JokaKuu
Platinum Member
- Jul 31, 2006
- 30,441
- 55,018
..jamani tukisema Zanzibar wanatunyonya Tanganyika mnadai tunachonga sana.
..lakini kuna bil 4 zimetengwa kwa ajili ya Makamu wa Raisi, wanasema kwa matumizi "yake" ya kawaida.
..huyu ndiye makamu wa Raisi ambaye muda mfupi baada ya kula kiapo, aliamua kwenda likizo na familia yake kutembelea mbuga za wanyama, badala ya kuwatumikia wananchi.
..halafu kuna bilioni 32 kwa ajili ya maendeleo ya wa-Zanzibari. Je, fedha kiasi gani zimetengwa na ofisi ya makamu wa raisi kwa ajili ya maendeleo ya wa-Tanganyika??
..mwisho, hii ofisi ndiyo inayoshughulikia kero za muungano, lakini makamu wa raisi, na waziri mwenye dhamana ya muungano wote ni wa-Zanzibari. yaani ktk suala la kero za muungano wanakaa wa-Zanzibari wawili na kufanya maamuzi wenyewe.
..lakini kuna bil 4 zimetengwa kwa ajili ya Makamu wa Raisi, wanasema kwa matumizi "yake" ya kawaida.
..huyu ndiye makamu wa Raisi ambaye muda mfupi baada ya kula kiapo, aliamua kwenda likizo na familia yake kutembelea mbuga za wanyama, badala ya kuwatumikia wananchi.
..halafu kuna bilioni 32 kwa ajili ya maendeleo ya wa-Zanzibari. Je, fedha kiasi gani zimetengwa na ofisi ya makamu wa raisi kwa ajili ya maendeleo ya wa-Tanganyika??
..mwisho, hii ofisi ndiyo inayoshughulikia kero za muungano, lakini makamu wa raisi, na waziri mwenye dhamana ya muungano wote ni wa-Zanzibari. yaani ktk suala la kero za muungano wanakaa wa-Zanzibari wawili na kufanya maamuzi wenyewe.
gazeti la mwananchi said:Makamu wa Rais atengewa Sh4 Bilioni
Friday, 06 July 2012 20:09
MAKAMU wa Rais, Dk Ghalib Bilal ametengewa Sh4 bilioni kwaajili ya matumizi yake ya kawaida.
Hayo yalibainishwa na Waziri wa Wizara hiyo, Samia Suluhu wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya fedha kwa mwaka 2012/13 bungeni.
Alisema ili kuhakikisha Makamu wa Rais anaweza kufanya shughuli zake za kawaida , waliliomba bunge liidhinishe maombi ya fedha ya wizara hiyo ambapo katika mchanganuo wa maombi hayo, wameomba Makamu wa Rais atengewa Sh4 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
Alisema mbali na fedha hizo za matumizi ya kawaida, ofisi yake pia imetengewa Sh42 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na Sh10 bilioni kwa shughuli za maendeleo, alisema Suluhu na kuongeza:
Kutokana na shughuli nyingi za Makamu wa Rais, tuliliomba Bunge likubali kuidhinisha Sh4 bilioni ambazo ni fedha kwa ajili ya matumizi yake ya kawaida, pamoja na Sh24 bilioni fedha za kawaida katika matumizi ya ofisi yake na Sh10 bilioni kwa ajili ya miradi ya maendeleo ili kuwezesha ofisi hiyo kufanya kazi vizuri,alisema.
Alisema makadirio ya fungu la 31 yanajumuisha Sh32 bilioni ambazo ni fedha za kibajeti kwenda Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kwaajili ya maendeleo katika visiwa hivyo.