Dowans; non si paga! Hatulipi!

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu Zangu,

Leo wakati nikitafakari deni letu kwa Dowans nimemkumbuka Mwalimu. Angekuwepo Mwalimu Nyerere hakika asingetafuna maneno katika hili la Dowans. Angesema neno moja tu; HATULIPI! kama vile kwenye tamthiliya ya M-Italia Dario Fo, mshindi wa tuzo ya Nobeli mwaka 1997 kwenye fasihi.

Hili la Dowans ni itikadi. Waafrika Wajamaa tusikubali mabepari hawa wafikie hatua ya kutunyanyasa hivi. Najiuliza; hivi ni kwa nini Serikali yetu inashindwa kesi nyingi za madai? Hivi hatuna wanasheria wa kupambana kuilinda nchi yetu na ufisadi huu?

Ndugu zangu,
Shilingi bilioni 94 ni nyingi. Hivi tunazitoa hivi hivi huku tunakenua meno. Tuseme tu HATULIPI. Kwani watatufanya nini? Si ina maana ya kesi kuendelea. Tujenge hoja mpya. Walau tuonyeshe tunapambana. Na tukishindwa raundi ya pili, basi, tuhakikishe "Tunakula sahani moja' na waliotuingiza kwenye deni hili. Maana tumefahamishwa majina ya wamiliki wa Dowans lakini bado hatuwajui wamiliki. Maana, kufahamishwa mtu ni kitu kimoja, lakini kumjua mtu ni kitu kingine.

Tusidanganyane, mtu hawezi kutoka Singapore akatua Dar akaenda mpaka CRDB bila ya kuonyeshwa njia na mwenyeji. Tuonyeshwe sasa hao Watanzania wenzetu waliowaonyesha wamiliki wa Dowans njia ya kwenda CRDB!

Ndugu Zangu,

Hata kama tunalazimishwa kulipa, basi, hata kupiga kelele tunashindwa. Tupige kelele; Hatulipi! Non Si Paga!
Na hilo ni Neno La Leo
Maggid
'Kwenye mgao wa umeme'
Iringa.
mjengwa

 
Angekuwepo Mwalimu Nyerere hakika asingetafuna maneno katika hili la Dowans. Angesema neno moja tu; HATULIPI!

Nadhani Nyerere angekuwepo au any responsible leader... tusingefika hata hapa tulipo....., hata hiki kitu DOWANS kisingetokea in the first place.

Now kusema hatulipi, wakati wale ambao ndio wanakusanya kodi zetu na kuziangalia wanalipa itasaidia nini?, mi naona kusema pekee hakutoshi, we should all use our powers kumtambua mwizi na kumfilisi mali zake zote... sababu huyo ni cancer kwa taifa
 
Chadema wamesema wataandamana nchi nzima kupinga malipo ya Dowans.
Waungeni mkono katika hili.
 
Wenyeji ni wale walioandika vimemo na kushinikiza Richmond in first place. Kwanza nashangaa hivi kwanini tunaongelea Dowans na si Richmond? Mkataba wetu ulikuwa na Richmonduli ambayo haikuwahi kuwepo duniani, sasa Dowans anaingiaje. Tunalipa Richmond, EL na RA.
Kuna mabepari wachache wana ubia na serikali, hawazidi 3 lakini wana nguvu ya pesa tena kodi zetu, wanafanya wanavyotaka si ndio KING MAKERS. !
 
Ndugu Zangu,

Leo wakati nikitafakari deni letu kwa Dowans nimemkumbuka Mwalimu. Angekuwepo Mwalimu Nyerere hakika asingetafuna maneno katika hili la Dowans. Angesema neno moja tu; HATULIPI! kama vile kwenye tamthiliya ya M-Italia Dario Fo, mshindi wa tuzo ya Nobeli mwaka 1997 kwenye fasihi.

Hili la Dowans ni itikadi. Waafrika Wajamaa tusikubali mabepari hawa wafikie hatua ya kutunyanyasa hivi. Najiuliza; hivi ni kwa nini Serikali yetu inashindwa kesi nyingi za madai? Hivi hatuna wanasheria wa kupambana kuilinda nchi yetu na ufisadi huu?

Ndugu zangu,
Shilingi bilioni 94 ni nyingi. Hivi tunazitoa hivi hivi huku tunakenua meno. Tuseme tu HATULIPI. Kwani watatufanya nini? Si ina maana ya kesi kuendelea. Tujenge hoja mpya. Walau tuonyeshe tunapambana. Na tukishindwa raundi ya pili, basi, tuhakikishe "Tunakula sahani moja' na waliotuingiza kwenye deni hili. Maana tumefahamishwa majina ya wamiliki wa Dowans lakini bado hatuwajui wamiliki. Maana, kufahamishwa mtu ni kitu kimoja, lakini kumjua mtu ni kitu kingine.

Tusidanganyane, mtu hawezi kutoka Singapore akatua Dar akaenda mpaka CRDB bila ya kuonyeshwa njia na mwenyeji. Tuonyeshwe sasa hao Watanzania wenzetu waliowaonyesha wamiliki wa Dowans njia ya kwenda CRDB!

Ndugu Zangu,

Hata kama tunalazimishwa kulipa, basi, hata kupiga kelele tunashindwa. Tupige kelele; Hatulipi! Non Si Paga!
Na hilo ni Neno La Leo
Maggid
'Kwenye mgao wa umeme'
Iringa.
mjengwa


Kwenye sheria za kimataifa kuna Mwalimu, au hujasikia alivyokataa kuwalipa LONRHO, unajuwa iliishaje? si alijidai anataifisha? nilibandika post yake humu JF, ukibisha sana ntakuwekea ujuwe huyo Mwalimu alivyoaibishwa na LONRHO.
 
Ndugu Zangu,

Leo wakati nikitafakari deni letu kwa Dowans nimemkumbuka Mwalimu. Angekuwepo Mwalimu Nyerere hakika asingetafuna maneno katika hili la Dowans. Angesema neno moja tu; HATULIPI! kama vile kwenye tamthiliya ya M-Italia Dario Fo, mshindi wa tuzo ya Nobeli mwaka 1997 kwenye fasihi.

Hili la Dowans ni itikadi. Waafrika Wajamaa tusikubali mabepari hawa wafikie hatua ya kutunyanyasa hivi. Najiuliza; hivi ni kwa nini Serikali yetu inashindwa kesi nyingi za madai? Hivi hatuna wanasheria wa kupambana kuilinda nchi yetu na ufisadi huu?

Ndugu zangu,
Shilingi bilioni 94 ni nyingi. Hivi tunazitoa hivi hivi huku tunakenua meno. Tuseme tu HATULIPI. Kwani watatufanya nini? Si ina maana ya kesi kuendelea. Tujenge hoja mpya. Walau tuonyeshe tunapambana. Na tukishindwa raundi ya pili, basi, tuhakikishe "Tunakula sahani moja' na waliotuingiza kwenye deni hili. Maana tumefahamishwa majina ya wamiliki wa Dowans lakini bado hatuwajui wamiliki. Maana, kufahamishwa mtu ni kitu kimoja, lakini kumjua mtu ni kitu kingine.

Tusidanganyane, mtu hawezi kutoka Singapore akatua Dar akaenda mpaka CRDB bila ya kuonyeshwa njia na mwenyeji. Tuonyeshwe sasa hao Watanzania wenzetu waliowaonyesha wamiliki wa Dowans njia ya kwenda CRDB!

Ndugu Zangu,

Hata kama tunalazimishwa kulipa, basi, hata kupiga kelele tunashindwa. Tupige kelele; Hatulipi! Non Si Paga!
Na hilo ni Neno La Leo
Maggid
'Kwenye mgao wa umeme'
Iringa.
mjengwa


01%2Bcopy.jpg
t.gif
03%2Bcopy.jpg
t.gif
 
mjengwa leo umemwaga point !! tuko pamoja mkuu na pole san na mgao.
USHAURI:Mjengwa ndugu yangu nunua hata kajenereta usiwaweke wale makamanda kwenye giza.
 
Mjengwa pole na mgao mnaohangaika nao Iringa.
Tambua kuwa hata huku bandari salama "Makao makuu mbadala" hali ndo hiyo tu, wala usiumie moyo kudhani labda wa Dar mambo yao mswanu. Na joto la huku si walijua, tunashindana vikwapa tu kwenye daladala!

Kuhusu Dowans hilo lingewezekana tu kama walipaji wasingekuwa wenye kufaidika na hizo bilioni 94.
Dowans ni mtoto wa serikali iliyoko madarakani na ni mtoto pendwa sana, utahitaji muujiza wa manabii ili wazo lako la kutolipa likubaliwe.
Tumechinjwa kama kuku wa kisasa maana kuku wa kienyeji hakubali kwa urahisi sharti umkimbize kama unataka awe kitoweo siku hiyo.

Umemzungumzia Nyerere; nitajie kiongozi yeyote wa serikali hii ambaye anamfanana Mwalimu japo kwa 10% tu. Tulidhani mtoto wa mkulima angejaribu kufurukuta - wapi bwana. Fisadi ni kama yule nyoka anaconda wa amazon, anakunyima pumzi kwanza kabla hajakumeza.

Wezi wetu wanjulikana lakini huwezi kuwakamata kwa sheria zetu maana hakuna mahali majina yao yanasomeka.
Unahitaji ujasiri wa yule mfalme aliye mtariki Malkia kwa vile tu alituhumiwa ugoni. Bahati mbaya sana katika safu ya uongozi wa sasa hayupo mwenye ujasiri wa kumwambia mwenzake "unaharibu nchi yetu kaa kando"!

Tutalipa hizo billioni kisha watatuambia tuinunue mitambo yao ama litapigwa zengwe majenereta ya Tanesco yasifanye kazi ili watanzania mpige kelele kisha wanakuja na mkataba mpya kwa Dowans na safari hii tutalipa Million 200 kwa siku.
Kuna watu wana Power of Attorney (PoA) kudraw hizo millioni na kugawa kwa wadau

Inauma lakini ndio ukweli!

Alamsiki!
 
Back
Top Bottom