DOWANS (BEHIND THE SHADOWS): What you were not supposed to know...!

Du inatisha mm nilishasema inawezekana kupinga malipo ya 185bn thread ya kwanza ya Invisible juzi Wanasheria watusaidie Mbona JK alitaifisha mashamba na mabenki 1967 na Msajili wa Majumba 1971. Uganda Idd amini aliwatimua wahujumu uchumi waasia? Mugabe aliwatimua maSettler? akagawa mashamba? na Jumuia za Ulimwengu hazijamfanya chochote?
yote yanawezekana kabla ya kuingia mitaani na leo huku kwetu ni mgao kutwa nzima bado LUKU imepanda
 
Of course.. tunaweza kuweka documents yenye majina ya nani wenye share humo... kama wao wenyewe hawatofanya hivyo..
 
Umesoma vizuri hiyo kesi ya dowans na rdevco inahusu nini lakini? Yaani ulitaka Serikali inunue mitambo ambayo ipo kwenye kesi!! Halafu unajua PPA ya TZ inasemaje kuhusu manunuzi?

Sikiliza, sasa hakuna cha kununuwa hiyo mitambo, hilo ni suala lilikuwa kabla hukumu haijatolewa. Ni mapendekezo ya walioona kuwa hili la kulipa gharama kibao litakuwepo ikiwa kesi itaendelezwa. Yalitukuta kwa kuvunja mkataba na IPTL hatujasoma.

Watu wanashindwa kuelewa kuwa hakuna mfanya biashara asiye taka faida, na katika hili la Dowans, mitambo ilishafikishwa pale Ubungo na ikawa-commissioned na miwili kati ya hiyo ni brand new. Leo uwaambie wafanya biashara hatuitaki, halafu wao wakae kimya, wanakutizama wanangoja wafilisike? Hakuna mahakama duniani itayoipa ushindi Tanesco kwenye kesi hii, iende itavyokwenda. Ingekuwa mitambo haijaletwa, au imletwa chini ya kiwango, au mibovu, au mitambo hewa, hapo ndio tungeweza kushinda.

Hawa mahakimu wanaotizama hizi kesi ni watu makini na wanapitia mikataba na wana-tazama real situation na wanajuwa biashara za kima-Taifa zinaendeshwaje.

Hata ukiwalaumu wana-sheria wa Tanesco, bure tu. Walijkuwa hawana cha kufanya kwa hili, na walijuwa kuwa hii kesi hatushindi, lakini na wao wamepelekewa kazi waikatae? Wangeikataa ndio hayo hayo malipo lazima, sasa wafanye nini, wajaribu bahati yao, na ndicho walichofanya. Sasa sisi tubaki na porojo tuu humu.

Mimi nasema, fungilia mbali Tanesco na waache wafanya biashara waendeshe, tena si kwa kuingia ubia au kuwapa waendeshe lakini mali yetu, hapana. Ya ama wainunuwe iwe mali yao 100% au hisa zingine wauziwe wa Tanzania, kama yalivyofanywa mashirika mengine yaliyokuwa yanatia hasara kila siku, mbona leo yanaingiza faida? simply ni kuwa, hata umuweke nani kuendesha haya mashirika ya uma hataweza! wacha wenye vipaji vyao wafunguwe mashirika. Serikali ibaki kuweka kanuni tu, kama tunavyoona kwenye mambo ya mawasiliano, lilipokuwa shirika la uma moja tu, bei za mawasiliano zilikuwa juuu sana, hamna ufanisi, una book simu leo ya kwenda nje unaweza uipate baada ya wiki. Baada ya kuruhusu mashirika binafsi ya mawasiliano si tunaona matokeo,leo mawasiliano ni rahisi kuliko miaka 30 nyuma, huoni ajabu hapo, halafu hilo shirika moja tu, likawa halina faida.

Leo hii ikiamuliwa yaje mashirika mengine ya kugawa na kufuwa umeme, utaona bei za hii nishati zitavyo poromoka na hautosikia sijui nani kaiba mitambo sijui nani kaiba transformer, sijui nani kaiba mafuta ya transformer.

Leo nilikuwa na msikiliza Mhando wa Tanesco, nikamshangaa sana, anasema wanaweka Tranformer mara tano sehemu moja na kila wakiweka inaibiwa mafuta. Yaani huu kama si upumbavu ni nini, umeshaweka mara ya kwanza, umeibiwa, ya pili umeibiwa, hujatafuta solution tu? wewe unaendelea kuweka Transformer nyingine mpaka mara tano. Halafu unakuja kujisifu kwenye TV? what a shame. Halafu ndio kampuni itaendelea kwa kuendeshwa na watu kama huyu?
 
Cite ya breala haisemi nani shareholder.

Kwanini waseme Mkuu na ili hali hawataki hao wamiliki wajulikane? Kama utakumbuka pale Brela pia kulifanyika usanii wa hali ya juu kwenye sakata la Mkapa kujimilikisha Kiwira Coal Mining katika mazingira ya kutatanisha. Wafuatiliaji pale Brela kutaka kujua ni nani wamiliki halali wa KCM basi baadhi ya documents zikaota miguu na kukosekana na nyingine kuingia kimiujiza ili mradi tu kuuficha ukweli. Brela si taasisi ambayo inastahili kuaminiwa hata siku moja
 
Asante sana Mzee. Nimesoma, jamani naombeni gongo kidogo nipunguze makali ya mawazo. Naomba kina Tindu Lissu watusaidie kutafsiri hii kiswahili ili wananchi wetu wafahamu mbivu na mbichi. So sad. Yaani tutakubalije kuilipa Richmond pesa? Namshukuru Mungu kwa kuleta utandawazi katika media maana tunapata tusiyotakiwa kuyafahamu. Kwa nini RA na EL watuchezee kiasi hiki? Hawa ni wazalendo kweli? Maaskofu na Wachungaji mnaowakumbatia hawa watu, je mnajuea mnapata mafungu ya kumi na sadaka za damu ya Watanzania. Nakufa, wosia nimwachie nani? Sina wa kumwamini!!! Akili zetu zimeshatekwa!


yaani ingekua poa ana
 
Ninaona Tanesco walikuwa wanamtambua Rostam Aziz kama mmiliki wa Richmond........................kutokana na power of Attorney aliyopewa ya malipo ya CRDB...................................Soma kifungu cha 17.11 kisemacho................



Jamiiforums
RostamAziz.jpg

 
Of course.. tunaweza kuweka documents yenye majina ya nani wenye share humo... kama wao wenyewe hawatofanya hivyo..

Weka, halafu useme hiyo ni siri pia unaifichuwa, wakati tumekuwekea hapa link ya BRELA abayo hiyo kampuni ipo na imesajiliwa ki halai na shria za BRELA unakwenda pale unalipia elfu sita (kama hawajapandisha) za official search unapata hiyo habari yooote, ya nani mwenye kampuni na ana hisa ngapi. Na kama hutaki BRELA unakwenda Tanzania Chamber of Commerce unapata data zooote. nini cha zaidi katika kupata majina ya wamiliki, yaani unafanya jambo kuwa ni la suspense kubwaaaaa kumbe ni pumba tu. Yaani nakwambia unawapata kweli wasiojuwa pa kuzipata hizo habari. Ama kweli "wajinga ndio waliwao".

Brela: http://www.brela-tz.org/

Tanzania Chamber of Commerce: http://www.tccia.com/tcciaweb/contacts.aspx
 
Du inatisha mm nilishasema inawezekana kupinga malipo ya 185bn thread ya kwanza ya Invisible juzi Wanasheria watusaidie Mbona JK alitaifisha mashamba na mabenki 1967 na Msajili wa Majumba 1971. Uganda Idd amini aliwatimua wahujumu uchumi waasia? Mugabe aliwatimua maSettler? akagawa mashamba? na Jumuia za Ulimwengu hazijamfanya chochote?
yote yanawezekana kabla ya kuingia mitaani na leo huku kwetu ni mgao kutwa nzima bado LUKU imepanda

Kweli usilolijuwa ni usiku wa kiza, for your information, JK alilipa mabenki yote ya wazungu alio jidai ka-taifisha na mashaamba yote ya wazungu yalilipwa walioonewa ni wenye mali wa Islam tu, ambao wengi hawajalipwa, mpaka alipokuja Mzee Mwinyi ndio waliokuwa hai na wanaokwenda kudai akaanza kuwarudishia mali zao, wengine ndio mpaka leo zimedhulumiwa. Wee, si unaiona Zimbabwe baada ya kujidai kuchukuwa mali na mashamba ya wazungu? sasa hivi wenyewe wameanza kulipa gharama kisiri siri.

Nyerere hujawahi kusikia sakata lake la LONRHO? alijidai kuichukuwa, weeee, kiama chake hata miezi miwili haijapita akairudisha. Na alivyowachukulia vyote akalipa.

Soma zaidi hapa kuhusu Lonrho na Nyerere: http://multinationalmonitor.org/hyper/issues/1980/02/ratner.html
 
Ujinga mtupu,
natumia cm ya mchna,nijuzeni, ati kikwete katajwa kuwa mmiliki wa Dowans au?
Kifungu Na. 17.11 kimeonyesha tanesco walikuwa wakielewa ya kuwa Rostam Aziz ndiye mmiliki wa Dowans kutokana na power of Attorney aliyopewa kuhusiana na malipo yaliyofanywa na tanesco kule CRDB.......................

Na alipo Rostam Aziz.......JK yumo kupitia RIDHIWANI na Lowassa...............................


RostamAziz.jpg
 
hivi kweli Dowans wanaweza kumpa RA power of attorney kama hawamjui au hawana uhusiano...... jamani hii ni aibu na fedheha kuendelea kuhoji DOWANS ni ya nani..? hivi unaweza ukamwadikia will chokoraa wa mitaani ukaacha mtoto wako wa kuzaliwa...... na kama RA ndio mmiliki basi pia EL anamaslahi na pia JK ana mkate katika DOWANS.... yangu macho
 
hivi kweli Dowans wanaweza kumpa RA power of attorney kama hawamjui au hawana uhusiano...... jamani hii ni aibu na fedheha kuendelea kuhoji DOWANS ni ya nani..? hivi unaweza ukamwadikia will chokoraa wa mitaani ukaacha mtoto wako wa kuzaliwa...... na kama RA ndio mmiliki basi pia EL anamaslahi na pia JK ana mkate katika DOWANS.... yangu macho

Mie nashangaa wasioijuwa Dowans ni ya nani si ndio hao wanao buruzwa na kina mkjj, wakati kila kitu kipo wazi.
 
Kifungu Na. 17.1 kimeonyesha tanesco walikuwa wakielewa ya kuwa Rostam Aziz ndiye mmiliki wa Dowans kutokana na power of Attorney aliyopewa kuhusiana na malipo yaliyofanywa na tanesco kule CRDB.......................

Na alipo Rostam Aziz.......JK yumo kupitia RIDHIWANI na Lowassa...............................

Mmkiliki halafu apewe PA? duh? yaani hiyo PA kajipa mwenyewe? au ana hisa?
 
Kifungu Na. 17.1 kimeonyesha tanesco walikuwa wakielewa ya kuwa Rostam Aziz ndiye mmiliki wa Dowans kutokana na power of Attorney aliyopewa kuhusiana na malipo yaliyofanywa na tanesco kule CRDB.......................

Na alipo Rostam Aziz.......JK yumo kupitia RIDHIWANI na Lowassa...............................

Na Mtikila mbona umemsahau, si huwa anaenda kuvuta kwa RA?
 
Dawa ni KUMKAMATA RA na kumshtaki kama MHUJUMU WA UCHUMI.

Unampa Songombingo hadi aseme wenzie ni nani.

Mambo yakiharibika, utasikia amekimbia sasa hivi au watam-Kolimba.

Jamaa ajihurumie nafsi yake na akiweza basi akimbie sasa hivi, vinginevyo, TISS wako nyuma yake.
 
Hapo umenena, hiyo ni haki ya msingi ya kila mtu, nami nikiwemo! Ingawa awamu ya kwanza ilitubana na katiba yetu! Unafikiri wakati wa Nyerere tungekuwepo hapa JF? duhhh, hata TV tulikuwa hatuna, magazeti ndio hivyo tena, Uhuru, Mzalendo na Ngurumo!

Halafu leo JMK mbaya!

Awamu ya kwanza ulijibana mwenyewe unawasingizia watu you think I will sympathize with you. Am not a loser sorry
 
Mie nashangaa wasioijuwa Dowans ni ya nani si ndio hao wanao buruzwa na kina mkjj, wakati kila kitu kipo wazi.
RostamAziz.jpg


Kama hujui kusoma shauri yako.........................
 
Back
Top Bottom