Dr. Mwandulame Amchana Babu wa Loliondo

kwa kweli kwa hili la serikali kumkumbatia mganga mmoja tu (na karibu baraza zima la mawaziri lilmeishakunywa kikombe), limenisikitisha sana

si kila mtu aniitaye "Bwana", "Bwana" ataurithi ufalme wa Mungu
bali yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni
...labda hujijui kwamba hutaurithi ufalme huo
kwa staili hii ya wivu n
 
jambo hili ni gumu halihitaji hukumu ya haraka. Kwa ubinadamu wetu lazima tuweweseke, lakini hebu tuangalie mazingira yake. Dawa ya babu inafahamika kama ni tiba kwa miaka mingi lakini si kwa dose moja kama afanyavyo babu. hii ndio ajabu ambayo haina majibu ya haraka. kwa mcha Mungu yeyote atabariki chakula kabla ya kula hata kikiwa na sumu haitadhuru, biblia inatueleza hivyo. babu anagawa dawa baada ya kuchemsha na kuibariki hatangazi dini kosa ni lipi! shetani anaingiaje hapa? Mungu ni dhaifu kuliko shetani hata ashindwe kusimamisha hili? Mbona wengi wamelaani na hata kufunga ili huduma ikome mbona inazidi kushamiri!!? Waganga wengi toka karne za nyuma kwa asilimia kubwa wameoteshwa hizo tiba je waliinuliwa kama babu? Mwacheni Mungu aitwe Mungu. Kwa kifupi dawa inahitaji imani mwenye imani anywe nawe usie na imani ukae kimya usije kujikuta unagombana na bosi wako (God)

Mwandulane, Majimarefu, Mzee wa Lupaso, Mama wa Tabora, Mwasapile, Mzee wa Sumbawanga wote ni waganga wa kienyeji tu kwa maoni yangu. Mwandulame anasema ameoteshwa na babu naye ameoteshwa!! Shetani naye ana nguvu zake, kumbuka Firauni alivyotuma nyoka kwa Mussa. Mijoka ile ilikuwa nguvu ya shetani. Ushetani wa hawa waganga wetu utajidhihirisha punde.
 
Hana hoja yoyote, soko lake tu limeyumba.
Kwani yeye anakosa nini kama si kukosa soko?

Tatizo ni kwamba Serikali inakumbatia Mganga mmoja tu wa kienyeji! Kama inaamini basi impe Babu ruhusa ya kuwa Hospitali ya RUFAA YA RUFAA, si watu wanatoka KCMC na MNH kwenda kuponea kwake. Nchi imekumbwa na pepo mchafu inabidi wenye dini zenu muiombee. Mimi sina matatizo na hao wote kwa kuwa imani yangu ni sawa na ya kwao yaani imani za asili. Ila ninyi wenye imani za kizungu kisha mnarudi huku kwetu kwenye imani za kienyeji na kumsingizia mungu wenu nawaonea huruma.
 
Bado nakuwa na wasiwasi na hii tiba mbadala,,
1, sijaskia mtu akisema huwa mimi nilikuwa hivi na sasa niko hivi,
2, je kikombe cha babu,, ni dozi moja tu!!
3, Mataktali wa taifa hii habari wanaithibitisha vipi?

God let us know the truth..
 
kwa kweli kwa hili la serikali kumkumbatia mganga mmoja tu (na karibu baraza zima la mawaziri lilmeishakunywa kikombe), limenisikitisha sana na sasa natambua wazi kuwa ushirikina umejikita sana mioyoni mwa viongozi wetu na wengi wetu

si kila mtu aniitaye "Bwana", "Bwana" ataurithi ufalme wa Mungu
bali yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni

Huyo mwandulami pamoja na baadhi ya viongozi wa dini wamepagawa kwa kupungukiwa wateja, hivi babu alijitangaza au aliomba atangazwe? bila shaka si hivyo! sasa watu kelele za nini? wote tunajua dhahiri kwamba kilichomtangaza ni matokeo ya tiba yake kwa kuwa inaponya! na waliopona wakashuhudia kwa wengine na wengine kwa wengine hivyo hivyo, hebu ona maajabu, babu yupo remote area samunge loliondo, barabara mbovu hakuna mitandao ya
mawasiliano lakini anavuma kuliko huyo mwandulami yupo kwenye barabara kuu ya makambako-songea na mawasiliano anayo, kaweka na sat. dishes kupata taarifa kutoka sehemu mbalimbali duniani lakini babu kamfunika! miss judith hao wanaosema wanaujua mti huo siku nyingi mbona hawakutibu? na ndo maana hawakuvuma kwa kuwa ni waongo. Kama umefatilia taarifa vizuri babu kasema kinachotibu si mti bali ni NENO lililopo ndani yake na kama wewe ni Mkristo unajua NENO ni nani! na utaona ndo maana babu hakufanya siri kuhusu mti na kaupanda mbele ya nyumba yake, maporini upo, kama wanaweza na wao wachukue watibu hayo magonjwa sugu wapate sifa! mti huo inasemekana ulitumika na baadhi ya watu kutuliza maumivu ya jino n.k lakini haukuweza kutibu magonjwa hayo sasa MUNGU anaonesha kwamba ana uweza! aweza kufanya vile ambavyo wanadamu wameshindwa na anaweza kumtumia mtumishi yeyote atakaemchagua kudhihirisha uweza wake, si lazima awe kakobe,mwingira au pengo! MUNGU amesikia kilio cha waja wake waliokuwa wanateseka na maradhi yasiyotibika na yenye gharama kwa ajili ya kupata nafuu ya muda na sasa wanapata tiba kwa gharama nafuu kabisa sawa na bure 'jero'!
 
Taarifa nilizo nazo na za uhakika Mwandulami amekwisha kunywa kikombe kwa Babu Loliondo
 
Samahani jamani, ni Dr Mwandulame yupi, kwani nasikia yupo mmoja Mtwango kule Njombe, mwingine Dar na mwingine yuko Mwanza.
 
Samahani jamani, ni Dr Mwandulame yupi, kwani nasikia yupo mmoja Mtwango kule Njombe, mwingine Dar na mwingine yuko Mwanza.

mi nadhani wanamaanisha wa kule mtwango-Njombe hao akina mwandulami wengine wapo kweli? mi sijawahi kuwasikia
 
Mzee wetu shupavu aliyejenga uchumi ambao JK anaubomoa, Benjamini Mkapa alikuwa anauita wivu kama wa Mwandulami kuwa ni WIVU WA KIKE.
 
Mganga maarufu wa tiba za asili maarufu kama Dr. Francis Mwandulame

usiseme Dr! sema moja kwa moja kuwa mganga wa kienyeji!!!
 
Ni kuhangaika tu, wanamponda yule mzee kwanza hana muda nao halafu hata hizi habari hazisikii, ni kupoteza muda tu kwanini wasiendelee na maisha yao?
 
Mh huyo usimwite DK hana heshima hiyo huyo ni mganga wa kienyeji. Na ukumbuke wote wanao mpiga Babu vijembe wanakosa masilahi waliyokuwa wanayapata kabla ya Babu kuibuka. wanaotaka kwenda LOLIONDO waende Babu hapigi ramli.hachanji.hakuna mashaiti ye yote unapata kikombe unaondoka ukiwa fresh. maneno mengi acha bwana.
 
kwa kweli kwa hili la serikali kumkumbatia mganga mmoja tu (na karibu baraza zima la mawaziri lilmeishakunywa kikombe), limenisikitisha sana na sasa natambua wazi kuwa ushirikina umejikita sana mioyoni mwa viongozi wetu na wengi wetu



si kila mtu aniitaye "Bwana", "Bwana" ataurithi ufalme wa Mungu
bali yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni

Sijakuelewa vizuri Miss,kutumia mitishamba kama mugariga ni ushirikina?
 
Sijakuelewa vizuri Miss,kutumia mitishamba kama mugariga ni ushirikina?

hiyo miti shamba kama mugariga imejaa tele sehemu nyingi tu nchini mwetu, si wakachimbe wachemshe majumbani mwao wanywe. kwa nini iwe lazima icheshwe na babu pekee na aigawe yeye tu tena kwa kuchotwa na kikombe kilichookotwa anachopanda nacho hadi kitandani!! kisichoshikwa na mtu mwingine yoyote!! na masharti mengine kibao?

hujaona tu ushirikina hapo?

fungua macho ndugu yangu, Mungu hawezi kutibu namna hiyo!
 
Mganga maarufu wa tiba za asili maarufu kama Dr. Francis Mwandulame wa Iringa amemjia juu babu kwa kitendo chake cha kuwahadaa watanzania kwamba amepewa ufunuo toka kwa Mungu. Gwiji huyo wa mitishamba anayetisha kusini mwa Tanzania amedai kuwa huo mti wa mugariga anaotumia babu yeye mwenyewe ameanza kuutumia kutiba watu maradhi mbalimbali kwa zaidi ya miaka 8 sasa. Anasema kuwa alioteshwa na marehemu mama yake, na kwamba unapatikana pia huko Iringa. Hivyo amemtaka babu kuacha kuwadanganya watu kuwa mti huo ni ufunuo wa Mungu. Anadai kwa babu wa Loliondo haoni jipya zaidi ya kutangazwa sana na vyombo vya habari.

Katika hatua nyingine Mwandulame amevishutumu vyombo vya habari na serikali kwa kushiriki kumtangaza mganga wa tiba za kienyeji. Ameyashutumu magazeti, TV na redio kwa kumtangaza babu huku waganga wengine wakitozwa pesa lukuki kwa ajili ya matangazo. Pia ameishukia serikali kwa kuruhusu babu kujitangaza kutibu magonjwa sugu na hata kushiriki kumtangaza wakati waganga wenzake wa jadi wamezuiliwa kufanya hivyo. Ameonya kuwa kama hali itaendelea hivyo itabidi na wao waanze kujitangaza bila kufuata taratibu.

Source: WAPO Radio - Kipindi cha matukio - 07:15 A.M

1 Cor 2:2 For I determined not to know any thing among you, save Jesus Christ, and him crucified.
IMG_5488.JPG


Mbona anapeta tu nae kaiga style ya babu.

Full story gonga hapa Francis Godwin ni mzee wa matukio daima
 
Back
Top Bottom