Mzee Kipara
Member
- Jan 3, 2011
- 83
- 43
Tatizo kubwa letu ni kutokutaka kuona hata mtu mwingine anapotuonesha. Hatuwezi kufika kamwe, tukiendelea kushabikia watu wanaotufanya sisi wajinga, watu ambao wanaposhindwa ndipo wanakumbuka kuwa kuna wananchi. Lakini hao si wabaya kama wale ambayo wanajaribu kuharibu majadiliano yenye lengo la kutafuta jawabu kwa kupindisha hoja na kusema mambo ya hovyo hovyo na mepesi katika koja nzito na zenye kutaka tafakuri
Anayetufanya sisi wajinga ni wewe na group lako la mafisadi, mtu mzima unakazania tu neno nakumbuka bila kusema unachokumbuka nini, huo ndo UNAFIKI mkubwa, unategemea nani mwenye akili zake timamu ataamini tuhuma ambazo hazijatajwa, mtajitahidi sana kutuharibia nchi, lakini hamtaweza kutudanganya, tuna uwezo wa kufikiria kuliko mnavyodhani, labda mtawadanganya wachache tu.