Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Ndugu zangu,

Suala hili linakuzwa sana bila sababu ya msingi. Kiasi kwamba tunafikia hata kuaminishwa kuwa rushwa nyingine sio rushwa na nyingine ndio rushwa. PCCB wana mamlaka yao ya kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria. Wabunge hatupo juu ya sheria.

PCCB wamepewa kazi hii na ofisi ya Bunge na ndio maana kule PCCB wana nyaraka za Bunge za malipo yote ambayo wabunge tumelipwa toka mwaka 2006. Kuhojiwa sio big deal maana wabunge wengi tumehojiwa. Mimi nilikuwa ujerumani nikaambiwa baadhi ya wajumbe wa kamati yangu wameitwa PCCB. Niliporudi kwa ajili ya kamati nikamwambia Katibu wangu awapigie simu PCCB kuwaambia kuwa ninataka wanihoji maana hawawezi kuhoji wajumbe wangu bila ya Mwenyekiti. Nikaenda kuhojiwa siku ya sikukuu ya Nyrere tarehe 14 Oktoba. Nilihojiwa kwa masaa mawili na kuwapa majibu yote waliyohitaji. Kwanini niogope kuhojiwa iwapo sina kosa?

Kuna watu wanataka kukuza suala hili kwa sababu ni dhahiri kuwa itagundulika makosa fulani fulani katika malipo ya Wabunge. Hivyo makundi yameanza kupigana ili kuonyesha kuwa kila mtu ni mlaji tu hapa nchini na ndio maana suala la Dkt. Mwakyembe limechukua prominance sana. Kwa vyovyote vile maadui wa Mwakyembe wanalishikia bango hili. Mwakyembe nae kama binadamu imebidi ajitetee. Hata hivyo kukataa kuhojiwa sio mwafaka maana kutotoa ushirikiano kwa chombo cha dola nalo ni kosa. Mbona Shelukindo kahojiwa, Mwambalaswa kahojiwa, wajumbe wote wa kamati ya POAC wamehojiwa na wabunge wengine wengi. Hata hivyo labda Mwakyembe kwa kuwa ni mjuvi wa sheria anajua kuwa kuna vipengele vinamlinda.

Suala hili pia halihusu kamati ya Nishati na Madini peke yake na wala halina mahusiano na sakata la Richmond. Kwenye Richmond Bunge haliwezi kuzibwa mdomo hata kidogo. Pia wabunge tusiizibe taasisi ya dola yenye mamlaka ya kisheria kutenda kazi yake.

Wasiwasi wangu ni kuwa tunajenga taswira katika jamii kuwa kuna mambo tunafichaficha kuhusiana na malipo haya ya wabunge. It is a public knowledge that wabunge tunalipwa sana zaidi ya stahili. Taasisi na Mashirika ya Umma pia yanalalamika kuhusu malipo haya. Hata PCCB wenyewe hulipa wabunge kama Mwakyembe alivyosema. Lakini haina maana kuwa hili sio kosa au PCCB wanakosa mamlaka ya kuchunguza.

Ninaamini kabisa uchunguzi wanaofanya takukuru utasema ukweli kuhusiana na masuala haya na hata kuondoa hisia mbaya dhidi ya wabunge kuwa wanalipwa mara mbilimbili kwa kazi zile zile. Ili kuthibitisha kuwa hakuna kosa katika malipo haya, ni vema kutoa ushirikiano kwa chimbo kinachochunguza.

Sasa hapa JF tunajadili watu badala ya kujadili issue. Jambo lililopo hapa ni kwamba je wabunge tunapolipwa zaidi ya mara moja kwa siku kwa kazi ambayo tumeshalipwa na ofisi ya Bunge ni halali au haramu? Is it ethical? Is it corruption? Haya majibu unayapata tu kwa uchunguzi na sio vinginevyo na chombo cha kufanya uchunguzi huo ni PCCB. Tunaipenda au kuichukia PCCB, lakini ndio wenye mamlaka.

Muhimu zaidi ni kuwa PCCB sio Hosea. Hosea anaweza kuwa mtuhumiwa lakini kuna vijana wazuri tu pale wazalendo ambao wanafanya kazi vizuri sana. Vyombo hivi vinafanya kazi kwa maandishi, hivyo ni dhahiri kuwa ni vigumu kupindisha ukweli mahakamani.

Suala hili ni zito sana. Ni kashfa ambayo inaweza kuwa ya historia na ni kashfa ambayo inaweza kubadili mfumo uliojikita ambao sisi wenye madaraka fulani fulani tunafaidika na uoza uliopo. Hili sio jambo la kuchezeachezea hata kidogo. Kumbukeni kashfa ya malipo ya aina hii ilimwangusha Spika wa Uingereza hivi majuzi.

Muhimu zaidi suala hili tusimhusishe Spika kwani yeye hahusiki na posho hizi kwa wabunge maana hatembelei taasisi wala mashirika. Pia Spika alitoa ushirikiano wa dhati kwa PCCB ili kufanikisha kazi yao. Sio kweli kuwa Spika ni kigeugeu katika hili isipokuwa wabunge (ambao ndio wapiga kura wake) tunamyumbisha ili atutetee. Hapana, Spika awe pembeni kwani akichafuka ni Taasisi nzima imechafuka na maadui wake wanamtafuta sana kwa kila hali. Spika aliruhusu uchunguzi ila kwa staha..........
 
.
mkuu jumboplate,
tangu mwanzo tulisema huyo masanio ni mjinga na anaushabiki wa kipumbavu.nafikiri ata baba yeke alikua hivyo hivyo.mwakyembe kwa sasa hana pa kukimbilia.watu wake wa karibu wote wamemwagwa serikali za mitaa.sasa leo hii anaongea kwa hasira eti hakuna wa kumtoa jimbon kwake,yeye ana hati miliki hapa kyela?

Vipi bwana mbona unaingia personal.....wewe ushabiki wako niuiteje? acha ufala dogo
 
Yani hata wakifanikiwa kumng'oa Hosea bado tutataka tujue mwisho wa tuhuma hizi. Yani kamati zinapiga kelele kwenye vyombo vya habari halafu vikienda kwenye mashirika au Halmashauri wanaomba rushwa??sasa tujiulize hiyo hongo/rushwa wanapewa ili wafiche nini???lazma kuna uozo katika mashirika au halmashauri hizo.......
 
Ndugu zangu,

Suala hili linakuzwa sana bila sababu ya msingi. Kiasi kwamba tunafikia hata kuaminishwa kuwa rushwa nyingine sio rushwa na nyingine ndio rushwa. PCCB wana mamlaka yao ya kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria. Wabunge hatupo juu ya sheria.

PCCB wamepewa kazi hii na ofisi ya Bunge na ndio maana kule PCCB wana nyaraka za Bunge za malipo yote ambayo wabunge tumelipwa toka mwaka 2006. Kuhojiwa sio big deal maana wabunge wengi tumehojiwa. Mimi nilikuwa ujerumani nikaambiwa baadhi ya wajumbe wa kamati yangu wameitwa PCCB. Niliporudi kwa ajili ya kamati nikamwambia Katibu wangu awapigie simu PCCB kuwaambia kuwa ninataka wanihoji maana hawawezi kuhoji wajumbe wangu bila ya Mwenyekiti. Nikaenda kuhojiwa siku ya sikukuu ya Nyrere tarehe 14 Oktoba. Nilihojiwa kwa masaa mawili na kuwapa majibu yote waliyohitaji. Kwanini niogope kuhojiwa iwapo sina kosa?

Kuna watu wanataka kukuza suala hili kwa sababu ni dhahiri kuwa itagundulika makosa fulani fulani katika malipo ya Wabunge. Hivyo makundi yameanza kupigana ili kuonyesha kuwa kila mtu ni mlaji tu hapa nchini na ndio maana suala la Dkt. Mwakyembe limechukua prominance sana. Kwa vyovyote vile maadui wa Mwakyembe wanalishikia bango hili. Mwakyembe nae kama binadamu imebidi ajitetee. Hata hivyo kukataa kuhojiwa sio mwafaka maana kutotoa ushirikiano kwa chombo cha dola nalo ni kosa. Mbona Shelukindo kahojiwa, Mwambalaswa kahojiwa, wajumbe wote wa kamati ya POAC wamehojiwa na wabunge wengine wengi. Hata hivyo labda Mwakyembe kwa kuwa ni mjuvi wa sheria anajua kuwa kuna vipengele vinamlinda.

Suala hili pia halihusu kamati ya Nishati na Madini peke yake na wala halina mahusiano na sakata la Richmond. Kwenye Richmond Bunge haliwezi kuzibwa mdomo hata kidogo. Pia wabunge tusiizibe taasisi ya dola yenye mamlaka ya kisheria kutenda kazi yake.

Wasiwasi wangu ni kuwa tunajenga taswira katika jamii kuwa kuna mambo tunafichaficha kuhusiana na malipo haya ya wabunge. It is a public knowledge that wabunge tunalipwa sana zaidi ya stahili. Taasisi na Mashirika ya Umma pia yanalalamika kuhusu malipo haya. Hata PCCB wenyewe hulipa wabunge kama Mwakyembe alivyosema. Lakini haina maana kuwa hili sio kosa au PCCB wanakosa mamlaka ya kuchunguza.

Ninaamini kabisa uchunguzi wanaofanya takukuru utasema ukweli kuhusiana na masuala haya na hata kuondoa hisia mbaya dhidi ya wabunge kuwa wanalipwa mara mbilimbili kwa kazi zile zile. Ili kuthibitisha kuwa hakuna kosa katika malipo haya, ni vema kutoa ushirikiano kwa chimbo kinachochunguza.

Sasa hapa JF tunajadili watu badala ya kujadili issue. Jambo lililopo hapa ni kwamba je wabunge tunapolipwa zaidi ya mara moja kwa siku kwa kazi ambayo tumeshalipwa na ofisi ya Bunge ni halali au haramu? Is it ethical? Is it corruption? Haya majibu unayapata tu kwa uchunguzi na sio vinginevyo na chombo cha kufanya uchunguzi huo ni PCCB. Tunaipenda au kuichukia PCCB, lakini ndio wenye mamlaka.

Muhimu zaidi ni kuwa PCCB sio Hosea. Hosea anaweza kuwa mtuhumiwa lakini kuna vijana wazuri tu pale wazalendo ambao wanafanya kazi vizuri sana. Vyombo hivi vinafanya kazi kwa maandishi, hivyo ni dhahiri kuwa ni vigumu kupindisha ukweli mahakamani.

Suala hili ni zito sana. Ni kashfa ambayo inaweza kuwa ya historia na ni kashfa ambayo inaweza kubadili mfumo uliojikita ambao sisi wenye madaraka fulani fulani tunafaidika na uoza uliopo. Hili sio jambo la kuchezeachezea hata kidogo. Kumbukeni kashfa ya malipo ya aina hii ilimwangusha Spika wa Uingereza hivi majuzi.

Muhimu zaidi suala hili tusimhusishe Spika kwani yeye hahusiki na posho hizi kwa wabunge maana hatembelei taasisi wala mashirika. Pia Spika alitoa ushirikiano wa dhati kwa PCCB ili kufanikisha kazi yao. Sio kweli kuwa Spika ni kigeugeu katika hili isipokuwa wabunge (ambao ndio wapiga kura wake) tunamyumbisha ili atutetee. Hapana, Spika awe pembeni kwani akichafuka ni Taasisi nzima imechafuka na maadui wake wanamtafuta sana kwa kila hali. Spika aliruhusu uchunguzi ila kwa staha..........

Mhe. Zitto, wajumbe wa kamati zenu na Dr. Slaa wanalipwa posho (hongo?) bila ya nyie kuhusishwa, wanafanya hivi wakifahamu kuwa nyie ni watu safi na iwapo watawahusisha lazma mtapinga kwa nguvu zote
 
Masanilo aka Ze Comedy,
Wewe beba tu mabox ya Wazungu huko Majuu; unashangaa hilo mbona hushangai mtu kuchukua posho mbili na bado akajiona hajakosea?

Wewe lipwa mara mbili kwenye hizo boksi zako tuone kama hutatupwa mpaka huko kwenu Mwanza.

Nipo Kyela unanihamisha?
 
wewe ndiye umeze nyembe.kabanwa sasa shoga yako na umma umeanza kuamini kuwa kumbe na yeye ni fisadi na phd yake aiendani na ujinga alionao

Wewe ni kiazi sana! Samahani kukuita hivyo....waende Mahakamani ...kwa kuna shida gani?
 
Mhe. Zitto, wajumbe wa kamati zenu na Dr. Slaa wanalipwa posho (hongo?) bila ya nyie kuhusishwa, wanafanya hivi wakifahamu kuwa nyie ni watu safi na iwapo watawahusisha lazma mtapinga kwa nguvu zote
Inaoneka wazi kuwa hujafahamu ni nini Zitto amejaribu kufafanua na kuelezea, ni vema ukarudi kusoma tena bandiko lake!
 
Mhe. Zitto, wajumbe wa kamati zenu na Dr. Slaa wanalipwa posho (hongo?) bila ya nyie kuhusishwa, wanafanya hivi wakifahamu kuwa nyie ni watu safi na iwapo watawahusisha lazma mtapinga kwa nguvu zote

Investigations might prove you wrong! Muhimu tuache PCCB wafanye kazi yao. Tusilinde uhalifu. Lawyers have a saying 'When you come to Equity come with clean hands'

Tunatoa wapi mamlaka ya kuingilia uchunguzi? We have even audacity to say, hii sio rushwa - kwamba tunalipwa mara mbili kwa kazi moja (ikiwa proven) sio rushwa? Kweli hatuoni aibu kabisa kutetea uvundo huu katika mfumo wetu wa utawala?

TAKUKURU wakithibitisha madai haya tutakuwa tumepiga hatua kubwa katika vita dhidi ya ufisadi maana wanasiasa tutaogopa kwani tutajua kuwa tunaangaliwa na wengine. Uchunguzi huu ukisimama itakuwa ni lost opportunity ya kufanya overhaul of the pervasive corrupt system.

Dont look at Mwakyembe ( he has genuine concerns though), look at the system! This culture of priviledges shall end! It must end........ this is a step, an important step!
 
Ndugu zangu,

Suala hili linakuzwa sana bila sababu ya msingi. Kiasi kwamba tunafikia hata kuaminishwa kuwa rushwa nyingine sio rushwa na nyingine ndio rushwa. PCCB wana mamlaka yao ya kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria. Wabunge hatupo juu ya sheria.

.........

Mheshimiwa,

Timing ya kuwahoji hawa wabunge wakiwa wanajiandaa kwenda bungeni kwenye sakata la richmod nadhani ndo limeleta shida. Pia kuhoji kwa kutumia simu hapo sijui sheria inasemaje. Pia Utumishi watoe mwongozo wa serikali nzima kuhusu haya mambo ya allowance kwani Kuanzia Mawaziri, Makatibu wakuu, wakurugenzi n.k hii kitu inawakumba siyo wabunge peke yao.
 
Ushabiki utakuuwa we jamaa!!!yani kwa kuwa uliichunguza polisi kwaiyo ata ukitenda kosa la jinai kama kuua usihojiwe na polisi? Eti dokta wa sheria!!!wakati hajui kuwa yeye ni mmoja wa wabunge waliopitisha sheria hii hii ya PCCA namba 11/2007 ambayo ukisoma section 10 (1) An officer of the Bureau investigating an offence under this Act may-
(a) order any person to attend before him for the purpose of being interviewed orally or in writing in relation to any matter which may assist investigation of the offence
halafu wandai wao ni wabunge eti ni watu wakubwa hawatakiwi kuhojiwa!!!!
Yaani huyu dokta ni kichekesho sana....ktk sheria hiyo hiyo kuna offence of disclosure of identity yani wakati uchunguzi unaendelea kuhusu jambo flani hakuna mtu anayepaswa kufichua utambulisho wa mtu anayechunguzwa au kitu kinachochunguzwa bila mamlaka ya kisheria kufanya hivyo!!Mwakyembe anapiga kelele kuwa anachunguzwa!hajui kuwa anajiongezea makosa... eti dokta wa sheria tene aliyeipitisha sheria yenyewe halafu haijui.


This is a substandard topic and a way of argument for in a forum like JF. Hata kama sheria inaruhusu busara ni logic ktk kufanya hivyo. Siyo tu kuonyesha nguvu yako.

To me Mwakyembe is a giant. Never before in the history of this country had we witnessed the Parliament exposing the stupidity of the Prime Minister to that extent.

Tusisahau Ufisadi wa walio umbuka na kuachia u-PM, na kuanza kumshambulia Mwakyembe.

Naamini vielelezo vya kuchukuwa pesa vipo kwa nini PCCB wasitinge mahakamani? Au ni kutaka kutunisha misuri tujue Hosea ni mkubwa? Hapo ndo tutaona Mwakyembe alisaini malipo ya aina gain na huenda Pinda na wafuasi wake walifanya hivyo hivyo.

Mwakyembe ni mbunge kama alivyo Mizengo Pinda au Waziri mwingine. Kwa nini mahojiano hayo yanawaruka wabunge wooote ambao ni Mawaziri? Nonsense exercise.

I can conclude that PCCB has a no useful boss.
 
Hii lame excuse wanayotumia baadhi ya wabunge "wanaopambana" na ufisadi kuwa "wanaandamwa na mafisadi" sasa imekuwa too much kiasi kwamba kila kitu kibaya kinachowatokea hio ndio inakuwa excuse yao...sasa tunaanza kuwa na wasiwasi na vitu wanavyosema. Sasa wabunge kupokea posho mbili kwa kazi moja unawasingiziaje "mafisadi"? Tatizo lingine ni kuwa wananchi wanaanza kuamini kuwa kuna baadhi ya watu ambao hawawezi kukosea, ndio maana katika masuala ya msingi kama haya tunaamua kuchoose sides. Tuache vyombo yulivyovipa mamlaka ya kufanya kazi husika vitimize wajibu wao pasipo kuingiliwa kama asemavyo Zitto
 

This is a substandard topic and a way of argument for in a forum like JF. Hata kama sheria inaruhusu busara ni logic ktk kufanya hivyo. Siyo tu kuonyesha nguvu yako.

To me Mwakyembe is a giant. Never before in the history of this country had we witnessed the Parliament exposing the stupidity of the Prime Minister to that extent.

Tusisahau Ufisadi wa walio umbuka na kuachia u-PM, na kuanza kumshambulia Mwakyembe.

Naamini vielelezo vya kuchukuwa pesa vipo kwa nini PCCB wasitinge mahakamani? Au ni kutaka kutunisha misuri tujue Hosea ni mkubwa? Hapo ndo tutaona Mwakyembe alisaini malipo ya aina gain na huenda Pinda na wafuasi wake walifanya hivyo hivyo.

Mwakyembe ni mbunge kama alivyo Mizengo Pinda au Waziri mwingine. Kwa nini mahojiano hayo yanawaruka wabunge wooote ambao ni Mawaziri? Nonsense exercise.

I can conclude that PCCB has a no useful boss.

Kama nilivyosema hapo juu tatizo letu ni kuwa tukishampenda/mchukia mtu hatutaki kusikiliza ukweli....Huwezi kwenda mahakamani pasipo kukamilisha uchunguzi, na uchunguzi unahusisha kuongea na mashahidi pamoja na watuhumiwa.
Wabunge wengi wamehojiwa ila tatizo ni Mwakyembe kwanini??yeye ni nani asihojiwe???kwani nani amemwambia kuwa yeye ni mtuhumiwa au ndio guilt mind hiyo???
 
Back
Top Bottom