If you argue with a fool,people may not notice the difference.HK is suppose to be ignored...a borer due to unethical issues like certs forgery.
Ame, ndg yangu. siwezi kukulazimisha uwe mteja wangu kwenye fani. Hujaelewa vizuri, mimi nimekwambia sina njaa ya kuja kukuomba ajira kama nikishindwa uchaguzi, nitaamua cha kufanya, kwa kuwa nina options nyingi sana, ujasiriamali ikiwa mojawapo. Hili wala si la kufucha, kwa kuwa ni kazi yangu halali na nimekuwa nikiifanya kiuhalali toka nilipoacha kazi ya udaktari. Pia mimi ni mwanataaluma na Mtaalamu Mshauri wa Mambo ya kutengeneza mifumo ya afya na mambo ya afya ya jamii. Pia ni mwanaharakati wa social justice. Na pia ni Mwanasiasa. Hivyo mimi ni multi-purpose na wala sifichi kwamba nipo ubiquitous katika maisha (Biologically!) I am not a seasoned politician with nothing else but politics na ndiyo maana nakuambia boldly kabisa kwamba 'sinunuliki' na wala sifanyi kazi kwa njaa ya tumbo langu...
Kuna wanasiasa wengine wanapenda maisha ya kifahari wakati hawana kazi za kufanya, hawa unatakiwa uwahurumie uwape kazi za kufanya. Kuna mmoja wao alikuja Mwanza akaishi hotel ya kifahari kabisa ya 'Gold Crest' wakati tunamjua hata kibanda hana! Mwanasiasa kama huyu ni lazima anunulike na atumike kama wakala wa wenye fedha...
Alipokosa kuteuliwa na CCM alizimia, maana chote alichopewa na matajiri zake alikimaliza kwa kuhonga wapiga kura akitegemea ni lazima atashinda na kuwa Mbunge apate ajira!
Ame, mimi sina tamaa ya kutajirika haraka na wala sibabaishwi na umaskini, maana nimezaliwa nao. Ila nina elimu, ujuzi na nguvu zangu na huu ndiyo mtaji wangu pekee! Ninaamini hata nikifilisika namna gani, sintofilisika katika uelewa wangu, na hii inatosha kunipa sababu ya kujiamini na kutulia katika msimamo wangu...
Hapo kwenye RED mkuu umeharibu, Uvivu wa watanzania unaanzia huko huko Kwenu hasa pala mnapogonga meza zetu za Bunge kwa kushangilia ujinga. Uvivu wa watanzania ni pale Viongozi wajinga wanaotuingiza kwenye Mikataba ya kijinga na ya Kifisadi. uvivu wetu sisi Watanzania ni pale tunaposhindwa kuchukuwa maamuzi magumu ya Kuwatimua kwa nguvu nyinyi mnaotuingiza kwenye Mikataba ya kifisadi. Naona mkiwa huko Bungeni mnatusema sana na kutuita sisi wananchi ni WAVIVu wakati wavivu ni nyinyi huko DODOMA mnashindwa hata ku-Creat JOBS kwa Vijana wanomaliza vyou, Kusign mikata inayonufaisha Taifa na mambo mengine muhimu katika Taifa letu. Kwa taarifa yako nenda kawaambie wenzako mnaotuita sisi Watanzania Wavivu kuwa wao ndio wavivu, ndio uvivu wao uliotupelekea Taifa letu kuwa Gizani, Huduma za Mahospitali kuwa mbovu, maji safi hakuna, Uvivu wenu ndio uliosababisha kushuka kwa Elimu yetu. Uvivu wenu ndio unaoliangamiza hili Taifa letu. Ipo siku tutawatoleeni Uvivu na kuwafukuza kama Kuku na hiyo siku haipo Mbali.
Mtakiona cha moto chenu hiyo siku itakapowadia, Wavivu wakubwa mlioliingiza Taifa kwenye matatizo.
Kwa Taarifa yako Vijana wa kitanzania sio Wavivu bali Wazee wa tanzania waliojaa huko DODOMA na Serikali inayokumbatia Rushwa ndio kumejaa Wavivu. Peleka Salamu kwa Magamba wenzako waache kutuita Vijana wa Kitanzania Wavivu.
hivi ni kwamba maraisi wote waliopita hawakuwahi kuwa na watoto??? kama watoto wanaostahili kujivunia kazi nzuri ya baba yao ni watoto wa JKN na si wengine....ulishawasikia wakiropokaropoka hovyo??? tena wako humble kwa kila mtu na wanaheshima hata kwa watu wasiowajua
lakini sio huyu bw mdogo, mimi pia namchukia namchukuia namchukia.....
very sad... ansema hawezi kuongelea watu, lakini yuko bize kwenye twitter, facebook nkNdugu zangu wanaJF,
Kuna watu wamepewa tenda ya kunifuatilia ninachopost kwenye mtandao ili wakilete huku nitukanwe, siyo? Nashukuruni sana ndugu zangu. Ila naomba mfahamu kabisa kwamba wengi wa wanaosoma hapa JF siyo wapiga kura wa Nzega. Chuki na hasira za hao wenye machungu ya kukatwa kwa jamaa yao kwenye kura za maoni mwaka jana ni sawa na machozi ya mamba...
Kelele zenu hazinikoseshi usingizi. Sana sana mnajaribu kuukata Mbuyu kwa kutumia kiwembe, nina hakika mtakwama tu. Ya Nzega tuachieni wanaNzega, ya CCM tuachieni wanaCCM.
Narudi kwenye mada ya aliyeipost hapa:
Mimi nilishajitetea sana hapa, nadhani sasa imetosha. Kama mimi ningekuwa na urafiki wa karibu na Ridhwan na ama Baba/Mama yake ningejidai sana, maana uwaziri na hata vyeo ndani ya chama na serikali vingenielekea. Hivi ni nani kati yenu aliwahi kuniona hata siku moja nikiwa karibu na Ridhwan ama Mama yake? Kwanza naweza hata kumpotea huyo Ridhwan nikikutana naye!
Vijana wa kitanzania siku hizi tumepotea na kuanza kuongelea watu zaidi ya issues, uvivu wa kufikiri na hata ule wa kufanya kazi umetamalaki halafu tunataka mafanikio! Mimi nimegombea nikapambana na watu waliokuwa na pesa ndefu ambako mnajua ilipotoka, sikukata tamaa hata dakika ya mwisho, sasa watu hawa wenye makundi walipokatwa na mimi kuteuliwa, basi imekuwa kila siku mnanihukumu na kuniita majina ya kila aina...mngejua hata Mama Salma hanijui, hata huyo Ridhwan hanijui! Kama ningejuana nao kwa hakika ningeomba 'mchongo' wa uwaziri kwa Mkuu wa Kaya ili nimsaidie kazi....maana naona hizi ndiyo fikra za watu wengi sana hapa, kwamba ukiwa karibu na Mkuu wa kaya ama na wanafamilia wake basi wewe utapewa cheo...vijana hatutaki kufanya kazi kwa bidii na ustadi ili tufanikiwe badala yake wengi wetu tumejaa fikra za 'mafanikio hayapatikani mpaka uwe na 'mchongo' 'channel' kwa Mkuu wa Kaya...
Amini usiamini, wengine hatuko hivyo. Tunajipanga na kushambulia maisha kwa nguvu na ujuzi wetu. Ikitokea umepata basi hiyo nayo ni bahati yako...lakini usiitegemee kukutana na bahati ukiwa umelala tu.
Ninachokisema ni kwamba Ridhwan asisulubiwe kwa kuwa na haki yake ya kuzaliwa na Rais na wala asihurumiwe kwa sababu ni mtoto wa Rais. Kuna watu wanamchukia, wanamsema vibaya, Ridhwan; wanadai anaingilia shughuli za serikali na za chama, anavuruga UVCCM n.k. lakini mimi sijawahi kuona ni kitu gani alichovuruga - labda mnijuze amewahi kuingilia mambo ya serikali wapi na kivipi? Mtu akijibu hili swali nitaelewa labda, na mkishindwa kutoa maelezo ya ushahidi basi nitaelewa chuki na husuda iliyowajaa vifuani mwenu nyie na hao mahasimu wake si kingine bali ni wivu na muendelezo wa hasira za kushindwa kwenye chaguzi mbalimbali ama kunyimwa 'michongo' (ambayo wengi wenu mnaona ndiyo msingi wa maisha yenu!)
Sipendi kujadili watu na majina yao lakini siasa za wengi wenu zimenifanya na mimi niingie huko.
Wakatabahu,
HK.
Kamuulize Meneja wa TANROADS wa Arusha, pia rejea picha za siku Mkuu alipokuwa anaapishwa mara baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka jana ambapo alifanya kitu kinyume na Protocal kwa kuingia yeye na mke wake uwanja wa Taifa akishukia pale ambapo hata mawaziri kwa sikku ile hawaruhusiwi kuingilia, namaanisha kuingia uwanjani na gari na kushukia kwenye red carpet, waulize maafisa usalama namna walivyokwazika na kujikuta wakilalamika chini chini.....Ndugu zangu wanaJF,
Amini usiamini, wengine hatuko hivyo. Tunajipanga na kushambulia maisha kwa nguvu na ujuzi wetu. Ikitokea umepata basi hiyo nayo ni bahati yako...lakini usiitegemee kukutana na bahati ukiwa umelala tu.
Ninachokisema ni kwamba Ridhwan asisulubiwe kwa kuwa na haki yake ya kuzaliwa na Rais na wala asihurumiwe kwa sababu ni mtoto wa Rais. Kuna watu wanamchukia, wanamsema vibaya, Ridhwan; wanadai anaingilia shughuli za serikali na za chama, anavuruga UVCCM n.k. lakini mimi sijawahi kuona ni kitu gani alichovuruga - labda mnijuze amewahi kuingilia mambo ya serikali wapi na kivipi? Mtu akijibu hili swali nitaelewa labda, na mkishindwa kutoa maelezo ya ushahidi basi nitaelewa chuki na husuda iliyowajaa vifuani mwenu nyie na hao mahasimu wake si kingine bali ni wivu na muendelezo wa hasira za kushindwa kwenye chaguzi mbalimbali ama kunyimwa 'michongo'
Wakatabahu,
HK.
Mzalendo80, sina shaka sana na 2015. Tusiandikie mate na wino upo. Nitashinda na kuwa Mbunge tena. Tusubiri tuone...
Wananzega wameshanikubali na hakuna wa kuwabadilisha
Aisee hamisi eh, niulizie kwa godfather wako kama naweza kupata viwanja vya kigamboni na arusha, naskia ana vingi sana aisee
vipi kuhusu zile dili za baclays bank? wale jamaa waliofukuzwa wamerudishwa au bado?? maana naskia wanamtaja sana kwa kuwaingiza mkenge jamaa mmoja (babko wa duniani) kwa kuwaingiza mkenge na warabu feki??
Mie ni simple mind, nazungumzia watu.... ila ukitaka niwe serious minds... ntazungumzia issues
BTW, punguza kubwabwaja mkuu unajitia aibu tu.... we want actions not loud moth witch!!!
HK ni fisadi wa elimu tunajua ni mama salma anayekulinda ndio maana anaogopa kutumia akili zake anabaki kushikiliwa
Ninachokisema ni kwamba Ridhwan asisulubiwe kwa kuwa na haki yake ya kuzaliwa na Rais na wala asihurumiwe kwa sababu ni mtoto wa Rais. Kuna watu wanamchukia, wanamsema vibaya, Ridhwan; wanadai anaingilia shughuli za serikali na za chama, anavuruga UVCCM n.k. lakini mimi sijawahi kuona ni kitu gani alichovuruga - labda mnijuze amewahi kuingilia mambo ya serikali wapi na kivipi? Mtu akijibu hili swali nitaelewa labda, na mkishindwa kutoa maelezo ya ushahidi basi nitaelewa chuki na husuda iliyowajaa vifuani mwenu nyie na hao mahasimu wake si kingine bali ni wivu na muendelezo wa hasira za kushindwa kwenye chaguzi mbalimbali ama kunyimwa 'michongo' (ambayo wengi wenu mnaona ndiyo msingi wa maisha yenu!)
Wakatabahu,
HK.