QUALITY
JF-Expert Member
- Sep 27, 2010
- 853
- 115
Nimekuwa natafakali sana kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka huu. sasa naona Dr. Slaa amemfunika Kikwete. Mimi nasafiri jijini dar mara kwa mara. nina ndugu, jamaa na marafiki katika mikoa mikoa ya Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Morogoro, dar es salaam, Mwanza, Arusha, Kagera, mara, Shinyanga, Dodoma n.k. Kote huko, Dr. Slaa anaongoza mijini na vijijini. hata ukifanya utafiti humu JF utaona kuwa JK anafunikwa vibaya sana.
Najua kesho ndo tunaenda kumhukumu Jk kwa mabaya yote aliyotufanyia kwa miaka mitano ikiwa ni pamoja na kushindwa kusimamia rasilimali za nchi ziwanufaishe watanzania badala ya wageni.
Sasa Dr. Slaa kura zake zikiongoza
mwenye jibu?
Najua kesho ndo tunaenda kumhukumu Jk kwa mabaya yote aliyotufanyia kwa miaka mitano ikiwa ni pamoja na kushindwa kusimamia rasilimali za nchi ziwanufaishe watanzania badala ya wageni.
Sasa Dr. Slaa kura zake zikiongoza
- Kikwete ataruhusu mkurugenzi wa NEC amtangaze Dr. Slaa kuwa ndiye Mshindi?
- Je Mkurugenzi wa NEC akimtangaza Dr. Slaa kuwa ndiye mshindi kinyume na matakwa ya JK, JK atakubali matokeo hayo na kukabidhi ikulu?
- Je kama JK akimkataza Mkurugenzi wa NEC na akakubali kumtangaza JK kama ndo mshindi halali, siri ikavuja (kwa maana hata NEC kuna wafuasi kibao wa Dr. Slaa) itakuwaje?
mwenye jibu?