua kuwa London South bank sio chuo cha maana.
hebu jaribu kupita kwenye Academic Departments za chuo cha LEICESTER University of Leicester au Warwick Welcome to the University of Warwick linganisha na chuo chako cha Southbank London South Bank University - become what you want to be halafu uje kutuambia kuwa walio rank ni wajinga.
pia pitia CV za staff wa vyuo hivi mfano kitengo cha sheria Leicester malecturer wao walivyokwenda shule.

kingine maeneo ya South Bank yanathibitisha sio chuo bora kwani kipo eneo la wajamaica ambao si wasomaji na hao ndio wanafunzi wa south bank.

yaani sawa na chuo kipo mtaa wa congo wakati Mzumbe au Udom au Udsm mandhari yake tu yanathibitisha kuwa wako kwenye eneo la kusoma.
watanzania muwe wenye kufanya utafiti hata kama hatujafika ulaya lakini information zote ziko kwenye mitandao.

hata kozi za south Bank nyingi ni part time kwa masters hilo linathibitisha hawana namba ya kutosha ya wanafunzi. mfano wa kozi ya MBA iko very shallow na haiko recognised na Association of MBA au kwa kifupi AMBA.
Tizameni MBA program ya Nottingham university na South bank halafu mjue kuwa pumba ni zipi na mchele ni upi?

kaka Yebo yebo naona hujanijibu tena, hoja sio kama DR.Shayo hajasoma ila amesoma kozi nyingine na kujifanya mtalaam wa uchumi.

Udsm kuna watu walikuwa wanasoma sociology lakini wanajifanya wako Law ni hulka ya watu.

WEWE WARWICK NA LEICESTER NDIYO UNAONA UNIVERSITIES ZA KUTOLEA MFANO? KWA TAARIFA YAKO OXFORD NDIO CHA KWANZA, CAMBRIDGE NI CHA PILI.

MIMI SISOMI HAPO ILA NAKIJUA SANA, NA MAHALI KILIPO NAKIJUA, KWA TAARIFA YAKO KIPO MAHALI PAZURI TU NA NI KIKUBWA, POINTI ZAKO WALA SIZIONA KAMA ZINA KICHWA HIVYO SINTAZIJADILI.

Kazi njema
 
mimi nashangaa, kwa nini tunakuwa tunajenga hoja kama watoto wachekechejea? Hivi unataka iandikwe bachelor of economics au? Hujui karibia kila kozi japo si zote wanafundishwa uchumi?, wanafundishwa project planning and management as a module? Hivi unadhani hata maainjinia hawali dozi za uchumi? Unafahamu source ya planners, hujui planning field imekuwa developed from engeneering?. Sometimes hoja nyingine zina bore sana samahanini kama nimekosea kukomenti hivyo but sina neno mbadala.

Mwenye digri ya medicine nae anajua uchumi kwani anampa mgonjwa dawa kwa kupiga hesabu na kupanga dawa hii muda huu na ile baada ya masaa kadhaa.anayechukua IT nae mchumi. unaweza kuwa na basic knowledge haikupi tiketi ya kujitangaza kwenye mablog kuwa wewe ni mtalaam wa uchumi.

Rais Aman karume na marais wa Africa mashariki walialikwa kwenye mambo ya uchumi Uingereza mapema mwaka huu,Dr.shayo akaposti kwa michuzi kuwa nae kaalikwa na serikali ya Uingereza kutokana na utalaam wake wa uchumi kitu ambacho si kweli.

unajua ilikuwaje hadi mzungu akapewa ukurugenzi wa hospital ya Muhimbili? kwa vile kulikuwa hakuna daktari mzalendo mwenye elimu ya uongozi mzungu alikuwa na MD plus MBA.kama kila somo lazima uzome uchumi hakukuwa na haja ya mzungu yule kupewa Muhimbili.pia haina haja ya watu kusoma digrii ya uchumi kama kila kozi inafundisha uchumi.
 
Jamani, mimi kwanza naanza kwa kumpongeza huyu mtu, kama anaweza kuongelea fani ambayo hana 'formal qualifications' nadhani anastahili pongezi, inawezekana akaweza kufafanua maswala (hoja ) ya uchumi kuliko hata wale wenye PhD za uchumi.
Pili, siku hizi kuna degree za online, inawezekana amefanya(au bado ni candidate wa) online degree ya mambo hayo ya uchumu, mfano MBA zipo za aina nyingi na zinapatikana kiurahisi duniani kote, hivyo nadhani anaweza akawa na sifa ya kuongea na kuchangia mada mbalimbali za uchumi.
Tatu, inawezekana huyu bwana ni 'SELF READER' wa maswala ya uchumi, yaani inawezekana kutokana na interest aliyonayo kwenye uchumi, akawa anasoma vitabu mbali mbali, journals, magazines nk za uchumi, mtu kama huyu anaweza akawa 'uptodate' kuliko hata mtu mwenye masters au PhD aliyopata, mathalani 1998, na akawa mzembe wa kujisomea(self continue proffesional education) naakaendekeza pombe tu .. ukiwapambanisha watu hawa wawili, nadhani huyu wa kwanza atamwaga cheche(points) kuliko mwenye PhD lakini cha pombe.
Nimalizie kwa kuwaomba watanzania wenzangu tu pende kujisomea mambo malimbali tofauti na fani yako, usikomae tu na Labda IT au Engeneering, soma basic madicine, uchumi,arts, genetics nakadha wa kadha.
Mwisho kabisa, sijafurahishwa na huyo Dr Shayo alivyo jitambululisha kuwa yeye anafundisha huko London, nadhani atakuwa anafanya Post-doctoral au kitu kingine, angejitambulisha kwa uhalisia wake, nadhani angepata sifa zaidi kuliko sasa hivi ambapo watu wanamnyooshea vidole.

Huwezi kuwa unasoma journals on line ukashindana na aliyekwenda darasani kwenye fani kama hii ya uchumi unataka kusema kuwa professor Abdallah Safari,DR Fauz Twalib au Professor Mgongo Fimbo hawa ni watalaam wa sheria wanaweza kupitwa na John Mashaka wa michuzi blog kwenye fani ya sheria kwa vile john Mashaka anasoma journals on line kuliko wao?

Ikitokea mhadhara wa mambo ya sheria tumuite John Mashaka badala ya hao watalaam? unajua dr.shayo hivi karibuni katoa mada kwa michuzi blog kama mtalaam wa uchumi? kwenye mazungumzo yake unajua kabisa huyu jamaa anadanganya na hana hakika anachokisema, ni sawa na wewe upate ugonjwa na ukipelekwe hospitali aje DR.Shayo aseme amesoma online-journal nyingi za medicine atakufanyia oparesheni jee utakuwa tayari kumuacha professor Mtulia au Mwakyusa waliosomea na kuifanyia kazi tiba na kumpa shayo?.

kibaya zaidi umeona alivyoweka Yebo yebo kuwa DR.Shayo ana business cards akiwaonesha kuwa ni Associate professor wa uchumi,watu wasio pima mambo kama Yebo yebo wanaamini kienyeji bila kufanya juhudi za kujua ukweli wa mambo.

kama kadi mimi naweza kutengeneza kuwa ni professor wa uchumi.Lutta Nelson alikuwa akijulikana kama DR.lutta kwa muda mrefu kumbe hata kidato cha sita hajafika alikwenda kuumbuka mahakamani kesi ya uchaguzi KIBAHA.
Kama angekuwa amesoma MBA Chuo anachofundisha kingesema au kama anafanya kozi kwenye eneo hilo,post ya Yebo yebo na associate professor ya uchumi imezidi kunipa mashaka juu yake labda iwe Yebo yebo kaandika kufurahisha mjadala lakini kama kweli DR.shayo anatembea na hizo kadi sio sahihi.

Mwisho jamaa ni kweli DR na anafundisha mambo ya Environment-Mazingira South bank hilo halina shaka kinachotia shaka kujitengenezea mazingira kama Mtaalam wa uchumi kiasi cha waingereza kumualika kwenye mjadala wa uchumi kwa nchi za Africa tizama kwenye michuzi kwenye picha za Rais Karume Uingereza.
 
Mwenye digri ya medicine nae anajua uchumi kwani anampa mgonjwa dawa kwa kupiga hesabu na kupanga dawa hii muda huu na ile baada ya masaa kadhaa.anayechukua IT nae mchumi. unaweza kuwa na basic knowledge haikupi tiketi ya kujitangaza kwenye mablog kuwa wewe ni mtalaam wa uchumi.

Rais Aman karume na marais wa Africa mashariki walialikwa kwenye mambo ya uchumi Uingereza mapema mwaka huu,Dr.shayo akaposti kwa michuzi kuwa nae kaalikwa na serikali ya Uingereza kutokana na utalaam wake wa uchumi kitu ambacho si kweli.

unajua ilikuwaje hadi mzungu akapewa ukurugenzi wa hospital ya Muhimbili? kwa vile kulikuwa hakuna daktari mzalendo mwenye elimu ya uongozi mzungu alikuwa na MD plus MBA.kama kila somo lazima uzome uchumi hakukuwa na haja ya mzungu yule kupewa Muhimbili.pia haina haja ya watu kusoma digrii ya uchumi kama kila kozi inafundisha uchumi.

Kanda2, kimsingi sitofautiani nawewe, na nilichokuwa nasema ni kama ulivyosema ila ifahamike kuwa hayo masomo kama uliyosema basic ni lazime yafundishwe na wataalamu (Nikisema wataalamu namaanisha kuanzia digrii ya pili).

Kwa habari ya kudanganya kama alifanya hivyo mimi simuungi mkono hata nukta.

Hoja yangu ni kwamba ili tumjaji kwamba siyo bingwa TUWEKEE HAPA CV yake. Tatizo hatuna CV yake ambayo ingetufanya tujue kasoma SHAHADA ZA UZAMILI KATIKA FANI IPI, NA SHAHADA YAKE YA UZAMIVU NI KATIKA FANI IPI.

Otherwise, itakuwa vigumu kukubaliana nawe kama hatutajua au hatutapata hizo information. Hiyo ndiyo pointi ninayoisema.
 
WEWE WARWICK NA LEICESTER NDIYO UNAONA UNIVERSITIES ZA KUTOLEA MFANO? KWA TAARIFA YAKO OXFORD NDIO CHA KWANZA, CAMBRIDGE NI CHA PILI.

MIMI SISOMI HAPO ILA NAKIJUA SANA, NA MAHALI KILIPO NAKIJUA, KWA TAARIFA YAKO KIPO MAHALI PAZURI TU NA NI KIKUBWA, POINTI ZAKO WALA SIZIONA KAMA ZINA KICHWA HIVYO SINTAZIJADILI.

Kazi njema

Umejadili halafu umesema hutajadili,nimekupa mfano wa NOTTINGHAM,LEICESTER NA WARWICK kama mfano najua vizuri sana kwani siwezi kuifananisha OXFORD au Cambridge huko sio kwetu mimi na wewe ndio nikakupa Nottingham wajipime na chuo chako-Southbank.

kukusaidia kama najua nikupe ranking za mwaka huu 2009.

1.Oxford 2.Cambridge 3.Imperial College.4.London school of Economics-LSE. 5.ST.Andrews. 6.Warwick 7.University College London-UCL.

8.Durham University. 9.York 10.Bristol 11-King's College London. 12-loughborough 13-Exeter University. 14-Leicester University.
15-Bath University 16-Nottingham.

ninajua chuo kama OXford wazuri zaidi kwenye utawala,siasa etc wakati Cambridge kwenye sayansi.

Kings college London kwenye sheria na medicine, LSE ni wakali kwenye uchumi na siasa. Warwick wazuri sana kwenye sheria,UCL kwenye sheria n.k
Naomba usiwadanganywe watanzania Southbank sio chuo bomba au unapata kamisheni kwa kuwapeleka hapo chuoni?

kukusaidia University ranking league table 2009 timesonline.co.uk wameonesha kuwa chuo cha London Southbank ndio cha mwisho kwa kushika nafasi ya mwisho ya 113.

watanzania vyema tuwe tunafanya tafiti kwenye kuchagua vyuo wenzetu wazungu wana guide maalum kwenye chaguzi za vyuo-THE ESSENTIAL GUIDE TO PICKING THE RIGHT PLACE kwenye vyuo vikuu.timesonline wana huduma hiyo.jaribuni kupitia website ya chuo kimoja hadi kingine hata kama gazeti lingine litakuwa na mtazamo tofauti hauwi mbali wanaweza kusema LSE ni ya nne na Imperial ni ya tano. lakini hawawezi kuweka Southbank nafasi hata ya 90 lazima kiwe mkiani kabisa.

ukitizama michuzi blog kuna chuo anakitangaza London school of Commerce kuwa wanatoa digri kwa miaka miwili au MBA kwa pound elfu 3900 na wana intake sita kwa mwaka kitu kama hicho waTanzania inabidi tufanyie utafiti wa kutosha kabla ya kujisajili, kwangu mimi hakijanikalia vizuri chuo cha intake sita kwa mwaka na digri kwa miaka miwili.kama MBA ni £3900 bora mtu usome IFM wana masters kozi zina link na chuo cha UK kwa fikra zangu.
 
Back
Top Bottom