Dr. Dau aingilia mchakato wa ugawaji viwanja Mafia

Mleta hoja kashindwa kurudi kwani majina ya waliopewa viwanjahayo hapo juu

DC, MP na Mkurugenzi wa manispaa wanahaha kumtafuta RK akubali walau kiwanja kimoja ili yaishe

mwenyewe kakataa na hataki kuhongwa kiwanja
 
Mleta hoja kashindwa kurudi kwani majina ya waliopewa viwanjahayo hapo juu

DC, MP na Mkurugenzi wa manispaa wanahaha kumtafuta RK akubali walau kiwanja kimoja ili yaishe

mwenyewe kakataa na hataki kuhongwa kiwanja

Nipo mkuu wangu, naangalia jinsi ambavyo mnaboresha yale ambayo nimesema. Majumuisho yanakuja na hasa wewe, Mizizi na Nasdaq mmethibitisha yale niliyosema. Mimi napenda mijadala na nimefurahi sana kwa nyie "kujifungua" na kuongea "hasa" yale yanayowakera watu wa Mafia.

Nadhani sasa wakati umefika sisi "watumwa" au watumishi "wakosefu" au "wafungwa wa kisiasa" au "watumishi tusio na uwezo" tuondoke tuwaachie Mafia yenu. Tunasubiri hayo majibu ya tume, sisi tuanze maana hatuna haki "huku". Lakini kumbukeni na sisi tuna "kwetu"! Nilibezwa mwanzo kwamba mm ni mdini, mkabila n.k. lakn sasa ukweli umeonekana.

Ilikuwa mada chokozi na kweli imewaibuwa!! Endeleeeni na Mafia yenu.
 
Mleta hoja kashindwa kurudi kwani majina ya waliopewa viwanjahayo hapo juu

DC, MP na Mkurugenzi wa manispaa wanahaha kumtafuta RK akubali walau kiwanja kimoja ili yaishe

mwenyewe kakataa na hataki kuhongwa kiwanja

Ni bora mngejipanga vizuri kutetea hili, kuingiza mambo ya "Ushoga" mmeonesha kabisa kuishiwa hoja!!
 
Nipo mkuu wangu, naangalia jinsi ambavyo mnaboresha yale ambayo nimesema. Majumuisho yanakuja na hasa wewe, Mizizi na Nasdaq mmethibitisha yale niliyosema. Mimi napenda mijadala na nimefurahi sana kwa nyie "kujifungua" na kuongea "hasa" yale yanayowakera watu wa Mafia.

Nadhani sasa wakati umefika sisi "watumwa" au watumishi "wakosefu" au "wafungwa wa kisiasa" au "watumishi tusio na uwezo" tuondoke tuwaachie Mafia yenu. Tunasubiri hayo majibu ya tume, sisi tuanze maana hatuna haki "huku". Lakini kumbukeni na sisi tuna "kwetu"! Nilibezwa mwanzo kwamba mm ni mdini, mkabila n.k. lakn sasa ukweli umeonekana.

Ilikuwa mada chokozi na kweli imewaibuwa!! Endeleeeni na Mafia yenu.

Hata mkiondoka ni sawa tu, hamna utumishi uliotukuka, kila kitu mafia ni tatizo, bado mnataka kupata heshima ya kutambulika kama watumishi wa wananchi! Mmefanya deal maisha ya wamafia kwa tamaa binafsi, kila kitu mafia hakipo sawa sawa! Mnafanya deal na kuleta makandarasi walio chini ya viwango, matokeo yake kila kitu ni cha kurudia rudia, angalia makaravati yaliyojengwa kwenye bara bara mbali mbali yalivyo chini ya kiwango, hasa lile pale karibu na idara ya maji. Hospitali ya wilaya haina jenereta la dharura umeme unapokatika kwa uzembe tu, kwani generetor limeharibika na halijafanyiwa matengenezo zaidi ya mwaka sasa. Angalia watumishi wa idara ya kilimo, wana nini cha kujivunia? Na wengine wanazeekea mafia. Wakati mnafanya kazi mnafanya kwa uzembe na ubinafsi kwa kuwa si wamafia na mnaleta dharau kwa wakazi wa mafia, leo mnalalamika mnataka viwanja mafia na mnaona ni sehemu inayowahusu!
 
Hata mkiondoka ni sawa tu, hamna utumishi uliotukuka, kila kitu mafia ni tatizo, bado mnataka kupata heshima ya kutambulika kama watumishi wa wananchi! Mmefanya deal maisha ya wamafia kwa tamaa binafsi, kila kitu mafia hakipo sawa sawa! Mnafanya deal na kuleta makandarasi walio chini ya viwango, matokeo yake kila kitu ni cha kurudia rudia, angalia makaravati yaliyojengwa kwenye bara bara mbali mbali yalivyo chini ya kiwango, hasa lile pale karibu na idara ya maji. Hospitali ya wilaya haina jenereta la dharura umeme unapokatika kwa uzembe tu, kwani generetor limeharibika na halijafanyiwa matengenezo zaidi ya mwaka sasa. Angalia watumishi wa idara ya kilimo, wana nini cha kujivunia? Na wengine wanazeekea mafia. Wakati mnafanya kazi mnafanya kwa uzembe na ubinafsi kwa kuwa si wamafia na mnaleta dharau kwa wakazi wa mafia, leo mnalalamika mnataka viwanja mafia na mnaona ni sehemu inayowahusu!

Safi sana mkuu, sasa muandike na barua TAMISEMI kwamba watumishi wote Mafia wawe ni "wazaliwa" wa Mafia maana sisi "mabwege" na kuwaharibia mazingira na kuchukua ardhi, hewa na kila kitu cha watu wa Mafia.

Andikeni turudi "makwetu" tuwaaaache na Mafia yenu!
 
Dk. Dau ni mnafiki na fisadi. Nani asiyekumbuka ule mradi mkubwa wa NSSF and Manji? Kule Mafia amesababisha mgogoro mkubwa baada ya kujenga shule yake kwenye kijiji chao cha Bweni, huku wananchi wa Kiriongwe, Banja na Kanga wakigoma kupeleka watoto wao kutokana na ubinafsi wake wa kuwatukana kwa kuwambia hawakwenda shule. Hana lolote mzushi mkubwa huyuuuu.
 
Dk. Dau ni mnafiki na fisadi. Nani asiyekumbuka ule mradi mkubwa wa NSSF and Manji? Kule Mafia amesababisha mgogoro mkubwa baada ya kujenga shule yake kwenye kijiji chao cha Bweni, huku wananchi wa Kiriongwe, Banja na Kanga wakigoma kupeleka watoto wao kutokana na ubinafsi wake wa kuwatukana kwa kuwambia hawakwenda shule. Hana lolote mzushi mkubwa huyuuuu.

Nothing, but wivu wa kike! Wewe kijijini kwako umepeleka nini? Unachosema si sahihi!
 
Dk. Dau anapita Mafia na kutamba kwamba hakuna mtu wa kumshughulisha, maana hata huyo Jakaya Kikwete nampa misaada. Katika uchaguzi mkuu uliyopita, amekipa chama zaidi ya Sh. 100 milioni. Hata mawaziri hawawezi kumshughulisha kwa kuwa yeye anawapa maekelezo. Anasema hababaishwi hata na jeshi, ndiyo maana meli ya Kasa inayomilikiwa na jeshi ilipoondoka Mafia bila kupakia magari yake, aliamrisha mkuu wa majeshi na kuirejesha meli hiyo iliyokuwa imekaribia kufika Dar es Salaam kuja kuchukua magari yake mawili aliyokwenda nayo Mafia kuyatumia wakati yeye na ndugu yake **** walipoenda kutoa msaada kwa CCM ili kutengeneza mazingira mazuri ya ubunge 2015.

 
Dk. Dau ni mnafiki na fisadi. Nani asiyekumbuka ule mradi mkubwa wa NSSF and Manji? Kule Mafia amesababisha mgogoro mkubwa baada ya kujenga shule yake kwenye kijiji chao cha Bweni, huku wananchi wa Kiriongwe, Banja na Kanga wakigoma kupeleka watoto wao kutokana na ubinafsi wake wa kuwatukana kwa kuwambia hawakwenda shule. Hana lolote mzushi mkubwa huyuuuu.

watu wanaongea kwasababu ametajwa Dr Dau! Unachoongea si cha kweli, mimi nimekaa bweni na nimefundisha hiyo shule kwa muda zaidi ya miezi 3, nimeona wanaffunzi kutoka sehemu mbalimbali, ikiwemo kanga, Kirongwe, banja, na hata chemchem! Kulikuwepo na wanafunzi kutoka utende, chole na jibondo! Huo ubinafsi unaoseema umepata wapi taarifa? Kijiji cha Bweni anapotoka Dr Dau kuna shule kuna shule moja tu ya msingi, ambayo haiwezi kutoa wanafunzi wa ku accommodate idadi ya anafunzi wanaohitajika kujiunga na kidato cha kwanza shuleni hapo! Dr Dau si mjinga kama wewe afanye hivyo! Kisha dr Dau si Mmiliki wa shule hiyo, na wala hizo pesa hakutoa mfukoni mwake, kwani hana ukwasi kiasi hicho! Suala la NSSF na Manji inaonekana huko updated, wenzako waliga kelele na walipopata ukweli wakanyamaza!
 
Dk. Dau anapita Mafia na kutamba kwamba hakuna mtu wa kumshughulisha, maana hata huyo Jakaya Kikwete nampa misaada. Katika uchaguzi mkuu uliyopita, amekipa chama zaidi ya Sh. 100 milioni. Hata mawaziri hawawezi kumshughulisha kwa kuwa yeye anawapa maekelezo. Anasema hababaishwi hata na jeshi, ndiyo maana meli ya Kasa inayomilikiwa na jeshi ilipoondoka Mafia bila kupakia magari yake, aliamrisha mkuu wa majeshi na kuirejesha meli hiyo iliyokuwa imekaribia kufika Dar es Salaam kuja kuchukua magari yake mawili aliyokwenda nayo Mafia kuyatumia wakati yeye na ndugu yake **** walipoenda kutoa msaada kwa CCM ili kutengeneza mazingira mazuri ya ubunge 2015.


Duh! Mkuu naona ndoto zako za kisiasa zimetikiswa! Tuwasiliane kaka nikupe relief!!
 
Wakuu,
Jamaa huyu ambaye ni Mkurugenzi wa NSSF Dr Ramadhani K. Dau amezuia mchakato wa ugawaji wa viwanja Mafia sababu yeye na mdogo wake Mbaraka hawajapata viwanja vyote wanavyovitaka!!
Madai yake kwamba waliopewa si "wenyeji" wa Mafia bali tu ni watumishi wa serikali walioletwa Mafia hivyo hawana "haki" ya kuwa na viwanja Mafia. Pia suala la "udini" limeingia kwamba waliopewa eti wengi ni wakristo!!

Dr Dau kaandika barua Tamisemi na sehemu nyingine akipinga kwamba utaratibu haukufuatwa kugawa viwanja Mafia.

My take: sisi watanzania ambao tunafanya kazi Mafia hatuna haki kama watanzania? Kupata kiwanja Mafia ni lazima uwe resident wa Mafia? And if so is Dr Dau a resident of Mafia? Na mtumishi wa serikali aliyekaa miaka 15 Mafia siyo mkazi wa Mafia?

Mnatukwaza sisi watumishi wa serikali ambao hata "hatujui" kesho tutakuwa wapi!!?
Kamaimekumeni rudin kwenu kwan mna msaada na MAFIA wewe nisawa na miongoni nawanaotaka kuolewa.
 
Information zinazoendelea ni kuwa on this Dr Dau ameonyesha uadilifu ambao viongozi wengi hawana

mfano jioni hii mkurugenzi wa halmashauri anahaha kutafuta watu wambembeleze Dr aende akapewe ardhi ili yaishe

na hapo ndugu yake (Muba) kapewa sasa katika hali ya kawaida Dr alitakiwa kuwa kimya lakini ameamua kulalamika kwani haki haijatendeka

as we speak Dr amekataa hii rushwa ya kupewa kiwanja ili yaishe

Haya ni mazuri kabisa na anastahili kupongezwa. Lakini kama analalamika kuwa kwanini Wakristu wanapewa viwanja Mafia au kama analalamika kwanini Watanzania wanaotoka sehemu nyingine wanapewa viwanja (wawe Wakristu au Waislamu) hapo anatatizo. Je, Dr analalamikia kwa namna yoyote component ya dini?
 
Nipo mkuu wangu, naangalia jinsi ambavyo mnaboresha yale ambayo nimesema. Majumuisho yanakuja na hasa wewe, Mizizi na Nasdaq mmethibitisha yale niliyosema. Mimi napenda mijadala na nimefurahi sana kwa nyie "kujifungua" na kuongea "hasa" yale yanayowakera watu wa Mafia.

Nadhani sasa wakati umefika sisi "watumwa" au watumishi "wakosefu" au "wafungwa wa kisiasa" au "watumishi tusio na uwezo" tuondoke tuwaachie Mafia yenu. Tunasubiri hayo majibu ya tume, sisi tuanze maana hatuna haki "huku". Lakini kumbukeni na sisi tuna "kwetu"! Nilibezwa mwanzo kwamba mm ni mdini, mkabila n.k. lakn sasa ukweli umeonekana.

Ilikuwa mada chokozi na kweli imewaibuwa!! Endeleeeni na Mafia yenu.

Mkuu, acha kujiliza ili kutafuta huruma ya wale waioifahamu Mafia. Awali ya yote, mimi sio mwenyeji na wala sina nasaba yoyote na Mafia hivyo sina interest yoyote kwa haya ninayosema tofauti na wewe ambae una interest ktk masuala ya viwanja. Si kweli hata kidogo, na huo ni uzushi uliovuka mipaka ambao unapaswa kuuonea aibu kudai kwamba kuna ubaguzi dhidi yenu. Generally speaking, over 95 % ya Wamafia ni Waislamu na majority ya watumishi wa umma ni Christians. Lakini hata hivyo, si kweli hata kidogo kwamba kuna ubaguzi wowote ule. Makanisa yote pale mafia, hususani Kilindoni yamezungukwa na wakazi wa mafia ambao ni waislamu huku kanisa la Lutheran likiwa karibu kabisa na Madrasa na lile la Katoliki likiwa umbali mfupi tu toka Msikiti Mkuu wa Mafia. Je, kungekuwa na huo ubaguzi unaosema wewe hayo ; yangefanyika?! Ukweli bado unabaki pale pale, hata kama nanyi mna haki ya kupata ardhi Mafia na Wamafia wenyewe wana haki hiyo hiyo. Na kwavile Watumishi wapo powerfully economically as well as kiutawala/mamlaka; hawa wenyeji lazima wapewe special attention kwavile hawana ubavu wa ku-compete na nyinyi kwenye fair(unfortunately, hata hiyo hapo sio fair) play ground. Hata mzazi mwenye busara, ana aina yake ya kum-treat mtoto aliye na mapungufu kwa kulinganisha na wengine. Nyerere aliposema madini yaachwe hadi Watanzania watakapokuwa na uwezo wa kuyachimba haikuwa ubaguzi bali alifahamu ktk mazingira kama yale Wa TZ wasingenufahika(ingawaje hata sasa hatunufaiki). Hivyo, ingawaje hatuwezi kusema viwanja mafia visigawanywe hadi wenyeji watakapokuwa na the same competitive power as watumishi wa umma (plz, usipotoshe, sio wageni na wakristo); lakini bado kuna umuhimu wa namna gani wenyeji wanaweza na wao kunufaika na ardhi za babu zao.Huo Mkuu, sio ubaguzi! Achana na kilio cha propaganda cha kuhitaji huruma ya watu humu ndani. Hebu angalia hiyo list, labda kama unaikana. Wengi hapo ni Watumishi wa halmashauri. Hapo fairness itatoka wapi?! Nami nina uhakika, wengi wao hapo wanachukuwa viwanja wakati walishapata awamu ya kwanza walipogawa viwanja vya Dongo; sasa kama sio ulafi tuite nini?! Likewise, wengine hapo wanachukua viwanja ili baadae waviuze wakati wengine shida yao wavitumie kwa makazi; wakishindwa kujenga wao, basi angalau watoto wao.
 
Information zinazoendelea ni kuwa on this Dr Dau ameonyesha uadilifu ambao viongozi wengi hawana

mfano jioni hii mkurugenzi wa halmashauri anahaha kutafuta watu wambembeleze Dr aende akapewe ardhi ili yaishe

na hapo ndugu yake (Muba) kapewa sasa katika hali ya kawaida Dr alitakiwa kuwa kimya lakini ameamua kulalamika kwani haki haijatendeka

as we speak Dr amekataa hii rushwa ya kupewa kiwanja ili yaishe

Kwa nini hakuonyesha uadilifu in the first place? Wacha kupiga hizi chapua za kizamani.
 
Tumewachka sana sasa, mmetujaribu sana kwa mda mrefu tumekaa kimya! Haimaanishi wamafia ni wajinga kama mnavyotuita! Ukweli sasa inatosha, na mnachokitafuta mtakipata mda si mrefu, na huu ndio mwanzo!
 
Haya ni mazuri kabisa na anastahili kupongezwa. Lakini kama analalamika kuwa kwanini Wakristu wanapewa viwanja Mafia au kama analalamika kwanini Watanzania wanaotoka sehemu nyingine wanapewa viwanja (wawe Wakristu au Waislamu) hapo anatatizo. Je, Dr analalamikia kwa namna yoyote component ya dini?

Sizani kama inahitaji shahada ya elimu yoyote kufahamu kwamba Dau hawezi kulalamikia Wakristo kupewa viwanja. Hata hivyo, anaweza kulalamikia Wageni kupewa viwanja ikiwa anaona wenyeji wanakosa hata kama taratibu zimefuatwa.....bado nasisitiza,popote pale; unfair competition haikubaliki! Duniani kote kunakokuwa na machafuko kuhusu ardhi sio kwamba wote wenye ardhi walijitwalia kwa nguvu; la hasha.....taratibu zilifuatwa lakini TWO teams with completely different power zikawekwa kwenye the same play field. Siku watu wanapoamka, ndipo wanapouliza, kama hapa ndio kwetu kwanini ni watwana na manokoa......huwezi kumwambia mtu kama huyo "na wewe nenda kwa hawa jamaa ukapate ardhi ya kwako....that's purely politics!
 
Ni bora mngejipanga vizuri kutetea hili, kuingiza mambo ya "Ushoga" mmeonesha kabisa kuishiwa hoja!!

Listi hiyo umepewa tuonyeshe wapi DR DAU kapewa kiwanja?

If anything wewe na huyo anyekutuma mmekuwa muflisi na nashauri mwende mkajipange vizuri huko bungeni
 
Back
Top Bottom