Kyela: Dr. Mwakyembe amtolea Uvivu Rostam

Mkandara said:
Recta,
Mkuu wangu sasa hivi sina muda ila nitakujibu baadaye..(Mwakyembe vs Rostam)..

Kifupi tu kuwepo kwa watu hao (mafisadi alowatosa) ktk Central Committe ya CCM na pia members wa NEC -CCM haina maana kabisa kuwa hawa watu wana wadhifa ndani ya Uongozi wa nchi hii, hata Asha Baraka ni member wa kamati za chama.. na kuamini kwamba member wa chama CCM ni mtu mkubwa sana ni imani ya kupotosha Demokrasia inavyofanya kazi.. CCM ni chama tu kama kilivyo chama Chadema au CUF, hivyo hizo Committe zinafanya kazi za chama na wakivuruga ktk maslahi ya Taifa wanatakiwa kushtakiwa kwa taratibu sawa na raia mwingine yeyote.. Na mfano mzuri ni Chenge kama nilivyosema hapo awali..JK hakushirikishwa ktk kumkamata, na kumfungulia mashtaka kwa sababu ni member wa kamati za CCM...
Kuhusiana na Ditto, nimesema kwa Lugha ya mtaani inawezekana nikasema Mkulu alijiua kutokana na JK kumbwaga..
Recta, mkuu kwa lugha nayotumia usidhani najaribu kumlaumu JK kumbwaga Ditto isipokuwa ni kuonyesha jinsi anavyoweza kuwa tofauti na viongozi wengine waliopita na hasa viongozi wa Kiafrika..Nyerere asingeweza kumtupa Ditto, Mwinyi asingeweza na wala Mkapa asingeweza kufanya hata nusu ya aliyofanya Kikwete ktk swala la Mafisadi tena watu wake wa karibu... Pamoja na sifa zote ambazo mimi humbwagia Nyerere naelewa kabisa kuwa alikuwa akiwalinda baadhi ya watu na kila walipoharibu aliwabadilisha wizara au madaraka tu. Mwinyi ambaye alihusika na mauaji ya vizee huko Shinyanga alikuja kuwa rais wa nchi.. Lakini tunaona JK kawabwaga kabisa viongozi wote aliowaondoa ktk serikali yake na sehemu za chama ambazo ana madaraka... Kikwete hana madaraka wala mamlaka ya kuwavua Mafisadi nafasi zao ktk kamati za chama ikiwa wamechaguliwa kulingana na taratibu za chama..Yeye ni mwenyekiti tu na inatakiwa nguvu kubwa ya wajumbe kuwavua uanachama au ujumbe wa kamati hizi..nguvu hiyo hana na ndicho nachotaka kuwaambia..He is (almost) standing alone!
Hivyo tusijaribu kumbebesha mzigo usio kuwa wake...

Mkandara,

..wacha kutufanya wana JF watoto wadogo. kesi ya Ditopile ushahidi wake ulikuwa wa waziwazi. hakuna mtu yeyote yule ambaye angeweza kumuepusha Ditopile na mashtaka yale.

..lakini pamoja na kufanya mauaji yale Raisi hakumfukuza kazi marehemu Ditopile. alimsubiri aandike barua ya kujiuzulu kazi na aliikubali. Raisi huyo huyo alikataa barua ya kujiuzulu ya Daudi Balali, na kuamua kumfukuza kazi. sasa jiulize kwanini alikubali barua ya Ditopile ya kujiuzulu, lakini akakataa ile ya Balali? binafsi nasema yote hiyo ilitokana na ushikaji wake kwa Ditopile.

..zaidi dhamana ya kesi ya Ditopile ilikuwaje? sidhani kama mtu mwenye kesi nzito kama Ditopile angeweza kuwa akisafiri freely kwenda Tabora kutafuta asali, mara yuko Morogoro anakagua mashamba etc etc. je, kuna mtu mzito aliyekuwa akimlinda?

..halafu unakwenda mbali na kusema ati Nyerere alikuwa na huruma na marafiki zake. umemsahau Bibi Titi Mohamed? vipi kuhusu Oscar Kambona? Mzee Kasela Bantu, na Balozi Kasanga Tumbo?

..unaposema Mwinyi alihusika na mauaji ya vizee Shinyanga una maana gani? je kuna ushahidi kwamba aliua kwa mkono wake kama alivyofanya Ditopile? Mwinyi alijiuzulu kutokana na makosa na uzembe wa watu waliokuwa chini yake. tena wahusika wenyewe walikuwa Shinyanga na yeye Mwinyi yuko makao makuu ya wizara ya mambo ya ndani DSM.

..kama unataka kumtetea Raisi Kikwete ufanye hivyo kwa kutumia maelezo yenye kueleweka. pia ingekuwa vizuri kama ungefanya hivyo bila kuanza kuwachafua wale waliomtangulia.

..yanayoendelea kati ya JK na maswahiba zake yananikumbusha ile michezo ya watoto watukutu ambapo husema hivi:-

..mtoto wa kwanza: "twende."

..mtoto wa pili: "wapi?"

..mtoto wa kwanza: "tukaibe"

..mtoto wa pili: "tukikamatwa?"

..mtoto wa kwanza: "SIMOOO!"
 
Tusimamishe Ukweli!
Binafsi naona Mwakiembe ni bonge la Kiongozi! Nikiacha ushabiki wa kisiasa kando, kwa ushujaa wa mtu huonekana katika mambo muhimu yanayohusu maslahi ya kitaifa kama jinsi Dr Mwakiembe anayopambana.

Hili swala la kusema kuwa alikuwa na maslahi binafsi kwenye swala la Dowans ni ujinga mtupu na mafisadi wamelichukulia kama mada ya kutuhamisha kwenye ukweli halisi uliopo, kwani kama kampuni yenyewe inayosemekana kuwa niya wazalendo na Mwakiembe akisemekana kuwa ni wenye share kwenye kampuni hiyo haina hata MItambo ambayo tayari imesha simikwa aridhini, haina hata Koleo, ni eneo tu lililoko wazi lisilo na hata kibanda cha mlinzi SWALA LA KUTANGAZA MGOGORO WA KI-MASLAHI HAPA UKO WAPI?

Watanzania wa leo si wale wa ndio mzee swala la kuyumbishwa na waandishi wenye njaa wanaofadhiliwa na mafisadi ndio limechangia kwa kiasi kikubwa kutukwepesha mambo muhimu yenye tija kwa Taifa na kuanza kuleteana mambo ya ajabu yasiyo na msingi wowote.

Mwakiembe wewe komaa na mafisadi usirudi nyuma japo uko nao kwenye meli moja kama wasemavyo wahenga kwenye "MSAFARA WA MAMBA KENGE NAO WAO"

Mwakiembe yuko sahihi! sema ccm inawakumbatia mafisadi kama kina Rostam, na sasa kiama chao kimefika.
Naungama na msemaji aliyesema kuwa CCM waamue wa kumkumbatia kati ya Mwakiembe na Rostam!
chabeby

 
JAMANI EEHEEE!!
Hivi vyombo vya habari ambavyo tunaambiwa vinamilikiwa na mafisadi ni vipi?
Mheshiwa mwakiembe alithubutu kutaja gazeti moja ambalolinamilikwa na Fisadi Rostam, Mimi na baadhi ya watanzania wenzangu tungependa kujua vyombo vingine ambaavyo vinamilikiwa na MAFISADI ili kuanzia leo tuvijue.

Lazima tujue mafisadi wa nchi hii wanamiliki vyombo gani vya habari ili kuanzia leo tusiviunge mkono maana kufanya hivyo ni kuwaunga mkono mafisadi.
 
Jokakuu,
Mkuu mara nimeshakua nawafanya watoto wadogo?... Duh, mkuu hizi ni hoja zangu kutokana na mazingira yaliyokuwepo na kibaya zaidi ni kwamba unashindwa kuelewa nachozungumza..
Kuna habari mbili hapa kwanza ni ya Mwakyembe ambaye wengi wamekuwa wakimtupia madongo sana kuhusiana na fisadi Rostam..Tunakubalkiana kwamba ROstam ni fisadi lakini wenzangu wanadai kuwa ufisadi wake unatokana na uzembe wa Kikwete na ndicho nachojaribu kusema kwamba Kikwete kafanya kila analotakiwa kama kiongozi wa nchi yoyote ile, kwanza kuwavua hao jamaa madaraka kisha kawaacha nje ili sheria ichukue mkondo wake..
Hakijafanyika kitu kwa sababu Bunge limekalia taarifa ya Mwakyembe na kutokana na taarifa za nyuma nimekuja gundua kwamba swala la Richmond limeisha zimwa. sababu ni kutokana na wajumbe wengi walipita Ubunge kutokana na takrima za Rostam/Lowassa..Kifupi ni kwamba hata Dr. Slaa alikiri kwamba ni vigumu sana hata kumshtaki Mkapa kisheria, kwa sababu hatua hiyo haiwezi kupita bungeni..haiwezekani kukusanya sahihi zinazotakiwa hata kufungua tu jarida la kesi zinazomkabiri..sababu bado ni zile zile..
Sasa nikirudi kwa Ditto, nadhani wewe hukunielewa... Nachojaribu kusema hapa ni kwamba JK kama viongozi wengine wazembe wachafu angeweza kabisa kumsave Ditto kama angependa kufanya hivyo. Tumeyaona haya wakati wa Mwalimu, Mwinyi na hata Mkapa wapo watu tena wakubwa wameondolewa maisha yao na marais wote walikaa kimya wakijua kimefanyika nini na nani mhusika..
Mkuu wapo viongozi kibao waliowahi kuua na ushahidi wote unawaandama wao lakini hakuna kilichofanyika na media coverage zote zilikuwa controlled na serikali..Na tukizungumzia Ufisadi, ufisadi umeanza toka wakati wa mwalimu lakini hata siku moja hakuna hatua kali imewahi chukuliwa kwa viongozi kama wakati wa Kikwete.. zamani adhabu kubwa kwa wanasiasa na viongozi ilitokana na kukiacha chama CCM..
Kwa hiyo hata kama Kikwete alimsaidia Ditto kupata dhamana bado haipo kinyume cha sheria. Chenge kaua wanawake wawili na yupo nje kwa dhamana, mafisadi wote wapo nje kwa dhamana tena basi wanaendelea kuendesdha biashara zao kama vile hawana mashtaka..Wakati wa mwalimu ukiwa na kesi kama hii unasimamishwa hata kazi na utaomba bora ungebaklia kizimbani..
Kuhusiana na Mwinyi, mkuu wangu mauaji ni mauaji sii lazima uweke mkono wako.. Mugabe au Bashir hawajaua mtu kwa mkono wao lakini kama kiongozi wamekuwa responsible direct na kila linalotokea.. hata Manazis wanahukumiwa kutokana na wadhifa waliokuwa nao ndani ya serikali hata kama hawakuua wao. Jaribu kutofautisha mtu kuua kama raia mtaani (Ditto) na kiongozi kuhusika na ruksa inayoruhusu vizee kuuawa... wale vizee hawakuuawa siku moja ni kameni iliyokwenda kwa muda mrefu sana Mwinyi akiwa waziri.. Mimi nilikuwa Dar wakati huo na tuliisikia kama tunavyosikia leo Ma Albino wakiuawa, tena basi kwa baraka za serikali nawatendaji walikuwa wakisaidiwa na askari wetu..nini zaidi unataka kunambia!
Nadhani hata Pinda alilaumiwa hapa kwa statement tu na hakika kama wananchi wangeua, kisha kikafuatia kujiuzuru kwake kutokana na mauaji hayo..basi bila shaka Pinda ANAHUSIKA..na rekodi hiyo inaweza kabisa kutumiwa kama atagombea Urais..
Hakuna mtu anawachafulia watu waliotangulia mkuu wangu huu ni ukweli ambao Mwinyi mwenye anaujua .. kwa nini alijiuzuru kama walivyofganya kina Lowassa, Karamagi na wengineo..kisha analia baada ya matukio kama kina Lowassa kuwa anaonewa.. Hivi kweli wewe unaamini Lowassa anaonewa?..ushenzi wote alofanya kuwafukuza watu kazi bila uchunguzi leo hii yamemkuta yeye anaonewa.. what a joke!
Halafu swala la Balali, mkuu Balali aliandika barua ya kujiuzuru akiwa Marekani tayari kwa matibabu.. Kikwete alikataa kujiuzuru huko kwa sababu swala la EPA bado lilikuwa ninafanyiwa uchunguzi..Kwa hiyo bado kulikuwepo na uwezekano wa kurudi nchini na kuyakabiri mashtaka..
Lakini baada ya kufahamu kwamba Balali hawezi kurudi ndipo alipomfukuza na kuondoa kinga yake.. trust me alipoondolewa kinga Mkapa, Rostam na kundi lake walituma watu US ahead ya wale wa UWT kuja kumnyamazisha..Balali tayari alikwisha kuwa aidha Raia au mwenye Landed na hakuna ushahidi wowote unaomweka yeye kuwa ndiye mwizi, hivyo asingeweza kurudishwa Tanzania. ushahidi wote unaonyesha kuwa kila alofanya kuna sahihi ya viongozi wakubwa wa serikali yetu.. kifupi hatuna kesi dhidi ya Balali isipokuwa Balali ni SHAHIDI wa kesi nyingi zinazohusiana na wizi mkubwa Benki Kuu..Hii ndiyo CCM inayotuongoza na ndio wao walioiba fedha zote toka wakati wa Mwinyi, Mkapa hadi leo hii..

Hata hivyo, my all point is, labda nijieleze mwisho (conclusion) ya mtazamo wangu kwa faida ya wote ambao wamekuwa wakinisikiliza kwa sababu hapa katika ti mnashindwa kabisa kunielewa nakowapeleka...
Ni hivi haya yote yanajengwa na watu ndani ya chama CCM. Chama CCM kimetekwa na Mafisadi na hakuna mtu hata mmoja anayeweza kukiokoa na wala wananchi hamtakiwi kujenga tumaini kwamba LABDA kuna mtu mwingine ndani ya CCM ataweza kuifanya kazi ya Kikwete kwa Ubora zaidi.. Hakuna mkuu wangu sii Salim, Mwandosya wala baba yake...tukumbuke tu kwamba chama ndicho kinaongoza na kimekwisha chukuliwa na Mafisadi sehemu zote kubwa za mabano ya uongozi, hivyo kelele zote za hawa watu wachache kina Mwakyembe, Mama kilango, Sitta na wengineo ni kati ya wachache wenye matumaini kwamba wanaweza kukiokoa chama hiki..lakini ndio Titanic mkuu wangu imeshagonga mwaba kelel za Malecela na madai yote aloweka ni upuuzi mtupu kutaka kutufumba macho sisi wananchi..
The ONLY solution kwetu sisi ni kuchagua chama kingine, tujikite ktk kupigania haki zetu with chama chenye mwongozo na uhakika wa kutuletea haki tunayostahili kwani Kikwete alone (he has done a lot though) hawezi na hakuna mtu ndani ya CCM anayeweza akiwa bado mwana CCM..Mnachotazama ni kioo cha uongozi ndani ya CCM na ndio maana mnafikiri kuwa ni mzembe kwa fikra zenu bila kuchungulia huko CCM kunani?...
CCM has to go..lakini kama tunapima watu mmoja mmoja basi Kikwete is the best leader CCM has at this very moment!...hakuna mwingine.
 
Mkandara

Ninakubaliana na wewe sehemu kubwa, naomba mifano ya hii kauli kwa faida yangu na wengine hapa JF

Mkuu wapo viongozi kibao waliowahi kuua na ushahidi wote unawaandama wao lakini hakuna kilichofanyika na media coverage zote zilikuwa controlled na serikali..
 
Masanilo,
Mkuu unataka majina ya viongozi waliouawa au walioua! mfano wa kesi zilizopuuzwa au unataka mifano ipi..
Kmbuka tu nimesema kuua sii lazima uuwe kwa mkono wako - AMRI au KUPUUZA mauaji na ukayajengea sababu kunaweza kukuweka kuwa muuaji..
Mfano mmoja Karume!
 
Jimbo ni la Mwakyembe. Kma CCM hawamtaki basi litauwa jimbo litakuwa la chama kitakachomtaka Mwakyembe.Sioni dalili ya Mwakyembe kuondoka CCM. Ni vizuri amemfunga paka kengele akiwa humo humo CCM.Ni ujasiri mkubwa ukilinganisha na ukimya wa watu wengine wa ngazi za juu wa cham hicho. Malecela naye amejitahidi sana. Lakini kina JK wako wapi,likizo? Kina Msekwa wako wapi au kwa vile Rosatm alishamfanya mwenyekiti wa VODACOM akiwaspika wa bunge ndiyo kamzibwa mdomo moja kwa moja?
Hivi sasa akisema kitu Msekwa tutamwelewa kweli? Lawama ndogo kabisa ambayo anaweza kuambulia kuhusu hili sakata, kama atalizungumzia, ni: 'Hivi muda wote alikuwa wapi?'
Na wanaosema Mwakyembe ana mgongano wa kimaslahi si wamshitaki bungeni basi ambako eti inasemekana kavunja sheria ya mgongano wa maslahi. Wanachelewa nini? Maana hili si swala la kujadiliwa juu juu au kwenye magazeti ya udaku.Rosatm ameharibu magazeti yetu ya Mtanzania na Rai- yalikuwa mazuri na makini wakati yupo Jenerali Ulimwengu.Sijui kama wengi mnaliona hili- kuwa na magazeti ya quality nzuri katika jamii ni baraka na tunu na kichochea maendeleo- sasa kachukua huyu jamaa haya magazeti ndiyo basi tena.
 
Masanilo,
Mkuu unataka majina ya viongozi waliouawa au walioua! mfano wa kesi zilizopuuzwa au unataka mifano ipi..
Kmbuka tu nimesema kuua sii lazima uuwe kwa mkono wako - AMRI au KUPUUZA mauaji na ukayajengea sababu kunaweza kukuweka kuwa muuaji..
Mfano mmoja Karume!

Mkuu Mkandara, huwa napenda sana kusoma unachoandika na mara nyingi unatoa tathmini sahihi kwa kiasi kikubwa. Ila ninachoona zaidi pia ni kuwa, unapoombwa kufafanua, huwa unapindisha hoja zako mwenyewe na hatimaye hoja zako nzuri zinabadilika na kuwa hoja tofauti kabisa (kwa kutumia maelezo marefu sana).

Swali la Masanilo ni la msingi sana katika kutetea hoja yako. Ila naona nalo umeanza kulipindisha/kulirahisisha na kutaka tuamini ulisema hivyo ukiwa na maana tofauti. Haya basi, taja walau hao viongozi walioua bila kutumia mikono yao wenyewe. Taja kadiri unavyoweza, ili kuweka mjadala sawa.

Mkuu, sikubaliani kabisa na hoja yako kuwa JK ndie kiongozi bora CCM so far na kuwa hakuna mwingine yeyote anaeweza kufanya mambo mazuri zaidi kwa kuwa mafisadi wamekishika chama pabaya (kitu kama hicho). Umesema pia kuwa njia mbadala ni kuchagua chama kingine ili kuleta mabadiliko yanayohitajika nchini kwa kuwa CCM imeshakuwa chafu sana na haibadilishiki. Mkandara ndugu yangu, hoja zako hizo, ni potofu sana. Ni potofu kwa kuwa si kweli kuwa CCM haiwezi kubadilika na kuwa bora. Misingi, Imani, Kanuni za CCM bado hazijabadilika na zinaweza kuendelea kutumika endapo viongozi watabadilika. Mafisadi waliopo CCM sasa wameingia katika uongozi wa juu wa CCM na Taifa pamoja na JK 2005. Imani yangu inanituma kuwa, JK akiondoka, ataondoka nao pia. Kinachohitajika ni nia ya wapiga kura ndani ya CCM kuamua hivyo bila uoga na kwa dhati kabisa.

Imani yangu pia ni kwamba, endapo CCM haibadiliki kwa kuwa Mafisadi wameishika pabaya, haitawezekana Chama chochote cha upinzani pia kushinda uchaguzi hata wakipata kura zote (100%). Kwa maana mafisadi wataziiba kura hizo na kuzifanya ziwe zao zote au kwa asilimia kubwa. Hivyo suluhu bado liko ndani ya CCM. Mafisadi watoke haraka na waachie chama kijiunde upya kulingana na katiba yake na kanuni zilizopo ndani ya chama. CCM ikiwa safi, ndipo pia upinzani utapata haki ya kushinda uchaguzi. CCM ikiendelea kuwa chafu, upinzani unapoteza nafasi zote za kushinda kwa haki.
 
Kuna tetesi ambazo nimezisikia hapa, nasema tetesi kwasababu siwaamini wanaozisema. Wanasema Dr. Mwakyembe anatafuta njia ya kuhamia CHADEMA.

Wanasema kwenye mkutano wa leo yule kijana wa CHADEMA aliyewahi kuwekwa ndani wakati ule wa ziara ya JK ndiye alikuwa mbele katika waandaaji. Pia wanataja uhusiano wa Dr. Mwakyembe na Mbowe pamoja na Mengi kama sababu za kuamini hivyo.

Pia inaelekea kuna mpambano mkali unaandaliwa Kyela 2010 kati ya Dr. Mwakyembe na jamaa mmoja nasikia yuko nje ya nchi.

Mimi nilikuwa hapa kwa muda na niliyoyaona leo sina hamu, hii wilaya imegawanyika kweli kweli. Sikuona viongozi wowote wa CCM pale mbele badala yake kulikuwa na wapambe wa mheshimiwa waliokuwa wanamwaga sifa kibao.

Angalieni hili jimbo 2010 inaelekea kutakuwa na vituko.

Filamu hii ni ndefu sana episode hii ilinipitia wapi sijui na ilikuwa kabla ya episode ya CCJ.
 
Makyembe akitaka kuandika historia katika nchi hii aachande na magamba ajiunge na makamanda wa M4C kwa ajili ya ukombozi wa taifa hili ila kama ataendelea kuhudhuria vkao vya ccm na kuvuta posho kisha kuja kuiga kelele nje tutashindwa kumtofautisha na magamba wengine! join forces now not later!
 
Mwakyembe fanya kazi wizara yako ni kubwa na na nyeti ,malumbano na Rostam hayasaidii kitu, yeye si mwanasiasa, wewe sasa ni sehemu ya selikali usilalamike chukuwa hatua vyombo vya sheria si vipo!, au kakuchukulia mkeo!?
Mara mbumbu , mbumbu angechukua dgree ya uchumi uk, au kwa madai yako angeweza kuidanganya na kuitapeli selikali mtu mbumbumbu?
 
RA jamani ni fitina saana....nasikia hata elimu yake ni fake na ana uraia nchi 3....alianzia kutumwa tumwa deals za watu...hapa mjini nae akapata access a wanene wenye tamaa...wanaomkumbatia shauri yao....hongera Kyembe...

RA ndiyo mfaidika no1 wa uroho, ufisadi, ubinafsi na tamaa ya kupindukia ya viongozi wetu na vile vile ujinga wa watanganyika walio wengi..Anadai ni Oxford graduate na watu wanaamini kwa sababu ni mweupe mweupe, hawajiulizi alisoma wapi kabla ya oxford na kama haikua scholarship ya tz ilikua ya wapi? wazazi wake au ukoo wake ulikua na hela kiasi gani na ushawishi gani wa yeye kua admitted. ( kwa maana oxford hauingii hivi hata kama wewe ni Bakhresa na una $1bil)....yote tunayouziwa tunanunua na kutumiwa ipasavyo hamna mtu ameteteresha nchi mpaka sasa zaidi ya huyu mpersia na bado anataka kuweka kikaragosi chake kingine hapo 2015
 
Hata mleta mada yuko biased. Hakuna mengine aliyoyaongea zaidi ya yale ya RA? Interest yako ilikuwa ni kutafuta unayodhani ni mabaya bila kujua kuwa si kila mtu atatafsiri kama wewe
 
Mwakyembe fanya kazi wizara yako ni kubwa na na nyeti ,malumbano na Rostam hayasaidii kitu, yeye si mwanasiasa, wewe sasa ni sehemu ya selikali usilalamike chukuwa hatua vyombo vya sheria si vipo!, au kakuchukulia mkeo!?
Mara mbumbu , mbumbu angechukua dgree ya uchumi uk, au kwa madai yako angeweza kuidanganya na kuitapeli selikali mtu mbumbumbu?

Umeangalia vizuri ni thread ya lini?
 
Back
Top Bottom