Wana JF;
Leo nimesikia Dr. Karume akipigiwa Wimbo wa Taifa wa Zanzibar.
Mjasiliamali naye alikuwepo.
I might be out of touch . . . Hii ya "Dr" na "Wimbo wa Taifa Zanzibar" imekaaje?
Muungano wenye mataifa mawili, safi sana. Na ili kunogesha sherehe hizo, wamesombwa wananchi toka mikoa yote ya Zanzibar. Uwanja umefurika, guess the cost!
Yakhe kwani weye ulikuwa ujui kuwa Rais wa Zanzbar ni Dakreri? Au mtangazaji kakosea? Maana kila wakati amtaja kama Dr. Karume?
Hebu nielemisheni . . . Au kuna mahali alipewa Udaktari wa Heshima?
Wakuu kuwa doktor sio kazi sana kama mnavyoweza kudhani. Ukitembelea chuo kikuu fulani mara mbili mara tatu unaweza kuvikwa kigauni na kakofia ka u-doktori.
Au mmesahau jinsi nduli wa uganda alivyowaagiza watu wamwite Dr. HE. General, CBE, Alhaji;;;;;;; yote yawezekana. Hata sio vigumu sana.
Kikubwa kinachopaswa kufanywa hivi sasa ni kuuangalia Muungano kwa mapana zaidi. Ni kweli kuwa tunauhitaji Muungano lakini si katika sura na muundo uliopo sasa kwa sababu unatuletea matatizo badala ya fanaka tuliyoitarajia. Umefika wakati sasa uandaliwe mjadala wa kitaifa kuhusu Muungano na ifikiwe muafaka wa nini kinachptakiwa na watanzania wengi. mtindo huu wa kuwa watumwa wa hitoria utaendelea kuturudisha nyuma kila siku kwa sababu badala ya kufanya mambo ya maendeleo tunapoteza muda na tasilimali nyingine kujadili masuala ambayo tungeweza kuyajadili mara moja na kukubaliana
Karume alipewa udaktari wa heshima na chuo kimoja cha Marekani. Ndio maana unasikia wanamwita Dr. Karume.
Zamani ukipewa PhD ya heshima basi kweli unaheshimika kwa mchango wako uliotukuka kwa jamii au dunia kwa ujumla.
Lakini siku hizi wanajigawia tu kama njugu,mara Dr.Kikwete,mara Karume,Mzindakaya sijui....
Wacha wivu wewe...!Zamani ukipewa PhD ya heshima basi kweli unaheshimika kwa mchango wako uliotukuka kwa jamii au dunia kwa ujumla.
Lakini siku hizi wanajigawia tu kama njugu,mara Dr.Kikwete,mara Karume,Mzindakaya sijui....