Dr.Paul Swakala ni kada mkubwa wa CCM!

IsangulaKG

JF-Expert Member
Oct 14, 2010
706
386
Wadau, taarifa nilizozipokea muda mfupi uliopita zimethibitisha kuwa Dr. Swakala, kiongozi wa kamati ya madaktari walioomba msamaha ni kada mkubwa wa CCM.
Dr.Swakala, akiwa Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo cha BUGANDO alifikia hatua kukigeuza Chuo kama Tawi la CCM kwa kuwashawishi wanafunzi wenzake kujiunga na CCM pamoja na kusambaza kadi. Pia daktari mwingine aliyetajwa, ambaye pia ni mmoja wa wale walioomba msamaha na mmoja kati ya wapishi wa move nzima Dr.Nuru Mwambola, aliwahi kutuhumiwa kuwahujumu wanafunzi wenzake wa udaktari akiwa Makamu wa Rais pale Kairuki mpaka kufikia kupigiwa kura ya kutokuwa imani nae.

Dr.Nuru, ambaye amekuwa Mwanachama mtiifu kwa CCM alikuwa akitumika kushawishi wanafunzi wenzake kujiunga na CCM akiwa chuoni. Ni kwa kutumia nafasi hiyo, yeye Nuru, pamoja na Swakala walikwenda kwa mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kinondoni Wakili Makene tar 21.08.2012 na kumuomba awakutanishe na Stephen Wassira ili waweze kuonana na Rais.
Wakili Makene aliwajibu kuwa Wassira yupo nje ya Dar ila ametoa maelekezo kuwa Rais yupo tayari kuwaona ila waombe msamaha kwanza kwa rais, serikali na wananchi. Baada ya agizo hilo ndipo wakaendelea na mchakato wa kukusanya majina ya interns, na kwa taarifa zilizopo ni kwamba ni inters 150 tu kati ya 319 ndio waliotuma majina yao.
Baada ya kutekeleza agizo la kuomba msamaha hapo jana, baadhi ya wajumbe wa kamati ya Madaktari wa CCM walikwenda wizarani ili kupata mrejesho, na Naibu Waziri aliwajibu kuwa Mwizi akikiri ameiba kinachofuata ni hukumu.

Habari hii ni kwa hisani ya Daktari ambaye hakupenda jina lake litajwe.

Shukrani Ritz kwa angalizo lako!
 
Daktari wa ukweli, aliye fikia ngazi ya udaktari kwa uwezo wake mwenyewe bila kuchakachua ama kubebwa kwa namna yeyote ile, anajiamini na anatumia akili yake kuamua. Huyo Dk. Swala Kala amajidhalilisha si mtofautishi na Dk. Tallwater anayelamba viatu vya wafilisi nchi!
 
Jamani msiumize vichwa kuhusu wasaliti hawa.Kwani kwenye msafara wa mamba hata kenge wamo.
 
Huyo ni "Sakala". Don't misuse the word Dr. Angekuwa Dr wa kweli asingefanya utumbo wa kuidhalilisha taaluma adimu namna ile.
 
Huyo ni "Sakala". Don't misuse the word Dr. Angekuwa Dr wa kweli asingefanya utumbo wa kuidhalilisha taaluma adimu namna ile.
`` huyu swakala ametufungua macho yetu nafikiri ni muda muafaka sasa kwa selikali kufungua kesi juu yao ya mauaji ya wa Tanzania kwa uzembe wao madaktari . Hakuna mungu nihurumie hapa hawa jamaa wanataka sisi tuamini kwamba DR ulimboka nae alipigwa kwa uzembe wake mwenyewe hii inatokana na kauli yao kwamba ati ``TUNAOMBA MTUSAMEE TULIFANYA MGOMO BILA KUJUA ATHALI ZAKE NASASA TUNAJUTIA MAKOSA YETU MBELE YA WATANZANIA MTUSAMEHE`` Hapa hakuna msamaha selikali ikiwasamehe hawa basi nawafungwa walioko jela waliofanya makosa bila kukusudia waachiwe wote wawe huru.
 
Huyo swala kala na wenzie waloandika hayo majina yao kuomba msamaha washitakiwe haraka,namuunga mkono naibu waziri.kwanza wamekiri makosa,pili wamewasaliti wenzao na watanzania kiujumla kwasababu mgomo ulikuwa ni kwa ajili ya ukombozi wa afya za watanzania wote
 
Duh! sikujua kama na siasa imo humu ndani ya sayansi ya tiba! wasira, kikwete, katibu wa ccm wilaya, hawa walipitia chuo gani cha tiba mpaka wahusishwe na muafaka wa madaktari?! Ki ukweli mimi nilipoona maombi hayo ya msamaha nilipandwa na hasira kiasi nilikaribia kupasua tv! Kuomba msamaha kwa kitendo kilichokuwa kinafanyiaka kwa haki ni upunguani na kuonyesha kuwa wale wote waliowaunga mkono katika harakati zao hawana akili!

Kama mapambano yalikuwa ni kudai waliyoainisha hakuna kuomba msamaha, bora kufa njaa kuliko kuweka ulimi puani!
 
Huyu Dr. Swala Kala nimesoma naye A-level na kwa jinsi nilivyokuwa namfahamu ni mtu ambaye kwa ujumla alikuwa mwoga sana, kwa maana nyingine hakuwa na msimamo. Ninavyofahamu mimi ni kwamba, kama akili zinafanya kazi sawa sawa unapokuwa unafanya jambo fulani ujue madhara yake ili uweke plan B. Inavyoonekana yeye aligoma bila ya kujua madhara yake na hivyo hakuwa na plan B, na pengine aliyokuwa nayo ndo hiyo ya kuomba msamaha. Kwa ujumla Dr. Swala Kala ni msabato feki kwani angekuwa halisia asingegoma tokea mwanzo kwa kuwa alijua kugoma kwake kutasababisha kupotea kwa uhai watu.
My take:
1. Walioomba msamaha wote wafunguliwe kesi ya kugoma.
2. Watakuwa ni kikwazo kikubwa kwa baadae kwa kuwa ikitokea tena wadai mahitaji ya madaktari wao hawatakuwa pamoja na wenzao.
3. Wataleta uhasama katika ofisi watakazokuwa wanafanya kazi kwani wenzao watawaona kama wasaliti.
 
Wakati wa kumpokea Ulimboka pale Airport alisema kapata kazi chuo cha KAM na anamshahara mzuri tu. Sas sijui nini kimemsibu?
 
Wadau, taarifa nilizozipokea muda mfupi uliopita zimethibitisha kuwa Dr. Swakala, kiongozi wa kamati ya madaktari walioomba msamaha ni kada mkubwa wa CCM.
Dr.Swakala, akiwa Rais wa Serikali ya wanafunzi Chuo cha BUGANDO alifikia hatua kukigeuza Chuo kama Tawi la CCM kwa kuwashawishi wanafunzi wenzake kujiunga na CCM pamoja na kusambaza kadi. Pia daktari mwingine aliyetajwa, ambaye pia ni mmoja wa wale walioomba msamaha na mmoja kati ya wapishi wa move nzima Dr.Nuru Mwambola, aliwahi kutuhumiwa kuwahujumu wanafunzi wenzake wa udaktari akiwa Makamu wa Rais pale Kairuki mpaka kufikia kupigiwa kura ya kutokuwa imani nae.

Dr.Nuru, ambaye amekuwa Mwanachama mtiifu kwa CCM alikuwa akitumika kushawishi wanafunzi wenzake kujiunga na CCM akiwa chuoni. Ni kwa kutumia nafasi hiyo, yeye Nuru, pamoja na Swakala walikwenda kwa mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kinondoni Wakili Makene tar 21.08.2012 na kumuomba awakutanishe na Stephen Wassira ili waweze kuonana na Rais.
Wakili Makene aliwajibu kuwa Wassira yupo nje ya Dar ila ametoa maelekezo kuwa Rais yupo tayari kuwaona ila waombe msamaha kwanza kwa rais, serikali na wananchi. Baada ya agizo hilo ndipo wakaendelea na mchakato wa kukusanya majina ya interns, na kwa taarifa zilizopo ni kwamba ni inters 150 tu kati ya 319 ndio waliotuma majina yao.
Baada ya kutekeleza agizo la kuomba msamaha hapo jana, baadhi ya wajumbe wa kamati ya Madaktari wa CCM walikwenda wizarani ili kupata mrejesho, na Naibu Waziri aliwajibu kuwa Mwizi akikiri ameiba kinachofuata ni hukumu.

Habari hii ni kwa hisani ya Daktari ambaye hakupenda jina lake litajwe.

Shukrani Ritz kwa angalizo lako!
Sina uhakika kama suala la madaktari linahusiana na vyama vya siasa, na kama hao wamefanya kwa interest ya vyama vya siasa na si kwa matakwa yao, wamepotea.
 
products za university za Accademy thats why. Nina imani angekuwa kapitia MUCHS haya msingeyaona.
 
Back
Top Bottom