Profesa
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 905
- 624
Nadhani wasioelewa wanaweza kuongea hisia zao na wasiongee ukweli wa mambo, wakijaribu kuunganisha na maswala mengine hasa yale yanayohusu maisha binafsi.
DOWANS ilikuwa kampuni na ilifanya kazi ya kuzalisha umeme kwa muda wa kuridhisha tu na tuliutumia umeme huo. Mkataba wao ambao tulipaswa kuuhoji mapema, kama ilivyo mikataba mingine huwa ina safeguards za kuepusha kampuni kupata hasara.
Tatizo swala hili sasa ni la kisiasa na limebadilishwa kabisa kutoka technical issue kuwa political issue, wale wanaolitumia wanajaribu kukusanya wafuasi na wanaelekea kufanikiwa sana. Ninashawishika sana kusema kuna wanasiasa wanataka kuitumia nafasi hii kunufaika kisiasa, si jambo baya na si la ajabu, hatari yake ni upotoshaji wa ukweli wa mambo na kuzungumzia hoja. Hapa mimi hoja ya msingi ninayoiona ni Wingi wa fedha zinazopaswa kulipwa kulinganisha na uchumi duni tulionao, na kama serikali itakusudia kutolipa, wakati ilionyesha ina uwezo, natamani mahakama iamue fedha hizo zitengwe na zipelekwe kwenye huduma muhimu mfano kujenga na kuweka vifaa kwenye shule na zahanati kwenye maeneo yanayohitaji huduma hizo.
Serikali inaweza kuwa na kiburi cha kutokulipa lakini serikali inayojali utawala wa kisheria ni lazima ifuate taratibu ili kujenga hoja ya kiburi hicho!
DOWANS ilikuwa kampuni na ilifanya kazi ya kuzalisha umeme kwa muda wa kuridhisha tu na tuliutumia umeme huo. Mkataba wao ambao tulipaswa kuuhoji mapema, kama ilivyo mikataba mingine huwa ina safeguards za kuepusha kampuni kupata hasara.
Tatizo swala hili sasa ni la kisiasa na limebadilishwa kabisa kutoka technical issue kuwa political issue, wale wanaolitumia wanajaribu kukusanya wafuasi na wanaelekea kufanikiwa sana. Ninashawishika sana kusema kuna wanasiasa wanataka kuitumia nafasi hii kunufaika kisiasa, si jambo baya na si la ajabu, hatari yake ni upotoshaji wa ukweli wa mambo na kuzungumzia hoja. Hapa mimi hoja ya msingi ninayoiona ni Wingi wa fedha zinazopaswa kulipwa kulinganisha na uchumi duni tulionao, na kama serikali itakusudia kutolipa, wakati ilionyesha ina uwezo, natamani mahakama iamue fedha hizo zitengwe na zipelekwe kwenye huduma muhimu mfano kujenga na kuweka vifaa kwenye shule na zahanati kwenye maeneo yanayohitaji huduma hizo.
Serikali inaweza kuwa na kiburi cha kutokulipa lakini serikali inayojali utawala wa kisheria ni lazima ifuate taratibu ili kujenga hoja ya kiburi hicho!