Dr. Manyuki Atinga Rasmi Mtandaoni, Matibabu ni kwa USD.

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,645
155,016
DR. MANYUKI KATINGA RASMI MTANDAONI NA ANAPATIKANA KWENYE WEBSITE HII:- http://www.drmanyuki.com/services1.html
NIMEIPATA WEBSITE YAKE LEO ASUBUHI MITAA YA MOROCCO NIKAONA BANGO KUBWA SANA LIMEANDIKWA ANWANI YA MTANDAO WAKE.
NIKAONA SIO MBAYA KUUTEMBELEA.
KWA KWELI MTANZANIA WA KAWAIDA HAWEZI KUMUDU GHARAMA ZA HUYU KIGAGULA AMBAYE ANATIBU KWA DOLA.
 
Dawa ya kuongeza nguvu ya kiume,
Dawa ya kuongeza nguvu ya kiume nambari moja barani Africa, ina vitamini na virutubisho. Dawa hii haina madhara yeyote, watu wengi wametumia imeonyesha mafanikio makubwa, kwa kazi tatu:-
  1. Kukakamaa kwa uume wakati wa tendo la ndoa.
  1. Uzalishaji wa mbegu za kiume yaani kuwa na manii mengi.
  1. Kuchelewa kukojoa manii.
Dozi
Dawa yenyewe iko katika hali ya maji iliyochanganywa na asali mbichi na dawa inaitwa HARAI.

GHARAMA:
USD. 250 kwa dozi ya siku 21.

Tiba ya kurefusha maumbile kwa urefu na unene
Hii dawa hutumika kwa watu wenye maumbile madogo ya uume wa nchi mbili kurefusha mpaka nchi saba, dawa hii haina madhara na watu wengi wametumia kwa jili ya kurefusha maumbile yao na kuonyesha mafanikio makubwa

Vitu visababishavyo mtu kuwa na maumbile madogo ni:-
  1. Wakati akiwa bado mdogo alikuwa hapashwi maji ya moto sehemu ya siri.
  1. Kuwa mnene sana.3
  2. Kuishiwa nguvu za kiume
Dozi

Kwa wenye matatizo haya dawa yao ya kutumia ni
  1. Kuchanja sehemu ya siri
  1. Kunywa
  1. Kupaka
Gharama ya tiba hii ni USD 350
Mwanamke asiyejisikia hamu ya tendo la ndoa.
Wanawake walio wengi tangu kuvunja ungo kwao anapofanya tendo la ndoa na mwanaume hata siku moja hajisikii hamu ya kutokwa na manii mwenyewe na kufurahia tendo la ndoa.
Kuna dawa ya kunywa na kupaka sehemu ya siri.
Gharama yake ni USD 150.


KWA WAATHIRIKA WA HIV.
Utafiti nimeanza kufanya tangu mwaka 1991, na kuonyesha mafanikio makubwa kwa waathirika waliotumia dawa hii yenye vitamini virutubisho ambavyo humfanya mgonjwa kuongeza kiunga ya mwili.
Ili mgonjwa apate huduma hii sharti awe na cheti cha kuonyeshwa kwenye screen HIV positive na kipimo kingine kinachoonyesha CD4 na CD8 mgonjwa anapotumia dawa hii CD4 hupanda, CD8 hushuka ambayo huonyesha maendeleo ya mgonywa kuwa mazuri mgonjwa hupata faraja na matumaini makubwa kutokana na vipimo kuonyesha uhakika na uelekeo wa maisha yake.

MASHARTI:
  1. Hatakiwi kufanya mapenzi wakati anatumia dawa hii.
  1. Asinywe pombe
  1. Asivute sigara.
GHARAMA
Gharama ni USD 1500. Tiba hii dozi yake ni mfululizo wa miezi sita. Dawa hii ni ya kuchemsha atatumia kila baada ya msaa sita (asubuhi, mchana, jino na usiku saa tano au saa sita)
Huduma hii hutolewa mahala popote ulipo duniani ila daktari atafika kwako kwa gharama zako na malipo ya dola 1500 yako pale pale.
Matatizo mengine ya kila siku katika jamii na familia

Dawa ya Kujenga umbo la mwanamke
Dawa hii isiyo kuwa na chemikali ni ya mitishamba iliyo katika hali ya unga au majimaji
Utumika koagea kuanzia kiunoni kushuka chini
Matunizi hayo hufanya mwanamke kuonekana na makalio makubwa na mapaja kujaa kuonyesha mvuto waumbo zaidi mbele ya watu wote
Dozi ya ni ya kutumia mara mbili kwa siku kwa mda wa wiki mbili
NB
Umuhimu wa hii dawa ni kumfariji mume wako , mpenzi wako, mchumba wako asiwaze msichana mwingine na kutoka nje kwa kasoro ya umbo
Bei

GHARAMA
Tsh 250000 au dola 200

Kaaazi kweli kweli
 
Daktari Manyuki ni mtaalamu wa kimataifa wa tiba asilia mwenye uzoefu katika madawa yote ya asili, anapatikana Tanzania na amethibitishwa kuwa mponyaji nambari wani anayeweza kufanya ndoto zako kuwa kweli na kusuluhisha matatizo yako yote.
Kupitia tiba maalum ya miti shamba Daktari Manyuki anaweza kufanya yafuatayo:
  • Anauwezo wa kukuondolea nuksi na mikosi mbalimbali
  • Anasaidia kurudisha mahusiano yaliyovunjika.
  • Anatibu matatizo ya mimba
  • Anakomesha uchawi wote, mizimu, nuksi, balaa, na mikosi.
  • Anarudisha mpenzi uliyepoteza naye kwa muda mrefu.
  • Anasaidia kufuta kesi, talaka, na madeni sugu.
  • Anavidonge vya kupunguza uzito.
  • Anasuluhisha matatizo ya kifedha na ya kifamilia.
  • Anauwezo wa kurudisha mali iliyopotea
  • Anaweza kukupa dawa ya mvuto kwenye biashara yako.
  • Anaweza kukusaidia kupandishwa cheo.
  • Ana mchanganyiko wa wa dawa za kuinua hamu ya kufanya mapenzi.
  • Ana dawa ya kunenepesha uume hivyo kuweza kumridhisha mwenzi wako.
  • Anaponya uchizi, msongo wa mawazo, utegemezi (addiction), kuugua kwa muda mrefu.
  • Anatibu magonjwa ya zinaa kwa muda mfupi.
  • Anatibu matatizo ya kufika kileleni kwa haraka.
  • Ana dawa maalum ya kukukinga na wezi wa gari lako, watekaji, wizi wa mali

Hizo zenye red sidhani kama zinahitaji mganga kweli..,wajinga ndio waliwao.
 
Bongo tambarale kila kitu kinawezekana.
Gharama zake zipo juu kweli kweli analipia na VAT nn tiba zake?
 
hahaha .......yaani serikali yetu ina raha .....mtu anapewa leseni ya kutibu "kurudishwa kazini" :D ....
 
Dawa ya kuongeza nguvu ya kiume,
Dawa ya kuongeza nguvu ya kiume nambari moja barani Africa, ina vitamini na virutubisho. Dawa hii haina madhara yeyote, watu wengi wametumia imeonyesha mafanikio makubwa, kwa kazi tatu:-
  1. Kukakamaa kwa uume wakati wa tendo la ndoa.
  1. Uzalishaji wa mbegu za kiume yaani kuwa na manii mengi.
  1. Kuchelewa kukojoa manii.
Dozi
Dawa yenyewe iko katika hali ya maji iliyochanganywa na asali mbichi na dawa inaitwa HARAI.


" siku hizi kina baba mna matatizo sana? mbona madawa yenu yanaongezeka kwa kasi ya ajabu
 
dawa ya kuongeza nguvu ya kiume,

dawa ya kuongeza nguvu ya kiume nambari moja barani africa, ina vitamini na virutubisho. Dawa hii haina madhara yeyote, watu wengi wametumia imeonyesha mafanikio makubwa, kwa kazi tatu:-
  1. kukakamaa kwa uume wakati wa tendo la ndoa.
  1. uzalishaji wa mbegu za kiume yaani kuwa na manii mengi.
  1. kuchelewa kukojoa manii.
dozi
dawa yenyewe iko katika hali ya maji iliyochanganywa na asali mbichi na dawa inaitwa harai.


" siku hizi kina baba mna matatizo sana? Mbona madawa yenu yanaongezeka kwa kasi ya ajabu


si unajua mambo ya nyumba ndogo...
Lazima ukatoe dozi ya kufa mtu ili kujenga heshima na jina.
 
Back
Top Bottom