Dr. Mwakyembe Vs. TAKUKURU

Mezeni nyembe mnaomchukia Dr Mwakyembe H, hatuna cha kuwasaidia ....anajua anachokifanya heko Harrison! Mafisadi na mapandikizi wao nafasi yao inazidi kuwa finyu kila mtego wao utawanasa wao wenyewe.
 
Haki na uongozi bora vinakuwepo pale tu ambapo utekelezaji wa sheria hauangalii cheo au sura ya mkosaji.

Kwa Tanzania tumefika mahali ambapo kosa linategemea cheo cha mtu na hilo ni hatari kweli kweli.

Wengine tumeshuhudia hapa UK, jinsi posho ndogo tu zilivyowayumbisha wabunge na mpaka karibu wabunge 200 kati ya 650 kulazimika kuachia ngazi hapo mwakani.

Maneno ya Spika ndiyo yamenitisha zaidi, kwamba mbunge ni mtu mkubwa na hata kuhojiwa kwake lazima kufanywe na watu wakubwa. Nijuavyo mimi sheria haina mkubwa wala mdogo na lazima watu wote wawe sawa mbele ya sheria.

Kutokana na kukiukwa kwa misingi hii ya haki sawa kwa wote, leo hii bunge letu lina criminals ambao walitakiwa kuwa jela, lakini wanapeta bungeni. Leo hii serikalini kuna watu ambao wanaona hawana sababu za kufuata sheria walizotunga wenyewe. Akina Chenge na kashfa zote hizo bado wako bungeni. Akina Zombe wanatoka huru mahakamani pamoja na ushahidi wote, akina Ditopile wanabadilishiwa mashitaka kwasbabu tu ni watu wakubwa, huku maskini kibao waliosingiziwa kesi za kuua wanasota mahabusu miaka na miaka.

Spika anataka kabla ya wabunge kuhojiwa mpaka yeye apewe taarifa kwanza, mbona hakusema hivyo walipohojiwa akina Mramba? Anatakiwa apewe taarifa ili awatonye wahusika?

Lazima kuwe na sheria moja kuanzia sisi maskini mpaka kule juu kwa rais. Tupige kelele hizo sheria zisipotekelezwa kama ambavyo tumekuwa tukifanya kwa mafisadi lakini jitihada ya kuhalalisha wizi wowote inaonyesha hatuko serious na hivyo vita tunavyojidai tunapigana navyo.
 
MODS hii topic ungeunganisha tokea jana tiyari tumeijadili ilitolewa na BAK kuhusu Spika sitta kudhalilishwa wabunge tiyari naona kuna nyingine chini hapa leo.
 
BENDERA KUFUATA UPEPO.
Kwani kuna mtu kakataa wabunge wasihojiwe? hata JK wamhoji lakini wafate sheria na sheria ni msumeno hauchagui Huyu Richmond, EPA,Mwakyembe.... Mi naona TAKUKURU isafishe kwanza ndiyo waanze kuhoji watu maana ni wachafu wachafu..
 
Ambao hammjui Mwakyembe mtapata shida sana, jamaa ni mpambanaji kwa mambo anayopingana nayo lakini yeye mwenyewe ni fisadi mkubwa kwenye mambo mengine ambayo anafaidika nayo.

Kuna kashfa nyingine inakuja ambayo kwa msaada wa spika Sitta kalipwa mamilioni ya pesa kwa kusingizia kwamba alienda kutibiwa nje (Ujerumani) wakati ule baada ya ajali wakati alikuwa amejifungia nyumbani kwake Kunduchi.

Nchi hii inaliwa na hao hao wanaojifanya wanailinda.
 
Mezeni nyembe mnaomchukia Dr Mwakyembe H, hatuna cha kuwasaidia ....anajua anachokifanya heko Harrison! Mafisadi na mapandikizi wao nafasi yao inazidi kuwa finyu kila mtego wao utawanasa wao wenyewe.

Masa...Huyo jamaa yenu naona sasa ananza kuchanganyikiwa,Yaani yeye tu ndo hawezi kukosea?Sasa ndo nimeelewa nani anayeleta ugomvi kule kwetu.
 
Jamani!!!!!!, TAKUKURU imeshindwa kuwaoji na kuwachukulia hatua stahili mafisadi sasa inawaoji wabuge? Naona hii ni mbinu ya mafisadi kuwaziba midomowabunge wanao piga vita ufisaidi nchini. Mbaya zaidi hawa wabuge wanadhalilishwa kwani watu wanaowaoji ni watu wa hali/nafasi ya chinikulingana na nafasi walizo nazo wabunge.

Jamani kwa mda sasa tunasubiri Maamuzi ya Serikali ambayo mengine ni ya Ikulu na zaidi sana ikihusisha hiyo TAKUKURU, Mbona hiyohiyo inatokea mlango mwingine kuwahoji wabunge kuhusu jambo lingine jipya kabisa tena la siku Nyingi? Hii ni kwa vile na Mwakyembe mwenyekiti wa Kmati ile yumo. USIKATAE!
pOSHO HIZI NADHANI ZINGEPIGWA MARUFUKU TU, Ingekuwa halina harufu ya Bifu. ikulu siku moja Kupitia Luhanjo Ilitoea mlango wa Nyuma nayo Kujibizana na watu wanaosema Rais naye yumo. ikajikanganya eti aliambiwa akashauri Mwisho- HAKUNA MKONO WA RAIS.
jamani ukucheck na kutafakari nchi inanuka uvundo wa viongozi wa juu wanaojiangalia wao tu, na kuanzisha malumbano ya jinsi wanavyokula hela zetu. sisi tusubiri Baada ya hili, ataibuka mwungine na Kusema TULISAFIRI KUATAFUTA KAMPUNI HEWA au WAWEKEZAJI HEWA, au KUWAPELEKA WATOTO WETU CHUO.
ngojeni tu.
 
ukitaka kujua ilikua mchezo wa mafisadi dhidi ya Dr Harrison Mwakyembe angalia tu habari ilivyopokelewa na machapisho ya pale Kijiweni, Sinza. walijuaje hizo habari kama si Hosea kuwajulisha kua Dr Mwakyembe aligoma kuhojiwa na TAKUKURU.
Katuika ujumla wake TAKUKURU ilipaswa kuanza na Mawaziri, maana hakuna hata mmoja ambae hajawahi kupokea posho mbilimbili, wala haiitaji uchunguzi.
Serikali kuu inawalipa Per diem, kisha wanalipwa posho za kuishi huko bungeni Dodoma, aende Mawizarani akaulize kama kuna waziri hajalipwa posho yakujikimu akiwa Dodoma, kisha akamuulize Muhasibu wa Bunge kama hawajalipa posho nyingine kwa mawaziri hao wakiwa DODOMA.
 
Masa...Huyo jamaa yenu naona sasa ananza kuchanganyikiwa,Yaani yeye tu ndo hawezi kukosea?Sasa ndo nimeelewa nani anayeleta ugomvi kule kwetu.

Kitu mnachosahau ni kwamba Mwakyembe ni mwanasheria aliyebobea....anajua anachokifanya....Mpaka kufikia 2010, Mwakyembe, Kilango na wabunge wenye kupinga ufisadi watapata misuko suko...lakini wananchi tutawarudisha jimboni....hongera Mwakyembe we need you Kyela and Tanzania!
 
Kutokana na kutojua sheria na kanuni za kazi zao matokeo yake ndio hayo yanayotokea sasa ..Tukukuru hawakuwa na sababu ya kuwapigia simu na kuwahoji waheshimiwa moja kwa moja kwa njia ya simu tena kwa muda wa zaidi ya masaa mawili,

Hata kama kile wanachokihoji ni ni wajibu wao. Ni uzembe wa hali yajuu. Hata kama ni mimi nisingekubali just kupokea simu kisha kuhojiwa kama mtoto mdogo kwenye mambo kama hayo ya kuchunguzana....Hapo ni kutafutana shida tu kwamba watu wana kidharau hiki chombo.. Si kweli ..Tukukuru wanajidharaulisha wenyewe.

Tena hii Tukukuru ni yakufungwa kwani pia wanapokea mishahara ya bure ,uwezo wao wa kufanya kazi tayari ushajionyesha kwamba ni mdogo sana , na kama upo uwezo basi ni kwa wale wanyonye wa Tanzania na si kwa wale wenye Kesi kubwa kubwa ,Na pia nimesikia sikia ndani ya Tukukuru wapo wale wenye kutajwa tajwa kwamba walishiriki kwa namna moja au ingine kwenye kashfa za Richmond.
 
Kuna kashfa nyingine inakuja ambayo kwa msaada wa spika Sitta kalipwa mamilioni ya pesa kwa kusingizia kwamba alienda kutibiwa nje (Ujerumani) wakati ule baada ya ajali wakati alikuwa amejifungia nyumbani kwake Kunduchi.

Nchi hii inaliwa na hao hao wanaojifanya wanailinda.

Hii ya Ujerumani nasikia ni kweli,Mwakyembe alichukua pesa na wala hakusafiri kwenda uko Ujerumani,yeye ukimwuliza anasema watanifanya nini,kwani kati yenu nani anajua sheria kunizidi mimi....
 
Heri yako wewe unayemjua!

Ambao hammjui Mwakyembe mtapata shida sana, jamaa ni mpambanaji kwa mambo anayopingana nayo lakini yeye mwenyewe ni fisadi mkubwa kwenye mambo mengine ambayo anafaidika nayo.

Kuna kashfa nyingine inakuja ambayo kwa msaada wa spika Sitta kalipwa mamilioni ya pesa kwa kusingizia kwamba alienda kutibiwa nje (Ujerumani) wakati ule baada ya ajali wakati alikuwa amejifungia nyumbani kwake Kunduchi.

Nchi hii inaliwa na hao hao wanaojifanya wanailinda.
 
Hii ya Ujerumani nasikia ni kweli,Mwakyembe alichukua pesa na wala hakusafiri kwenda uko Ujerumani,yeye ukimwuliza anasema watanifanya nini,kwani kati yenu nani anajua sheria kunizidi mimi....

Nasikia wewe ni Mbeya sana!
 
Kutokana na kutojua sheria na kanuni za kazi zao matokeo yake ndio hayo yanayotokea sasa ..Tukukuru hawakuwa na sababu ya kuwapigia simu na kuwahoji waheshimiwa moja kwa moja kwa njia ya simu tena kwa muda wa zaidi ya masaa mawili,

Hata kama kile wanachokihoji ni ni wajibu wao. Ni uzembe wa hali yajuu. Hata kama ni mimi nisingekubali just kupokea simu kisha kuhojiwa kama mtoto mdogo kwenye mambo kama hayo ya kuchunguzana....Hapo ni kutafutana shida tu kwamba watu wana kidharau hiki chombo.. Si kweli ..Tukukuru wanajidharaulisha wenyewe.

Tena hii Tukukuru ni yakufungwa kwani pia wanapokea mishahara ya bure na humo humo wapo wale wenye kutajwa tajwa kwenye kashfa za Richmond.

Sawasawa kabisa.Wanaacha kuchunguza mambo makubwa yanayotuingizia hasara kubwa zaidi za mabilioni wanataka kujipatia ujiko kwenye elfu 20 za viposho.walikuwa wapi toka zamani .Wizara kibao hapa zinachemka na huduma ni mbovu kwa wananchi lakini huko mbona hawaendi?
 
Hata ufanye mazuri gani wataalamu wa kusema watasema tu. Mtu afanye lile analoamini ni sahihi na alisimamie bila kujali yanayosemwa.
 
Nadhani kwenye suala hili, ipo hatari ya kuacha suala la msingi na kujikuta tunajadili siasa zaidi.

Kupewa chai, lunch nk kwenye vikao ni jambo la kawaida sana (hospitality). Lakini kama nimesoma vizuri, mwanzo wa sakata hili ni wabunge 'KUDAI' malipo wanapotembelea wizara na mashirika ya umma. Sasa, ni vizuri wakatuambia ni lipi kati ya haya mambo mawili linalozungumziwa.

Sidhani kama mtu unaweza kuwa na kinga kwa kufanya makosa ambayo yamekuwa yakifanyika kwa miaka kadhaa, kwa sababu tu wale waliofanya makosa hayo zamani hawakukamatwa!
 
mwanzisha thread wewe ndiyo una matatizo!mpaka leo ulikuwa hujamwelewa Mwakyembe? mwana CCM damu, anagonga cheers na kucheka na wale anaowaita mafisadi, kesho atagombea ubunge kwa chama hicho hicho, watakaompitisha ni hao hao mafisadi!

hana lingine zaidi ya unafiki, unafiki uliokumbatiwa na watanzania wengi, wakimwona kama shujaa, kumbe ni walewale
 
Nasema Mwakyembe atakwenda kupambana na VIJANA wa TAKUKURU ambao nao wamesoma sheria na wanazifahamu Sheria.

Suala hapa siyo MTU KUWA MPAYUKAJI ili watu wakujue kwamba unajua VITU.

Unamkumbuka Dr. Masumbuko Lamwai- unakumbuka alivyokuwa anatesa na Sheria zake za Kidokta yuko wapi.
kama ni vijana waliosoma sheria walishindwa nini kuanza na Richmond..
Kama mtu ni mpayukaji lakini kwenye vitu vinavyoisaidia jamii bora, je wewe ambaye siyo mpayukaji umesaidia nini Jamii...
Mwakyembe amesoma unataka anyamaze ili iweje, elimu yake itakuwaina msaidia nini sasa..asingeenda shule akabaki anachunga ng'ombe za baba ake...Mwacheni aongee kwenye vitu ambayo anaufahamu navyo, au yeye ndiyo alitunga hizo kanuni, kuna mbunge alishalalmika kuhusu mishahara ya wabunge na posho akidai zipunguzwe matokeo yake zikaongezwa..sasa hivyi wanalipwa mamilioni wakati kunawatanzania wanakosa mpka shilingi hamsini (TZS50) ya kununua kilo moja ya mahindi..
 
Mwakyembe kaza uzi. Ukilegeza, wanakumaliza. Wanatafuta 'loophole' yoyote ile ili wakuchafue. Kwa bahati nzuri kichwa chako kizuri...umeshawashtukia. Usikubali kuhojiwa, kama wanataka waende mahakamani. Tupo nyuma yako.
 
Back
Top Bottom