Baada ya Dr Kafumu kuapishwa rasmi bungeni hivi leo.,Chama cha CCM kimemuandalia sherehe fupi ya kumpongeza na kumkaribisha rasmi akiwa kama mbunge mpya kupitia chama iko kutoka katika Jimbo ambalo lilikuwa na ushindani wa hali ya juu..,katika maneno yake Dr Kafumu amedai kuwatumikia watanzania, wanaccm lakini hasa wanaigunga ndio hasa msingi wa msukumo wake katika kuwania ubunge ambao anashukuru kuwa wanaigunga wamemteuwa.
Dr kafumu ameendelea kudai kuwa kwa sasa hana jambo lingine linalomsubiri mbele yake isipokuwa kutimiza azma yake ya muda mrefu ya utumishi kwa umma na katika hilo hatojali ama kuzingatia nani alikuwa adui kwake kipindi cha harakati za uchaguzi bali anawakaribisha watu wote katika kumshauri, kumrekebisha na kushikamana nae katika Dhamira yake hii.
Sherehe hizo fupi zinafanyika ukumbi wa CCM-Dodoma, Makao Makuu, ambapo msafara wa Dr Kafumu utapokelewa na Mheshimiwa Nape ambae amerejea jana kutoka Marekani alikokwenda kukagua uhai wa chama na maendeleo yake.
Dr kafumu ameendelea kudai kuwa kwa sasa hana jambo lingine linalomsubiri mbele yake isipokuwa kutimiza azma yake ya muda mrefu ya utumishi kwa umma na katika hilo hatojali ama kuzingatia nani alikuwa adui kwake kipindi cha harakati za uchaguzi bali anawakaribisha watu wote katika kumshauri, kumrekebisha na kushikamana nae katika Dhamira yake hii.
Sherehe hizo fupi zinafanyika ukumbi wa CCM-Dodoma, Makao Makuu, ambapo msafara wa Dr Kafumu utapokelewa na Mheshimiwa Nape ambae amerejea jana kutoka Marekani alikokwenda kukagua uhai wa chama na maendeleo yake.