Amosam
Senior Member
- Jan 15, 2009
- 154
- 5
Nilikuwa nangalia kipindi cha Mch.Isaack Ndodi wa Haleluya Sanitarian Clinic kinachorushwa na kituo cha televisheni ya Star jumanne 08/09/09.
Katika mafundisho yake kuhusu madhara ya ulaji mbovu ambao unasababisha magonjwa mengi katika mwili wa binaadamu,aligusia na kusisitiza kuwa Nyama ya Kitimoto(NGURUWE) ni hatari na pia haikuruhusiwa na aliyeumba ulimwengu(Mungu).Amesema kuwa nguruwe ana vijidudu vya magonjwa mengi ambayo ni hatari kwa afya ya binaadamu.Alipoulizwa je sisi tunaekula kitimoto tutakuwa tumepata wapi agizo la kutumia nguruwe,alijibu namnukuu 'Mkristo yeyote atakayeweza kunitajia andiko linaloruhusu matumizi ya nyama ya nguruwe aje ofisini kwangu pale magomeni mwembechai nitamkabidhi gari yangu mpya NISSAN PATROL iwe yake moja kwa moja'.Akatoa baadhi ya maandiko yanayokataza ulaji wa nyama ya nguruwe kama walawi 11..tena akatoa andiko linalosema 'YESU KRISTO NI YULE YULE JANA,LEO HATA MILELE' hivyo hoja ya kusema eti walawi,kumbukumbu ya torati ni agano la kale halimuingii akilini.
Kwahiyo wenye maandiko katika vitabu vitakatifu vinavyoruhusu kuliwa kitimoto waende kwa Ndodi kwani Nissan Patrol ipo kwa ajili yao.
Onyo kama huna cha kuchangia mjadala huu angalia kisha ondoka, nahitaji wenye hekima na busara katika kuchangia,ukitoa pumba nitajua wewe ni walewale waliopitia shule lakini hawakuelimika.
Katika mafundisho yake kuhusu madhara ya ulaji mbovu ambao unasababisha magonjwa mengi katika mwili wa binaadamu,aligusia na kusisitiza kuwa Nyama ya Kitimoto(NGURUWE) ni hatari na pia haikuruhusiwa na aliyeumba ulimwengu(Mungu).Amesema kuwa nguruwe ana vijidudu vya magonjwa mengi ambayo ni hatari kwa afya ya binaadamu.Alipoulizwa je sisi tunaekula kitimoto tutakuwa tumepata wapi agizo la kutumia nguruwe,alijibu namnukuu 'Mkristo yeyote atakayeweza kunitajia andiko linaloruhusu matumizi ya nyama ya nguruwe aje ofisini kwangu pale magomeni mwembechai nitamkabidhi gari yangu mpya NISSAN PATROL iwe yake moja kwa moja'.Akatoa baadhi ya maandiko yanayokataza ulaji wa nyama ya nguruwe kama walawi 11..tena akatoa andiko linalosema 'YESU KRISTO NI YULE YULE JANA,LEO HATA MILELE' hivyo hoja ya kusema eti walawi,kumbukumbu ya torati ni agano la kale halimuingii akilini.
Kwahiyo wenye maandiko katika vitabu vitakatifu vinavyoruhusu kuliwa kitimoto waende kwa Ndodi kwani Nissan Patrol ipo kwa ajili yao.
Onyo kama huna cha kuchangia mjadala huu angalia kisha ondoka, nahitaji wenye hekima na busara katika kuchangia,ukitoa pumba nitajua wewe ni walewale waliopitia shule lakini hawakuelimika.