Dr. Hussein Mwinyi kugombea Urais wa Tanzania 2015?

CCM Mlete mtoto wa Mwinyi ILI watanganyika TUungane tuFANYE KAMPENI ZA UTANGANYIKA VS UZANZIBARI TUONE MATOKEO, MKICHAKACHUA TUNAINGIA MSITUNI MARA HII!!!!!!
 
Mnashangaa nini?! yaleyale ya Mzee Ben na kumpigia chapuo karume Jr. akachukua nchi, sasa anaandaliwa Hussein Mwinyi kuchukua nchi! na bado Hussein Mwinyi akishachukua nchi ya Wadanganyika na Watanganyika, naye ataanza kumuandaa Riz1....ah jamani! si ndio mchezo wa utawala wa kiimla? tunalindiana maslahi yetu, au siyo? kama hakuna mabadiliko ya Katiba na tukiendelea kuukumbatia huu Muungano feki ndio tunakokwenda! tunafanywa vichwa vya wendawazimu!
 
Inawezekana ni wewe unayenekana mwehu manake wakuu wa mkoa wa Dar wengi wao huwa wanakuwa na tabia ya wehuwehu hivi.

Anachosema Gosbert ni utabiri lakini in a way siyo utabiri. Anajaribu kuangalia mazingira yaliyopo na ku-predict future kwa basis ambayo is more scientific than utabiri unaofanywa na kipenzi chako shekhe yahaya.

JF Senior Expert Member Vs Senior Member, hakuna mechi hapo kwani matokeo yanajulikana. Lakini mingine JF Senior Expert Member anaweza kujisahau katika mechi nimeona.
 
Are u great thinker or great jinga? unawezaji kulalamikia utabiri? Yaani wewe kwa akili yako inavyoonyesha jamaa akikutabiria kufa utataka pia afe na muislam kwanza. Da! imenihuzunisha kweli, mtu kuanza kulalamikia assumptions. wewe UDINI unakusumbua . Basi na mimi natabiri Serikali ijayo yote itaongozwa na Wakristo, tena wa dhehebu lako na baba yako akiwemo. Haya furahia utabiri huo, teh! teh!
Greese Thinker
 
Kaka me nazan na wewe pia ni mwehu maana katika kundi lote hili ts only u uliyejua sisi ni wehu! Nazan na wewe ni mwehu maana wapemba wanajua kwa vilemba

tehe tehe tehe tehe,jf iko poa,walahi sijuti kujiunga nayo
 
Ndugu zangu waJF,

Miezi kadhaa iliyopita nilipost thread mbili humu jamvini zote zikimtabiria Mzee Mukama kuwa ndiye possible candidate wa kikwete kwenye kiti cha ukatibu mkuu wa ccm. Hatimaye utabiri huo ulitimia. Chanzo changu cha uhakika kutoka kwenye system kilinipa guts za kupost hizo threads.

Sasa naomba kwa mara nyingine na mwisho niwaambie jambo moja. Kama mtakumbuka miezi kadhaa imepita tangu vijana wa ccm mkoa wa pwani walipotoa tamko lao la kulaani wazee hususan mawaziri wakuu wastaafu wanaokikosoa chama na serikali yake. Katika laana hiyo walitamka jambo moja ambalo huenda wengi wetu hatukulitilia maanani na tukalipuuza japo Mzee Sumaye alilitolea kauli kwenye mwitikio wake kuhusu laana hiyo ya vijana.

Wale vijana waliwatuhumu wazee wastaafu kuwa wanautafuta urais na wakawaonya kuwa wasipoteze muda kuusaka urais kwani anayemjua rais ajaye ni kikwete peke yake. Katika fukuafukua yangu nimebaini kuwa wale vijana hawakuwa wajinga kama wengi wetu tulivyowapuuza. Walitumwa kuwavunja mioyo siyo wazee wastaafu tu bali na wengine wanaofikiria kutangaza nia kwa tiketi ya CCM.

Kwa taarifa yenu na naomba msipuuze hata kidogo, mgombea urais kwa tiketi ya CCM atakuwa ni mtoto wa mzee mwinyi anayefahamika kwa jina la Husein Mwinyi ambaye kwa sasa ni waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa. Kwa wanaoijua vema siasa ya nchi yetu, watahitaji dakika chache tu kujikumbusha mambo kadhaa kabla ya kuunga mkono utabiri huu.

Kazi kwetu wanaJF kumjadili huyo jamaa.

Kwa nini asiwe Madaraka Nyerere au Makongoro Nyerere? au kwa sababu Baba yake alishafariki? Mbona Amani Karume alipewa wakati baba yake alishafariki?

Kwa mtazamo wangu enzi ya Chama kimoja hilo lingewezekana lakini enzi hizi za Vyama vingi watu 1,000,000 kuwatawala watu 40,000,000 itahitaji kampeni ya pesa nyingi sana. Labda mgombea mwenza awe mtu mashuhuri sana kama Lowasa
 
Kama ndivyo hvyo basi UDINI utaandaliwa tena iwe zengwe kwa CDM kwa maana CCM wanajua hvihvi hawataweza kufua dafu kwa Dr.Slaa hvyo ili kubalance mchezo itabidi zipikwe kampeni za UDINI kati ya mwislamu (Mwinyi CCM) Vs mkristo (Dr.Slaa CDM)

kama hili tulikuwa hatujalifahamu basi CDM tuanze kulifikiria pia,tujipange vzuri kuruka kiunzi hiki,
 
Rais ajaye atakuwa either mzanzibari (nakubaliana na Gosbert kwamba anaweza kuwa Dr. Hussein Mwinyi) au anaweza kuwa mwanamke, na hapa Dr Rose Migiro anaweza kupeta!

My Take: Dr Rose Migiro ana-stand chance nzuri zaidi ya kuwa Rais kwa sababu already kulikuwa na maneno wakati Amani Karume alipogombea kwamba inakuwa kama "usultani" vile, kwa sababu baba yake aliwahi kuwa Rais wa Zanzibar .... hivyo nadhani logically, kuna watu (walioko kwenye maamuzi) wataona ni afadhali mwanamke achukue kuliko mtoto wa Rais mstaafu!
 
Sheikh Yahaya in tha making! Enheee mnajimu wangu tuambie na mwisho wa dunia ni lini?au wewe unatabiri ktk siasa tu?okey kma ni siasi tu tutabilie mkuu wa mkoa mpya wa dsm ni nani?

wewe ni mnafiki na umekaa kinafki,hasa the way unavyouliza.....don act as a stupid
 
CCM wana kura milioni tisa kibindoni ujue. Hazina mgogoro hizo
Hizo kura milioni tisa zilikuwa 2005 kabla ya watu kutambua geresha za ******. Uchaguzi wa 2010 CCM iliambulia kura milioni 4. Kufikia 2015 watakuwa wamebakiwa na milioni mbili tu. Na kuhusu Mwinyi huyu mtu hafai hata kuwa waziri, sembuse rais wa nchi. Ni daktari ambaye hajawahi kutibu, pale wizara ya Ulinzi anapwaya, i.e mbagala na gongo la mboto. Bungeni amekaa tu kama pambo la maua dirishani. Mtu kama huyu hawezi kuiongoza Tanzania katika karne hii ya 21. Na kuhusu Asha Rose Migiro ngoja nichunie comments zangu mpaka wakati muafaka. Tunaweza kudhani tumepata kumbe tumepatikana.
 
Habari ndani ya Habari

CCM kupitia Katibu Mkuu wake mpya, imefichua mengi kutokana na kauli ya sentenso moja tu wakati kiongozi huyo alipojibu kwa jazaba swali kama CCM haielekei kaburini.

Kiongozi huyo alisikika akisema kwa sauti iliyosikika na kila mtu kwamba vyama vitakavyokufa ni vile vilivyoanzishwa na IMF, na hapo ndipo palipo pa tamu.

Kwa kauli hiyo, yaani kelele na majigambo yote ya CCM kujivua gamba imedhihirika ni unafiki na ghiliba tupu kwa Watanzania.

Tofauti na tulivyoamini sio kwamba Nyerere ndiye aliyeshawishi CCM ikubali mfumo wa vyama vingi, wala sio upevu wa kiakili na uono wa mbali wa viongozi wake ndio ulioona busara na hekima ya kukubaliana na maoni ya wachache (waliosoma na kwenda shule) na kukataa ya wengi (wasiosoma na wasiojua dunia ilikotoka na inakoelekea) bali ni SHINIKIZO LA IMF ndilo lililoanzisha NCCR-Mageuzi, CUF, CHADEMA, TLP na vyama vingine mbadala nchini.

Katibu Mkuu huyo mpya pamoja na kuogopewa na waandishi wa habari kwa kauli zake za kujibu kimkato na kidharaudharau hakujua kuwa anaitumia nafasi hiyo kuonyesha kuwa CCM sio kwamba imejivua gamba bali imeongeza gamba lingine la viongozi wasiokubali ukweli, wasioielewa hali halisi ya wananchi na hususan vijana na matarajio yao na kwamba siye mtu anayeweza kuleta mabadiliko ya msingi katika chama hicho tofauti na alivyokuwa aliyemtangulia uongozini.

NInadiriki kusema kwa maoni yangu CCM ilichokifanya kwa kumbadili Makamba na kiongozi huyu wa sasa ni kutoka kwenye kikaango na kuangukia kwenye moto ambao ndio umeanza kuwaka kiwelikweli sasa.
Propaganda za kuchafuana na kuvitakia mabaya vyama mbadala ni mambo yaliyopitwa na wakati na kiongozi bora wa chama cha kisiasa ni yule anayekubali ukweli kuwa sasa tuna vyama vingi na tofauti na tulivyodumu na chama kimoja kwa maguvu kwa miaka takriban 30 hili la kuwepo vyama vingi litadumu kwa hiari yetu sote milele.

Kiongozi huyo kadhihirisha kwamba haamini katika demokrasia na hatoweza kujenga demokrasia ndani ya chama chake katika ngazi za chini wala juu, sembuse kuchangia la maana katika demokrasia ya nchi. Lo, bahati mbaya CCM imepoteza nafasi ya kufunga goli la ushindi katika dakika za mwisha kabisa kwa kuchagua kiongozi ambaye asiyeamini katika demokrasia na mfumo wa vyama vingi.

Inavyoelekea hata hili la kuandikwa kwa katiba mpya ndugu yetu mpendwa anaamini ni kutokana na shinikizo la IMF. Naam, lakini katika hali kama aliyonayo na vijana wanaotakiwa kwenda kusoma digrii nje, sio rahisi hata unapojijua siye unayeweza na siyo mwanademokrasia halisi kukataa nafasi ya dhahabu kama hiyo ambayo ndani ya miaka miwili tu unaweza kujiikuta unshasema baibai kwa ulalahoi yakhe!
Na nyie waandishi wa habari jamani jaribuni kusoma kidogo na kutazama vipindi vya mahojiano kama ED show cha msnFox au Riz Khan wa Aljazeera au Hardtalk cha BBC ili muweze kuitendea jamii haki kwa kuwauliza viongozi wetu maswali yatakayotusaidia kutambua viongozi kwelikweli na wababaishaji!
 
wewe ni mnafiki na umekaa kinafki,hasa the way unavyouliza.....don act as a stupid

We ndo mnafiki na mvivu wa kufikiri pia,kwann uanze kushabikia utabiri na usijenge taifa?uchaguzi 2015 c tunabishana ccm watamsimamisha nani?inahusuu? Ttz lenu nyie mabwana mtu akiwa na msimamo tofauti kdg na nyie anakua mnafiki,fisadi etc! Fanya kazi achana na mambo ya utabiri mjumbe
 
Sina uhakika na Mwinyi kugombea Urais 2015 lakini naamini CCM lazima watatoa mgombea kutoka Zanzibar! Haitakuwa fair kwa Wazanzibar kwa mara ya 3 mfululizo wanakosa mgombea wa Urais vinginevyo huu Muungano wa 'kijanja' hautakuwa na maana yoyote!
 
Nafikiri na mimi nilisikia kuwa huyo atakuwa wa Zanzibar!!!................ Nways ni utabiri ngoja tungoje
 
Mozze,

Naomba nikupe angalizo hili: Kwa katiba hii iliyopo na muundo wa tume ya uchaguzi, yeyote atakayesimamishwa na ccm atapita tu, hata ungekuwa wewe. Utaratibu wa kumpata Rais baada ya uchaguzi ni yule atakayetangazwa na tume. Kwa hiyo swala siyo wingi wa kura hapa, ila ni nani katangazwa na tume. Na kwa vile tume itaendelea kuwa ya kuteuliwa na rais, jibu hapa ni rahisi, mgombea wa ccm lazima atangazwe mshindi.
 
GosbertGoodluck heshima kwako!

Ingawa huna kosa lolote ktk ku-predict presidential candidate wa CCM 2015, utabiri wako nauogopa na ninaomba isiwe kweli maana endapo Dr Mwinyi akashinda (kwa zengwe) basi hilo litamaanisha another decade ya Uongozi dhaifu kwa nchi yetu.
Taratibu naona amani ya nchi yetu inatoweka maana sidhani watanzania bado wana uvumilivu wa kiwango hicho!
 
Hili la Mwinyi nimeshalitabiri siku nyingi tu, tangu tu alipoacha kuwa Mbunge wa kwetu Mkuranga na kwenda zanzibar nilishawaambia ndugu zangu kuwa ndg yetu ameenda kuijiaandaa kwa uraisi wa Bara
 
Back
Top Bottom