Dr. Lawrence Gama ameaga dunia

Huyu mzee aliwahi kuanzisha, kuonyesha mfano na kusimamia mapinduzi ya kilimo (kama sikosei iliitwa 'kilimo mlale/ulale') sina uhakika na programu hiyo iliitwaje. Ruvuma hawakuwa wazalishaji wakubwa wa mahindi kabla ya programu hiyo.

Huyu Mzee amejenga kiwanda cha kusaga mahindi (Msamala milling co.) sembe za Azam haziendi Ruvuma. Kule unga unakula kwa bei karibu na bure na unasambazwa hadi ktk maeneo ya makazi na wabeba baiskeli. Upo packed ktk mifuko ya ujazo mbalimbali. Anazo mashine za kisasa kabisa.

Wananchi wa mkoa Ruvuma hawataweza kumsahau huyu mzee.

Soko la kisasa lililopo Songea mjini ni jitihada za huyu Mzee, alijenga soko hilo baada ya lililokuwepo kuungua moto.

Jeshi la Wananchi La kujenga Taifa (JKT) lilianzishwa na huyu mzee gama. Japo wengi hamliafiki lakini kwa wale waliohudhuria mafunzo ya jeshi hakuna atakaye -regret.

Jamani yapo mengi mazuri ya kuyakumbuka yaliyotokana na huyu mzee.
 
Pumzika kwa Amani huko peponi mzee Gama. Tutaendelea kukumbuka kwetu Tabora kwa kusimamia ujenzi wa uwanja wetu wa kisasa wa Ali Hassan Mwinyi
 
Nilimfahamu Marehemu Lawrence Gama alipokuwa Katibu Mkuu wa CCM. Wakati huo Chama kilikuwa tofauti sana na hiki cha Yusuph Makamba. Yeye na shemeji yake Mwalimu Nyerere walizingatia uadilifu na uzalendo kweli kweli.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi. Amina.
 
This is really sad news!! Dr. Gama has done alot for wana Lizombe. I mean for the Songea people: Majimaji stadium, the tarmac road from Songea to Makambako, just to mention a few. Poleni wana Songea and all Tanzanians
 
RIP Mzee wetu Gama. Poleni wafiwa.

Tutakukumbuka kwa mengi: JKT, michezo(soka), kilimo, na muumini wa ujamaa.
 
..Mzee Gama aliwahi kuwa Mkuu wa JKT, na baada ya hapo Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa. baada ya hapo nadhani ndiyo alianza kuwa posted mikoani.

..kwa kumbukumbu zangu kila mkoa alioteuliwa kuongoza basi uli-excell ktk kilimo au michezo. mkoa wa Ruvuma ni mmoja wa mikoa hiyo.

..MWENYEZI MUNGU AMLAZE MAHALA PEMA PEPONI.
 
ni nani ataishi milele? e Bwana utufundishe kuzihesabu siku zetu

na jumla ya miaka yetu ni sabini na tukiwa na afya njema themanini, na mingi ya hii miaka ni ubatili na taabu tupu

ya nini kujilundikia mali za dunia hii kama wewe lowasa, chenge na wenzake? wekeni hazina mbinguni kusiko na nondo wala mchwa, kumbukeni mali mnazochuma kwenye migongo ya maskini, yatima, wajane kama epa nk ni vifusi yaani rubbles! mheshimiwa lowasa zile ghorofa zako, magari ya kifahari etc ni rubbles, yaani vifusi, mgeukia sasa muumba wako
 
huyu ni gama bwana ...moja ya boardguards wa [aide camp] wa kwanza wa MWALIMU alitrain ISRAEL .....kwa mwalimu ...akampata dada yake mwalimu[alishakufa zamani]..akawa shemeji wa mwalimu..baada ya hapo...mwanzililishi wa JKT...akiwa na maj gen kaswende[enzi hizo mkuu wa jkt anaitwa director kama TISS]....,akahamia usalama kama director..mkuu wa mikoa mbalimbali ,mbunge ....katibu mkuu wa CCM.

ANAKUMBUKWA KAMA MPENDA MICHEZO ALIJENGA VIWANJA MAJIMAJI,ALI HASSAN MWINYI....AKAANZISHA TIMU MAJIMAJI, na MIRAMBO[YA Akina Feruz telu..mnamkumbuka..?]...kimsingi ni daktari wa uchumi wa kijamaaa na kwa matendo na maendeleo aliyoshirikisha watu ...anastahili kuitwa DR...ma dr wa siku hizi PHD zao zimesaidia nini wananchi??? hakuwa fisadi...?? alikuwa mjamaa wa vitendo...nasikitika comrade mwenzake kama KINGUNGE hatapata bahati ya kuacha alama hizi akifa..kwani ameshaitukana historia yake.....kwa mzee ni muhimu kufa kwa heshima...

huyo ndie CHIFU LAWRENCE MTAZAMA GAMA comrade wa kiukweli ukweli!!
 
Poleni ukoo wa mzee Gama kwa tuliokuwa Songea enzi hizo akiwa mkuu wa Mkoa tutamukumbuka kwa kujenga uwanja wa MajiMaji na kuutangaza mkoa wa Ruvuma uliokuwa nyuma kimaendeleo kwa kuhamasisha kilimo,michezo na alikuwa ni social kwelikweli,nampa pole mwanae Stephen na dada zake.Wote ndio njia yetu ,tunapishana tu wengine wametangulia nasi tutafuata
 
R.I.P mzee , nakukumbuka enzi uko tabora na mimi nikiwa Tabora boys oooh ....... God gives and takes
 
Bujibuji, you are very right, huu ni msiba mzito sana kule Ruvuma, hususani mji mzito wa songea na vitongoji vyake ambako aliwahi kuwa mbunge kwa miaka mingi.
Sio kwamba aliisaidia tu timu ya Majimaji, ila huyu ndio Mwanzilishi wa hii timu, na alihusika sana katika kuiimarisha pia akihamasisha ujenzi wa Uwanja a Majimaji na pia akileta wachezaji hodari kama vile Abdallah "King" Kibaden (Mputa), Madaraka Seleman (Mada), Peter Tino, Mhando Mdeve, Octavian Mrope, Celestine "Sikinde" Mbunga na wengineo,.
RIP LMG.Amen

Achana na hiyo list ya MAJIMAJI nitalia ...hiyo ndiyo list iliyopeleka majimaji kombe la afrika.....acha bana!!!...enzi za mwalimu.....hizo..hata mikoani walikuwa na oppportunity ya ku excel kaama dar es salaam,maendeleo kwa sawa...mnamkumbuka SHAFIE BORAH......kulikuwa pia na yule wa TUKUYU STARS akiiitwa "KAKA"....hawa walikuwa wafadhili wa kiukweli ukweli .....pamoja na yule mzee wa yanga...BOBY SOAP....na wale wa simba kama FAKHRUDIN AMIJEE,SALAMA TRAVEL,JABIRI SHIKAMKONO...etc.....na yule wa AFRICAN SPORTS na COAST ..Acheni bana mnatupa hasira sana!!

WAPI MZEE ES...nadhani hukosi cha kusema kuhusu comrade Gama......hii ndio JF bwana ......hatupondi tu hata walioacha alama za kutukuka kama Gama .....tunawasifia bila kupigiwa debe!!!
 
Mwenyezi mungu amlaze Mahali Pema Peponi Mzee Laurence Mtazama Gama.Mzee Gama ni miongoni mwa viongozi wachache wenye Moyo wa mapenzi ya dhati kwa Nchi yao Tanzania na Watanzania kwa ujumla,Alikuwa Mtumishi aliyetukuka!....Pamoja na kushika nyadhifa kubwa mbalimbali katika chama na serikali bado alikuwa Mtu wa kutokujikweza, alikuwa mtu wa kawaida kabisa na mpenda watu.

Nilibahatika kumuona Mzee Gama akiwa Hospitali,na najua kuwa kulikuwa na utaratibu unafanywa ili apelekwe ng'ambo kwa matibabu,lakini Mauti yamemfika kabla mipango hiyo haijafanikiwa...Sisi sote tupo njiani! Sala na maombi yetu yaelekezwe kwa mpiganaji huyu.
Amen!
 
Back
Top Bottom