Huyu ni mkurugenzi wa NSSF jana amesema hakuna fao la kujitoa wakati akijua fika yafuatayo;-
1. Suala hili limerudishwa bungeni.
2. Kwa miaka kadhaa watu wamekuwa wakijitoa NSSF na ama kujiunga na mifuko mingine ama kurudi tena NSSF.
3. Hoja yake ameiunganisha na sheria za kimataifa lakini hajatuambia kuwa wenzetu wa nje wanakatwa asilimia ngapi katika mshahara wa jumla, hii 10% ni kubwa mno kukaa kwao na eti kusubiri miaka 55, kama yeye kazeeka ajue kuna watu wana miaka 30-40 ambao wanamipango ya kujiajiri hivyo wangependa kutumia mtaji uliopo ambao ni haki yao. kusubiria milioni 3 kwa miaka 20 huu ni sawa sawa na wendawazimu, kipindi hicho kampuni nyingi zitakuwa hazipo ama zimefungwa nani atatujazia fomu zetu. Asifikiri Kampuni binafsi ni sawa na serikalini. Achilia mbali makampuni yanayobadilisha majina kama vinyonga.
4.Mipango yao ya kutukopesha fedha zetu wenyewe kupitia Sacoss ni kutuibia kwa mlango wa uani.
5.Tunajua ahadi zao ni nyingi lakini hazitekelezeki, mfano mfumo wa kadi mpya tukaambiwa kutakuwa na mashine mpaka leo hakuna kitu.
6. Eid Njema.
1. Suala hili limerudishwa bungeni.
2. Kwa miaka kadhaa watu wamekuwa wakijitoa NSSF na ama kujiunga na mifuko mingine ama kurudi tena NSSF.
3. Hoja yake ameiunganisha na sheria za kimataifa lakini hajatuambia kuwa wenzetu wa nje wanakatwa asilimia ngapi katika mshahara wa jumla, hii 10% ni kubwa mno kukaa kwao na eti kusubiri miaka 55, kama yeye kazeeka ajue kuna watu wana miaka 30-40 ambao wanamipango ya kujiajiri hivyo wangependa kutumia mtaji uliopo ambao ni haki yao. kusubiria milioni 3 kwa miaka 20 huu ni sawa sawa na wendawazimu, kipindi hicho kampuni nyingi zitakuwa hazipo ama zimefungwa nani atatujazia fomu zetu. Asifikiri Kampuni binafsi ni sawa na serikalini. Achilia mbali makampuni yanayobadilisha majina kama vinyonga.
4.Mipango yao ya kutukopesha fedha zetu wenyewe kupitia Sacoss ni kutuibia kwa mlango wa uani.
5.Tunajua ahadi zao ni nyingi lakini hazitekelezeki, mfano mfumo wa kadi mpya tukaambiwa kutakuwa na mashine mpaka leo hakuna kitu.
6. Eid Njema.